OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Mtendaji mkuu wa Klabu ya Simba (CEO), Senzo Mazingiza amethibitisha kupokea ripoti ya kocha Sven Vanderbroeck kuhusu Usajili wa msimu ujao Katika ripoti hiyo Kocha Sven anataka wachezaji 5 wa nguvu ikiwa wawili wachezaji wa ndani na watatu wachezaji wa nje na kazi ya kutafuta wachezaji hao imeanza mara moja.
Katika ripoti hiyo Kocha Sven amesema kigezo cha umri na uwezo kitumike haswa kuchagua wachezaji hao wachezaji wanaotakiwa ni mabeki watatu ikiwa wawili wa Kati na moja wa kulia, kiungo mkabaji mmoja na mshambuliaji mmoja. Senzo amesema wameanza kubainisha wachezaji hao kabla ya kuwachuja na kufanya Usajili.
Kimsingi nafasi anazohitaji kocha zina matatizo makubwa,ukweli usemwe. Simba SC haina beki wakushiba. Simba SC ina shida ya striker wa kumsaidia Kagere Meddie.
Repoti inasema kocha anataka wachezaji wa nje watatu. Hapa ndio umakini wa kiwango cha lami unahitajika,tusifanye makosa kama tuliyofanya kwa Wabrazili. Kwa maoni yangu hao wageni wawe ni Striker mmoja msaidizi wa Kagere. Beki mmoja wa kati anahitajika sana maana upepo wa Nyoni umekwisha. Pia mgeni mmoja wa kumsaidia Shomari Kapombe.
Katika hizo nafasi 2 za local prayers napendekeza uongozi wa Simba SC wamuulike Lusajo wa Namungo na Nondo Mwamnyeto.
Kuna strikers kadhaa wa kigeni wanatajwa kufanya mazungumzo na Simba SC, mmojawapo akiwa Justin Shonga wa Orlando Pirates. Kama tetesi hizi ni kweli basi itakuwa bonge moja la usajili. Kiukweli Simba sc inahitaji wachezaji wenye speed kama Shonga.
Wapo wachezaji ambao inabidi wapewe mkono wa kwa kheri hata kama ni kwa mkopo. Mmoja wapo ni Beki wa Kati Mbrazili, Haruna Shamte, John Bocco, Saidi Ndemla, Mlipili na Nyoni. Wako baadhi bado ni wazuri ila sioni namna watakavyoweza kupata nafasi ya kucheza.
Haya ni maoni yangu binafsi. Jambo la msingi ni kuwa usajili uliopita Simba Sc iliboronga. Ni matumani tetu msimu mtatumia akili kubwa kwa sababu ya uongozi imara chini ya CEO Senzo.
Katika ripoti hiyo Kocha Sven amesema kigezo cha umri na uwezo kitumike haswa kuchagua wachezaji hao wachezaji wanaotakiwa ni mabeki watatu ikiwa wawili wa Kati na moja wa kulia, kiungo mkabaji mmoja na mshambuliaji mmoja. Senzo amesema wameanza kubainisha wachezaji hao kabla ya kuwachuja na kufanya Usajili.
Kimsingi nafasi anazohitaji kocha zina matatizo makubwa,ukweli usemwe. Simba SC haina beki wakushiba. Simba SC ina shida ya striker wa kumsaidia Kagere Meddie.
Repoti inasema kocha anataka wachezaji wa nje watatu. Hapa ndio umakini wa kiwango cha lami unahitajika,tusifanye makosa kama tuliyofanya kwa Wabrazili. Kwa maoni yangu hao wageni wawe ni Striker mmoja msaidizi wa Kagere. Beki mmoja wa kati anahitajika sana maana upepo wa Nyoni umekwisha. Pia mgeni mmoja wa kumsaidia Shomari Kapombe.
Katika hizo nafasi 2 za local prayers napendekeza uongozi wa Simba SC wamuulike Lusajo wa Namungo na Nondo Mwamnyeto.
Kuna strikers kadhaa wa kigeni wanatajwa kufanya mazungumzo na Simba SC, mmojawapo akiwa Justin Shonga wa Orlando Pirates. Kama tetesi hizi ni kweli basi itakuwa bonge moja la usajili. Kiukweli Simba sc inahitaji wachezaji wenye speed kama Shonga.
Wapo wachezaji ambao inabidi wapewe mkono wa kwa kheri hata kama ni kwa mkopo. Mmoja wapo ni Beki wa Kati Mbrazili, Haruna Shamte, John Bocco, Saidi Ndemla, Mlipili na Nyoni. Wako baadhi bado ni wazuri ila sioni namna watakavyoweza kupata nafasi ya kucheza.
Haya ni maoni yangu binafsi. Jambo la msingi ni kuwa usajili uliopita Simba Sc iliboronga. Ni matumani tetu msimu mtatumia akili kubwa kwa sababu ya uongozi imara chini ya CEO Senzo.