Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 79
- 1,444
Trump amewawekea vikwazo vya kifedha na Visa kwa maafisa wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC baada ya mahakama hiyo kutoa hati ya kukamatwa kwa viongozi wa juu wa Israel Israel na washirika wengine wa USA.
Mtakumbuka kwamba mwaka jana 2024 mahakama hiyo ya kimataifa ilitoa hati kukamatwa kwa viongozi wa juu wa Israel na Hamas kwa uhalifu dhidi ya binadamu maeneo ya Palestine na Israel katika vita inayoendelea eneo hilo. Kwa tafsiri hiyo ni kwamba USA walitaka hati ya kukamatwa kutoka mahakama ya kimataifa ICC iwalenge viongozi wa Hamas peke yao na Israel iachwe kwa sababu tu ni mshirika wa USA.
Huo ni uwendawazimu, hawa USA si ndio walimuwekea vikwazo mtekaji Albert Bashite A.K.A Makonda RC wa Dar es salaam kwa makosa ya utekaji na kuua watu? Sasa kwanini wao na washirika wao hawataki kuchukuliwa hatua kwa makosa hayohayo? Au wao wana kinga ya kutoshtakiwa kwa makosa ya uhalifu wa kibinadamu kwenye sheria za kimataifa? Ama mahakama ya ICC iliwekwa kwa ajili ya uhalifu wa kivita Africa tu? Kwamba Ulaya na USA ni watakatifu hawastaili kushtakiwa katika mahakama ya ICC?
Mtu & kiongozi yoyote mwenye akili timamu asiye mnafiki wa kutegemea fadhila za Trump atasimama na mahakama ya ICC. Uhalifu ni uhalifu tu unapaswa kupingwa hata kama uhalifu huo unafanywa na askofu au sheikh.
Kwenye hili binafsi nasimama na mahakama ya kimataifa ICC dhidi ya uhalifu wa binadamu unaofanywa na taifa lolote dunia. Vikwazo vya USA kwa mahakama ya ICC haviwezi kuwa kikwazo cha kupinga uhalifu dhidi ya binadamu. Lakini pia USA sio mbinguni wala peponi kwamba ni lazima nifuate baadhi ya misingi hata kama ni ya kijinga ili nifike. USA imepoteza uhalali wa kupinga uhalifu kwa kuwatetea viongozi wa juu wa Israel waliofanya uhalifu wa kibinadamu na Hamas kule Israel na Palestine.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Mtakumbuka kwamba mwaka jana 2024 mahakama hiyo ya kimataifa ilitoa hati kukamatwa kwa viongozi wa juu wa Israel na Hamas kwa uhalifu dhidi ya binadamu maeneo ya Palestine na Israel katika vita inayoendelea eneo hilo. Kwa tafsiri hiyo ni kwamba USA walitaka hati ya kukamatwa kutoka mahakama ya kimataifa ICC iwalenge viongozi wa Hamas peke yao na Israel iachwe kwa sababu tu ni mshirika wa USA.
Huo ni uwendawazimu, hawa USA si ndio walimuwekea vikwazo mtekaji Albert Bashite A.K.A Makonda RC wa Dar es salaam kwa makosa ya utekaji na kuua watu? Sasa kwanini wao na washirika wao hawataki kuchukuliwa hatua kwa makosa hayohayo? Au wao wana kinga ya kutoshtakiwa kwa makosa ya uhalifu wa kibinadamu kwenye sheria za kimataifa? Ama mahakama ya ICC iliwekwa kwa ajili ya uhalifu wa kivita Africa tu? Kwamba Ulaya na USA ni watakatifu hawastaili kushtakiwa katika mahakama ya ICC?
Mtu & kiongozi yoyote mwenye akili timamu asiye mnafiki wa kutegemea fadhila za Trump atasimama na mahakama ya ICC. Uhalifu ni uhalifu tu unapaswa kupingwa hata kama uhalifu huo unafanywa na askofu au sheikh.
Kwenye hili binafsi nasimama na mahakama ya kimataifa ICC dhidi ya uhalifu wa binadamu unaofanywa na taifa lolote dunia. Vikwazo vya USA kwa mahakama ya ICC haviwezi kuwa kikwazo cha kupinga uhalifu dhidi ya binadamu. Lakini pia USA sio mbinguni wala peponi kwamba ni lazima nifuate baadhi ya misingi hata kama ni ya kijinga ili nifike. USA imepoteza uhalali wa kupinga uhalifu kwa kuwatetea viongozi wa juu wa Israel waliofanya uhalifu wa kibinadamu na Hamas kule Israel na Palestine.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.