Huduma za ndege duniani kote huwa ni cheap sana, tulibakia Tanzania na kuonekani ni usafiri wa anasa!
Exactly. Tena nchi nyingi za Ulaya, kusafiri incountry kwa basi ama treni ni expensive kuliko kwa ndege. Sababu moja ni kwamba, kwa njia za ardhini, inakuwa ni zaidi ya safari; inajumuisha na aesthetic values, ambazo unazipata.
Tena hata kwa nchi kwa nchi, kwenye miji iliyo mipaka, usafiri wa ndege ni nafuu sana. Mfano, mtu anakaa Bremen na kufanya shughuli zake Zurich. Kwa ndege ni kama dakika 50 hadi 60+.
Kwa Tanzania, usafiri wa ndege unaonekana ni wa wenye pesa tu.
Serikali ingekuwa makini, ingefanya kinyume na hali ya sasa. Mfano, mtu anayesafiri kwa basi kutoka Dar hadi Iringa-Mbeya kwa basi, analipa si zaidi ya Tsh. 100,000. Na hii ni hata kwa wageni kutoka nchi za nje; hawa watu wanapita Hifafhi ya Taifa ya Mikumi na kuona wanyama kwa bei nafuu kabisa. Licha ya hiyo, wanapita na kuona pia mandhari ya Mlima Udzungwa, kwa bei sawa na bure. Na mandhari nyingi za kupendeza wanamopita barabarani.
Vivyo hivyo kwa wasafiri wa kutoka Arusha kwenda Mugumu via Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Mamlaka ya Uhifadhi ya Ngorongoro. Hawa nao wanapata aesthetic values kwa bei chee kabisa.
Serikali makini ingewekeza katika usafiri wa anga; kisha iweke usafiri wa ardhi (basi na treni) uwe wa luxury, hususani kwa maeneo ambayo aesthetic values zake ni kubwa mno kutolipiwa zaidi.