Uraia Pacha Tanzania: Siasa ya Bernard Membe na hatma yake

Uraia Pacha Tanzania: Siasa ya Bernard Membe na hatma yake

ndutu

Swala la uraia wa nchi mbili silikatai moja kwa moja nilichosema ni kwamba lazima tuangalie mambo ya msingi kwanza kama kuleta mfumo wa uwajibikaji. Hii ni kuwezesha kudhibiti uwezekano wa watu ambao siyo raia wa Tanzania (wale ambao hawakuwahi kuwa Watanzania) au ambao hawana mapenzi na Tanzania kuiharibu nchi.

Wewe mwenyewe umesema kuwa mafisadi wanauraia wa nchi mbili. Kwani unafiri sijui jinsi wanavyofanya kuingia na pasi ya Tanzania na wakati wa kutoka kupitia Nairobi na kuondokea na Pasi ya nje? Nafahamu ndiyo maana nikasema tuyadhibiti hayo kwanza. Je unafahamu kwa mfano pasi za Marekani zina kuwa tracked na GPS kwahiyo wanajua pasi iko wapi 24-7? Sasa sisi hatuna hata mfumo unao eleweka wa kutunza rekodi za vyeti vya kuzaliwa ndo tukimbilie hayo ya pasi mbili?

Ninapoongelea mfumo wa uwajibikaji nina maanisha sheria kufuata mkondo wake bila ya kuwa na bla bla. Mfano Marekani ukitaka kusajili kampuni unafuata vipengele 1, 2, 3 umemaliza, tena unaweza fanya matandaoni bila tatizo, baada ya muda unaletewa employer identification number (EIN) na IRS bila shida, unaanza kuingiza pesa.

Polisi akikukamata kwa kuendesha kasi anakupa faini (ticket), mwenyewe unakwenda kuilipa mahakamani. Usipofanya hivyo baada ya muda wanakutumia warrant, unaikuta kwenye mail box, usipolipa wanakuja kukugongea au wanakufuata unapofanya kazi. Huo ndio mfumo/utaratibu unaoeleweka. Sasa hebu nia mbie ukitaka kuanzisha kampuni bongo kwamfano utaweza kufanya kwa mlolongo unao eleweka? Si utazungushwa mpaka mwenyewe utoe kitu kidogo.

Unajua Tanzania tuna mifumo mingi mibovu lakini haya ni mambo ya ndani, sasa unapoleta mambo ya uraia wa nchi mbili unazungumzia mambo ya usalama wa Taifa. Kuna uwezekano wa nchi yetu kuingiliwa na wale ambao hawana mapenzi ya kweli na nchi yetu. Sasa hivi haya yanafanyika kama ulivyosema lakini kichini chini tukiruhusu bila ya kuwa na mfumo unaoeleweka itakuwa balaa.

Kwa Watanzania walio nje mimi sioni tatizo mbona wengi wanawekeza TZ bila ya kuwa na uraia wa nchi mbili? Kwa taarifa yako wapo wengi tu waliokataa kuukana uraia wa Tanzania japokuwa wanaweza kufanya hivyo. Mtu anayetaka kuwekeza atawekeza tuu uraia wa nchi mbili siyo kikwazo kwake.
 
Last edited by a moderator:
Jamani hili la raia wa nchi mbili ndio linasubiri katiba mpya au!!!! Nilisoma kwenye magezeti mwaka jana Membe akisema mwaka jana usingeisha sheria ya kuruhusu uraia wa nchi mbili ingekuwa imepitishwa!! Limepotelea wapi?
 
Jamani hili la raia wa nchi mbili ndio linasubiri katiba mpya au!!!! Nilisoma kwenye magezeti mwaka jana Membe akisema mwaka jana usingeisha sheria ya kuruhusu uraia wa nchi mbili ingekuwa imepitishwa!! Limepotelea wapi?

Teh teh teh labda wanasubiri katiba mpya, maana kama kumbukumbu zangu hazichanganya mambo, kuna kipindi walisema uraia hauwezekani bila kubadili katiba.
 
if tanzanians feel like they need a new constitution then they should march and demand it cuz the government/status quo does not want and will never want a new constitution. so it up to the common Tanzanian to demand a new set of laws.
 
Mimi nashangaa watu mnalilia urai wa nchi mbili. Wewe jichukulie uraiwa wa nchi yeyote ile, ukitaka kukumbuka vumbi, panda pipa na pass yako ya nyerere, ukifika kaeapoti kenu ka dar, waonyeshe kijani chenu. Who cares. Ukirudi kwa Obama tumia ya nyumbani kwa obama. Kanchi kenyewe hakana hata ID.
 
Mimi nashangaa watu mnalilia urai wa nchi mbili. Wewe jichukulie uraiwa wa nchi yeyote ile, ukitaka kukumbuka vumbi, panda pipa na pass yako ya nyerere, ukifika kaeapoti kenu ka dar, waonyeshe kijani chenu. Who cares. Ukirudi kwa Obama tumia ya nyumbani kwa obama. Kanchi kenyewe hakana hata ID.
Ulichozungumza hapo juu ni next to impossible.Soma tena ulichobandika utagundua ninachokwambia,yani it dont make no sense.

Unachosema kinawezekana ONLY kama una uraia wa nchi zote mbili,hapo unaweza kuchagua passport ya kuwaonyesha.

I stand to be corrected tho.
 
Ulichozungumza hapo juu ni next to impossible.Soma tena ulichobandika utagundua ninachokwambia,yani it dont make no sense.

Unachosema kinawezekana ONLY kama una uraia wa nchi zote mbili,hapo unaweza kuchagua passport ya kuwaonyesha.

I stand to be corrected tho.

Wewe sio rai wa nchi labda. Ndio maana unasema usemalo. I have both pass.
 
Kwa wale watanzania wanaoishi UK baadhi yao wanaweza kufahamu kwamba tarehe 6 & 7 Mei 2011 kulikuwa na mkutano wa Tanzania Diaspora UK. Mimi sikuweza kuhudhuria Diaspora kwa sababu nilikuwa na udhuru kidogo. Ila napenda kutoa maoni yangu kidogo kwenye hili swala la Dispora na maendeleo ya Tanzania.

Kwanza ningependa kuishauri Serikali chini ya muheshimiwa Rasi Kikwete kwamba huu sio wakati wa siasa na maneno yasioyokuwa na utekelezaji. Nakumbuka (kama kumbukumbu zangu zipo vizuri) rais alishawahi kusema wakati akiwa US miaka ya nyuma kwamba "watanzania walioko nje wanaonea wivu watanzania waliopo Tanzania ndo maana wanataka uraia wa nchi mbili". Samahani kama nitakuwa nimenukuu vibaya ila tafsiri yake ndo hiyo.

Sasa kama Tanzania kweli ipo serious kwa maendeleo yake ni bora ikaruhusu hili swala la uraia wa nchi mbili. Wenzetu Kenya wameshalipitisha hili na katika hii East African Community wao watakuwa wanabenefit zaidi kwa sababu wanayo access kwenye market ya Tanzania and at the same time Wakenya waliopo nje ya nje wanauhuru wa kufanya investment nchini kwao. Jamani viongozi wetu wa Tanzania, tusidharau wananchi walipo nje. Huku nje ya nchi (mfano UK nilipo mimi) hata mfanyakazi wa ndani anapata hela inayomwezesha walau kujenga kajumba ka kawaida bongo na kupangishia na serikali kupata mapato kupitia property tax.

Naishauri serikali iharikishe mchakato wa kuwaruhusu watanzania kuwa na uraia wa nchi mbili au zaidi ili kupata mapato ya wanzania walio nje ya nchi. Kwa sasa inaonekana kama watanzania walio nje ya nchi wana tamaa lakini tuangalie mbeleni hili swala ni kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania na Watanzania kwa ujumla wake. Tuambiane ukweli ni kwamba mwisho wa siku kama mimi naishi nje ya nchi na serikali hairuhusu uraia wa nchi mbili ili kuniwezesha kufanya investment popote Tanzania ninapotaka mwisho wa siku nitakuwa naifikiria familia yangu tu na ndugu zangu waliopo Tanzania.

Lakini tukiangalia kwa mapana watanzania tuliopo nje tunaweza kufnaya investments kwa udogo wake ambazo zitaweza kutoa ajira kwa watanzania wenzetu. WAKUU WA SERIKALI EMBU LIANGALIENZI HIL KWA UPESI JAMANI...Hata kama Serikali itaendelea kuuzuia uraia wa nchi mbili, ukweli ni kwamba Tanzania haina Ajira za kutosha kuwashawishi watanzania waliopo nje kurudi. Alternative itakuwa kwa hao watanzania waliopo nje kujilipua(kuukana uraia wa Tanzania) na kuchukua uraia wa nchi walizopo.

Hivyo basi serikali itafakari hili swala na kulifanyia maamuzi kwa haraka. Poleni kwa kuwachosha kusoma ila ni mtazamo wangu tu kwa maendeleo ya Tanzania.

Jee mnadhani suala la uraia wa nchi zaidi ya moja kwa watanzania liharakishwe?
 
Ni wazo zuri likitekelezwa esp. kama Kenya wamepitisha dual citizenship then raia wao walioko diaspora watakuwa na advantage esp ktk opportunities kwenye EAC.
Ita-make helluva sense endapo Tanzania watakataa kuipitisha dual citizenship na at the same time watoke EAC.
 
everybody

Kwa wale wanaohudhuria diaspora inafikiriwa kua sio mara ya kwanza swala la dual nationality kujadiliwa. Lilijadiliwa mwaka jana na ahadi nyingi zikatolewa lakin halikuweza kua materialised mpaka leo. Ndugu aliezungumza hapo juu inaonekana aliangalia sana upande wa advantage tu kuliko kuangalia disadvantage.

Wale wanaoangalia upande wa disadvantage wasiwasi wao mkubwa uko ktk uslama wa nchi iwapo swala hilo litapitishwa. Moja kati ya wasiwasi uliopo ni majiran kuchukua advantage hiyo na kumiliki ardhi kubwa na uwezekano mdogo wa kuwadhibiti kwa kua watakua na uraia wa nchi mbili. Hali ya siasa ilivyo Tanzania hivi sasa kwa wale wataalam wa politics wanakubali kua Tanzania iko ktk crossroad in terms of political handover.

Hii ina maana mabadiliko ya aina yoyote yanatakiwa yaangalie sana disadvantage kuliko advantage. Nini disadvantage za dual nationality? Tunaomba maelezo kwa wale wataalam
 
Last edited by a moderator:
Mkuu NgomaNgumu, na wale wengine walio na mawazo kama wewe, coin huwa na pande mbili ambazo utaziangalia zote kabla ya kufanya maamuzi. Hapa kama nimemsoma huyo muheshimiwa wa UK, ni wa TZ walio nje ndio wanapoteza zaidi kwa kukosekana hiyo dual citizenship.

Main reason ikiwa kwamba wanafanya kazi na biashara zao kule na kupata mahela mengi tu, lakini wakiwa kama TZ Citizens kule nje wanakosa baadhi ya priviledges kwa vile wanatumia Visa na passport za kigeni. Ili wapate full priviledges lazima wawe na citizenship za pale (nchi wanazoishi). Kwa ajili ya uzalendo wao wanashindwa kuukana U - TZ, jamani wanastahili kusikilizwa.

Kwenye Dis unataja usalama wa nchi, ina maana mtu akiishi nje anakua tishio au sijakusoma vzuri, ni yule yule ambaye anatuma proceeds kwa ndugu na jamaa zake hapa. Wasiwasi wa nchi jirani kwangu naona kama excuse kwa sababu ile ni ya kuwafaidi wa TZ, na kama akiomba mtu mwingine basi kuwepo na sheria zake ambazo zitakuwa ndo ulinzi wetu.

Otherwise hiyo dual citizenship ilikuwa ni ya kuwafaidi wa TZ ambao wanaishi nje na sio wageni wanaoishi TZ, nadhani inatakiwa kuangalia na straight thinking hapa.
 
Last edited by a moderator:
where is the so called Bernad Membe ajibu haya, alikuwa anapenda sana kuzungumzia Diaspora
 
watanzania walioko nje wanabaguliwa kwa sababu ya sheria hii mbovu, huu uwoga wa nini
 
Kwa ninavyojua kulingana na sheria za Tz hili litakuwa gumu sana kukubalika lakini wana JF naomba mnisaidie nitawezaje kupata uraia wa nchi zaidi ya 2? sababu kubwa ya kutaka uraia wa nchi 2 ama 3 ni kuchoshwa na mambo ya Tanzania na uozo wa viongozi wetu.

Sihitaji kurudia wala kuorodhesha uozo huo lakini kila mtu anajua hata mtoto aliyezaliwa last week anajua maana anajua tabu aliyoipata pale Amana, temeke na Mount meru alipokuwa anazaliwa.


Nisaidieni jamani nitafanyaje ama niende tu nikaikane nchi yangu?
 
Fanya mpango ufike AFRIKA KUSINI au Botswana, upate nativity proof hata ya kufoji, then ishia hapo, siku mambo yakinuka unaenda nayo kwenye taifa lako jipya unaclaim uraia... Kwishney!
 
Mi bado naendelea kuishangaa nchi yetu. Leo tunajiandaa kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wetu, lakini viongozi wapenda hela na maisha bora yao na familia zao waliopo madarakani wamesahau kabisa majukumu muhimu ya ustawi wa jamii yote ya kitanzania. Utakuta wanatanua na magari na wanaishi kwa kodi za wavuja jasho, lakini bado hawana lolote la klusaidia wavuja jasho hao. Kwa mfano: swala la vitambulisho vya uraia lilipaswa lifanyikle miaka 20 iliyopita, lakini hadi le hakuna kitu!

Leo wanahangaika na suala la Dowansa na muwekezaji mpya wa uzalishaji umeme wakati tuliwashauri wakati ule kwamaba ni bora tuitaifishe mitambo ya dowans ili izalishe umeme, wakakataa, tukawashauri tena kwamba wainunue kwa gharama kidogo ili itusaidie ukiachilia mbali ushauri wa kufufua mgodi wa makaa ya mawe wa mchuchuma na mingine, miradi ya umeme wa upepo pia ni muhimu kwa maeneo mengi ya nchi yetu nk. Lakini waheshimiwa wanang'ang'ania tu mikataba feki ya aki na SYMBION ili wajipatie mapato binafsi.

Wameua MKUKUTA na kuifanya kuwa MKUKUBI (Mapango wa kukuondoa Umaskini na kukuza Uchumi Binafsi) wa kujinufaisha wao wenyewe tyu na familia zao maana watoto na ndugu zao hawasomi wala hawatibiwi kwenye hospitali na shule za hapa nchini. TUNAELEKEA WAPI?

Sasa le rafiki unang'ang'ania uraia wa nchi mbili, nani atakusikiliza? kama wameanzisaha mashule ya kata wakayatelekeza bila msaada wowote, wameanzisha zahanati, vituo vya afyua na hopitali na kuziacha kama zilivyojengwa, wanaingia mikataba feki kibao, wameanzisha VIJIJI, KATA, TARAFA, WILAYA na MIKOA MIPYA kibao; vyote vinahitajie Fedha, vifaa na uwezeshwaji wa rasilimali watu nk, leo watakubali ombi la uraia wa nchi mbili ili mkimbie?????????????????????????????????????????????

Sijui, labda tuendelee...............................................................................................!
 
Pole pole ndugu yangu. Dwans na shule vinauhusiano gani na suala la uraia wa nchi mbili au na madai ya pension ya watu wa Afrika ya Mashariki? Mazungumzo ya uraia wa Nchi mbili hauzuii kamwe mengine hayo unayoyasema. Tuwe construction and serious. Uraia wa nchi mbili ni kwa yeyote atakayetaka kama wewe hutaki je watoto au ndugu zako na kwa vyovyote hapa si mahala pake. Hapa budget haihusiki.

Ukitaka kuzungumza unachoombwa hapa ni madhara na faida za kufanya hivyo ukiwa unajua na ushahidi wa dhati unao period na kama hujui usiogellee hadi kuzama na kuzamisha wengine wanaokuja kukuokoa.
 
Hivi faida yake nini?
umuhimu wake katika kujenga nchi na wananchi wapenda nchi, wazalendo, hasa ni nini?
najua itasaidia wale wachache ambao hupenda kuwa 'yupo lakini hayupo' yani kule kukiota majani anahamia huku, hivyo commitment yake kwa damu yake ni ya kutilia mashaka.
je watu hawa wanapewa urai aina gani, wataruhusiwa kugombea nafasi za kuchaguliwa?
kuwa wanasiasa?
wataruhusiwa kumiliki ardhi?
kurithi ardhi?
wataruhusiwa/ watatakiwa kuingia jeshini?
 
Haika, suala kuwa lina faida gani kwa nchi ni kwamba chochote kilicho na faida kwa mtanzania mmoja mmoja au wengi ni cha faida kwa nchi ili mradi hakivunji sheria au kuleta madhara kwa nchi husika. Nchi ni watu.

Kila siku tunaambiwa uraia wa nchi mbili unaleta maendeleo nyumbani hata iwe kidogo vipi ni faida kuliko lakini hili haliwaingilii kwa kufikiria kuwa huyu mtu atafaidika, basi nongwa ni hiyo tu. Kuhusu faida kwa wazalendo ni suala lenye hisia ya wivu tu maana nani ana uhakika ni nani mzalendo na mpenda nchi hii kwa dhati maana kama baadhi ya wabunge (ambao ndio mfano mzuri kuliko wa kuitwa wazalendo) uzando wao ni wa mashaka makubwa sana hapa wewe unataka kusema nini.

Kumbuka Tanzania inatoa uraia kwa watu ambao si watanzania na hapa ndipo inafaa kuuliza maswali yanayoulizwa kuhusu ni faida gani au uzalendo kwa nchi yetu na kwangu ni rahisi zaidi kumwamini Mtanzania kuliko huyu. Kila ninaposikiliza wanaopinga suala hili hawasemi madhara gani kuwa na uraia wa nchi mbili bali ni maelezo ya kupotosha tu kwa makusudi na bila kuona mbali ya kwamba sasa hivi hailimuhusu au ndugu yake.

Kama huna shaka Mtanzania kuishi nje kama Mtanzania (raia) kinakuuma nini huyu anapochukua uraia wa huko kitu ambacho nchi nyingi zinafanya na hatusikii madhara yatokanayo. Wa kuuliza maswahi haya zaidi ni huko ambako Mtanzania anataka kuchukua uraia.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom