Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Bernard Kamillius Membe alizaliwa Novemba 9 mwaka 1953 mkoani Lindi. Ni mwanasiasa ambaye ni mwanachama wa Chama cha Mapinduzi na alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania kuanzia 2007 hadi 2015. Pia alikuwa Mbunge wa Jimbo la Mtama kuanzia mwaka 2000 hadi 2015.


Membe alisoma Shule ya Msingi Rondo-Chiponda na alijiunga na Shule ya Sekondari, Seminari na Namupa kwa ajili ya mosomo ya O-Level. Masomo yake ya A-Level alosoma katika Seminari ya Itaga (Itaga Seminary High School).


Baada ya kumaliza hapo alijiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambapo alisoma Sayansi ya Siasa (Political Science). Alisoma pia Uhusiano wa Kimataifa (International Relations) kutoka Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani mwaka 1990 hadi 1992.


Member alijiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika utumishi wa mwaka mmoja ambapo alikuwa katika Kambi ya Jeshi ya Oljoro iliyopo jijini Arusha.



Kuanzia mwaka 1978 hadi 1989, Bernard Membe alikuwa mchambuzi wa masuala ya usalama wa taifa katika ofisi ya Rais. Baada ya kumaliza masomo mwaka 1992 nchini Marekani, alipangwa kuwa mshauri katika Ubalozi wa Tanzania uliopo Ottawa nchini Canada ambapo alifanya kazi hadi mwaka 2000.



Mwaka 2000 aligombea Ubunge katika Jimbo la Mtama mkoni Lindi ambapo alichaguliwa mfululizo hadi mwaka 2010. Akiwa Mbunge, Rais Dkt Kikwete alimteua kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Kufuatia mabadiliko ya baraza la mawaziri mwaka 2006, Membe alitolewa wizara hiyo ambapo sasa aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini.



Mwaka 2007 aliteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (sasa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki) baada ya aliyekuwa Waziri, Asha-Rose Migiro kuteuliwa na Umoja wa Mataifa (UN) kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.



Mbali na kuwa waziri na mbunge alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuanzia 2007 ambapo alichaguliwa tena mwaka 2012 katika mkutano mkuu wa 8 wa CCM, Dodoma.



Mwaka 2013 Membe aliwaambia wapigakura wake katika Jimbo la Mtama kuwa asingegombea tena katika uchaguzi wa mwaka 2015, na hivyo kuzua minong’ono miongoni mwa watu wengi kuwa huenda alijipanga kugombea urais.



Moja ya skendo kubwa ambazo ziliikumba nchi Membe akiwa waziri ni skendo la ununuzi wa rada ya ulinzi ya Tanzania toka kwa kampuni ya BAE Systems ya Uingereza. Licha ya kuwepo kwa tuhuma za rushwa katika ununuzi wa rada hiyo, Edward Hosea, aliyekuwa Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mwaka 2012 iliripotiwa kuwa alisema hakuna mtanzania aliyehusika katika skendo hiyo.



Akiwa Waziri wa Mambo ya Nje, aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Utendaji la Umoja wa Afrika kwa mwaka mmoja wakati Tanzania ilipokuwa mwenyekiti wa umoja huo mwaka 2008. Chini ya uongozi wake, uanachama wa Mauritania na Guinea ulisimamishwa kutokana na mapinduzi ya kijeshi yaliyotokea katika nchi hizo mwaka 2008.


Mwaka 2012 Membe aliitahadharisha Malawi kusitisha mara moja utafutaji wa mafuta na gesi katika Ziwa Nyasa (Malawi huliita Ziwa Malawi) hadi hapo mgogoro wa umiliki wa ziwa hilo utakapotatuliwa. Mgogoro huo ulitokana na mabishano ambapo Tanzania inadai mpaka wa nchi hizo umepita katika ya ziwa, huku Malawi ikishikilia kuwa mpaka upo upande wa Tanzania (ziwa lipo Malawi) kwa mujibu wa mkataba wa Heligoland–Zanzibar wa mwaka 1890.



Karibuni kuibuka kwa tetesi kuwa mwanasiasa huyo ana mpango wa kugombea urais mwaka 2020, na hivyo amekuwa akiendesha kampeni za chini chini ndani ya chama. Kufuatia hatua hiyo, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally amemtaka mwanasiasa huyo kufika ofisini kwake, kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.
 
Yani watu wengine wapo siku zao wanaona humu ndio sehemu ya kutupia pedi.

Upuuzi mtu.

Membe for presidency!
 
Hatuna cha kupoteza kwasababu hata saizi hagusidiwi na chochote
 
Inawezekanaje?Binafsi Sijaelewa Kwamba Membe Anaweza Vipi kumkwamisha Mhe Rais Kwa Kuanza Mchakato Wa Kampeni Mapema Kabla Ya 2020.

Naamini Mhe Rais Anapendwa Na Kuaminiwa Na Sisi Wana CCM Wote Pamoja Na Wananchi Kule Kwenye Vyama Vya Upinzani Na Wale Wasiokua Na Vyama Kabisa
 
M
Bashiru ana mihemko, anahisi nafasi yake iko matatani. Unafanya mchezo na mshahara wa milioni 10, nyumba, usafiri ada za watoto, matibabu na mengi kama hayo. Unafikiria anatamani kurudi kwenye miti mingi pale mlimani, pasipo na heshima yoyote? Muache aendelee kulinda maslahi yake binafsi. Ila iko siku atakumbuka kuwa mchezo anaoucheze ni hatari kwake binafsi na hao wanaomtuma.
Mimi naamini hakuna binadamu asiye mbinafsi, Bashiru anaonekana kwa SABABU YA nafasi yake.jichunguze
 
#KaziNaBata
IMG_20181202_214951.jpg
 
Ugomvi ukitokea Kati ya watawala na walioonja utawala si ugonvi wa kuuchekelea, maana kitakachotokea kila mtu atajuta. NI wakati wa kuiweka nchi kwenye MAOMBI si wakati wa USHABIKI. Hapa Ndipo inapohitaji hekima na akili. USHABIKI wenu usituangamize.

Well said but viongozi pia wanapaswa kuweka tofauti Zao pembeni. Si kila jambo linahitaji nguvu kulitatua
 
CCM bila dola na bila Tume hii isiyo huru,hiki kiburi chenu kisingekuwepo na ndio maana mnakwepa swala la katiba mpya.
 
Inawezekanaje?Binafsi Sijaelewa Kwamba Membe Anaweza Vipi kumkwamisha Mhe Rais Kwa Kuanza Mchakato Wa Kampeni Mapema Kabla Ya 2020.

Naamini Mhe Rais Anapendwa Na Kuaminiwa Na Sisi Wana CCM Wote Pamoja Na Wananchi Kule Kwenye Vyama Vya Upinzani Na Wale Wasiokua Na Vyama Kabisa
 
Baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), bashiru Ally kumtaka aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mtama na Waziri wa Mambo ya nchi za nje, Benard Membe kwenda ofisini kwake kujibu tuhuma dhidi yake za kuanza Kampeni za kuwania urais 2020, Mwanasiasa huyo Mkongwe na anayesemekana kuitumikia taasisi nyeti ya Idara ya Usalama wa Taifa ya Tanzania akiwa nje ya nchi aliitikia wito wa Dkt. Bashiru lakini akalalamikia utaratibu uliotumika kumuita huku akimtupia lawama mwanaharakati huru Cipryan Musiba kuwa ndiye aliyezusha madai kuwa anajiandaa na urais 2020.

Hata hazijapita siku mbili tangu KM kumtaka Membe aende ofisini kwake na Membe kuitikia wito, wamejitokeza marafiki zake wa.muda mfupi kurusha picha wakiwa naye na maneno ya hapa na pale kutaka kuuonesha Umma kuwa Membe ndiye na Wako na Membe na kamwe hawatamwangusha. Wanaahidi kula naye bata. Watu hawa ndiyo walewale ambao wamediriki hata kuhujumu jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika kuleta maendeleo, Kupambana na ufisadi na kutetea rasilimali za Taifa. Mbaya kabisa watu hawa wanaweka picha wakiwa na Membe na wazungu ambao uvibaraka wao kwao katika kulihujumu taifa ndiyo kwanza umepamba moto. Wameshindwa hata kuficha hisia zao na kumfichia siri mbobezi wao kama wanavyomuita. Kwanini Watanzania tusiamini alichokisema KM B. Ally? Kwanini Watanzania tusiamini mbobezi wao yuko nyuma ya ukibaraka wao ili wampigie debe kuelekea 2020?

Niwakumbushe akina Zitto, Lema, Jusa, Yeriko Nyerere na weingine ambao leo ndiyo wamjazao upepo mbobezi wao kwamba, 2015 Membe na Lowassa waliingia tano bora kwenye kutafuta ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM lakini kukatwa kwa Membe haikuwa habari ya mjini bali kukatwa kwa Lowassa. Maana yake ni nini? Kama umaarufu wa kisiasa ungekuwa unaonekana na ukapinwa kwa urefu, basi Membe hamfikii Lowassa hata kwenye magoti. Lowassa alikatwa, akahamia Upinzani kwa mbwembwe, akateuliwa kugombea urais akakosa , hadithi ikaishia hapo na maisha yakaendeleo. Leo Lowassa anaonekana msaliti tena kwa Chadema kwa sababu tu ya kutaka angalau aonekane anazungumza na Mkuu wa nchi ikulu. Membe ni nani? Atakatwa, atahamia CHADEMA au ACT, mnajua hatakuwa na. Madhara yoyote kama ilivyotarajiwa kwa Lowassa, angalau Lowassa alifurukuta. Endeleeni kumjaza upepo bila shaka na nyie mmepata pa kupumulia baada ya kukosa hoja za kushindana na Serikai ya awamu ya tano, Serikali ya wanyonge, Serikali ya SGR, serikali ya stieglers Gorge, Serikai ya Madege, Serikali ya elimu bure, Serikali ya Maji kwa kila Mtanzania, Serikali ya Umeme nchi nzima, Serikali ya Barabara za juu na chini, Serikali inayowajali Wamachinga, Serikali ibayowatetea Wakulima wake waoate bei bzuri yq mazao yao, Serikali inayolinda rasilimali za nchi, Serikali inayopinga kwa nguvu zote Ushoga.

Aidha nimtahadharishe Membe. Apime uwezo wake na uwezo wa Lowassa kisiasa. Hawa wanaomjaza upepo leo ndiyo waliouanika ufisadi wa Lowasaa wakamuita kila aina ya jina mara Paka shume, mara Fisadi, mara jizi, ndiyo hao hao 2015 waliosema CCM haina uwezo wa kumkata Lowassa, Akakatwa akahamia. Kwao wakiamini sasa Upinzani unaingia ikulu kupitia yeye. CCM siyo Chama cha Mwenyekiti wa kudumu, CCM siyo chama. Cha Kiongozi wa Chama (Yule mwenyekiti alipoteuliwa kuwa RC basi Kiongozi wa Chama akavaa kofia zote, Chama kimebaki kuwa mali yake ). Lakini hata hivyo tangu lini Zitto, Lema, Yeriko Nyerere, Jusa na Upinzani kwa ujumla wao wakawa marafiki wa Membe? Lini? Labda mwenye kumbukumbu atuje.

CCM ni Taasisi, Lowassa alkatwa, Membe atakatwa na yeyote anayedhani anaweza kuwa juu ya CCM atakatwa tu na atang'ong'wa na hao anaodhani wanampenda kumbe wanatafuta pa kupumulia baada ya kufilisika kisiasa.

Labda tofauti ya hawa watu kwa Membe na Lowassa ni kwamba Lowassa walimtukana kwanza kabla ya kimtumia na sasa wanamuona mzigo, Kwa.Membe wameanza na kumpenda ili baadaye wamtumie na mwisho wake watamtukana na watamalizia na kumuona mzigo. Yote kwa yote hakuna atakayenufaika na kiki hizi, Siyo Membe, siyo Wapinzani wanaomtumia. Ni kama ilivyokuwa kwa Lowassa.

Nawasilisha
Ko unajifanya hujui kama 2015 bao LA mkono ndo liliwabeba?
 
Back
Top Bottom