Urinary Tract Infection (UTI): Chanzo, Dalili na Kinga/Tiba yake

Urinary Tract Infection (UTI): Chanzo, Dalili na Kinga/Tiba yake

UNAWEZA KUDHIBITI U.T.I MWENYEWE..!

U.T.I ni ugonjwa sugu unaosumbua sana watu wengi hivi sasa, wakubwa kwa wadogo. U.T.I (Urinary tract Infection) ni ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo na huweza kusababisha maumivu makali na unapojiimarisha mwilini kwa muda mrefu

huathiri figo pia. Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na mtu kusikia haja ya kukojoa kila wakati na kusisimka wakati wa kujisaidia, kusikia maumivu, kutoa mkojo mchafu na hata kutoa haja ndogo iliyochanganyika na damu.

Wataalamu wetu wa masuala ya tiba wanatueleza kuwa tatizo hili hujitokeza pale mlango wa njia ya haja ndogo inaposhambuliwa na bakteria ambao husambaa na wasipotibiwa mapema huenea hadi kwenye figo na athari zake ni mbaya.

UNAWEZA KUDHIBITI U.T.I KWA TIBA MBADALA


Kwa kawaida kila ungonjwa una tiba mbadala, siyo lazima kwenda hospitali. Unaweza kuudhibiti au kuponya ugonjwa huu kwa kunywa maji mengi (Ya Uvuguvgu) pamoja na juisi itokanayo na matunda halisi, iwapo utawahi kabla tatizo halijawa sugu.

Kwa maana nyingine, unaweza kujikinga na ugonjwa huu kwa kuwa na mazoea ya kunywa maji
(Ya Uvuguvgu) ya kutosha kila siku. Ukinywa maji (Ya Uvuguvgu)ya kutosha yatakufanya uende haja ndogo kila mara na kwa njia hiyo wale bakteria watakuwa wakitoka

na hatimaye kuisha kabisa. Aidha, njia nyingine ya kuudhibitibi ugonjwa huu ni kunywa maji mengi
(Ya Uvuguvgu) au kwenda haja ndogo mara baada ya kufanya tendo la ndoa, kitendo hiki husaidia kuwaondoa mapema bakteria wote ulioambukizwa wakati wa kujamiiana na mwenzio.

Katika hali ya kawaida, ugonjwa wa UTI hutoweka ndani ya siku tatu mara baada ya kuanza kutumia tiba asili ya kunywa maji mengi
(Ya Uvuguvgu)na juisi ya matunda halisi, iwapo ugonjwa utaendelea kuwepo baada ya siku hizo, hiyo itakuwa na maana ugonjwa wako umeshakomaa na hivyo hauwezi kutibika kwa tiba hii ya nyumbani.

Katika hali kama hii, utakuwa huna njia nyingine isipokuwa kwenda hospitalini na kuonana na daktari ambaye atakufanyia uchunguzi na kukupatia dozi sahihi ambayo utatakiwa kuizingatia bila kukosa. Uamuzi huu ni muhimu hasa

kama unasikia maumivu makali ambayo yanaweza kuwa yanasababishwa na kuathirika kwa figo. Kwa kawaida tiba ya kidaktari kwa ugonjwa huu huhusisha matumizi ya dawa kali za '
antibiotics', ambazo watu wengi wanazikimbia kutokana na athari zake za baadae (side effects). Lakini ni muhimu kufuata ushauri wa dokta na kumaliza dozi ili kuepuka uwezekano wa kurejea kwa ugonjwa, tena kwa kasi kubwa.

KUZUIA
Ili kujiepusha na ugonjwa huu, suala la usafi na kuwa na tabia ya kunywa maji ya kutosha ni jambo muhimu sana. Hakikisha unajisafisha vizuri mara baada ya kwenda haja na kubadilisha mara kwa mara nguo yako ya ndani, hasa kwa akina mama.

Vile vile usikae na haja ndogo kwa muda mrefu, nenda kajisaidie mara nyingi kadri unavyosikia kufanya hivyo. Kitu cha mwisho cha kuzingatia kwa mgonjwa wa UTI ni kupunguza unywaji wa pombe na vinywaji vingine vyenye sukari, kwa sababu sukari ni chakula cha bakteria hivyo kwa kuendelea kunywa kinywaji chenye sukari kutaifanya hali kuendelea kuwa mbaya. Ugonjwa huu ni rahisi kuepuka kwa mtu anayependa kunywa maji ya kutosha na kunywa juisi halisi kila siku.

DAYATI MUHIMU KUDHIBITI UTI

Katika kuudhibiti ugonjwa huu, pendelea kula vyakula ama vinywaji vyenye kiwango kikubwa cha vitamini C ambayo utakipata kwenye matunda ya aina mbalimbali yakiwemo machungwa, mboga za majani n.k. Jiepushe na ulaji wa

vyakula vya ‘kupaki' kama vile ‘chizi', chokoleti na bidhaa nyingine zilizotengenezwa kutokana na maziwa. Pia jiepushe na ulaji wa vyakula vyenye viungo vingi kama pilau, epuka vyinywaji vyenye ‘caffeine', kilevi na sigara na mwisho achana na vinywaji kama soda na vinavyofanana na soda.
 
Achana na sindanao, tafuta duka la dawa unaloliamini nunua dawa inayoitwa AZITHROMYCIN (Capsule USP 500mg). Dose ya uhakika ni vidonge 5 kwa siku 5, kila siku 1.

×
×

dawa unamuambia atumie za nini tena na huku keshachomwa sindano? Sio kwamba ajue inatibika tu, na baada ya wiki mbili akapime tena na dr atamshauri kama haijaisha atumie dawa gani tena?
 
UNAWEZA KUDHIBITI U.T.I MWENYEWE..!

U.T.I ni ugonjwa sugu unaosumbua sana watu wengi hivi sasa, wakubwa kwa wadogo. U.T.I (Urinary tract Infection) ni ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo na huweza kusababisha maumivu makali na unapojiimarisha mwilini kwa muda mrefu

huathiri figo pia. Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na mtu kusikia haja ya kukojoa kila wakati na kusisimka wakati wa kujisaidia, kusikia maumivu, kutoa mkojo mchafu na hata kutoa haja ndogo iliyochanganyika na damu.

Wataalamu wetu wa masuala ya tiba wanatueleza kuwa tatizo hili hujitokeza pale mlango wa njia ya haja ndogo inaposhambuliwa na bakteria ambao husambaa na wasipotibiwa mapema huenea hadi kwenye figo na athari zake ni mbaya.

UNAWEZA KUDHIBITI U.T.I KWA TIBA MBADALA


Kwa kawaida kila ungonjwa una tiba mbadala, siyo lazima kwenda hospitali. Unaweza kuudhibiti au kuponya ugonjwa huu kwa kunywa maji mengi (Ya Uvuguvgu) pamoja na juisi itokanayo na matunda halisi, iwapo utawahi kabla tatizo halijawa sugu.

Kwa maana nyingine, unaweza kujikinga na ugonjwa huu kwa kuwa na mazoea ya kunywa maji
(Ya Uvuguvgu) ya kutosha kila siku. Ukinywa maji (Ya Uvuguvgu)ya kutosha yatakufanya uende haja ndogo kila mara na kwa njia hiyo wale bakteria watakuwa wakitoka

na hatimaye kuisha kabisa. Aidha, njia nyingine ya kuudhibitibi ugonjwa huu ni kunywa maji mengi
(Ya Uvuguvgu) au kwenda haja ndogo mara baada ya kufanya tendo la ndoa, kitendo hiki husaidia kuwaondoa mapema bakteria wote ulioambukizwa wakati wa kujamiiana na mwenzio.

Katika hali ya kawaida, ugonjwa wa UTI hutoweka ndani ya siku tatu mara baada ya kuanza kutumia tiba asili ya kunywa maji mengi
(Ya Uvuguvgu)na juisi ya matunda halisi, iwapo ugonjwa utaendelea kuwepo baada ya siku hizo, hiyo itakuwa na maana ugonjwa wako umeshakomaa na hivyo hauwezi kutibika kwa tiba hii ya nyumbani.

Katika hali kama hii, utakuwa huna njia nyingine isipokuwa kwenda hospitalini na kuonana na daktari ambaye atakufanyia uchunguzi na kukupatia dozi sahihi ambayo utatakiwa kuizingatia bila kukosa. Uamuzi huu ni muhimu hasa

kama unasikia maumivu makali ambayo yanaweza kuwa yanasababishwa na kuathirika kwa figo. Kwa kawaida tiba ya kidaktari kwa ugonjwa huu huhusisha matumizi ya dawa kali za ‘
antibiotics’, ambazo watu wengi wanazikimbia kutokana na athari zake za baadae (side effects). Lakini ni muhimu kufuata ushauri wa dokta na kumaliza dozi ili kuepuka uwezekano wa kurejea kwa ugonjwa, tena kwa kasi kubwa.

KUZUIA
Ili kujiepusha na ugonjwa huu, suala la usafi na kuwa na tabia ya kunywa maji ya kutosha ni jambo muhimu sana. Hakikisha unajisafisha vizuri mara baada ya kwenda haja na kubadilisha mara kwa mara nguo yako ya ndani, hasa kwa akina mama.

Vile vile usikae na haja ndogo kwa muda mrefu, nenda kajisaidie mara nyingi kadri unavyosikia kufanya hivyo. Kitu cha mwisho cha kuzingatia kwa mgonjwa wa UTI ni kupunguza unywaji wa pombe na vinywaji vingine vyenye sukari, kwa sababu sukari ni chakula cha bakteria hivyo kwa kuendelea kunywa kinywaji chenye sukari kutaifanya hali kuendelea kuwa mbaya. Ugonjwa huu ni rahisi kuepuka kwa mtu anayependa kunywa maji ya kutosha na kunywa juisi halisi kila siku.

DAYATI MUHIMU KUDHIBITI UTI

Katika kuudhibiti ugonjwa huu, pendelea kula vyakula ama vinywaji vyenye kiwango kikubwa cha vitamini C ambayo utakipata kwenye matunda ya aina mbalimbali yakiwemo machungwa, mboga za majani n.k. Jiepushe na ulaji wa

vyakula vya ‘kupaki’ kama vile ‘chizi’, chokoleti na bidhaa nyingine zilizotengenezwa kutokana na maziwa. Pia jiepushe na ulaji wa vyakula vyenye viungo vingi kama pilau, epuka vyinywaji vyenye ‘caffeine’, kilevi na sigara na mwisho achana na vinywaji kama soda na vinavyofanana na soda.

ubarikiwe Mkuu,axante sana
 
dawa unamuambia atumie za nini tena na huku keshachomwa sindano? Sio kwamba ajue inatibika tu, na baada ya wiki mbili akapime tena na dr atamshauri kama haijaisha atumie dawa gani tena?

thanx nmekupata ! lol
 
akipata resistance/asipopona atarudi tena hapa. Mwambie aende hospitali kubwa akafanye uchunguzi. Ulishawahi ona uti inatibiwa kwa sindano? Uti inakuwa na maumivu sehemu zote za siri mpaka pumbu? Yawezekana huyo bwana mganga hajamwambia tatizo lake kwa uwazi.

Mkuu sindano za UTI zipo na huwa afadhali sindano kuliko dawa za kunywa mara nyingi dawa inakuwa resistance kwa ugonjwa huu.madaktari wengi hasa hawa wa dispensary hawachunguzi ni sehemu gani ya mfumo wa mkojo imeathiriwa au kuwa chanzo na dawa hizi mara nyingi huitaji combination ya antibiotics.Amikacin na gentamicin ni sindano mojawapo zinazotumika kutibu uti.
 
nae apunguze kuchamba, maambukizi yanapitia njia ya haja kubwa pia

kwa hiyo unamaanisha asiwe anachamba akijisaidia awe anakaa hivyo hivyo usije shangaa ukaenda kupima na ukakutwa nalo maana dalili zake nyingi zinafanana na za magonjwa mengine.Nakushauri tafuta habari kuhusu ugonjwa huu utashangaa mwenyewe.
 
Mkuu sindano za UTI zipo na huwa afadhali sindano kuliko dawa za kunywa mara nyingi dawa inakuwa resistance kwa ugonjwa huu.madaktari wengi hasa hawa wa dispensary hawachunguzi ni sehemu gani ya mfumo wa mkojo imeathiriwa au kuwa chanzo na dawa hizi mara nyingi huitaji combination ya antibiotics.Amikacin na gentamicin ni sindano mojawapo zinazotumika kutibu uti.

nashukuru mkuu bt now npo DISpensari nyingine nimepima tena URINE MAJIBU YAMETOKA NA NMEGUndulika na EP-cells H, sasa sijui imekaaje hii waheshiwa endeleem kunipa MSAADA kuhusu hil ,MUNGU awabariki wote
 
kwa hiyo unamaanisha asiwe anachamba akijisaidia awe anakaa hivyo hivyo usije shangaa ukaenda kupima na ukakutwa nalo maana dalili zake nyingi zinafanana na za magonjwa mengine.Nakushauri tafuta habari kuhusu ugonjwa huu utashangaa mwenyewe.

toilet paper is god given gift use it.
 
jaman wanajamii nlikua napenda kufaham ukifanya tendo la ndoa na mkeo ambaye ametoka kumaliza dozi ya UTI jana..kuna uwezekano wa mwanaume kupata maambukizii??!
 
Hata sijui, ngoja wataalamu waje; ila ni bora ungepeleka JF doctors.
Logically kama hajapona, basi atakuambukiza halafu utakuja kum-reinfect upya.
 
jaman wanajamii nlikua napenda kufaham ukifanya tendo la ndoa na mkeo ambaye ametoka kumaliza dozi ya UTI jana..kuna uwezekano wa mwanaume kupata maambukizii??!

ndugu masakafyuku, mwanamke huwa njia yao ya mkojo ni fupi na ipo karibu na uke na njia ya haja kubwa nyuma yake, mara mke anaponawa kwa kutoka nyuma kuja mbele huleta vijidudu ambavyo ni vya kawaida kwenye haja kubwa ila kwenye njia ya uke na mkojo huleta maabukizi na kusababisha infection, hii ni pamoja na kunawa na makopo ya chooni amabyo wakati mwingine hatujui mtumiaji aliyetangulia alikuwa ana maambukizi ama la, na hivyo kupelekea mwingine kupata maambukizi. Wananwake huonyesha dalili ya kuumwa kama mkojo kuchoma, kutoka uchafu ukeni na tumbo kuuma wakati mwingine, wanaume wengi hawana dalili, hivyo mwanamke anapopata maambukizi anapopewa dawa hushauriwa pia na mumewe atumie dawa kwani huenda kuwa ana maambukizi bila yeye kujua na wanapotumia dawa hawatakiwa kukutana kimwili bila kinga kwa maana ya condom, sasa wewe hapo sijui huyo ni mkeo na alikuwa anatibiwa UTI kama UTI ama alikuwa pia na uchafu unaotoka ukeni kwa maana watu wengine huchanganya na kuita UTI pia.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom