Urusi yafunga Ofisi za DW kulipiza kisasi kwa Ujerumani

Urusi yafunga Ofisi za DW kulipiza kisasi kwa Ujerumani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Urusi imesema leo kuwa itajibu kwa njia sawa kama Ujerumani itaumaliza mzozo kuhusu vyombo vyao vya habari, lakini itauongeza mvutano huo hata zaidi kama Berlin itaamua kufanya hivyo.

Urusi ilisema jana kuwa inazifunga shughuli za shirika la habari la Ujerumani - DW mjini Moscow na kuwapokonya wafanyakazi wake vibali vya kazi katika hatua ya kulipiza kisasi baada ya Berlin kuyafungia matangazo ya televisheni ya Russia Today nchini Ujerumani.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Urusi Maria Zakharova amesema mpira sasa upo katika upande wa Ujerumani.

Mkurugenzi Mkuu wa DW Peter Limbourg ameapa kuwa shirika hilo la utangazaji la umma litaendelea kuripoti kuhusu matukio ya Urusi bila kuzuiwa. Umoja wa Ulaya umelaani uamuzi huo wa Urusi huku msemaji wake wa masuala ya kigeni Peter Stano akisema haukubaliki na hauna uhalali wowote.
 
Russia Today inawatibulia wa magharibi ugali wao........na inapata umaarufu sana kwa sasa kupita vyombo vya hao wamagharibi
Unailinganisha RT na vyombo gani vya wamagharibi?

Kama unailinganisha RT na some local channels za wamagharibi, sawa. Sio the likes of BBC News, Fox News, CNN International, Euronews, Sky News na hata hiyo DW.
 
Unailinganisha RT na vyombo gani vya wamagharibi?

Kama unailinganisha RT na some local channels za wamagharibi, sawa. Sio the likes of BBC News, Fox News, CNN International, Euronews, Sky News na hata hiyo DW.
RT anakula sahani moja na hao wakina CNN hadi kuna baadhi ya watangazaji wa CNN kawavuta na idhaa yake ya kiingereza imeanza kujulikana na watu wengi wa magharibi......wakichoka propaganda za wakina BBC na CNN wanahamia huko kupata ukweli wa mambo
 
Urusi imesema leo kuwa itajibu kwa njia sawa kama Ujerumani itaumaliza mzozo kuhusu vyombo vyao vya habari, lakini itauongeza mvutano huo hata zaidi kama Berlin itaamua kufanya hivyo.

Urusi ilisema jana kuwa inazifunga shughuli za shirika la habari la Ujerumani - DW mjini Moscow na kuwapokonya wafanyakazi wake vibali vya kazi katika hatua ya kulipiza kisasi baada ya Berlin kuyafungia matangazo ya televisheni ya Russia Today nchini Ujerumani.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Urusi Maria Zakharova amesema mpira sasa upo katika upande wa Ujerumani.

Mkurugenzi Mkuu wa DW Peter Limbourg ameapa kuwa shirika hilo la utangazaji la umma litaendelea kuripoti kuhusu matukio ya Urusi bila kuzuiwa. Umoja wa Ulaya umelaani uamuzi huo wa Urusi huku msemaji wake wa masuala ya kigeni Peter Stano akisema haukubaliki na hauna uhalali wowote.
RT inatumika sana na serikali ya Moscow kuendesha propaganda zake za kitaifa huko nje ya nchi yao....hata DW pia hutumika kueneza ushawishi wa Ujerumani huko Ulaya mashariki, Asia na hata Africa...

Tatizo hutokea pale kunapotokea mgongano wa kimaslahi.
 
RT anakula sahani moja na hao wakina CNN hadi kuna baadhi ya watangazaji wa CNN kawavuta na idhaa yake ya kiingereza imeanza kujulikana na watu wengi wa magharibi......wakichoka propaganda za wakina BBC na CNN wanahamia huko kupata ukweli wa mambo
So, unasema "anakula sahani moja", kisha unasema "imeanza kujulikana". Unajichanganya wewe mwenyewe. Wakati RT imeanza kujulikana, hao wengine niliowataja, tayari ni popular na wana coverage kubwa sana duniani.

Watu wanahamia RT ili kupata "ukweli wa mambo"?! Give me a break!
 
So, unasema "anakula sahani moja", kisha unasema "imeanza kujulikana". Unajichanganya wewe mwenyewe. Wakati RT imeanza kujulikana, hao wengine niliowataja, tayari ni popular na wana coverage kubwa sana duniani.

Watu wanahamia RT ili kupata "ukweli wa mambo"?! Give me a break!
Vyote ni vyombo vya propaganda .....mtu asipopenda propaganda za hao mabeberu wenu wa magharibi anahamia upande wa 2 kupata hiohio habari katika mtazamo tofauti.........anakula kwani nimesema alikula? Na mimi nimeongelea sasa hao wamagharibi vyombo vyao vipo muda sana ila kwa sasa wanaanza kutolewa kamasi na wenzao wa upande wa pili kwa propaganda.....uongo ule ule waliokua wanasambaza kipindi hawana upinzani ndo wanapimiwa vilevile na hao wanaoibuka
 
Russia Today ikifungiwa ni sawa ila DW ikifungiwa sio sawa...


Madhalimu wana run hii dunia
Kwa kweli Kuna wazungu hua Ni mataahira Sana.Wanaanza wao kurusha ngumi halafu ukitaka kumrudishia ngumi anakwambia usinipige ngumi usoni nipige za miguuni tu 😄😄😄
 
Kwa kweli Mimi kwny TV za mabeberu hua naiangalia RT sana,hawa BBC, SKY,CNN etc propaganda zao zinanichosha.

Propaganda za warussi hua nazielewa mno.
 
Back
Top Bottom