kwanza kwa maelezo uliyogusa kuhusu yesu na eliya uko mbali sana na ukweli. Na ulipomalizia kwa kusema nitakumbuka nikifa, kwanza nianze kwa kupinga hilo kutoka katika biblia ambayo hata wewe umejaribu kuitumia kama muongozo, soma mhubiri 9:5-6 uone biblia inavyozungumzia kuhusu wafu. Pia hata mimi sina kumbukumbu kama nilipozaliwa ilikuwa mara yangu ya kwanza au nilishawahi kuzaliwa hapo kabla na nikafa. Au jiulize mwenyewe, je ulishawahi kuishi kabla? Na kama bado, je unataka kusema watu waliokuwepo kipindi hicho hawakuwa wametosha mpaka kuwe na ulazima wa wengine kuzaliwa? Ilihali kwa maelezo yako, ingewezekana hao hao wa zamani, ndio wangekuwa wanazaliwa, wanakufa kisha wanazaliwa tena.