Upinzani tusigeukane kwenye critical times baada ya Uchaguzi Mkuu

Upinzani tusigeukane kwenye critical times baada ya Uchaguzi Mkuu

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Udhaifu wa vyama vya upinzani ni kugeukana kwenye critical times baada ya uchaguzi mkuu kupita.

1. Critical time ya kwanza ni 2015 baada ya kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu Zanzibar. Baada ya Tume ya uchaguzi Zanzibar kufuta matokeo ya uchaguzi chama Cha CUF kupitia Maalim Seif walipinga na kujitoa kwenye uchaguzi wa marudio.

Cha kushangaza wakati Maalim seif akipambana ili haki ipatikane Zanzibar, akaibuka Prof Lipumba ambaye alikuwa amejiuzulu na kuanza vioja dhidi ya Maalim Seif na kurudi kwa nguvu kwenye uongozi wa chama. Mpaka zikawepo CUF mbili ya Maalim Seif na Lipumba aliyekuwa anasaidiwa na Msajiri wa vyama.

Hivyo, katika critical moment ambayo CUF ilikuwa inapigania haki ya uchaguzi kule Zanzibar, akaibuka mpinzani Prof Lipumba na kuanza kufifisha hizo harakati na hatimaye zikafa. Muda mwingi ukatumika kwenye kesi mahakamani na hoja ya uchaguzi Zanzibar ikafa.

Leo Prof Lipumba anawaomba msamaha wa Zanzibar na kuwaomba warudi CUF na wasahau yaliyopita. Cha kujiuliza kipindi kile aliwageuka wenzake wa Zanzibar kwa sababu gani? Na kwa lengo gani?

2. Critical time ya pili ni mwaka 2020, baada ya madhaifu yalionekana kwenye uchaguzi Mkuu, chama Cha CHADEMA kilipinga matokeo na kudai kutoyatambua. Baadhi ya madhaifu wagombea wengi wa Upinzani kuenguliwa bila sababu za msingi,. Wakurugenzi kuonesha ushabiki wa wazi, Tume kuwafungia kufanya kampeni wagombea wa upinzani, kupatikana kwa kura feki, majimbo karibia yote kupelekwa CCM hata Kama mshindi hakuwa CCM na kuzimwa kwa mitandao ili kupunguza kupashana habari kuhusu kinachoendelea kwenye uchaguzi.

Wakati CHADEMA wakiwa katika Hali ya kuonesha msimamo wa kutokuukubali uchaguzi huo na kuupinga likaibuka kundi la wanawake 19 wa viti maalum CHADEMA ambao wengi wao waligombea majimboni na kwenda kuapishwa bungeni mbele ya spika Ndugai. Hivyo wakaondoa kabisa ile nguvu ya kupinga uchaguzi mkuu, ingawa chama kilikataa kuwatambua na kuwavua uanachama lakini bado wapo bungeni.

Ushauri wangu kwa vyama vya upinzani, tusigeukane kwenye critical time baada ya uchaguzi mkuu , bali tushikamane mpaka kile tunachopigania kipatikane.
 
Ukiielewa nguvu ya CCM kidola kuuvuruga upinzani utawahurumia tu upinzani badala ya kuwalaumu wanageukana.
Sasa hivi ACT ndio wanaishambulia kwa kasi CDM!
Ground haipo fair alafu mtu anatapika utumbo et ingefanya ivi ingefanya vile wakati unaona kabisa chamatawala inatumia system nzima ya nchi kuwamaliza upinzani kwakua wanategemewa kifedha na kiulinzi
 
Ukiielewa nguvu ya CCM kidola kuuvuruga upinzani utawahurumia tu upinzani badala ya kuwalaumu wanageukana.
Sasa hivi ACT ndio wanaishambulia kwa kasi CDM!

Kweli kabisa. Shida ipo hapo kwenye dola. CCM Ni chama dola, hivyo inatumia apparatus za dola Kama polisi na mahakama kuwashusha wapinzani.
 
Ground haipo fair alafu mtu anatapika utumbo et ingefanya ivi ingefanya vile wakati unaona kabisa chamatawala inatumia system nzima ya nchi kuwamaliza upinzani kwakua wanategemewa kifedha na kiulinzi

Kweli ground haipo fair, lakini ndio wapinzani wageukane wao kwa wao katika kipindi ambacho wanahitaji umoja kupambana na CCM ?
 
Kweli ground haipo fair, lakini ndio wapinzani wageukane wao kwa wao katika kipindi ambacho wanahitaji umoja kupambana na CCM ?
Elewa point yangu tambua taifa haina system yake isiyofungamana na chama bali ina system iliyofungamana na chama ambacho ni ccm.
Kama mifumo ya serikali inayosimamia taifa ni ya kichama unadhani vyama vya upinzani vitafanyann isipokua kutegemea rwaction za wananchi ambao bado wana uelewa mdogo.

serikali makusudi inauwezo wa kuamua nani apewe ruzuku ama mshahara nan asipewe, hii inakamilisha maamuzi yao nani ashinde nani asishinde hivyo ni ngumu kupata umoja wa wapinzani ikiwa ubinafsi umo ndani ya wanasiasa ambao wengi wao wamo ccm na serikalini
 
Elewa point yangu tambua taifa haina system yake isiyofungamana na chama bali ina system iliyofungamana na chama ambacho ni ccm.
Kama mifumo ya serikali inayosimamia...

Nimekuelewa mkuu, kumbe hi ndio root cause.
 
Kwenye siasa hakuna common enemy, kuna permanent interest yaani kushika dola

Labda theoretically, lakini practically Kuna common enemy yani chama tawala. kwani kuna unyama upinzani wanatendewa kiasi kwamba huwezi kujenga maelewano na chama tawala hadi ukitoe madarakani.

In short huwezi kupata permanent interest bila kumuondoa common enemy chama tawala. CHADEMA haiwezi kupata madaraka Kama haitamshinda CCM kwanza ambaye ndio common enemy wake politically.
 
Labda theoretically, lakini practically Kuna common enemy yani chama tawala. kwani kuna unyama upinzani wanatendewa kiasi kwamba huwezi kujenga maelewano na chama tawala hadi ukitoe madarakan...
Kuna approaches na strategies tofauti tofauti at their disposal kufikia lengo kuu (kushika dola), ikiwa ni pamoja na kujiunga na chama tawala. So, siyo lazima chama tawala kiwe enemy au common enemy as you suggested
 
Kuna approaches na strategies tofauti tofauti at their disposal kufikia lengo kuu (kushika dola), ikiwa ni pamoja na kujiunga na chama tawala. So, siyo lazima chama tawala kiwe enemy au common enemy as you suggested

Asante mkuu.
 
Kujiunga na chama tawala kama ACT Zanzibar?
Kuna approaches na strategies tofauti tofauti at their disposal kufikia lengo kuu (kushika dola), ikiwa ni pamoja na kujiunga na chama tawala. So, siyo lazima chama tawala kiwe enemy au common enemy as you suggested
 
Back
Top Bottom