USAID haiwezi kufutwa kwa Executive Orders; watetezi kwenda Mahakamani kuzuia uamuzi wa Donald Trump

Hii ni Taasisi inayotumika ku deploy US Spy ,deep state hawawezi kukubali ifutwe Bora Trump afe ila sio USAID
 
China hawana hela za kuchezea kama za Marekani. China awape hela tu mle na mnunue v8 bure bure tu bila sababu, hakuna kitu kama hicho.

Utelezi wa USAID ukikata lazima tunyooke.
Lakin ndo ilikuwa inapanu ukibwa wa usa .. na kutawala dunia kupiti hiyo dollar yake sasa abaki tu na pesa zake tuone
 
Ok fine.

Mjinga kapewa nchi kubwa aongoze.

Haya wewe mwerevu wa huko kijijini kwenu Madongo kuinama umeshawahi hata kupewa uongozi uwe mwenyekiti wa mtaa?
Zaidi ya hapo.

Na hiyo haiondoi ukweli kuwa Trump ni mjinga.
 
Sasa kaa kwa kutulia mjinga awanyooshe ninyi werevu ambao mmeshindwa kuutumia huo werevu wenu hadi mnalilia misaada ya nchi za watu kama vile ni haki yenu.
Of course ni haki yetu maana Amerika wameibia babu zetu na kuwatumikisha kwa karne.

Hiyo misaada ni njia ya kutulipa fidia tunayostahili kwa maovu yao.

Kwetu na kwa babu zetu.
 
Pa

Pale Iringa kuna chuo cha ualimu cha Kleruu. Niliwahi kuambiwa kuwa baadhi ya majengo yalijengwa kwa msaada wa Russia kwa njia ya off-site.
Mbona zinatafutwa kwa tochi, hiyo ilikua kwenye karne gani.
 
Kwani wao hiyo misaada inawahusu nini? Sisi hatuitaki sasa.., hawa jamaa vipi?
 
Trump anachosema sio kufuta USAID bali ni ku review shughuli zake kama zinaendana na sera yake ya America First! Kuna vitu ambavyo utawala wake unaamini shirika linavifanya lakini havina maslahi kwa taifa. Ndo maana anataka ikiwezekana liwe chini ya control ya Federal kuliko kuwa huru kama lilivyo sasa. Naamini review ikiisha kuna miradi itaendelea na mingine itafutwa mazima. Kikubwa hapa ni somo kwamba tuendelee kujipanga namna ya kujitegemea na vya kwetu. Okonkwo anasema "A man brags his own penis however tiny". mdogomdogo Tujipange na vyetu hii misaada iko siku itatuumbua
 
Hao Russia ni matapeli tu hawana msaada wowote wanaotoa tofauti na kuuza silaha.

China yeye ni msanii tu, yeye anachofanya ni kujenga miundombinu feki ambayo ndani ya miaka mitatu imeisha kisha anaendelea kudai pesa yake aliyotumia kukujengea na riba yake ya kufa mtu.

China na mwandani wake Russia hawana lolote na kama hao ndio wa kutegemewa kujaza ombwe inayoachwa na Marekani mbona ni kichekesho na huku wananchi wao wenyewe tu ni choka mbaya.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…