Ushauri jamani: Nanyanyasika ukweni, eti nimemchezea muda mrefu

Ushauri jamani: Nanyanyasika ukweni, eti nimemchezea muda mrefu

Eti ulikuwa unaogopa mkiachana mtagawana mali wakati yeye ni mama wa nyumbani. SELFISHNESS inakukula. Mtu mmezaa, tena unampenda halfu ujifanya kuishi mguu ndani mguu nje. ukomeee
Walikuwa wanamdanganya kwao, kuna wazazi anamwambia kabisa mwanaye oa mwanamke mwenye kazi ili mwanamke awe anajisaidia mwenyewe hata kama ni kwao,. PhD ya ubinafsi, utazani hao watoto waliwabeba wote tumboni, sasa aoe mwenye kazi yake ili wasaidiane kulea watoto.
 
#KATIKA WANAUME WASIOJITAMBUA WW UTAKUA KIONGOZI WAO_MIAKA 39 HUNA HATA AKILI ZAKUJIONGEZA
 
Wewe jamaa sijui nikutakane,

Anyway si ameshaondoka.......nenda kachukue mahari yako uile na watoto

Tafuta mfanyakazi wa ndani ambaye alishawahi kufanya kazi za ndani na anajua kulea watoto muajiri mlipe 200k kwa mwezi

Mnunulie na mashine ya kufuria afu usiwe mnoko mnoko mlipie king'amuzi ili asiwe mzururaji mjari kama mdogo wako mlozaliwa Mama na Baba mmoja

Miaka 39 bado kijana kabisa, jipende, nenda Barbershop fanya scrub ya mvuke utoe mwonekano wa kizee zee, kula matunda kwa wingi kunywa na maji mengi ili kuboresha afya yako

Kwa sasa huhitaji mwanamke wa kukuumiza kichwa kwa sasa unahitaji kutafuta pesa hakikisha wanao wanainjoi, wewe kula goodtime maisha yaendelee

Lea wanao vizuri hakikisha afya yao ina imarika maradufu wakatie na Bima ya Afya kabisa kama hawana

Huyo shukuru kaondoka kuliko angekuwepo angekuua kabisa na wala usimng'ang'anie achana nae

Mimi nna miaka 38 mpaka mwisho wa mwaka natimiza 39, nna mke na watoto wanne watatu nilizaa na mtalaka wangu, mwaka juzi nikaoa mtoto mbichi tena bikra kabisa nilioa akiwa na miaka 24 huku mimi nikiwa na 37

Na mpaka sasa nimezaa naye mtoto mmoja, na mwenyewe anajua kabisa sitaki ubabaishaji akichoka ndoa aseme kila mtu aishi kivyake
 
Hakuna kitu kibaya kama kujiona una control halafu upigwe tukio la ghafla. Unaweza kuchanganyikiwa

Hata hivyo mkuu Kama ni kweli, wengine hatuna cha kukushauri maana hatujaona tatizo. Mali uliyotaka kuilinda bado unayo pamoja na watoto, mwanamke kaenda kule anapoona anathaminiwa. Move on tu mkuu
Naunga mkono hoja.

Sister hood , mother hood, bongo hood and all of the hoods are proud of this woman.
 
Ukishatoa mahari na wazazi wakapokea ni ndoa hiyo, wanasemaje umemchezea na mahar umetoa?

Kama ameondoka muache, mbona amekutengenezea faida na mtaji wako umerudishiwa, yaani amekupa watoto na mahari umerudishiwa kubali yaishe hilo amelichuma na wazazi wake atalinywa. Kuwa mpole lea watoto wako
 
mimi ni mbabaz wa miaka 39, sijaoa lakini naishi na mwanamke ambaye naweza kusema kuwa ni kama mke wangu kwani nilishamtolea mahari, tumeishi pamoja kwa miaka kumi bila ndoa, sikuona umuhimu wa kufunga naye ndoa kwani yeye ni mama wa nyumbani, nilijua kama nikifunga naye ndoa ikatokea tunatengana basi tunaweza kugawana mali hivyo nikawa nafanya mambo yangu kimya kimya.

Kila mara alikua akilalamika kufunga ndoa mimi nampiga chenga, lakini siku za karibuni amekua haulizii tena mambo ya ndoa, alikaa kimya kwa meizi sita mpaka na mimi nikaanza kuwa na wasiwasi. Nilianza kuchunguza kwani nilihisi kuwa ana mwanaume mwingine, huwezi amini nimegundua kuwa mke wangu ana mwanaume mwingine, tena mtu mzima ambaye alishaoa na kufiwa na mke wake pamoja na mtoto mmoja, alikua hajaoa muda mrefu baada ya kufiwa na mke wake.

Baada ya kuona hivyo niliongea na mke wangu akaniambia kuwa hakuna kitu kama hicho, nilimuambia suala la kuoana nikamuambia kuwa sasa hivi mimi niko tayari lakini yeye ndiyo akawa mtu wakunipiga chenga mara nyumbani hawajajiandaa, nymbani hivi na nyumbani vile. Mimi niliamua tu kwenda mwenyewe lakini cha ajabu nimefika huko wakwe zangu wamekataa mimi nisimuoe binti yao, eti wanaseam nimemchezea muda mrefu hivyo wamenirudishia mahari yangu ingawa mimi nimekataa kuzipoke.

Nimemuuliza mke wangu anajifanya hajui kitu,a naniambia lakini kama wazazi wameamua yeye si wakuwapinga. Nimefuatilia kumbe kashampeleka yule mwanaume kwao na kajitambulisha na kutoa mahari. Nilipombana na kumpiga kidogo aliondoka, niliamua kumtishia na kumuambia kama anaondoka na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine basi anaichie wanangu akanijibu hakuja kwangu na mtoto hivyo ni sawa tu nikibaki nao kwani ni wakwangu hata kama nikiamua kuwanyanyasa ni mimi, ananitumia meseji ananiambia tena ni afadhali kwani ingemuwia shida kuanza ndoa mpya na watoto. Tuna watoto watatu na mke wangu kaondoka na kuniachia nao, sijui hata nifanyeje
Ulitaka wazazi wake waendelee kumlea mkeo na wanao?
Kweli hauna akili.
Hauni aibu kuuliza ujinga kama huo mbele za wanaume?
Halafu unajisifia ujinga. Kaa na wanao uwatafutie mama wa kambo .
 
Naunga mkono hoja.

Sister hood , mother hood, bongo hood and all of the hoods are proud of this woman.
Sema tatizo mwanadada kaondoka Ila bado moyo upo kwa jamaa maana kama angetaka kuondoka, asingesubiria kufukuzwa. Kwa hiyo hii move ni aidha kadhamiria au kafanya kumkomoa ambavyo vyote vitaamua kama atapats furaha anayoitafuta au la

Ila kwa sasa jamaa asihangaike. Mwanamke kashadhamiria
 
Mwanamke akichoka hapo ndiyo mwisho, ukiona kila siku analalamika hicho kitu na anapuuzwa, ukiona kimya hiyo tayari ulishatolewa kwenye mfumo, Simba aliyekamata hapigi kelele [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].

Zamu yako nawewe katafute single mother huko msaidiane kulea watoto wenu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jinga kabisa, unacholilia ni nin ? Wanao si amekuachia ? Tafuta mtoto mdogo wa elfu 2, muoe mzalishe mtoto mmoja tu , ule nae uzee
 
Sio chaguo lako we lea mabao yako hayo maisha yaendelee. Watoto watatu si haba jombaa
 
kwa uchoyo wa mali ulionao ni wakati sasa ulee watoto wako kwa kushirikiana na jamaa zako ili mlinde ulichochuma.
 
mimi ni mbabaz wa miaka 39, sijaoa lakini naishi na mwanamke ambaye naweza kusema kuwa ni kama mke wangu kwani nilishamtolea mahari, tumeishi pamoja kwa miaka kumi bila ndoa, sikuona umuhimu wa kufunga naye ndoa kwani yeye ni mama wa nyumbani, nilijua kama nikifunga naye ndoa ikatokea tunatengana basi tunaweza kugawana mali hivyo nikawa nafanya mambo yangu kimya kimya.

Kila mara alikua akilalamika kufunga ndoa mimi nampiga chenga, lakini siku za karibuni amekua haulizii tena mambo ya ndoa, alikaa kimya kwa meizi sita mpaka na mimi nikaanza kuwa na wasiwasi. Nilianza kuchunguza kwani nilihisi kuwa ana mwanaume mwingine, huwezi amini nimegundua kuwa mke wangu ana mwanaume mwingine, tena mtu mzima ambaye alishaoa na kufiwa na mke wake pamoja na mtoto mmoja, alikua hajaoa muda mrefu baada ya kufiwa na mke wake.

Baada ya kuona hivyo niliongea na mke wangu akaniambia kuwa hakuna kitu kama hicho, nilimuambia suala la kuoana nikamuambia kuwa sasa hivi mimi niko tayari lakini yeye ndiyo akawa mtu wakunipiga chenga mara nyumbani hawajajiandaa, nymbani hivi na nyumbani vile. Mimi niliamua tu kwenda mwenyewe lakini cha ajabu nimefika huko wakwe zangu wamekataa mimi nisimuoe binti yao, eti wanaseam nimemchezea muda mrefu hivyo wamenirudishia mahari yangu ingawa mimi nimekataa kuzipoke.

Nimemuuliza mke wangu anajifanya hajui kitu,a naniambia lakini kama wazazi wameamua yeye si wakuwapinga. Nimefuatilia kumbe kashampeleka yule mwanaume kwao na kajitambulisha na kutoa mahari. Nilipombana na kumpiga kidogo aliondoka, niliamua kumtishia na kumuambia kama anaondoka na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine basi anaichie wanangu akanijibu hakuja kwangu na mtoto hivyo ni sawa tu nikibaki nao kwani ni wakwangu hata kama nikiamua kuwanyanyasa ni mimi, ananitumia meseji ananiambia tena ni afadhali kwani ingemuwia shida kuanza ndoa mpya na watoto. Tuna watoto watatu na mke wangu kaondoka na kuniachia nao, sijui hata nifanyeje
Sasa wewe ulitaka umchezee mpka lini?Mkuu
 
Back
Top Bottom