Urembo bandia mimi unanikera

kinachokera ikatokea umeamua kumuudhi Mungu kwa kuvunja amri ya sita...ukavunja amri na mwenye urembo bandia stimu inakukatika kutokana harufu ya uchafu kutoka kichwani
 
huyo nilimuuliza kama hii picha ndo ya kwake, jiiii kaingia mitini.....
Mkuu, Kumradhi ktk hili, Hizi ni hulka za kike na Siku zote baadhi ya wanawake huamini kuwa wanamapungufu fulani, So wanakamilisha kwa Urembo na mapambo kadhaa !! kwa Mtazamo wangu hiyo ni haki yao wajipodoe, wapendeze kadri ya uwezo wao !!

Sasa laajabu mbona Vidume siku hizi huvaaga hereni na mitepesho !! hapo mbona hukemeei ????!! mwaj waukweli mjukuum
 
Last edited by a moderator:
sio hilo tu mkuu,mimi nashangaa kuna threads zangu za maana tu na za manufaa kwa umma nikiziandika tu kama zinamhusu baadhi ya watumishi serikalini au ccm haziwekwi watu wachangie.

ahaa.. Kwa hiyo patakuwa na jambo hapo.... Hawa mod wana lao jambo eti?
 

Nikiri mapungufu hapo mtu wangu. Hawa wanaume wanaotoboa pua na masikio na kuvaa vipuri nao hao lao moja na hawa wenye manywele ya bandia. Kutafuta kujibadili kwa kasi ya namna hiyo ni ugonjwa wa akili ujue.... kwa hiyo si tatizo dogo hili.
 
kaazi kweli wadau wenzangu. tunajikana na kuyakana wenyewe maumbile yetu ya asili, tunajidharau na kujilani wenyewe sababu tunajihisi tunakasoro za kimaumbile, aaaaarghhhh. kweli legacies za ukoloni hazikuishia kwenye nyanja za kiuchumi na kisiasa lakini hata kwenye tamaduni na mila zetu za kiafrika. ulisikia wapi mabo hayo? by the way moja ya legacies za ukoloni kwenye utamaduni kwanza ni kumfanya ajitukane na ajikane yeye mwenyewe na ahisi kwamba ilikuwa ni makosa yeye kuumbwa kwa sura na taswira aliyonayo, na mbili, hatimae psychologically asijiamini na atumie nguvu na mda wake almost wote kujikarabati ili aweze kulandana wale ambao anahisi walipendelewa (Westerners). hatimae ndio hapo adjustments, alterations additions to their natural bodies take place. Huo ndio ukweli wa mambo. Tuendelendelee kujadili hili janga wadau
 
ndo mana wazungu wanatudharau, wacha tu waturushie ndizi
 
yaani mi nna nywele ndefu saana natural but natan hata kuzinyoa. na umri huu cjawahi vaa wigi maishan mwangu huo ndo ushamba wangu nkisema hivyo hadi mashoga zangu hawaamin wanacheka sana

Me nakushauri uzinyoe tu hakuna madhara yoyote na kuna tofauti ya wigi na weaving
 
kinachokera ikatokea umeamua kumuudhi Mungu kwa kuvunja amri ya sita...ukavunja amri na mwenye urembo bandia stimu inakukatika kutokana harufu ya uchafu kutoka kichwani

haswaaa...kumbe we unajua inavokuwa.
 
Mmmh !!! jee ulishawahi ona mdhungu akivaa wigi la nywele za kibantu?!! Labda...

yaani ni kujidharaulisha sana...unakiri dunia nzima ijue wewe si mzuri kabisa. kumbe wakati huo unazalau nywele zako vilevile unakiri una upungufu wa akili. puuuu.....
 
Wacha weee, embu cheki mzungu wa bongo anavokuwa....

 

Waone watu wanaohusika na matatizo ya kisaikolojia watakusaidia...usipuuzie
 
Waone watu wanaohusika na matatizo ya kisaikolojia watakusaidia...usipuuzie

fafanua mkuu. watu huwa wanapeana misaada hapa jf. tatizo langu ni lipi hasa. nipo tayari kujifunza na kujirekebisha. sijasema najua kila kitu.
 
hii mada imenikuna maana mimi ni mfuasi wa urembo halisi na sio wa viwandani. many of the so called divas and superstars ukiondoa makorokoro waliojitwika wanakuwa kama ni mtu mwingine kabisa. sign of low self esteem
 

Nimekuwa nikilichunguza sana hili swala na nimegundua wanawake wanavaa mawigi na kushonea nywele ni kwa sababu hawana nywele ndefu za asili na fahari ya mwanamke ni nywele.Wengi nywele zimeharibiwa na madawa na wengine vipilipili so tuwahurumie na kuwavumilia tu.
Ila raha sana kuchezea nywele za mwanamke hasa zikiwa natural.
 

ndugu yangu we umesema vizuri hapa. labda niseme ukweli hapo kuna raha fulani haielezeki kuhusu kushika nywele za mwanamke. lsipati raha sana kushika vibutu ingawa hivi SI kero. tatizo hizi za kushonea; nazani wanatia gundi alo. kuna siku nilikuwa baa nikakutana na medi mmoja kanyoa kama polisi...kwani nilichelewa. mbona nimemwita tuongee. maskini asijue sababu ilikuwa kule kujikubali kuwa natural. nawapenda sana wanaokubali mungu alivotuumba sisi watu weusi. yaani nawapenda sana. ni kiashiria cha kujiamini, kujikubali na kujiona wewe ni mzuri hivyo hivyo ulivyo. ingawa si vizuri kuwa wazi sana lakini nikupe tu hili kwamba huyu wa kujikubali sana akipewa atapewa kwelikweli nakwambia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…