Usajili wa Yanga naona safari hii wamejaza washambuliaji wengi kuliko wakabaji

Ni kweli lakini pia Aziz Andambwile akiaminiwa na kupewa nafasi ana uwezo mkubwa sana kua back up ya Aucho kijana yuko vizuri..
Lakini kwa Azizi Andambwile na Gerson Gwalala, me ningeenda na Gwalala.
 
Aucho,Mkude,Andambwile bila kisahau Mudathir na Max wanauwezo wa kukaba na kushambulia.Bila kusahau Job nae mechi ya Medeama nail Ahly alicheza kiungo mkabaji vizuri tu.

Haya nitajie viungo wakabaji wa 5imba kwa sasa.
Mkude yupo Singida pamoja na Guede.
 
Mkude Singida kaenda lini?
Nimesoma huu uzi uzi nikamkuta Mkude ndani ya Singida.
 
Msimu uliopita
Mechi ya ufunguzi pale Tanga
Simba 4 Yanga 1
Ligi Simba 1 Yanga 2
Ligi Simba 1 Yanga 5

Jumla Yanga 8 Simba 6

Yanga mlizidi goli mbili tu.
Ila mnajitoa ufahamu.
Huwa wanajitoa ufahamu Kama Sasa hivi walivyoanzia raundi ya awali.
 
Na ww ukaziamini tetesi,Singida wametambulisha wachezaji wawili mpaka sasa Guede na Lyanga.

Kwenye kipindi cha usajili tetesi ni kawaida ila husiconclude mpaka uone mchezaji katambulishwa na timu husika.
 
Nadhani Kila nafasi inatakiwa kuwa na Wachezaji wawili wa viwango na bàadhi ya nafasi ndo huwa na wàchezaji 3. Naona Aucho kama first choice, back up yake ni Aziz.
 
Wapiga ngeta mbona wapo kila kona ya Jiji la Dar es Salaam.
 
Msimu uliopita
Mechi ya ufunguzi pale Tanga
Simba 4 Yanga 1
Ligi Simba 1 Yanga 2
Ligi Simba 1 Yanga 5

Jumla Yanga 8 Simba 6

Yanga mlizidi goli mbili tu.
Ila mnajitoa ufahamu.
Wewe utakuwa ni kijana mtiifu wa rage bila shaka! Siyo kwa takwimu hizi! Ile mechi ya ngao ya jamii ilikuwa hivi; Full time Yanga 0 Simba 0 (pen. 1-4).
 
Wamemsajili pia Azizi Andambwile kutoka Singida Fountain Gate kama sijakosea. Ni kiungo mkabaji huyo. Ila hoja yako ina mashiko. Angepatikana kiungo mkabaji mwingine mahiri wa Kimataifa kwa ajili ya kumchallenge Aucho.
Umebadilika sana siku hizi unachambua soccer ndugu zako ukihoji jambo wanakushambulia badala ya kujibu kwa hoja!
 
Aucho,Mkude,Andambwile bila kisahau Mudathir na Max wanauwezo wa kukaba,kutengeneza nafasi na kushambulia.Bila kusahau Job nae mechi ya Medeama nail Ahly alicheza kiungo mkabaji vizuri tu.

Haya nitajie viungo wakabaji wa 5imba kwa sasa.
Hata Pacome pia anajua kukaba timu inaposhambuliwa na kuanzisha mashambulizi kwa haraka timu inapokua ina miliki mpira.

Hivyo sijaona tatizo la yanga kumuongeza Duke Abuya kwakua Abuya anacheza nafasi nyingi uwanjani winga zote mbili,kiungo mkabaji na pia kiungo mshambuliaji.
 
Nimeuliza swali je kwasasa Yanga ina replacement ipi ya Aucho? Maana Mkude kaenda Singida na Mauya hakuwa na kiwango na pia sio sehemu ya kikosi tena. Au ndio tetegemee kuona Sure boy kama back up ya Aucho?
Nani kakwambia mkude kaenda singida? Umempeleka wewe!
 
Wakabaji wapo wengi sana. Au ukiongeza waliokuwepo msimu uliopita bado huoni tu. Wewe kachambue mchezo wa mdako tu, huku hapakufai
 
Hii Yanga ni next level, Eng Hersi ni mtu mbad na hana nia njema na ligi yetu, yaani hataki timu yoyote kupata japo droo mbele ya Yanga.

Mi naona kila idara imejaa, hakuna gepu, Yanga inaweza kuwa timu pekee duniani yenye vikosi vya kwanza viwili na nusu, yaani unatoa 11 unaweka 11 na goli ni zile zile 5 - 0 kama kawa.

Mbumbumbu kazini kwao kuna kazi. Ni ngumu sana kwao kurudia ufalme wao zilipendwa!

Yanga washambuliaji ni moto mkali, viungo moto, mabeki moto na kipa la dunia Diarra limesalia jangwani.

Ili kuitendea haki timu, Yanga iombe friendly match na Madrid au PSG. Hiyo ndio level yetu kwasasa!!

Hersi hafai, ametisha mno. Na tumpe maua yake kwa usajili wa kuua ligi. Yaani Hersi ameleta SMG kuua mbu tu!
 
Nimeuliza swali je kwasasa Yanga ina replacement ipi ya Aucho? Maana Mkude kaenda Singida na Mauya hakuwa na kiwango na pia sio sehemu ya kikosi tena. Au ndio tetegemee kuona Sure boy kama back up ya Aucho?
Mkude yupo Avic Town mzeee..

Eneo la kati kati bado kwa Yanga lina watu...
Azizi andabwile
Aucho
Muda
Abuya (anaweza kucheza hiyo namba)
Mkude

Na Gamondi anaweza akafanya jeuri aka muanzisha Babu kaju eneo hilo😁
 
Nimeuliza swali je kwasasa Yanga ina replacement ipi ya Aucho? Maana Mkude kaenda Singida na Mauya hakuwa na kiwango na pia sio sehemu ya kikosi tena. Au ndio tetegemee kuona Sure boy kama back up ya Aucho?
Yupo aziz adambwile
 
Inakwenda kucheza na timu ya Bundesliga South Africa kwenye Mpumalanga cup.
 
Aucho,Mkude,Andambwile bila kisahau Mudathir na Max wanauwezo wa kukaba,kutengeneza nafasi na kushambulia.Bila kusahau Job nae mechi ya Medeama nail Ahly alicheza kiungo mkabaji vizuri tu.

Haya nitajie viungo wakabaji wa 5imba kwa sasa.
Wewe jitoe ufahamu tu.Simba sc imefanya usajili wa kisayansi msimu huu.

Kiungo Cha ukabaji kuna wanaume wawili wa maana,Agustine Okejepha na Yusuph Kaghoma..Debora atakua juu yao kama Double pivot ila hata chini anaweza kucheza...Msimu uanze tupunguze maneno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…