Ushauri: Kama una mke au binti nyumbani kwako mshauri aache tabia ya kuposti picha zake mtandaoni

Ushauri: Kama una mke au binti nyumbani kwako mshauri aache tabia ya kuposti picha zake mtandaoni

Kutokana na ukosefu wa ajira vijana wengi wamejiingiza kwenye biashara ya utapeli wa kimapenzi.
Ni vijana wa kiume kabisa wanatengeneza account Facebook, Instagram na Whatsapp wakijifanya mabinti.
Hutumia majina ya kike na kupakia picha mbalimbali za wanawake.
Jamii haiwezi kuielewa, siku jirani yako akiona mke wako au dada yako anauza malighafi mtandaoni atajua ni yeye kwa 100% , hajui kuwa ni vijana wa kiume wanajifanyia upatu kwa kutumia picha za mabinti kulaghai wanaume.
Mkienda deep mpaka video za ngono anakutumia akijifanya binti kumbe kazichota mtandaoni.
Sasa hivi hii biashara ya kuuziana video za utupu inalipa sana , unfortunately vijana wa kiume ndio huifanya sana.
Be careful binti, achana na mambo ya kujitupia picha mtandaoni. Waoaji wako kazini kwako, kanisani kwako, mtaani kwako.

Kweli kabisa Mwamuzi wa Tanzania . Kuna kisa kimoja kilitokea marekani. Kijana wa kiume wa miaka kati ya 17 & 19 alikuwa akichati na mtu mwingine feki (aliyejifanya mwanamke), ambaye baadaye ilikuja kujulikana alikuwa ni kijana wa miaka kati ya 19 & 21. Sasa wakawa wana wasiliana kwa jumbe za kawaida. Baadaye wakaanza kuwasiliana kwa jumbe za kimahaba. Baadaye yule binti feki akawa hata anamtumia picha za utupu. Hata video, sasa sijui ndiyo zile unazosema wanazichota mtandaoni!!? Baada ya muda, yule kijana ambaye siyo feki naye akaanza kutuma picha na video za utupu. Yule binti feki alivyojiridhisha kwamba sasa ana picha ambazo siyo feki na kijana ambaye siyo feki, akamtisha kwamba hizi picha zako za hovyo ulizonitumia zita go viral kama hutanilipa kiasi fulani cha dolari. Yule kijana alivyojua katapeliwa, ikabidi afanye maarifa ili amlipe yule mtu zile pesa. Haikuishia hapo, akawa mara kwa mara akimtaka alipe pesa vinginevyo anazipeperusha picha hizo hewani kama manyoya (na sijui kuna yeyote ambaye ataweza kuyakusanya tena hayo manyoa). Hiyo ikampelekea kijana huyo kuwa na sonona na stress nyingi. Mama yake (ambaye alikuwa singo maza kwa mtoto huyo pekee), anaeleza kwamba ghafla hali ya kijana wake ikabadilika, akawa ni kijana mkimwa, hachangamki, anapenda kujitenga muda mwingi. Akiulizwa nini kina msibu, hasemi. Kilichotokea baada ya muda mfupi, yule kijana akajiua. Walivyoanza kufuatilia ndiyo wakagundua haya niliyoyaeleza. Kwa kweli vijana wetu tunahitaji kuwaasa sana na mambo ya cyber (bullying). Siyo madogo au rahisi kama tunavyodhani
 
Kuna binti mmoja hua tunaheshimiana sana hapa mtaani, katika pitapita zangu mitandaoni nikabahatika kukutana na A/c kwenye mitandao ya jamii imejaa picha zake halafu imewekwa mpaka bei elekezi.
Kuanzia siku ile heshima kwa yule binti nimeishusha kwa asilimia kubwa sana.
Huenda kuna mtu unatumia picha zake pasi na yeye kujua au inawezekana ni yeye mwenyewe kaamua kufungua biashara mtandaoni, ila maisha halisi tunayoishi nae hapa mtaani hayaendani hata kidogo na kile nilichokiona mtandaoni.
 
Kweli kabisa Mwamuzi wa Tanzania . Kuna kisa kimoja kilitokea marekani. Kijana wa kiume wa miaka kati ya 17 & 19 alikuwa akichati na mtu mwingine feki (aliyejifanya mwanamke), ambaye baadaye ilikuja kujulikana alikuwa ni kijana wa miaka kati ya 19 & 21. Sasa wakawa wana wasiliana kwa jumbe za kawaida. Baadaye wakaanza kuwasiliana kwa jumbe za kimahaba. Baadaye yule binti feki akawa hata anamtumia picha za utupu. Hata video, sasa sijui ndiyo zile unazosema wanazichota mtandaoni!!? Baada ya muda, yule kijana ambaye siyo feki naye akaanza kutuma picha na video za utupu. Yule binti feki alivyojiridhisha kwamba sasa ana picha ambazo siyo feki na kijana ambaye siyo feki, akamtisha kwamba hizi picha zako za hovyo ulizonitumia zita go viral kama hutanilipa kiasi fulani cha dolari. Yule kijana alivyojua katapeliwa, ikabidi afanye maarifa ili amlipe yule mtu zile pesa. Haikuishia hapo, akawa mara kwa mara akimtaka alipe pesa vinginevyo anazipeperusha picha hizo hewani kama manyoya (na sijui kuna yeyote ambaye ataweza kuyakusanya tena hayo manyoa). Hiyo ikampelekea kijana huyo kuwa na sonona na stress nyingi. Mama yake (ambaye alikuwa singo maza kwa mtoto huyo pekee), anaeleza kwamba ghafla hali ya kijana wake ikabadilika, akawa ni kijana mkimwa, hachangamki, anapenda kujitenga muda mwingi. Akiulizwa nini kina msibu, hasemi. Kilichotokea baada ya muda mfupi, yule kijana akajiua. Walivyoanza kufuatilia ndiyo wakagundua haya niliyoyaeleza. Kwa kweli vijana wetu tunahitaji kuwaasa sana na mambo ya cyber (bullying). Siyo madogo au rahisi kama tunavyodhani
Aisee hiki kisa sijawahi kukisikia ila ni kizito sana.
Dunia iko kasi
 
Kuna binti mmoja hua tunaheshimiana sana hapa mtaani, katika pitapita zangu mtandaoni nikabahatika kukutana na A/c kwenye mitandao ya jamii imejaa picha zake halafu imewekwa mpaka bei elekezi.
Kuanzia siku ile heshima kwa yule binti nimeishusha kwa asilimia kubwa sana.
Huenda kuna mtu unatumia picha zake pasi na yeye kujua au inawezekana ni yeye mwenyewe kaamua kufungua biashara mtandaoni, ila maisha halisi tunayoishi nae hapa mtaani hayaendani hata kidogo na kile nilichokiona mtandaoni.
Yawezekana wagalatia wamepita naye while yeye hajui chochote
 
Ilo kupost ni lazima. Mwanamke akipendeze au akienda sehem nzuri wengi lazima aonyeshe na wengine mtandaoni. It's nature
 
Back
Top Bottom