Urinary Tract Infection (UTI): Chanzo, Dalili na Kinga/Tiba yake

Urinary Tract Infection (UTI): Chanzo, Dalili na Kinga/Tiba yake

Kutokana na maumbile, UTI mara nyingi haiwapati akina baba, cha msingi mshirikishe 'mwenzako' nae kwenye hizo tiba, manake unajidunga mwenyewe midawa na yeye unamsahau. Kwa kifupi, hata ulale kwenye pipa la dawa, kama yeye hatibiwi, unaweza kujikuta unaendelea nayo kwa miaka mingi ijayo.....
 
Mkuu madhara ya hii kitu ni makubwa kama ikiendelea kwa muda mrefu. Fanya juu chini upate tiba ya kukuponya na hili liwe na kipaumbele kikubwa toka kwako. Kila la heri.

nakushukuru kwa ushauri wako ila naomba kuuliza kama kuna madhara yoyote yanayo sababishwa na U.T.I
 
Kwanza kabisa nieleze U.T.I ni nini?kwa wale wasio faham U.T.I ni mchafuko wa mkojo
pili nielezee historia ya tatizo langu kwa kifupi tatizo langu limenianza toka 2012 mwezi wa nne sababu kubwa iliyo nipelekea kupata huu ugonjwa nimatumizi ya vyoo vya umma hapa nazungumzia vile vyoo vya kukojolea hasahasa vyo hivyo vinapatikana stendi mahotelini ambavyo vimedizainiwa kwa ajili ya WANAUME TU.
Juhudi nilizo zifanya nipamoja na kwenda hospitali kama mara kadhaa hivi ambapo mara ya kwanza niliandikiwa cipro,mara ya pili nilipewa dox mara ya tatu nilipewa amoxlin,flagly na panado na la nyongeza nimesha tumia hadi mitishamba lakin hali bado sionzur na mwez wakumi mwaka huu nimeenda hospitali nimechomwa pawasef moja nikapewa flagly na dox lakini bado umekuwa ukipona kidogo na kujirudia rudia
hata hivyo kwenye familia yetu hakuna mwanye ugonjwa kama huu
mpaka sasa nipo njia panda wadau naombeni mnisaidie cha kufanya.
mi ni daktari umenichekesha sana inaonekana we ni mjuaji ndo maana hupati msaada mzuri wa matibabu.

Wewe badala ya ueleze dalili ya ungonjwa unatwambia definitions za uti wakati umeikosea.
Kwanza huenda huna uti wewe umekalia kutufurahisha. Pm
 
pole sana mkuu fwta ushauri wa mamndenyi kunywa sana maji kama mwehu
usiogope 2012 -2013 ,kuna tuliosoma pugu tukaumwa fungus 199-2002 yaani nimeingia chuo na fungus namaliza degree nayo inamalizaa kuhakiki mwilini ikaondoka ..so mwaka mmoja usikusumbua tafuta ma dk wazuri wakusaidie na Mungu mtangulize kwanza kwa hili
 
Mkuu madhara ya hii kitu ni makubwa kama ikiendelea kwa muda mrefu. Fanya juu chini upate tiba ya kukuponya na hili liwe na kipaumbele kikubwa toka kwako. Kila la heri.
mkuu mskikiliz jamaa tafuta tiba madhara yake wala ayafai kuongeelea humu adi watoto wanasoma .....usiwaze bado sana ikichukua 3-4yrs kidogo kuna tatizo
 
Kwanza niseme mleta maada ambaye amejipambanua kama mgonjwa ana kitu kisaikolojia tunaita self-consciousness(kujishitukia),coz anajua hadi maana ya ugonjwa husika but ameshindwa kujizuia kupata tena au kupata tiba,kifupi kwa miaka ya hivi karibuni watu wengi sana wamekua na tabia ya kusingizia U.T.I yale magonjwa mengi yanayohusiana na sexual transmitted,ikiwemo gonorea,coz its obvious leo hii ukitaja una ugonjwa wa zinaa ni aibu,tofauti na magonjwa kama U.T.I yana tamkika kirahisi mbele ya jamii,coz watu huamini ni mchafuko wa mkojo,kumbe sometimes unaweza ukawa umevagaa gonjwa la zinaa then unajitibu kisaikolojia kuwani U.T.I,now natoa mchango wangu:Kama walivyoeleza wadau wengine kua ni mchafuko wa mkojo,kwa wanaume sio mara nyingi kuupata lakini tatizo lipo sana kwa wanawake,chooni ni sehemu ambako bakteria hawa wanaweza kupatikana,lakini sio lazima choo ndio iwe source ya mtu kupata hayo maambukizi huko,coz sometimes hata kujaamiana kunaweza kusababisha hatari ya kuwapata bakteria hao toka kwa mtu ambae anao,na mara nyingi wanapatikana kwenye njia ya haja kubwa, so risk kubwa sometimes kwa wale mnaopenda kufanya kinyume na maumbile,cha msingi ni kuimarisha usafi wa choo,ukiwa haja kubwa wakati wa kujisafisha(kutawaza),jisafishe ukitokea mbele kwenda nyuma na sio nyuma kwenda mbele coz bakteria hao wanapatikana sehemu ya haja kubwa sana,na kuepuka ngono zembe,kumbuka wadudu hao wakiwa sugu sana huenea mpaka kwenye figo,so figo inaweza kupata madhara,dalili zake ni kupata haja ndogo mara kwa mara lakini kiasi cha mkojo kinakua kidogo sana,coz wale wadudu wanaathiri sensor za mkojo kwenye kibofu so sensor zinaasume kibofu kimejaa ndio maana mara kwa mara mtu hujisikia kwenda kukojoa,sometimes mkojo huambatana na maumivu ya kuchoma n.k
 
pole sana mkuu fwta ushauri wa mamndenyi kunywa sana maji kama mwehu
usiogope 2012 -2013 ,kuna tuliosoma pugu tukaumwa fungus 199-2002 yaani nimeingia chuo na fungus namaliza degree nayo inamalizaa kuhakiki mwilini ikaondoka ..so mwaka mmoja usikusumbua tafuta ma dk wazuri wakusaidie na Mungu mtangulize kwanza kwa hili

shukran sana mkuu hata hivyo sijakata tamaa
 
choma moto chupi zako zote , ununue mpya. Kila siku vaa chupi tofauti na kufua, usirudie kuvaa siku ya pili. Zisuuze na Dettol.
Nunua chupi za cotton (pamba) siyo za kitambaa cha mpira.
Inaelekea hufui chupi mara kwa mara, Badili tabia, kuwa msafi.
 
choma moto chupi zako zote , ununue mpya. Kila siku vaa chupi tofauti na kufua, usirudie kuvaa siku ya pili. Zisuuze na dettol.
Nunua chupi za cotton (pamba) siyo za kitambaa cha mpira.
Inaelekea hufui chupi mara kwa mara, badili tabia, kuwa msafi.

mkuu moony
ndio maana ameletwa jukwaa la wastaarabu angepeleka kule kwa wahuni ningetajaribu maneno hapo juu
umeanza vizuri lakini umemaliza na usumbufu wa ufahamu.....kivipi..unaweza kuwa msafi ukipita choo kina hilo jidudu hata iweje utalikwaa ...alina tofauti na kale kadubwasha chetu utatumia mpira ikipasuka siku mnarudi uwanjani upya..na hilo ndilo la kusisitiza afue na dettol..umeanza vizuri kumaliza na gundu anyway
jitahidi
mtie moyo yoyote anaekuja kuomba msaadaa humu jamvini...mi nina mtu kanilipia nusu ya ada kutokana na mawazo ya mada za mapenzi simaanishi styles bali makabaliano ya nguvu za ndoa vs nguvu za binadamu ndani ya ndoa zosi days ujazaliwa ahumu ndani..so ujui nani atakusaidia baaddae hata kama si msaada hata kushukuru u will blsd much

kamata upako wangu uushikilie
 
naomba nisaidiwe dalili za UTI ambazo ni common,kama ishu ni vyoo nami natumia sana na sijawahi kuumwa ,hofu yangu isijekuwa ninao sijijui

Maambukizi kwenye njia ya mkojo


Wanawake na wanaume wanaweza kupata maambukizo kwenye njia ya mkojo, lakini zaidi kwa wanawake kwa sababu ni rahisi bakteria kuingia kwenye njia ya mkojo. Dalili za maambukizo ni:

Kutaka kukojoa mara kwa mara
Kusikia maumivu makali wakati wa kukojoa
Mkojo kuchanganyikana na damu.


Maambukizi haya yanaweza kuepukwa kwa kujiweka safi hasa kwa kusafisha eneo la via vya uzazi kila siku na kuhakikisha unanawa baada ya kwenda haja kubwa. Wakati wote unasafisha kutoka mbele kuelekea nyuma. Ukisafisha

kutoka nyuma kwenda mbele unaweza kusambaza bakteria kutoka kwenye haja kubwa kwenda kwenye tundu la

mkojo. Hatua nyingine za kuchukua ili kuepuka maambukizo haya ni kunywa maji mengi; kukojoa mkojo mara kwa mara (usijaribu kubana mkojo kwa muda mrefu) na hasa baada ya ujamiiana, na kuvaa chupi za pamba na nguo pana zinazoweka sehemu za siri kavu.

Iwapo unafikiri unayo maambukizo kwenye mrija wa kupitisha mkojo, kunywa maji mengi na nenda
kamwone mhudumu wa afya kwa ajili ya matibabu. Usijamiiane mpaka dalili zote ziwe zimetoweka.
 
mkuu moony
ndio maana ameletwa jukwaa la wastaarabu angepeleka kule kwa wahuni ningetajaribu maneno hapo juu
umeanza vizuri lakini umemaliza na usumbufu wa ufahamu.....kivipi..unaweza kuwa msafi ukipita choo kina hilo jidudu hata iweje utalikwaa ...alina tofauti na kale kadubwasha chetu utatumia mpira ikipasuka siku mnarudi uwanjani upya..na hilo ndilo la kusisitiza afue na dettol..umeanza vizuri kumaliza na gundu anyway


jitahidi
mtie moyo yoyote anaekuja kuomba msaadaa humu jamvini...mi nina mtu kanilipia nusu ya ada kutokana na mawazo ya mada za mapenzi simaanishi styles bali makabaliano ya nguvu za ndoa vs nguvu za binadamu ndani ya ndoa zosi days ujazaliwa ahumu ndani..so ujui nani atakusaidia baaddae hata kama si msaada hata kushukuru u will blsd much

kamata upako wangu uushikilie


Mi sikuelewi, lakini lazima niseme ukweli; mara nyingi ni uchafu hasa wa chupi especially kama ulikuwa na ugonjwa, ukaoga halafu ukavaa tena nguo chafu. Sina sababu ya kuzunguka zunguka: fua chupi kila siku
 
Kwanza niseme mleta maada ambaye amejipambanua kama mgonjwa ana kitu kisaikolojia tunaita self-consciousness(kujishitukia),coz anajua hadi maana ya ugonjwa husika but ameshindwa kujizuia kupata tena au kupata tiba,kifupi kwa miaka ya hivi karibuni watu wengi sana wamekua na tabia ya kusingizia U.T.I yale magonjwa mengi yanayohusiana na sexual transmitted,ikiwemo gonorea,coz its obvious leo hii ukitaja una ugonjwa wa zinaa ni aibu,tofauti na magonjwa kama U.T.I yana tamkika kirahisi mbele ya jamii,coz watu huamini ni mchafuko wa mkojo,kumbe sometimes unaweza ukawa umevagaa gonjwa la zinaa then unajitibu kisaikolojia kuwani U.T.I,now natoa mchango wangu:Kama walivyoeleza wadau wengine kua ni mchafuko wa mkojo,kwa wanaume sio mara nyingi kuupata lakini tatizo lipo sana kwa wanawake,chooni ni sehemu ambako bakteria hawa wanaweza kupatikana,lakini sio lazima choo ndio iwe source ya mtu kupata hayo maambukizi huko,coz sometimes hata kujaamiana kunaweza kusababisha hatari ya kuwapata bakteria hao toka kwa mtu ambae anao,na mara nyingi wanapatikana kwenye njia ya haja kubwa, so risk kubwa sometimes kwa wale mnaopenda kufanya kinyume na maumbile,cha msingi ni kuimarisha usafi wa choo,ukiwa haja kubwa wakati wa kujisafisha(kutawaza),jisafishe ukitokea mbele kwenda nyuma na sio nyuma kwenda mbele coz bakteria hao wanapatikana sehemu ya haja kubwa sana,na kuepuka ngono zembe,kumbuka wadudu hao wakiwa sugu sana huenea mpaka kwenye figo,so figo inaweza kupata madhara,dalili zake ni kupata haja ndogo mara kwa mara lakini kiasi cha mkojo kinakua kidogo sana,coz wale wadudu wanaathiri sensor za mkojo kwenye kibofu so sensor zinaasume kibofu kimejaa ndio maana mara kwa mara mtu hujisikia kwenda kukojoa,sometimes mkojo huambatana na maumivu ya kuchoma n.k

Mbona hii so na coz imekuwa kama ndio trade mark ya wasomi wa kitanzania?
 
Please see a dr...inaweza kua ugonjwa very serious. UTI ni rare kwa wanaume...na haiambukizi....Are u sure sio gonorrhea? Kama ni gono ndo maana huponi as unakunywa dawa unapona unamrudia binti huyo huyo anakuambukiza and then unasema UTI.
 
Asanteni wataalamu kwa maelezo yenu ya ufafanuzi na maelekezo.
 
Wana jf naombeni msaada kuhusu ugonjwa wa U.T.I,chanzo chake pamoja na dalili zake.
 
UTI ni nini ?

Maambukizi katika sehemu yeyote ya njia ya mkojo husababisha maradhi na matatizo ya aina mbalimbali. Mara nyingi tunapozungumzia UTI, huwa tunalenga maambukizi yanayosababishwa na vimelea
(bakteria) au chochote kile kinachoweza kusababisha UTI huingia katika njia ya mkojo kutokea aidha nje ya mwili au hata ndani ya mwili kwa njia ya damu au vinginevyo.

UTI huweza kumpata mtu yeyote bila kujali jinsia au umri. Hata hivyo, yapo makundi ambayo kutokana na sababu za kibiologia na kinga ya mwili kushuka au kuwa ndogo huathiriwa zaidi na tatizo hilo. Makundi hayo ni pamoja na watoto, wazee na wanawake.

Watoto ni waathirika wakubwa wa UTI na yaweza kusababisha maambukizi kusambaa hadi kwenye damu na mwiili mzima na hatimaye kusababisha kifo. Maumbile ya watoto na utegemezi walio nao wakati wa kujisaidia inaweza kuwa ni sababu hatarishi kwa wao kupata

tatizo hili. Vile vile kinga yao ya mwili bado huwa bado haijakomaa kuweza kuhilili uvamizi wa vijidudu mbalimbali kwenye miili yao.

Wanawake kwa upande wao huathiriwa na UTI hasa kutokana na mfumo mzima wa maungo yao hasa ya mfumo wa mkojo kuwa na urahisi wa kuingiliwa na bacteria. Mathalani, mrija wa mkojo yaani urethra ya mwanamke ni fupi sana ukiliganisha na ya mwanaume na hivyo vijidudu au bakteria kupata urahisi wa kuingia ndani.
Ukubwa wa tatizo

UTI ni tatizo kubwa katika jamii na jinsia. Hata hivyo hakuna data au taarifa kamili juu ya ukubwa wa tatizo hili katika maeneno mengi Duniani hasa katika nchi zinazoendelea zilizo na miundombinu duni na changa ya afya. Utunzaji wa kumbukumbu ni tatizo linachongia pia ukosekanaji wa taarifa.

Kwa kiasi kikubwa tatizo la UTI huathiri wanawake zaidi kuliko wanaume, zaidi ya mara mbili kwa kukadiria. Karibu kila mwanamke katika maisha yake anaweza wa kupata UTI japo mara. Pia uwezekano upo kwa tatizo kujirudia mara kwa mara.

Sababu za UTI


UTI yaweza kusababishwa na vijidudu vya namna nyingi. Mathalani ni vimelea (bakteria) japo pia na jamii nyingine ya vijidudu vinaweza kusababisha UTI. Bakteria aina ya Escherichia coli kwa kiasi kikubwa ndio inayosababisha UTI japo pia bakteria wengine wapo. Vijidudu hivi vyaweza kuingia katika njia ya mkojo kutokea nje ya mwili au hata kwa kupitia damu ya mhusika.


Kwa wanawake, fangasi katika sehemu za siri imekuwa ni tatizo kubwa sana. Uwepo wa fangasi hasa kwenye uke na maeneo jirani pia huweka mazingira ya mvuto kwa bakteria kuvamia maeneo hayo na kuleta maradhi, hasa UTI.

Kwa wanaume mara nyingi kutokana na maumbile yao na mfumo mzima wa mkojo na viungo vyake, huwa siyo waathirika wakubwa wa UTI.

Vihatarishi

Sababu hatarishi
(risk factors) za UTI zipo nyingi, kulingana na umri, jinsia na mazingira ya mhusika. Mfano sababu hatarishi za mtoto mchanga kupata UTI si sawa na mtu mzima jinsia ya kike. Maumbile na mfumo wa kibiologia ya mwanamke humweka katika nafasi hatarishi zaidi ya kupata UTI. Vile vile ngono, tena ya mara kwa mara ni moja ya sababu zinazoweza kuchangia mtu kupata UTI.

Kwa kupitia ngono, bakteria waliopo katika sehemu za siri za mhusika vinaweza kupata nafasi ya kupenya na kuingia katika mfumo wa njia ya mkojo kwa urahisi zaidi.

Sababu nyingine ni upungufu wa kinga mwilini kwa sababu yeyote, ikiwamo ujauzito kwa wanawake na ugonjwa wa kisukari (diabetes). Lakini pia, sababu nyingine kadha wa kadha zinazosababisha upungufu wa kinga mwilini.

Dalili za UTI je?

Dalili za UTI kwa kiasi kikubwa hutokana na umri na jinisia ya mhusika, lakini zaidi kisababishi
(cause) ya UTI. Dalili zinaweza kuwa kusikia maumivu wakati wa kukojoa, homa na maumivu katika viungo vya mkojo, kuhisi kuhitaji kukojoa mara kwa mara na pia mkojo kuwa na hali ya kuunguza wakati wa kukojoa.

Nyingine ni maumivu ya tumbo chini ya kitovu na au mgongo kwa chini. Mkojo wenyewe unaweza onekana wenye damu au usaha.

Kwa watoto dalili pekee kubwa ni homa. Hii inaweza kuambatana na kushindwa kula vizuri, kulia lia sana na hata kutapika.
Matibabu ya UTI

Matibabu ya UTI kwa kiasi kikubwa unapatikana bila shida na usumbufu mkubwa maadam tatizo lijulikane mapema na kwa usahihi. Utaratibu mzima wa matibabu hutegemea majibu ya maabara, kisababisho cha UTI na umri pia wa mhusika


Pamoja na hayo, UTI ni ugonjwa unaozuilika. Kwa ujumla suala zima la kuzingatia kanuni za afya bora hasa ya mwili na mazingira ni suluhisho tosha kwa tatizo la UTI.


Unywaji wa maji mengi ili kupata mkojo mwingi ili pengine uweze kusafisha njia ya mkojo nayo pia inashauriwa. Inashauriwa pia kukojoa mara tu baada ya tendo la kujamiiana. Kwa watoto ni muhimu kuzingatia matumizi sahihi ya pampers hasa kubadilisha kwa wakati
.

Kwa hisani ya MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
DAWA NZURI YA UTI

U.T.I ni ugonjwa sugu

unaosumbua sana watu wengi hivi sasa, wakubwa kwa wadogo. U.T.I
(Urinary tract Infection) ni ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo na huweza kusababisha maumivu makali na unapojiimarisha mwilini kwa muda mrefu huathiri figo pia. Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na mtu kusikia haja ya kukojoa kila wakati na kusisimka wakati wa kujisaidia, kusikia maumivu, kutoa mkojo mchafu na hata kutoa haja ndogo iliyochanganyika na damu.

Wataalamu wetu wa masuala ya tiba wanatueleza kuwa tatizo hili hujitokeza pale mlango wa njia ya haja ndogo inaposhambuliwa na bakteria ambao husambaa na wasipotibiwa mapema huenea hadi kwenye figo na athari zake ni mbaya.

UNAWEZA KUDHIBITI U.T.I KWA TIBA MBADALA

Kwa kawaida kila ungonjwa una tiba mbadala, siyo lazima kwenda hospitali. Unaweza kuudhibiti au kuponya ugonjwa huu kwa kunywa maji ya Uvuguvugu mengi pamoja na juisi ya miwa au juisi ya matikiti maji au juisi itokanayo na matunda halisi, na maji ya Madafu. Iwapo utawahi kabla tatizo halijawa sugu.

Kwa maana nyingine, unaweza kujikinga na ugonjwa huu kwa kuwa na mazoea ya kunywa maji ya kutosha kila siku. Ukinywa maji ya kutosha yatakufanya uende haja ndogo kila mara na kwa njia hiyo wale bakteria watakuwa wakitoka na hatimaye kuisha kabisa. Aidha, njia nyingine ya kuudhibitibi ugonjwa huu ni kunywa maji mengi au kwenda haja ndogo mara baada ya kufanya tendo la ndoa, kitendo hiki husaidia kuwaondoa mapema bakteria wote ulioambukizwa wakati wa kujamiiana na mwenzio.

Katika hali ya kawaida, ugonjwa wa UTI hutoweka ndani ya siku tatu mara baada ya kuanza kutumia tiba asili ya kunywa maji mengi na juisi ya matunda halisi, iwapo ugonjwa utaendelea kuwepo baada ya siku hizo, hiyo itakuwa na maana ugonjwa wako umeshakomaa na hivyo hauwezi kutibika kwa tiba hii ya nyumbani.

Katika hali kama hii, utakuwa huna njia nyingine isipokuwa kwenda hospitalini na kuonana na daktari ambaye atakufanyia uchunguzi na kukupatia dozi sahihi ambayo utatakiwa kuizingatia bila kukosa. Uamuzi huu ni muhimu hasa kama unasikia maumivu makali ambayo yanaweza kuwa yanasababishwa na kuathirika kwa figo. Kwa kawaida tiba ya kidaktari kwa ugonjwa huu huhusisha matumizi ya dawa kali za ‘antibiotics', ambazo watu wengi wanazikimbia kutokana na athari zake za baadae (side effects). Lakini ni muhimu kufuata ushauri wa dokta na kumaliza dozi ili kuepuka uwezekano wa kurejea kwa ugonjwa, tena kwa kasi kubwa.

KUZUIA
Ili kujiepusha na ugonjwa huu, suala la usafi na kuwa na tabia ya kunywa maji ya kutosha ni jambo muhimu sana. Hakikisha unajisafisha vizuri mara baada ya kwenda haja na kubadilisha mara kwa mara nguo yako ya ndani, hasa kwa akina mama.

Vile vile usikae na haja ndogo kwa muda mrefu, nenda kajisaidie mara nyingi kadri unavyosikia kufanya hivyo. Kitu cha mwisho cha kuzingatia kwa mgonjwa wa UTI ni kupunguza unywaji wa pombe na vinywaji vingine vyenye sukari, kwa sababu sukari ni chakula cha bakteria hivyo kwa kuendelea kunywa kinywaji chenye sukari kutaifanya hali kuendelea kuwa mbaya. Ugonjwa huu ni rahisi kuepuka kwa mtu anayependa kunywa maji ya kutosha na kunywa juisi halisi kila siku.

DAYATI MUHIMU KUDHIBITI UTI

Katika kuudhibiti ugonjwa huu, pendelea kula vyakula ama vinywaji vyenye kiwango kikubwa cha vitamini C ambayo utakipata kwenye matunda ya aina mbalimbali yakiwemo machungwa, mboga za majani n.k. Jiepushe na ulaji wa vyakula vya ‘kupaki' kama vile ‘chizi', chokoleti na bidhaa nyingine zilizotengenezwa kutokana na maziwa. Pia jiepushe na ulaji wa vyakula vyenye viungo vingi kama pilau, epuka vyinywaji vyenye ‘caffeine', kilevi na sigara na mwisho achana na vinywaji kama soda na vinavyofanana na soda.
 
shukrani mkuu Horseshoe pamoja sana

Dawa ya Maradhi ya UTI:

Kwa Mtu Mgonjwa wa Maradhi yoyote inatakikana awe anakunywa maji Uvuguvugu anapo Amka Asubuhi

kabla ya kupiga mswaki Unywe Glasi 2 za Maji ya Uvuguvugu na baada ya kupiga Mswaki Unywe glasi 1 na

kabla ya kunywa chai unywe Glasi moja ya maji ya Uvuguvugu kila siku Ufanye hivyo kwa wakati wa

asubuhi.
Na Wakati wa Mchana Dakika 15 au dakika 30 kabla ya kula chakula cha Mchana unywe maji ya Uvuguvugu Glasi 1.

Na Wakati wa chakula cha Usiku unatakiwa unywe Maji ya Uvuguvugu Glasi 2 kabla ya kula chakula cha usiku.


na unywe Maji ya Uvuguvugu Glasi 1 kabla ya kwenda kulala usiku. Jumla utakuwa umekunywa glasi 8 kwa siku huu ndio


utaritibu wa kutibu kila maradhi hapo juu uwe unakunywa kila siku mpaka upone hayo maradhi yako na huenda


ikachukuwa muda wa miezi 3 ukifulululiza kunywa hayo maji ya Uvuguvugu utakuwa umekwisha pona maradhi yako



Unywaji wa maji mengi ili kupata mkojo mwingi ili pengine uweze kusafisha njia ya mkojo nayo pia inashauriwa. Inashauriwa pia kukojoa mara tu baada ya tendo la kujamiiana. Kwa watoto ni muhimu kuzingatia matumizi sahihi ya pampers hasa kubadilisha kwa wakati.

TIBA MBADALA YA MARADHI YA (UTI) PATA MAFUTA YA KHARDALI KUNYWA KIJIKO KIMOJA ASUBUHI KIJIKO KIMOJA MCHANA NA KIJIKO KIMOJA USIKU KWA MUDA WA SIKU 3 AU SİKU 7 KISHA NENDA KAPIME HAYO MARADHI YAKO YA (UTI) UTAKUTA HAKUNA TENA INSHALLAH.

ImageProxy.mvc

MAFUTA YA KHARDALI KWA KIINGEREZA YANAITWA MUSTARD OIL.


Dawa ingine ya kutibu Maradhi ya UTI ni hi hapa kwa jina inaitwa Grape seed extract

ImageProxy.mvc

Mustard oils for UTI treatment

Mustard oils derived from horseradish root and the nasturtium herb can be used as treatment for UTI, according to a 2006 study published in the Arzneimittel-Forschung journal. The study found that a combination of extracts from

horseradish and nasturtium, two plants from the mustard family containing volatile mustard oils as the

active ingredients, demonstrated antimicrobial properties, meaning they kill or inhibit the growth of

microorganisms like bacteria. Researchers stated that the combination of these two supplements is a rational treatment for UTI and upper respiratory infections.

In a similar study published in the
Arzneimittel-Forschung journal that same year, participants took either antibiotics or an herbal drug combining horseradish and nasturtium. The group who took the antibiotics

experienced a 87.9 percent decrease in symptoms versus 81.2 percent in patients who took the herbal drug.

However, researchers found that the herbal drug had a clear advantage because the participants taking the supplement needed fewer supportive procedures and administration of concurrent medication.

Grapeseed extract

Grapeseed extract may also be an effective treatment for UTI and other infections. The supplement promotes activity to fight bacteria that are causes of urinary tract infections .

Grapeseed extract also has antifungal and antiviral properties to treat infections caused by fungi or viruses.
The University of Maryland Medical Center recommends taking 100 milligram capsules or five to 10 drops of liquid grapeseed extract three times a day for treating infections.
 
Back
Top Bottom