Usawa utapunguza mauaji ya wenza Afrika

Usawa utapunguza mauaji ya wenza Afrika

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Nimeangalia takwimu za Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji ya wenza duniani, Afrika ina rate kubwa ya mauaji kuliko mabara mengine. Kwanza tujue katika mauaji haya, wanawake ni waathirika wakubwa zaidi kuliko wanaume. Data zinaonesha wanawake wanaouawa ni mara mbili zaidi ya wanaume wanaouawa kwenye mapenzi.

Inmate Killings
Year
Male​
Female​
2010
98​
192​
2011
85​
166​
2012
94​
185​
2013
94​
184​
2014
106​
208​
2015
112​
218​

Aidha rate ya mauaji kwa Afrika ni kubwa zaidi kuliko mabara mengine
Screenshot 2024-05-27 083016.png


Idadi kubwa ya mauaji inayotokea Afrika mimi inanifikirisha kwa namna kadhaa na kuona kuna haja ya kuangalia upya mahusiano ya kiuchumi kati ya mwanamke na mwanaume katika ndoa/mahusiano ya kimapenzi.

Nikiangalia kwenye data naona nchi ambazo zinausawa wa kijinsia mkubwa kwenye mahusiano ni nchi ambazo zina mauaji machache kuliko nchi zinazotaka mwanaume awe kila kitu. Afrika, mwanaume anatoa kila kitu kumtunza mkewe, hali ambayo inamfanya amshushe mwanamke kutoka kuwa mtu hadi kuwa kitu chake. Ni case kama hiyo kwa wanawake ambao huwahudumia wanaume kwa kila kitu hivyo mtu huwa kitu na sio mtu tena. Hali hii inaathiri sana inapotokea kuna tofauti kidogo kwenye mahusiano, hapo ndipo mtu huweza hata kufikia kuua.

Nadhani kwenye mahusiano kunapaswa kuwa na kutegemeana badala ya kutegemea. Nchi za Afrika mwanaume akiwa na mwanamke mwenye hela basi anategemea, mwanamke anaona kumtegemea mwanaume ni jambo la haki yake ya msingi. Na ukishamtegemea mtu lazima ukubali kuwa "Kitu" na sio "mtu" tena. Jambo hili sio jambo linalohitajika lakini ni jambo litakalookoa wengi kutoka kwenye vifo

Mathalani, ukisikia mtu kamsomesha mtu, kamjengea nyumba, kamnunulia gari, waafrika wengi, huwa wanaona ni halali mtu huyo kuuawa kisa amefanya kosa fulani au hataki kuendelea na mahusiano na mtu aliyemfanyia vitu hivyo. Hii justification inaonesha umuhimu wa mtu kuwa bora kiuchumi badala ya kuwa tegemezi, yaani mtu ambaye ana jenga kwa hela yake nk, akipata madhara watu hujiuliza imekuwaje ikiwa haumuhudumii mtu.

Nirudi kwenye mada kuu, mauaji ya wapenzi yanaweza kuzuiwa ikiwa kwanza tuta-define upya mahusiano ya kiuchumi. Usawa usiishie kwenye siasa, bali hadi kwenye ngazi ya familia ili kuhakikisha kwamba watu wanachangia vyema maendeleo ya familia badala ya kudhani kwamba mmoja inabidi atendewe kila kitu.

Natoa hoja
 
Usawa au upendo?Watu waache kuchepuka na wajenge uchumi bora ili kuepusha sonona kwenye familia.
 
Nimeangalia takwimu za Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji ya wenza duniani, Afrika ina rate kubwa ya mauaji kuliko mabara mengine. Kwanza tujue katika mauaji haya, wanawake ni waathirika wakubwa zaidi kuliko wanaume. Data zinaonesha wanawake wanaouawa ni mara mbili zaidi ya wanaume wanaouawa kwenye mapenzi.

Inmate Killings
Year
Male​
Female​
2010
98​
192​
2011
85​
166​
2012
94​
185​
2013
94​
184​
2014
106​
208​
2015
112​
218​

Aidha rate ya mauaji kwa Afrika ni kubwa zaidi kuliko mabara mengine
View attachment 3000348

Idadi kubwa ya mauaji inayotokea Afrika mimi inanifikirisha kwa namna kadhaa na kuona kuna haja ya kuangalia upya mahusiano ya kiuchumi kati ya mwanamke na mwanaume katika ndoa/mahusiano ya kimapenzi.

Nikiangalia kwenye data naona nchi ambazo zinausawa wa kijinsia mkubwa kwenye mahusiano ni nchi ambazo zina mauaji machache kuliko nchi zinazotaka mwanaume awe kila kitu. Afrika, mwanaume anatoa kila kitu kumtunza mkewe, hali ambayo inamfanya amshushe mwanamke kutoka kuwa mtu hadi kuwa kitu chake. Ni case kama hiyo kwa wanawake ambao huwahudumia wanaume kwa kila kitu hivyo mtu huwa kitu na sio mtu tena. Hali hii inaathiri sana inapotokea kuna tofauti kidogo kwenye mahusiano, hapo ndipo mtu huweza hata kufikia kuua.

Nadhani kwenye mahusiano kunapaswa kuwa na kutegemeana badala ya kutegemea. Nchi za Afrika mwanaume akiwa na mwanamke mwenye hela basi anategemea, mwanamke anaona kumtegemea mwanaume ni jambo la haki yake ya msingi. Na ukishamtegemea mtu lazima ukubali kuwa "Kitu" na sio "mtu" tena. Jambo hili sio jambo linalohitajika lakini ni jambo litakalookoa wengi kutoka kwenye vifo

Mathalani, ukisikia mtu kamsomesha mtu, kamjengea nyumba, kamnunulia gari, waafrika wengi, huwa wanaona ni halali mtu huyo kuuawa kisa amefanya kosa fulani au hataki kuendelea na mahusiano na mtu aliyemfanyia vitu hivyo. Hii justification inaonesha umuhimu wa mtu kuwa bora kiuchumi badala ya kuwa tegemezi, yaani mtu ambaye ana jenga kwa hela yake nk, akipata madhara watu hujiuliza imekuwaje ikiwa haumuhudumii mtu.

Nirudi kwenye mada kuu, mauaji ya wapenzi yanaweza kuzuiwa ikiwa kwanza tuta-define upya mahusiano ya kiuchumi. Usawa usiishie kwenye siasa, bali hadi kwenye ngazi ya familia ili kuhakikisha kwamba watu wanachangia vyema maendeleo ya familia badala ya kudhani kwamba mmoja inabidi atendewe kila kitu.

Natoa hoja
hakuna kitu kinachoitwa usawa wa kijinsia. huo ni ushetani, tuukimbie
kila mtu achukue nafasi yake katika mahusiano
 
Usawa wa kijinsia ndicho chanzo kikubwa cha migogoro ndani ya mahusiano ya kisasa kitu ambacho miaka ya nyuma hakikuwapo.

Huko unaposema magharibi walipita hatua hii ya mauwaji na baada ya kuweka sheria kali kuwabana wanaume imeleta madhara makubwa sana kushinda hata mauwaji na kwasasa jamii za magharibi zinadhoofu na kuharibika.

Wewe haujiulizi ushoga, low birth rate, talaka kuwa juu, wanawake wasio na uelekeo, wanaume wasiooa kabisa hadi umri wa miaka 50 kwenda juu, kiwango kikubwa cha magonjwa ya akili especially wanawake, matumizi ya dawa za kulevya, ongezeko kubwa la immigrants ambao wanakwenda kureplace work force inayopungua kwa kasi kutokana na kupungua kwa idadi ya wazawa, ongezeko kubwa na violence kwenye jamii especially mauwaji, hayo yote ni matokeo ya moja kwa moja ambayo kitaalam unaweza ya link na 50/50 na ushahidi upo wa kitaalam.

The only way dunia inakuwa sehemu salama ya kuishi ni kama kutakuwa na familia bora maana raia bora hutokea kwenye familia bora na hivyo basi kama utaanza kumuaminisha mwanamke kuwa yeye na mwanaume ni sawa kwenye kila eneo ndipo pale mwanamke anapoanza kubehave kama mwanaume na kuleta migogoro isiyo ya lazima na mume wake na hatimae mauwaji hutokea kama hatua ya kwanza ya kushindwana kuishi pamoja kati ya wanaume traditional na wanawake wanaoishi kisasa kwa kufuata mitazamo, fikra na lifestyle za wanawake wenzao wa kimagharibi.

Tujikite kwenye kusimamia kila jinsia ikae kwenye majukumu na wajibu wake wa asili. Hiyo 50/50 hakuna sehemu imeshawahi kuwa na faida au kuleta matokeo chanya.
 
Back
Top Bottom