Pre GE2025 Ushauri: Abdul aende mahakamani kumshtaki Lissu ili kujisafisha na tuhuma za RUSHWA zinazoelekezwa kwake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam, Shalom!!

TUNDU Antipas Lissu amekuwa akirudia sana kuwa mtu aitwaye Abdul,amewahi kumfuata na kutaka kumhonga na kushindwa kutimiza Nia hiyo Kwa Lissu.

Lissu amekuwa akirudia mara Kwa mara jambo hili, Jana tena amesema akihojiwa na Ndugu Odemba Star tv.

Sasa ni muhimu Ndugu Abdul aende court kupitia wanasheria wake Ili kujisafisha na tuhuma hizi kubwa dhidi yake.

NB: Ukimya nao ni jibu.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Amen

Pia soma:Kuelekea 2025 - Tundu Lissu: Abdul (mtoto wa Rais Samia) alitaka tukutane kwenye hoteli moja Masaki anihonge, nikamwambia njoo kwangu
 
Duuh
 
Kama hajipendi aende huko ila navyojua ni ktego kwake na mama kisheria lisu yupo vizur na mahakama inaogopa hilo pia
 
Mkapa alipokua Rais haya mambo hayakuepo hata Magufuli hakuruhusu wanae wasogelee Urais wake.
Huyu kijana anasemwa sana kwa mambo mengi ambayo yanakua na taswira si nzuri kwa mama yake ni jukumu la Mama yake kumuambia kijana wake atulie amuachie afanye kazi zake.
 
Na Lissu anachotaka kitokee
 
Sidhani kama ni rahisi maana Lissu ni mwanasheria nguli hawezi kusema kitu asichokuwa na uhakika nacho na inawezekana amesema hivyo aone kama atabisha ili aweke ushahidi zaidi.
 

Lissu alijibu kimtego lile swali la nyumbani kwako kuna camera? Akasema hakuna πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€
 
Mahakama anayo mfukoni mwake haki itatendeka?
 
Kwa Lisu, sheria siyo taaluma pekee bali ni sehemu ya ubongo wake. Kama Abdul anataka kuumbuka athubutu kukanyaga mahakamani.
Anaweza kuzitumia mahakama kumsafisha Kwa kudai fidia kama Ile ya Manji dhidi ya Mengi!!
 
Unauhakika? What if alirekodiwa au camera zilimnasa walipo kutana? Atakataa

Punguza mihemko kaka, bongo politics ni kitu kingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…