Ushauri kuhusu mtoto kufariki tumboni kwa mama

Nzugumo

Member
Joined
Feb 25, 2018
Posts
13
Reaction score
14
Habari zenu wana JF,

Mimi ni mgeni humu nimekuja kwenu kuomba ushauri na mawazo yenu maana humu kuna wataalamu mbalimbali.

Mama watoto wangu ni mjamzito wa takribani miezi 8 na point na amekuwa akihudhuria kilinic vizuri kabisa.

Alitakiwa kujifungua 09.02.2019 kwa mujibu wa maelezo ya kliniki yake lakini mnamo tarehe 29.01.2019 nikiwa sipo nyumbani alinipigia simu usiku akilalamika kuwa hajamsikia mtoto akicheza tumboni siku nzima.

Nilimpa ushauri awahi hospital haraka na ndipo kesho yake alifanya hivyo lakini baada ya kufanyiwa vipimo iligundulika kiumbe alichobeba kilikuwa tayari kimepoteza maisha.

Daktari alimwambia arudi kwanza nyumbani ili kusubiri siku zake za kujifungua zifike. Hivyo mpaka sasa nabaki njia panda. Je, kama kiumbe tayari kishafia tumboni ina maana ukuaji wake hauendelei mwanamke anawezaje kuja pata uchungu na akajifungua?

Je, hali hiyo ya kukaa na kiumbe mfu tumboni haiwezi mletea madhara mama huyu? Je, hakuna njia nyingine rahisi ya kutumia kuweza kukitoa kuliko kusubiri siku yake ya kujifungua kufika?

Naimani JamiiForums iko na watu wa kila aina na pengne wapo ambao washakumbana na tatizo hili hivyo naombeni ushauri wenu mwenzenu niko njia panda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee na je anajisikiaje kulala na kushinda na maiti ndani ya tumbo anyway ngoja waje wajuvi wa mambo na fkl utapata majibu mazuri ila pole sana ndugu.
 
Hiyo ishawahi kumtokea shemeji yangu ni kawaida msiweke presha, nendeni kwa wataalam kuna dawa ya kulazimisha uchungu na huyo mtoto atatolewa tu akiwa katika hali hiyo, then huyo dada atasafishwa na atakuwa ok , nendeni Hospitali akatolewe huyo mtoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo hali inatokea na madokta wanaweza wakakuacha ukae nayo hadi utakapotolewa

Sent using Jamii Forums mobile app
Bro kwani kuna sehemu nimoengea vibaya? Kwa mfano ungekuwa wewe ndo mwanamke alafu unaambiwa hvyo hiv ukiachwa peke yako kwenye nyumba unaweza kupata usingizi kweli?
 
Usiwe na shaka ndugu, mtoto akishafariki tumboni kweny siku za karibia na tarehe ya kujifungua huwa inashauriwa mjamzito aachwe mpk atakapojifungua mwenyew pale tarehe zikitimia.
Km ikizid wiki 4 bdo hajapata uchungu ndipo watampa dawa za kuleta uchungu [induction].
 
Mbona tatzo la kawaida san hilo?
Bro kwani kuna sehemu nimoengea vibaya? Kwa mfano ungekuwa wewe ndo mwanamke alafu unaambiwa hvyo hiv ukiachwa peke yako kwenye nyumba unaweza kupata usingizi kweli?
 
Pole sana Ndugu Yangu Hakuna kitu Kinauma Kama Kupoteza Mtoto halafu ni Miezi 8 umelea tumboni Mungu Akupe Nguvu..

Ila Usiogope Mwili wenyewe huwa Unatoa Ishara Zake baadae atasikia Uchungu na Usipotokea Basi watamchoma Sindano za Uchungu watakitoa Kiumbe

?geqA;LS^NToY&'n]9dt
 
Aisee ndo maana wamama wenye mimba wanakufa sana, how can you say ni kawaida mama kukaa na mimba ya mtoto aliekufa? First of all usikute uzembe wa hospitali mpaka mtoto kafa coz kama ni wafatiliaji wa procedures zote mwezi kwa mwezi wangejua mtoto ana tatizo hata mapigo ya moyo wangeona yanashuka wakamzalisha premature, pili, pengine mama nae hakuwa makini kusikiliza movements ziki slow down mapak zikastop kabisa.

Either way , there could be a way kumtoa huyo mtoto kabla hajafa maana miezi 8 ni almost full term anaishi poa kabisa. Now mtoto kafa unamwambia mama rudi nyumbani how? Aisee...
Kama una uwezo mpeleke private atolewe. Huenda kuta hata hajafa ila kwa uzembe akafa kweli

Mtoa mada, nna mtoto mmoja na ali slow down movements kidogo tu, madokta hawakukawiza hata dakika sifuri alitolewa hapo hapo! Mtoto kufikia hadi kufa dalili hazianzi siku moja.
 
Huduma zetu za afya si nzuri sana, mama mjamzito anatakiwa apime mkojo kuangalia infections, apime PB na mkunga asikilize mapigo ya moyo angalau kila baada ya wiki mbili hasa baada ya 3rd trimester.
 
Huduma zetu za afya si nzuri sana, mama mjamzito anatakiwa anime mkojo kuangalia infections, apime PB na mkunga asikilize mapigo ya moyo angalau kila baada ya wiki mbili hasa baada ya 3rd trimester.

Na pia proteins kwa ajili ya kifafa cha mimba
Ila wakati mwingine me nadhani ni jukumu la mzazi pia kama una uwezo unalipa unapimwa kila mara kadiri uwezavyo kwa usalama


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Na pia proteins kwa ajili ya kifafa cha mimba
Ila wakati mwingine me nadhani ni jukumu la mzazi pia kama una uwezo unalipa unapimwa kila mara kadiri uwezavyo kwa usalama


Sent from my iPhone using JamiiForums
Ya protein inaionekana kwenye mkojo. Hizi ni huduma zilitakiwa zitolewe kwa mama wajawazito wote lakini uwezo wetu haujafika huko.
 
Aende hospital nyingine akamuone dakatari afanye ultrasound!
Kama itakuwa hivyo watamuwekea dawa ya uchungu atafanya mazoezi ya kutenbea/ kupanda Ngazi kisha atapata uchungu atapelekwa leba kiumbe kitatolewa vizuri tu!
Aende hospital kubwa au binafsi!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…