Ushauri: Engine ya gari inatetemeka na kuunguruma sana

ulaji wa mafuta utaludi palepale usipoangalia, maan hiyo utakayoweka utaipa mzigo mkubwa, so nayo itahitaji wese la kutosha,,
 
Kwenye matumizi ya mafuta tazama injection yake Wenda imejaaa uchafu inashindwa kufunga na kufungua kuruhusu ewa inayoitajika kwenda kwenye engine pia nozel zake umezisafisha kipindi gani oil unatumia original au za kuungaunga vyote vinaweza kusababisha gari kura mafuta kama ccm wanavyokura taifa retu
 
hahaha, CCM TENA. NOZZLE NIMESAFISHA TWO MONTHS AGO, JINJECTION KWA KWELI SIJACHEKI, OIL HUWA NA WEKA YA BP ORIJINO,
 

unajua madhara ya kufunga engine ya 1NZ kwenye Rav 4?

nikufungue tu macho

Drivetain ya gari yako ni AWD while hiyo 1NZ inatumika kwenye gari za FWD

pili mjapani hakuwa mjinga kuweka engine ya 1.8 ltr to 2.0 ltr kwenye rav 4 alafu ww ufanye swap ya 1.3 ltr engine ni sawa mbilikimo ambebe hasheem thabit

na hata ukifanikiwa itakuwa kwa gharama kubwa sana na utapoteza 4×4 kitu ambacho kwenye rav 4 hata mlima wa changarawe utakuwa unapanda kwa kuslip

turudi kwenye hilo tatizo embu kacheki engine mountin za ndan na nje nina uhakika zitakuwa zimeisha au nenda kwa fundi kwa ushauri zaidi

ila sikushauri eti ufunge 1NZ kwenye rav 4 kama kutakuwa na ulazima wa kufunga engine mpya hizi ni engine za rav 4

for old model
2.0 L 3S-FE I4 (gasoline)
2.0 L 3S-GE I4 (gasolin

for kili time
1.8 L 1ZZ-FE I4 ( gasoline )
2.0 L 1AZ-FE I4 ( gasoline )
2.0 L 1CD-FTV I4 ( diesel)

ukipata hii diesel itakuwa magoli sana sema ni hadimu sana kupatikana
 
ahsante mkuu kwa maelekezo mazuri, hebu naomba pia nifafanulie kdogo kuhusu hili la kwenda kupima engine kwenye computer kujua matatizo yote ili ikibidi nifanye ili kuweka injini iliyopo iwe kwenye hali nzuri niendelee kuitumia pasipo kuingia gharama kubwa ya mafuta kila siku
 
hahaha, CCM TENA. NOZZLE NIMESAFISHA TWO MONTHS AGO, JINJECTION KWA KWELI SIJACHEKI, OIL HUWA NA WEKA YA BP ORIJINO,
Nunua piki piki nzuri mkuu iwe inakupeleka kazini afu gari tengeneza taratibu usiuze, tumia kipindi cha mvua, hayo makorongo ndo yamekuharibia gari lako ulipendalo.
 

hyo process inaitwa computer diagnosis kwenye gari yako hapo kuna cable ya diagnosis na pia gari yako ina kitu kinaitwa Engine Control Unit (ECU) ndicho kitakachotoa majibu ikipimwa kwenye computer

(ECU) hii ni computer ya gari inahifadhi data zote za gari na ndiyo inaendesha mifumo yote ya umeme katika engine ya gari lako

nenda GEREJI KUBWA uwaambie umeenda kufanya diagnosis

wakishafanya hiyo ECU itaonyesha matatizo yote ya kimfumo yaliyopo kwenye gari lako mkuu
 
Duh, safi sana ,nashukuru sana mkuu. natumiaga tu gari bbila kuwa na utaalamu wowote, ngoja nitaulizia wanakofanya na abaut cost kama nta mudu,ila nashukuru,umenipa pa kuanzia
 
Ahsante, gari yangu ni kili time, ngoja nimtafute fundi mzuri tuifanyie service ya maana labda itaweza cutulia. Pia naomba kufahamu, hamnaga namna ya kufanya kupunguza consuption ya gari hata ikiwa na CC kubwa?
 
Injini inatetemeka unapowasha gari au? Embu jaribu kucheki mounting, hasa ile iliyo chini ya engine inawezekana imekatika.
Ni kweli inaonyesha tatizo ni hio mounting,ila tatizo linakuja jingine hapo itakubidi ubadilishe mounting zote kwa kuwa utakayoweka itakuwa na attetion sana tofauti na zitakazobaki, inshort badilisha zote.
 
Ahsante kwa ushauri mkuu, Ni kweli injini yangu ndo D-4 1998 na gari bado naipenda maana nakaa vijijini sana so sitaweza kutumia gari za chini, SO HILI WAZO LA KUWEKA VVTI YA CC 1,290 LINGEFAA INGEKUWA POA SANA.
D-4 kimeo kitakatifu. Toa hiyo, weka engine ya kluger vvti. Au weka kavu ya rav4 old model. Kwenye kunguruma na kubwia mafuta ndio mwanzo tu....utapiga rngine chini mpaka ushangae. Zina oil filter moja ya kijinga ndani kwenye engine...kenge kwelikweli.
 
Ahsante, gari yangu ni kili time, ngoja nimtafute fundi mzuri tuifanyie service ya maana labda itaweza cutulia. Pia naomba kufahamu, hamnaga namna ya kufanya kupunguza consuption ya gari hata ikiwa na CC kubwa?

kwa uzoefu wangu kwa magari ya kisasa hakuna hiyo njia na hata ikiwepo itakuwa ni mwanzo wa kuuwa engine

hiyo michezo ilikuwaga kwenye magari ya kizamani enzi zile engine zenye caburator lakini sio kwa hizi engine za kisasa zilizojaa sensor kwenye kila eneo

lakin mkuu siumesema gari yako ni Kili time kama ni engine mpya weka hiyo 1ZZ-FE vvti ni 1.8 ulaji wake ni economical kabisa mkuu
 
Hahahah aisee[emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Kwanza endapo engine ina nguruma kwa sauti kubwa yaweza ikawa selesa iko juu sana jaribu kufuatilia mfumo wake
lingine kubadilisha mfumo wa engine kuweka ndogo aiwezi kuhimili bodi ya gari yako pili aito ingiliana pia ita kupa garama kubwa sana kubadilisha mfumo wake kurudisha mwingine tuseme bodi itakuwa kubwa
cha msingi kama ina kula mafuta uza ununue yenye capacity ndogo ambayo uta imili garama zake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…