Upinzani - walio waoga (cowards) si Wafuasi

Upinzani - walio waoga (cowards) si Wafuasi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Imekuwa kawaida kusikia watanzania wakiwaita watanzania wenzao kuwa ni waoga (cowards). Maajabu ya Mussa. Kwani hao wanaowaita wenzao kuwa cowards utaifa wao si ni huu huu au wao ni walamba asali?

Uhalisia wa mambo ni kuwa wanaowaita hivyo wenzao, nia yao ni kutokuwepo mstari wa mbele kunakofahamika kuwa ni hatari zaidi.

"Wako kwenye kuwasakizia wenzao kama mbwa tu, ili wakawapambanie."

IMG_20220826_161105_738.jpg


Watu hao hawataki kuwa sehemu ya kulipa gharama zilizo kubwa kwenye mapambano. Nia yao, "panga pangua" wasidhurike kabisa. Kama vipi hiyo iwahusu zaidi wowote wengine. Lakini si wao wala familia zao.

Hawa ni "opportunists' tu, wenye kuangalia zaidi maslahi yao na familia zao.

Hawana taabu kujilia matunda yatakayopatikana (kwa raha zao), hata kama wote walioyapigania watakuwa walikufa au kupotelea mbali kwenye mapigano yaliyoleta matunda hayo.

Kimsingi ni watu wenye ubinafsi uliopitiliza.

Mbaya zaidi watu hawa wakiwa ni viongozi, ilikuwa hii ni vizuri wakaachia ngazi wenyewe au wakafurushwa madarakani pasipo na kuchelewa. Wa hivi ndiyo viongozi mizigo sasa. Kwa hakika viongozi wa namna hii hawatufai.

Viongozi wa hivi ni sawa tu na wale wakazi wa DRC wanaomtaka MONUSCO apigane kwa niaba yao, huku wakimlaumu kuwa hapigani kwa moyo au bidii ya kutosha.

Watu wa namna hii utawajua kwa kauli zao. Wanadhani mtanzania wa leo ni mjinga kuliko wao. Wanasema hamtokei mitaani, kama vile wao wanatokea mitaani.

"Kwanini tusitokee wote mitaani? Kwani JKNIA au Kiluvya ilikuwa je? Kwani viongozi wetu hawakuwa pale? Wafuasi hawakuwepo? Au walikuwa wao peke yao?"

Ifahamike jaribio la kuwaita watu kumwagika mitaani wakati awaye yote yuko nyumbani kwake, labda akiwa kwenye Runinga haliwezi kuwa na tija.

Tufike mahali asilaumiwe dobi. Tulipo yupi anaweza kujivua kuwajibika na tulipofikishwa?

Tukae chini kujitathmini - kutambua tulipokwamia. Mbona tulikuwa vizuri mno?
 
Kumbe hata wale wanaowaita wengine cowards nao ni cowards pia, ndio maana hao wanaojiona jasiri huwa wanashindwa kufanya chochote pale cowards wasipoonekana!.

Hili taifa lina watu amazing sana.

Bahati mbaya zaidi ninadhani kuwa cowards hasa ni hawa wanaowaita wenzao hivyo.

Wamwita mwingine mwoga kwa ujasiri upi uliouonyesha wewe wapi? Au kwa kuwa nyuma ya huyu Bobbi?

IMG_20220826_161105_738.jpg
 
Wanaogopa kukosa keki maana ndo watakuwa wa kwanza kunyakuliwa.

Kama ni hivyo ndiyo mawazo yao kumbe mwoga nani basi?

Kwa upande mwingine nao:

"Wananyakuliwa vipi wao? Mbona hakunyakuliwa mtu JKNIA au Kiluvya kwenye zama hatari kama za jiwe?"

Mbona kuna kama watu kuhofia vivuli vyao wenyewe?
 
Huyo ni Lissu mkuu, huyo si mwingine awaye yote. Ndiyo maana hakuwa peke yake JKNIA au Kiluvya.

Tusitembelee nyota za wengine. Chonde chonde ndugu kila mtu atokee hapa kama alivyo.

Acheni utani kwenye mambo serious kama haya.

...

1661532438886.png
1661532507476.png
 
..nakushauri uiandame serikali, badala ya kuwaandama wapinzani.

..wanaotutesa Watanzania ni serikali, hatuteswi na wapinzani.

..sielewi kwanini unawalaumu wapinzani, badala ya kulaumu serikali na Ccm.
 
..nakushauri uiandame serikali, badala ya kuwaandama wapinzani.

..wanaotutesa Watanzania ni serikali, hatuteswi na wapinzani.

..sielewi kwanini unawalaumu wapinzani, badala ya kulaumu serikali na Ccm.

Sina ninapowalaumu au kuwaandama wapinzani.

Hata hivyo ninawalaumu na kuwaandama waoga wote wanaowaita wenzao waoga huku wakiwatumia mashujaa kama kina Lissu kama ngao zao.

Lawama kwa walamba asali ni kupoteza muda. Hao ni wakufurusha:

Tunataka haki? Hatutaki tozo? Tukutane Tahrir.
 
Mkuu JokaKuu Ingependeza kusikia kauli za viongozi wetu. Pamoja nao ikiwapendeza tukutane Tahrir.

Waoga hatuwahitaji, wala hatuhitaji kuonyeshwa mwoga ni nani na awaye yote ambaye labda hata hatuja wahi kuuona ujasiri wake.

Zaidi sana hatuwajui waoga wala hatuwahitaji. Kimsingi hata wakiuchuna tu popote waliko, kwa hakika ni sawa tu.
 
..nakushauri uiandame serikali, badala ya kuwaandama wapinzani.

..wanaotutesa Watanzania ni serikali, hatuteswi na wapinzani.

..sielewi kwanini unawalaumu wapinzani, badala ya kulaumu serikali na Ccm.

Sina hakika uliona wapi nikilaumu japo bila shaka hukupenda kuziona frustrations za kupelekwa sokoni.

Ikikupendeza angalia tarehe zile.

Taabu yetu ujuaji saana!

imhotep, Proved, GWAMAKA USWEGE, waliomo na wasiokuwamo au nasema uongo?
 
Sina hakika uliona wapi nikilaumu japo bila shaka hukupenda kuziona frustrations za kupelekwa sokoni.

Ikikupendeza angalia tarehe zile.

Taabu yetu ujuaji saana!

imhotep, Proved, GWAMAKA USWEGE, waliomo na wasiokuwamo au nasema uongo?

..umma unahitaji kuandaliwa.

..pia umma unahitaji kiongozi anayeaminika.
 
..umma unahitaji kuandaliwa.

..pia umma unahitaji kiongozi anayeaminika.

Ndiyo maana wengine tumekuwa na taabu na mwamba kwa muda mrefu:

Gg1mKSLWYAAyvA9.jpeg


Kwamba wanashangilia Slaa kukamatwa, au kubagaza shughuli zozote za upinzani?

Kwamba wako na CCM kwenye lolote?

Gf8b-vhawAEan-I.jpeg


Hawana misimamo inayoelrweka Gaza, Ukraine, LGBTQ nk?

Hawana falsafa, elimu duni, wananunulika?

Ama!?

Sisi siyo bidhaa za kuchuuzwa sokoni!
 
brazaj ,

..wengine tulikuwa na matumaini makubwa maridhiano yafanikiwe, na ilikuwa vigumu kukubali kuwa Ccm na Samia walikuwa wanafanya ulaghai.
 
brazaj ,

..wengine tulikuwa na matumaini makubwa maridhiano yafanikiwe, na ilikuwa vigumu kukubali kuwa Ccm na Samia walikuwa wanafanya ulaghai.

Tatizo letu kubwa ni ujuaji badala ya kupingana kwa hoja:

Wapi red flags hazikuwapo?

Unawaonaje kina Retiree, Erythrocytes, Fundi Nchundo, Mshana Jnr, Fortilo, Drlfter, ntobi, yericko, MMM, yai na wenzao?

Hawa si bora kina @johnthebatist?

Unadhani ipo siku yoyote hoja inaweza kuwa na maana yoyote kwao zaidi buku 7 kama kina Lucas Mwashambwa au Tlaatlaah?

Anasomeka imhotep ukifika wakati akasema big NO!

binti kiziwi au nasema uongo?
 
Back
Top Bottom