#COVID19 Upotoshaji wa Chanjo ya CoVid 19: Nusura nijeruhiwe na Wanakijiji

#COVID19 Upotoshaji wa Chanjo ya CoVid 19: Nusura nijeruhiwe na Wanakijiji

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Mods and Wachangiaji, ninachoandika hapa ni kitu kikubwa na nashauri tahadhari ichukuliwe mapema. It is very serious.

Siku ya Jana nikiwa kwenye majukumu yangu ya kutafuta riziki, nilipaswa kufika kwenye shule X huko kanda ya MAGHARIBI ili kuonana na Mkuu wa shule kwa akili issue Fulani.

Nilikua na kijana ambaye ndio aliyekua Mwenyeji wangu kwa eneo lile. Yule kijana alinipokea bag langu ambalo lilikua na laptop, kikoi cha kimasai na documents kadhaa hivyo kulifanya lionekane kutuna.

Wakati tunaingia eneo la shule ile, ni shule ya msingi ilikua ni muda wa SAA NNE asubuhi ambapo walikua mapumziko. Niseme ukweli, sikujua kitu, kumbe watoto walikua wakitimua mbio wakidhani tumeenda shuleni "kuwachanja" chanjo ya COVID-19.

Mwalimu mmoja wa kike alianza kucheka na kutujulisha kuwa watoto wale walikua wanakimbia wakidhani tumeenda pale kwa ajili ya chanjo na kwamba inaonekana Wazazi wao wamewaonya watoto wao kutokukubali kupata chanjo kwa madai kwamba watakufa.

Niliingia ofisni kwa Mkuu wa shule na nilimweleza masikitiko yangu, hata hivyo Mwalimu wa zamu aligonga kengele na kuwakusanya tena maana walishakimbilia porini.

Wakati tunaondoka pale shuleni, nje kidogo ya shule kuna Wenyeji wa pale vijana na watu wazima walikua wakippakia mizigo (nadhani ni magunia ya maharage au mahindi) basi waliitana wakaanza kuturushia maneno ya dhihaka na kejeli huku wakitutisha kwamba, Ole wetu kama tungewapa chanjo watoto wao.

Kumbe walikua wakifuatilia tukio lile kwa mbali na walikua wakiongea kilugha.

Wito wangu kwa serikali, HII BRAINWASH ni kubwa sana na huenda ikaja kuleta madhara kwa wahudumu wetu wa afya, serikali iwaelimishe watu wake na WAPOTOSHAJI wachukuliwe hatua.

Hiki nilichoandika ni serious na ni tukio halisi
 
Mods and Wachangiaji, ninachoandika hapa ni kitu kikubwa na nashauri tahadhari ichukuliwe mapema. It is very serious.

Siku ya Jana nikiwa kwenye majukumu yangu ya kutafuta riziki, nilipaswa kufika kwenye shule X huko kanda ya MAGHARIBI ili kuonana na Mkuu wa shule kwa akili issue Fulani.

Nilikua na kijana ambaye ndio aliyekua Mwenyeji wangu kwa eneo lile. Yule kijana alinipokea bag langu ambalo lilikua na laptop, kikoi cha kimasai na documents kadhaa hivyo kulifanya lionekane kutuna.

Wakati tunaingia eneo la shule ile, ni shule ya msingi ilikua ni muda wa SAA NNE asubuhi ambapo walikua mapumziko. Niseme ukweli, sikujua kitu, kumbe watoto walikua wakitimua mbio wakidhani tumeenda shuleni "kuwachanja" chanjo ya COVID-19.

Mwalimu mmoja wa kike alianza kucheka na kutujulisha kuwa watoto wale walikua wanakimbia wakidhani tumeenda pale kwa ajili ya chanjo na kwamba inaonekana Wazazi wao wamewaonya watoto wao kutokukubali kupata chanjo kwa madai kwamba watakufa.

Niliingia ofisni kwa Mkuu wa shule na nilimweleza masikitiko yangu, hata hivyo Mwalimu wa zamu aligonga kengele na kuwakusanya tena maana walishakimbilia porini.

Wakati tunaondoka pale shuleni, nje kidogo ya shule kuna Wenyeji wa pale vijana na watu wazima walikua wakippakia mizigo (nadhani ni magunia ya maharage au mahindi) basi waliitana wakaanza kuturushia maneno ya dhihaka na kejeli huku wakitutisha kwamba, Ole wetu kama tungewapa chanjo watoto wao.

Kumbe walikua wakifuatilia tukio lile kwa mbali na walikua wakiongea kilugha.

Wito wangu kwa serikali, HII BRAINWASH ni kubwa sana na huenda ikaja kuleta madhara kwa wahudumu wetu wa afya, serikali iwaelimishe watu wake na WAPOTOSHAJI wachukuliwe hatua.

Hiki nilichoandika ni serious na ni tukio halisi
Wito wangu kwa serikali, HII BRAINWASH ni kubwa sana na huenda ikaja kuleta madhara kwa wahudumu wetu wa afya, serikali iwaelimishe watu wake na WAPOTOSHAJI wachukuliwe hatua. [emoji1545][emoji1533]
 
That's too serious.....

Muda huu nimepita nyumba ya jirani nimekuta kundi la WANAWAKE wa ushirika wa kidini wanafanya kikao chao....nilipowapita nilisikia mwongoza kikao akifafanua kuhusu CHANJO YA UVIKO na uwepo wa "666" ndani yake....nilipunguza mwendo....Yule mwanamke kiongozi alikuwa anaongea kwa kujiamini kabisa kuwa SERIKALI inataka KUWAFANYA mateka wa shetani huyo.....daah it's havoc kwa kweli......

Brainwashing yao si ya kitoto.....

Umetupa ushauri kuntu kabisa.....
 
Wito wangu kwa serikali, HII BRAINWASH ni kubwa sana na huenda ikaja kuleta madhara kwa wahudumu wetu wa afya, serikali iwaelimishe watu wake na WAPOTOSHAJI wachukuliwe hatua. [emoji1545][emoji1533]
Kwa mwendo huo kwa kweli tukifumbia misimamo hasi ya kina Gwajima...hususani ya upotoshaji kwa jamii basi tujiandae na vilio vikubwa....
 
Waziri wa Afya ilibidi ajiuzuru wadhifa wake....

Kwasababu zifuatazo

1. Yeye na jopo lake ndio waliuaminisha umma kuwa nyungu ndio tiba enzi za mwendazake

2. Huyo huyo leo anawaaminisha watu kuwa chanjo ni Bora kuliko nyungu


RAISI SAMIA TUONDOLEE WATU VIGEUGEU KWENYE IDARA ZAKO, Mnawapa mtihani watoa huduma za afya katika kuirejesha jamii kwenye mstari sahihi
 
Hiyo serikali ndio yakulaumiwa maana walitubrainwash mwaka jana mzima kuwa tumeomba Tanzania Corona hakuna mpaka unajiuliza ina maana maombi yetu yana nguvu Sana kuliko hata Vatican na Macca, tena tukawa tunasindikiza na tangawizi,vitunguu,malimao Sasa ghafla wanakuja tena Corona ipo na ina ua mbaya zaidi walewale waliotuambia Corona hakuna ndio hao tena wanapiga kampeni ya chanjo ni uuupuzi
Ilitakiwa waziri wa afya na naibu wake wajiuzuru, Raisi atoe hutuba kuomba radhi kwamba walidanganya wananchi huku wakiwaachia wataalumu kufanya kazi yao kuelimisha a kuhamasisha chanjo, kutoa takwimu sahihi za wagonjwa na vifo
Kumjaza mtu ujinga ni rahisi kuliko kumtoa ujinga
 
Kumbe hata ukichanjwa bado uwezekano wa kuambukizwa corona upo na barakoa utaendelea kuvaa...kwa hali kama hiyo umuhimu chanjo ni UPI? Bado haijangia akilini...tusiwe watu wakuletewa na kupokea kila kitu kunaumuhimu pia wa kuvifanyia tathmini..pia tusiwakejeli wenye maono tofauti na chanjo kilamtu na mtazamo wake na anahaki ya kutoa maoni yake.
 
Hiyo serikali ndio yakulaumiwa maana walitubrainwash mwaka jana mzima kuwa tumeomba Tanzania Corona hakuna mpaka unajiuliza ina maana maombi yetu yana nguvu Sana kuliko hata Vatican na Macca, tena tukawa tunasindikiza na tangawizi,vitunguu,malimao Sasa ghafla wanakuja tena Corona ipo na ina ua mbaya zaidi walewale waliotuambia Corona hakuna ndio hao tena wanapiga kampeni ya chanjo ni uuupuzi
Ilitakiwa waziri wa afya na naibu wake wajiuzuru, Raisi atoe hutuba kuomba radhi kwamba walidanganya wananchi huku wakiwaachia wataalumu kufanya kazi yao kuelimisha a kuhamasisha chanjo, kutoa takwimu sahihi za wagonjwa na vifo
Kumjaza mtu ujinga ni rahisi kuliko kumtoa ujinga
Kama hakuna hatua madhubuti zitachukuliwa basi nawahakikishia tunaweza kupoteza Wahudumu wa afya kutoka kwa wana jamii
 
Majukwa yanatawala pro chanjo tu, anti chanjo wamepotea, Sasa kama chanjo ni hiari ya nini kuparurana kati ya wanaochanjwa na wasiochanjwa? Au ni kutaka sifa tu kuwa wamechanjwa wengi covax wafurahi? Kama waliaminishwa tangawizi na malimao yana kinga tatizo liko wapi? Hiyo chanjo watachanja tu kadiri ya muda unavyoenda na hali ya maambukizi itakavyokuwa
 
Nimecheka mpaka machozi yanitoka
Hii hbr ya chanjo huko vijijini huwambii kitu haawataki kabisa hii kitu chanjo
Wanakwambia ukichanjwa unakuwa zombi yaani zezeta unatoka udenda tu muda wotee
Ghafla nikakumbuka picha ya wale watafiti wa Arusha waliochomwa moto kule Dodoma miaka ile.
 
Back
Top Bottom