Uchaguzi 2020 Upinzani kwenye kampeni wazunguke na vijijini, vinginevyo Urais watausikia na kuhisi wanaibiwa kura

Uchaguzi 2020 Upinzani kwenye kampeni wazunguke na vijijini, vinginevyo Urais watausikia na kuhisi wanaibiwa kura

Clever505

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2020
Posts
1,183
Reaction score
2,256
Mimi ni Mwananchi niishie Dodoma katika walaya ya Mpwapwa, nakaa kijijini naweza kupaita porini kabisa. Tumeishi miaka yote bila huduma muhimu kama maji na umeme ambapo maji tumekuwa tukiyapata mbali visimani.

Tangu aingie madarakani JPM ameweza kusimamia vizuri ambapo umeme pamoja na maji vipo kwa uhakika. Na huku kwetu hamna kabisa habari za upinzani, sasa najiuliza ina maana wapinzani hawaoni kwamba na huku wanahitajika kufika kuongea na wananchi? Huku kila kitu ni CCM. Mfano kuna ofisi ya kijiji ambayo kwa mapenzi ya wananchi juu ya CCM haiitwi ofisi ya kijiji wanaiita ya CCM, huku viongozi wa CCM wanapita tu bila upinzani.

Tundu Lissu huku hawamjui kabisa, ni sisi tu wachache tulio mitandaoni ndio tunaona akizungumziwa, wapinzani mnakosea sana kudili na watu wa mjini tu mnasahau kwamba mnapaswa kuingia kila kona ya nchi. Nashangaa sana ninapoona kuna watu wanaamini CCM itatoka madarakani mpo serious kweli?

Mnatukanana tu mitandaoni kwa mambo yaliyowazi tu, hivi ni Tanzania hiihii ninayoijua mimi wapinzani waitoe madarakani CCM? Mkitaka kuishinda CCM hangaikieni kwanza ngazi zote kuanzia viongozi wa vijiji.

Wanakijiji kwa kijiji chetu wanajua kwamba bila Magufuli hadi leo tusingekuwa na umeme wala maji, mnafikiri watu hawa watamchagua mwingine zaidi ya Magufuli? Hivi nyie watu wa mjini mnahisi nyie huko peke yenu mnatosha kumuondoa Magufuli? Washaurini viongozi wa upinzani wajikite na vijijini pia maana hawajulikani huku.

Upinzani kuitoa CCM madarakani sio kazi rahisi kama mnavyofikiria, endeleeni kufarijiana tu kwamba 2020 Magufuli anang'oka madarakani huku mnasahau kwamba kuna maeneo mengi yana watu wa CCM pekee.

Kuna mambo mengi sana ya ovyo yanafanywa na CCM kwa mfano nasikia kuna watu wanaenguliwa tu na kisha wanamuacha mgombea mmoja tu wa CCM, hii kiukweli inatia hasira lakini hayo mambo ni wachache sana huku vijijini ambao wanaweza kujua kwamba ni hujuma zinafanywa na ccm...kwa mfano kwenye jimbo letu mpwapwa mgombea ubunge ni mmoja tu wa CCM mnafikiri nyie upinzani nani atampigia kura Tundu?

Waambieni viongozi wa upinzani kwenye kampeni wazunguke na vijijini vinginevyo urais mtausikia tu na kuhisi mnaibiwa kura kumbe mna wapiga kura wachache.
 
wiki jana nilikuwa vijiji vya Katavi, Rukwa na Songwe - wanasubiri Masia wa kuwaondoa kwenye lindi la ufukara walilomo.
waliposikia Tundu Lissu yupo Tunduma walitamani kwenda kumlaki lakini shida nauli!
 
Vijiji vya aina kama ya hicho Kijiji chako havizidi 3.
 
watajitangazaje ilhali wamepigwa pin kwa miaka5?
 
Clever505,
Umejiunga mwezi uliopita uje na propaganda hizi? Hao wajinga wa huko porini tunakupa jukumu la ww kuwaamsha. Hao wajinga wa huko ndio mtaji wa ccm. Ila fahamu watu wa huko vijijini wao kazi yao ni kuburuzwa na watu wa mjini, kama ww umefanikiwa kuamka, na hao wenzako wataamka tu.
 
Umejiunga mwezi uliopita uje na propaganda hizi? Hao wajinga wa huko porini tunakupa jukumu la ww kuwaamsha. Hao wajinga wa huko ndio mtaji wa ccm. Ila fahamu watu wa huko vijijini wao kazi yao ni kuburuzwa na watu wa mjini, kama ww umefanikiwa kuamka, na hao wenzako wataamka tu.
Ndio mzee nimejiunga humu mwezi uliopita ila nimeshangaa sana kuona vijana mnatukanana ovyo kwa mambo ya kishabiki. Niamini mimi mzee huku kwetu upinzani haupo wakumbushe viongozi wako waje wajipatie wafuasi.
 
watajitangazaje ilhali wamepigwa pin kwa miaka5?
Keshokutwa kampeni zinaanza wakumbusheni waje na huku vijijini kuna wapiga kura wengi sana wanachukuliwa na ccm tu
 
Ndio mzee nimejiunga humu mwezi uliopita ila nimeshangaa sana kuona vijana mnatukanana ovyo kwa mambo ya kishabiki. Niamini mimi mzee huku kwetu upinzani haupo wakumbushe viongozi wako waje wajipatie wafuasi.

Subirini kwanza mpaka mzoee kutumia umeme na maji, kwa sasa mtaishia kutupotezea muda. Mtakapoacha kushikiwa akili na kuona hizo huduma sio hisani bali ni wajibu wa serikali yoyote, hapo ndio tutakuja.
 
Sasa waliosababisha huduma zote hizo uchelewe kupata si hao hao ccm ..

Unadhani maisha yanaishia kunya vichakani na kuchimba viazi , kweli shughuli ipo
 
Mi ni mwananchi niishie Dodoma katika walaya ya Mpwapwa, nakaa kijijini naweza kupaita porini kabisa. Tundu Lissu huku hawamjui kabisa, ni sisi tu wachache tulio mitandaoni ndio tunaona akizungumziwa...
\
Kijana Clever505, ngoja nikupe ushauri kidogo nikianzia na kaswali kadogo kuhusu neno clever ulilolitumia kwenye avatar yako hapo juu, je unajua tafsiri sahihi ya neno hilo? Mh. Tundu Antiphas Lissu kabla ya kurejea nyumbani, dhihaka dhidi yake ziliendeshwa hivyo hivyo kwa dhana potofu kuwa mashabiki wake ni wa mtandaoni tu.

Siku aliyotua uwanja wa ndege Dar es Salaam bila shaka ulishuhudia umati uliompokea na ghafla, kama vile wametoka katika usingizi mzito, utawala uliduwaa, ulipigwa bumbwazi! Je unajua kwa nini? Ni kwa sababu watu waliodhaniwa ni wa mtandaoni kume wapo na walijitokeza na kuifuta kabisa imani na ujinga uliowaganda watu kama wewe!

Umeanza kwa kudai wewe unaishi kijijini, ndani kabisa panapoweza kuitwa porini ambako watu hawamjui kabisa wala hawajawahi kumsikia Mh. Tundu Antiphas Lissu, jasiri aliyegoma kuanguka pamoja na kumiminiwa risasi za kumwangusha tembo. Naomba tena nikuulize kijana Clever505, wewe huyu shujaa aliyegoma kufa, uliwezaje kumjulia?

Alipoanza kuzunguka mikoani akiwatafuta wadhamini, je unakubali kapitia mikoa zaidi ya 10 na kaweza kuzoa maelfu kwa maelfu ya mashabiki na wadhamini wa kumwaga kama sheria ilivyomtaka? Je unakiri kuwa kati ya wagombea wote wa nafasi zozote zile katika uchaguzi ujao ameweza kuwaacha kwa mbali hadi wenzake waliodaiwa kupendwa zaidi?

Clever505, ushauri wangu kwako ni huu, kwa kuwa umebahatika kuuona mwanga ambao wakazi wa porini unakodai kukaa hawajaweza kuuona, unaonaje ukiteuliwa kuwa mjumbe wa kueneza ujio wake? Labda utaniuliza ujio wake nani? Nafurahi kukufahamisha kuwa ni ujio wa mpigania uhuru, haki na usawa kwa wote, Mh. Tundu Antiphas Lissu!
 
We uko kijiji gani wenzio tuko huku huku kijijini watu wanasuburi tarehe ifike wamvhagua mgombea wao kampeni zanini tena wakati Lissu ameshasikika msg na picha zinatembea kwenye makundi ya watu ukiona watu wakusanyika pamoja ujuwe wanasikiliza hotuba za Lissu YouTube
 
We uko kijiji gani wenzio tuko huku huku kijijini watu wanasuburi tarehe ifike wamvhagua mgombea wao kampeni zanini tena wakati Lissu ameshasikika msg na picha zinatembea kwenye makundi ya watu ukiona watu wakusanyika pamoja ujuwe wanasikiliza hotuba za Lissu YouTube
Kijiji gani anakuja nami nije nimuone?
 
Back
Top Bottom