Katiba haijamzuia Membe kugombea, wala mwanachama ye yote.
Je, anafuata taratibu kikatiba na kikanuni?
Kosa la Membe liko hapa.....👇🏼👇🏼
Kwanza ifahamike Membe ni miongoni mwa Makachero waliopata heshima ya kuwa viongozi ktk taasisi hiyo.
Membe alikuwa Mkuu wa Sekretarieti ya Usalama wa Taifa iliyopo Ikulu ambayo ndiyo hufanya uchambuzi wa taarifa zote kutoka mikoani.
Wakati huo wa enzi za ujana wa akina Membe miaka ya 70 (1970), Vijana walijiunga na idara hiyo ya "TISS" walikuwa wamechunguzwa kwa muda mrefu na kufanyiwa usaili wa kutosha.
Membe amewahi pia kuwa Waziri, na kwa mara ya mwisho alifikia kuomba nafasi ya juu kabisa ktk nchi hii "URAIS" na ktk kuiomba nafasi hiyo alipata heshima ya kuingia "TANO BORA".
Kura hazikutosha, zikatosha za Dk. Magufuli.
Inashangaza sana mtu aliyepitia uongozi mhimu wa Usalama wa taifa na kwamba ktk nafasi ya kisiasa amefikia uwaziri tena mhimu vile vile, halafu ukamsikia ktk tuhuma za kutaka kumhujumu kiongozi aliyepo madarakani!?
Hii inaweza kujidhihirisha ktk mambo na sehemu mbalimbali kama zifuatazo:-
(1): Kutokana na watu wako wa karibu, wanaokuzunguka na hata kukubalika kwa maadui wa kiongozi aliyepo madarakani wanayetaka akwame kwa maslahi yao binafsi.
(2): Kupitia watu unaowashawishi waungane na hujuma hizo kutoa taarifa zako sehemu husika.
(3): Kauli na matendo yako yanayopingana moja kwa moja na kumuunga mkono aliyepo madarakani na ukiwa na maana pia ya kuchochea mawazo yako potoshi kwa watu wengine 'umma'.
(4): Kujiandaa na uchaguzi kabla ya muda uliopangwa kikatiba.
Na nafikiri hiyo huenda ndiyo iliyopelekea kuitwa kwa Membe ktk ofisi na uongozi wa Chama ili akakanushe tuhuma hizo.
Hii ingewahusu pia wanasiasa wengine waliotajwatajwa kutaka kuhujumu, si waliotajwa na musiba tu bali hata kwa taarifa za ndani na nje huko mitaani ambazo hazikutajwa hadharani.
Suala la kumtaka musiba aambatane ktk kwenda kujibu tuhuma za Membe sio hoja ya msingi na haina mashiko.
Kama musiba alichokiongea ni cha uongo, na ni cha kizushi basi wao waliotajwa wapate wasaa mwingine sasa wa kupeleka malalamiko juu ya ya tuhuma alizozitoa musiba ili naye akatoe ushahidi wake.
Hii habari ya kumtaka na mtu ambaye hajaitwa ni kutaka marumbano yasiyo na tija kabisa.
Narudia tena, Membe hajazuiwa kikatiba kuomba nafasi anayoitaka, Shibuda alifanya hivyo pia kipindi cha JK ktk miaka mitano yake ila ni baada ya muda ulipofika.
Muda ukifika na si kufanya mikakati hiyo kabla ya wakati.
Na ni lazima uwe na sababu za msingi za kitaifa kuhusu kwa nini isitumike busara ya kumuacha aliyepo kumaliza miaka kumi, ueleze kwa kina juu ya maslahi ya kufanya hivyo na yalenge taifa na si genge lako na hasira za kushindwa kwako huko nyuma.
Kujiandaa kabla ni kuvunja katiba na kanuni za chama, ni hujuma, uhani na usaliti mkubwa.
Kufanya hivyo ni kumhujumu JPM, ni kwahujumu wanachama na Watanzania kwa kujumla kwani kanuni ziko wazi, sitarajii kwa mtu kama Membe kutuhumiwa au kukutwa na tuhuma kama hizo.
Kinachoshangaza ni aina ya watu wanayemtetea Membe baada ya kuitwa na uongozi au kumuunga mkono kwa kauli zake.
Angalia 1, 2, 3, na 4 jibu unalo huhitaji kwenda shule.