USAID Boresha Afya Southern Zone, mtalipa lini madai ya community testers?

USAID Boresha Afya Southern Zone, mtalipa lini madai ya community testers?

Status
Not open for further replies.
Namimi nilikuwa nawaza hivi mkuu.
How come jamaa awadai USAID?🤔🤔
Shirika linaitwa USAID Boresha afya mkuu

_20211110_151940.JPG
 
Sio sahihi kuiweka USAID na hayo mashirika uliyoyataja.
USAID is something big.
Ndio mfadhili wa hayo uliyotaja kulingana project husika.
Mkuu tatizo liko wapi? Usaid ni donor tu. Hapa hahusiki moja kwa moja kwenye hii lawama ila title ya shirika ndo iko hivyohivyo na mimi sijapunguza wala kuongeza japo nukta
 
Shida sio hayo mashirika Amref sijui MDH Usaid
Shida Ni wabongo wanaofanya kazi Apo walioshikilia vitengo mbali mbali..! Ni wapigaji balaa unakuta mzungu asha disburse hela zaman sana.
Na mara nyingi huwa hawafanyi kazi yoyote ile bila kuitengea hela.
 
Sio sahihi kuiweka USAID na hayo mashirika uliyoyataja.
USAID is something big.
Ndio mfadhili wa hayo uliyotaja kulingana project husika.
Sawa mkuu wanakuwa wako chin yake ila kweny ulipaji wa hela imekuwa ni changamoto sasa sijui kama USAID ndo anachelewa kutoa ela au hela inatolewa mapema sema labda wabongo wanafanyia kazi kwanza then ndo wanalipa watu maana suala la malipo imekuwa shida kidgo siku hizi
 
Sawa mkuu wanakuwa wako chin yake ila kweny ulipaji wa hela imekuwa ni changamoto sasa sijui kama USAID ndo anachelewa kutoa ela au hela inatolewa mapema sema labda wabongo wanafanyia kazi kwanza then ndo wanalipa watu maana suala la malipo imekuwa shida kidgo siku hizi
Shida itakuwa kwa hao watekelezaji wa mradi.
Ninavyojua mimi Taasisi kama USAID au UKAID hawafanyi fanyi kazi yoyote bila kuwa na enough fund.
Ukiona mradi umetekelezeka jua fungu lake ndilo lilianza kutengwa.

Kinachotokea unakuta shirika linalotekeleza mradi husika ndio wanashindwa kuweka utaratibu wa malipo.

Cash unakuta ipo ila pengine kuna mafyongo fyongo mengine yanayoweza kuchelewesha malipo, wengine mpaka wafanue tathmini au Uhakiki wakikuta safi ndio wanaizinisha malipo.

Nakubaliana na wadau wengine hapo juu kuna mashirika yana udhaifu sana kwenye kutoa pesa waliokwisha kupewa.

Kuna mradi mmoja UKAID ndio waliokuwa wana u fund kupitia Save the Children kama implementer. Duh jamaa walizingua sana!
 
Ni kweli kusema tatizo sio USAID wenyewe huenda tatizo tukawa sisi wabongo tuliopewa nyazifa mbalimbali pale boresha afya, lakini bado Boresha afya wenyewe wanayohaki ya kulaumiwa juu ya uzembe huu. Mfano kwa mkoa wa Ruvuma yapo Mashirika ambayo yanafanya kazi na boresha afya kama NICE na ROA lakini tangu watu wamalize mikataba yao hawajalipwa pesa za nauli na posho mbalimbali wakiwemo Biomedical providers na CBHSP's, labda uzembe huu au upigaji huu umetokea kwenye mashirika haya ya NICE na ROA ila ikumbukwe USAID anafanya kazi na DELOITTE kama consultant wake. Point yangu ni hii, wa kulaumiwa wa kwanza ni USAID BORESHA AFYA SOUTHERN ZONE na partner wake DELOITTE, lakini pia haya mashirika yaliyofanya kazi na USAID pia wakulaumiwa na wanapaswa kuwajibishwa juu ya hili. Tendeni haki lipeni watu stahiki zao, mnawafanyakazi wenye mkataba na wasio na mkataba na wote wana haki ya kulipwa kwasababu walifanya kazi zenu vile mlivyowatuma.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom