Asate sana mheshimiwa
Dkt. Gwajima D , sikuwa na nia ya kukukatisha tamaa, lakini Kwa polisi ya Tanzania, wenyeviti wa vijiji, vitongoji na maafisa maendeleo/ustawi Moja ya majukumu yao ni kukusanya rushwa za ndoa za utotoni na wanafunzi.
Mtendaji wa Kijiji au afisa maendeleo mwenye mwaka mmoja kazini Kwa tgs b2 ana ng'ombe 25 na hana mkopo popote, je amezipata wapi na kwao ni masikini?
Mkuu, mie ni mdau wako lakini ukiwapelekea polisi au WEOs wapiga maokoto na danadana kibao.
Kwa sakata hili watavuta muda usahau na upepo utulie Kisha "anatoroka tena".
Vinginevyo piga amshaamsha ya adabu. Atakayekukwamisha umfyeke, kama ni rpc ongea vzr na mama amle kichwa.
NB, kesi za mimba Kwa watoto na wanafunzi huku mitaani sio issue tena, hata ukidakwa uko kifuani Kwa mtoto ukiwa mpooele na "mfuko umetuna" utalala selo siku mbili wakivuta upepo mwanasiasa gani anafuatilia.
Nikipata taarifa za ukatili nitakutaarifu kupitia jf pm