Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Hahaha hivi unafikili ni kwanini watu wameamua kumuunga mkono Membe?
Je Jiwe hakuna lolote alilolifanya..?
Je watu wameamua kumchoka mapema hivi kwanini?
Ajitathimini tu aone wapi anakosea....?
 
Membe,Lowasa, Makamba J....hakuna tofauti.

Tatizo la Magufuli ni roho mbaya yake tu.
 
Membe again?
The same Membe?????
Daaaah huyu jamaa mpeni jukwaa tupumzike kheeeeeee!!!!!?
 
Utani utani afu mwishowe inakuwa kama kampeni sasa. Na wanaccm wanavyomponda mwanachama mwenzao Utadhani anatokea upinzani, kumbe yumo chama tawala. Hivi akitoa tamko kuwa ni uzushi na fitina yeye anasapoti utawala uliopo na ataendelea kuusapoti mpaka 2025 itakuwaje? Mtaanza kumsifia? Maana wapinzani wao Wataanza tu kucheka sababu si mtu wao na hawana cha kupoteza maana ni mwana ccm na ni sawa akisapoti.
 
Wanaccm tuna kila sababu ya kumtaka member, kama makamanda nao wanatuunga mkono in vizuri ili turudishe umoja wa kitaifa
 
Nyie makamanda nyie, mko desperate sana nyie.

Eti mnamtaka Membe ndo awe rais 2020.

Rais John Pombe Joseph ‘Jiwe’ Magufuli ni bora mara 100 kuliko huyo Membe wenu.

Acheni masikhara bana. Membe ni bomu kabisa. Bomu kushinda hata Magufuli.

Kuna mtu, ni Rutashubanyuma nadhani, aliwahi kusema Membe ana ‘limited brain power’.

Hiyo ni kweli kabisa. Afadhali hata Magu yeye tunajua na yeye mwenyewe anajua kuwa hajui Kiingereza.

Lakini huyo Membe wenu, awe anaongea Kiingereza chake cha pre-school au hata Kiswahili chake, anaboa kupita maelezo halafu ni kama analazimisha aonekane ana akili nyiiiiingi wakati hana lolote.

To hell na huyo Membe wenu.
IMG_20181201_162833.jpg
 
Wanaccm tuna kila sababu ya kumtaka member, kama makamanda nao wanatuunga mkono in vizuri ili turudishe umoja wa kitaifa

Kwendraaaaa kafie, chadrama mcharuko mkubwa wewe
 
Naona watu wanatokwa povu kishen.zi ! Hivi kama JIWE alichaguliwa hata Membe nae anaweza kuchaguliwa pia , haijalishi namna itakavyokuwa Judged ! Nchi hii hamna Rais ambae hajawahi kutu disappoint ! Membe Ana haki zote za kuwa Rais wa nchi hii kama walivyokuwa wengine
 
Membe hafai kabisa kuwa rais, sijui watu wanamtaka ili afanye nini. Magufuri yuko vizuri, akipunguza tu kidogo tabia ya kunyanyasa watu atakuwa super. Magu aache tu tabia ya kuona barabara ni bora kuliko binadamu, haiwezekani mstaafu umpige panga mafao yake halafu barabara ndo uziongezee hela ili zidumu zaidi.
 
Hata mkigongewa wake zenu mtailalamikia Chadema. Pambaneni na hali yenu Bana. Ebo!
 
Kwa heshima na taadhima napenda kuwakilisha mawazo yangu juu ya huu mjadala unaoendelea kati ya wanaotamani membe awe mgombea 2020 na wale wasiotaka kusikia hata kidogo kuhusu wazo hilo.nchi yetu tangu tupate uhuru imetawaliwa na Chama kimoja na Chama hicho kimejiwekea utaratibu wa kuheshimu mazoea ambayo hayapo katika katiba yao lakini imekuwa kama sheria.Jambo la kwanza ni kuhusu dini ya mgombea hakuna katiba yoyote inayozungumzia kuhusu wagombea kupokezana kutokana na dini lakini kama utafuatilia vizuri utagundua kuwa Rais wa kwanza alikuwa mkristo tena mkatoliki,Rais wa awamu ya pili alikuwa mwislam,Rais wa awamu ya tatu alikuwa mkristo tena mkatoliki,Rais wa awamu ya nne alikuwa mwislam,sasa tuna Rais wa awamu ya tano ni mkristo tena mkatoliki,kwa mtiririko huo inaonyesha wazi kuwa kwa utaratibu huo uliojengeka si raisi kuwa na Rais wa awamu inayofuata mkristo.kwa vyovyote vile anatakiwa awe mwislam hapo 2025. Kutokana na hali hiyo ni vigumu sana kwa membe kuwa Rais baada ya Rais wa sasa kumaliza kipindi chake hapo 2025.
Jambo lingine ambalo halipo kwenye katiba ya Chama tawala lakini imekuwa ni mazoea ni kwamba Rais aliyemadarakani amekuwa akipewa nafasi ya kuwa mgombea wa Chama hicho ili kujihakikishia ushindi bila matatizo maana ni vigumu sana kwa Rais aliye madarakani kuondolewa au kushindwa kwa sababu hiyo ni Afadhali awe mgombea kuliko kuwa na mtu mwingine ambaye Chama hakina uhakika kama atashinda kwa sababu hiyo sioni namna ambayo ccm wanaweza kumwacha Magufuli na kumweka membe.ila wakiamua kukiua Chama Chao na kukiondoa madarakani basi wanaweza kufanya jaribio hilo la hatari sana kwao.wengi wa wanaounga mkono wazo la kuwa na membe 2020 ni wapinzani wa ccm ambao wanajua Fika kuwa ccm wakifanya uamuzi huo watakuwa wamejimaliza na kuondoka madarakani.
CCM sio wajinga kiasi cha kuamua kufanya uamuzi wa kijinga unaowaweka katika hatari ya kuondoka madarakani.Lakini vile vile wale wanaompigia debe Membe wamekosea sana maana wamemmaliza membe na napenda kuwahakikishia bila kuficha membe hatakuwa na wala haitatokea kuwa Rais kupitia ccm kwa sababu tayari amejengewa uadui mkubwa na watawala ambao ndio walikuwa na nafasi ya kumjenga.
Kwa sababu hiyo wale wote wanaopiga kelele kuhusu membe wanammaliza kisiasa kimya kimya lakini kwa hakika.
Huko sahihi kabisa, lowasa alianza mapema sana kampeni zake. Ikatokea misuguano na wenye kuamua nani agombee urais. Kilichompata kila mtu anajua,namuona Membe tayari kaanza misuguano na wenye kuamua nani agombee urais.Anasuguana na Bashiru, Je atatoboa?UKWELI MCHUNGU NI MEMBE HATAKUJA KUWA RAIS WA TANZANIA hata siku moja kama ilivyo kwa LOWASA.
 
Wakuu pole na shughuli za kulijenga taifa.

Wikendi hii nilikuwa Bukoba, sasa ikabidi niende sokoni kununua vitu hasa Samaki nilikuwa nimewamisi kweli.

Sasa katika pitapita yangu sokoni, kila mtu alikuwa anamzungumzia Membe, chakushangaza ata watu kama bodaboda nao eti wanajadili siasa, yaani Rwamishenye, Kashai na Hamugembe kote Membe anazunguzwa tena sio kwa mabaya bali watu wanataka agombee uraisi eti wamechoka na JPM.


CCM tuwe wakweli JPM hapendwi kama zamani, watu wanamchukia balaa, sijui kwa nini.

Ukweli mchungu Membe amepata wafuasi wengi sana, apa Bukoba.
images.jpeg
 
Back
Top Bottom