Ushauri kuhusu NMB

Ushauri kuhusu NMB

Orketeemi

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
5,063
Reaction score
12,866
Habari.

Siku ya Leo tar 24/01/2022 nimefika katika Tawi la NMB Kwa lengo la kutoa pesa kwenye ATM machine ya pale.

Nimeingiza Kadi na kufuata process zote lakin machine haikutoa pesa ilihali SMS ya muamala nilipata.

Nilivyomuuliza mlinzi akanambia niingie ndan ya Tawi ambako nilipewa form na kuambiwa nisubir masaa 24.

Ninaomba ushauri maana tatizo hilo limeniletea usumbufu mkubwa na ninatakiwa kuingia gharama zingine kufuatilia pesa hizo.

NMB nimewahoji kuhusiana na ni nani Kati ya Mimi na wao anayepaswa kubeba gharama za usumbufu huo wanasema nibebe Mimi ilihali tatizo ni la mfumo wao.
 
Hiyo pesa itarudi kama ulivyoambiwa,hakuna shida umesha ripoti huwa inatokea kw yeyote na hata usingeripoti pesa yako ingerudishwa
Imewahi kunikuta kwenye Bank tatu tofauti hakukuwa na shida wala gharama za kufuatilia
Ndo ushaambiwa sasa kuhusu gharama
 
We Relax.... Huo Muamala Utarudi Kwenye Akaunti Yako wenyeeeeewe!! Dah ila hizi pesa Zetu Za Mawazo hizi.....Ukute mtu Kutwa Mara 3 Unaingiza Kadi Kwenye ATM kusiklizia Kama Mchongo Umetiki.. Sasa hiyo mara Ya 3 kitu kimetiki,...halafu Machine Inakuletea Uduanzi....aaaaaaagh ..!!!
 
Hiyo pesa itarudi kama ulivyoambiwa,hakuna shida umesha ripoti huwa inatokea kw yeyote na hata usingeripoti pesa yako ingerudishwa
Imewahi kunikuta kwenye Bank tatu tofauti hakukuwa na shida wala gharama za kufuatilia
Najua Itarud lakini kuna gharama nimeingia na nyingine nitaingia Kwa ajili ya kurud kuichukua hiyo hela. Sasa nataka kufaham ni Kwa nini usumbufu huu uliojitokeza niugharamie Mimi ilihali si kosa langu?
 
Najua Itarud lakini kuna gharama nimeingia na nyingine nitaingia Kwa ajili ya kurud kuichukua hiyo hela. Sasa nataka kufaham ni Kwa nini usumbufu huu uliojitokeza niugharamie Mimi ilihali si kosa langu?
Pole mzee unaweza kuta moja kati ya noti uliyotakiwa uipate ilikuwa imejikunja inazuia pesa zote zisitoke
 
Naomba kuuliza, mfano nina akaunti ya benki ya hapa tz, baada ya siku kadhaa nikasafiri kwenda nchi za mbali je nitaweza kuendelea kutumia hiyo benki na kupata huduma kama kawaida.? Na vipi kama hiyo nchi niliopo hakuna hiyo benki.?
 
Naomba kuuliza, mfano nina akaunti ya benki ya hapa tz, baada ya siku kadhaa nikasafiri kwenda nchi za mbali je nitaweza kuendelea kutumia hiyo benki na kupata huduma kama kawaida.? Na vipi kama hiyo nchi niliopo hakuna hiyo benki.?

Inawezekana ndio, nadhani crdb wana kadi zao zinakuwezesha kufanya miamala!
 
NMB ni wazuri kwenye huduma ya mikopo ya wafanyabiashara, NMB mobile na ike kitu inayoitwa "Salary Advance" 😋! Nasikia pia wana kamisheni nzuri kwa mawakala wao wa huduma za kifedha. Huduma nyingine zilizobakia naona ni majanga tu kwa mtazamo wangu.

Foleni kama kawa! Ni kawaida kukuta madirisha manne ya kutolea huduma, lakini ukakuta ni mawili tu yenye wahudumu! ATM mashine zao kukosa hela, au kuwa out of service! ni jambo la kawaida sana na hasa maeneo ya pembezoni! Mikopo kwa wafanyakazi ni kiduchu ukilinganisha na benki nyingine!
 
Naomba kuuliza, mfano nina akaunti ya benki ya hapa tz, baada ya siku kadhaa nikasafiri kwenda nchi za mbali je nitaweza kuendelea kutumia hiyo benki na kupata huduma kama kawaida.? Na vipi kama hiyo nchi niliopo hakuna hiyo benki.?
Kwa uzoefu wangu kama una kadi zile za Visa au Mastercard utaweza kutoa hela ambayo ipo kwenye account yako hata ukiwa nje ilimradi tu upate ATM yenye Visa au Mastercard kulingana na card yako.
 
Habari.

Siku ya Leo tar 24/01/2022 nimefika katika Tawi la NMB Kwa lengo la kutoa pesa kwenye ATM machine ya pale.

Nimeingiza Kadi na kufuata process zote lakin machine haikutoa pesa ilihali SMS ya muamala nilipata.

Nilivyomuuliza mlinzi akanambia niingie ndan ya Tawi ambako nilipewa form na kuambiwa nisubir masaa 24.

Ninaomba ushauri maana tatizo hilo limeniletea usumbufu mkubwa na ninatakiwa kuingia gharama zingine kufuatilia pesa hizo.

NMB nimewahoji kuhusiana na ni nani Kati ya Mimi na wao anayepaswa kubeba gharama za usumbufu huo wanasema nibebe Mimi ilihali tatizo ni la mfumo wao.
... pole sana ndugu. Iliwahi kunitokea nili-park kwenye tawi moja nitoe pesa za mafuta niko safarini na familia naelekea mkoani; kadi ilidumbukia kwenye ATM na ilikuwa Jumapili asubuhi. Dah, sikuwahi kuchafukwa kama siku ile! Staki hata kukumbuka hilo tukio.
 
Najua Itarud lakini kuna gharama nimeingia na nyingine nitaingia Kwa ajili ya kurud kuichukua hiyo hela. Sasa nataka kufaham ni Kwa nini usumbufu huu uliojitokeza niugharamie Mimi ilihali si kosa langu?
Mkuu unisamehe lakini sijajua hasa unacholalamika wewe ni nini?

Let's say mwanzo ulitumia bodaboda kuitafuta hiyo ATM yao ilipo ukaipata but unfortunately mpango wako ukakwama,ukaingia ndani wakakusikiliza vizuri kwamba hiyo pesa itarudi kwenye acc yako ndani ya muda fulani sasa utatumia tena gharama gani kuifata ilhali ikisharudi kwenye acc yako utakuwa na uhuru wa wakuitoa popote karibu na wewe?

Kuna mambo wakati mwengine unaachana nayo tu.
 
Najua Itarud lakini kuna gharama nimeingia na nyingine nitaingia Kwa ajili ya kurud kuichukua hiyo hela. Sasa nataka kufaham ni Kwa nini usumbufu huu uliojitokeza niugharamie Mimi ilihali si kosa langu?
Hizo ni changamoto za kawaida, km gari kupata pancha, maharage kuungua jikoni, kukatika umene, maji, mafuriko, wewe mwenyewe kuugua nk.
Relax.
Gharama zipo, wa kubalance ni wewe
 
Naomba kuuliza, mfano nina akaunti ya benki ya hapa tz, baada ya siku kadhaa nikasafiri kwenda nchi za mbali je nitaweza kuendelea kutumia hiyo benki na kupata huduma kama kawaida.? Na vipi kama hiyo nchi niliopo hakuna hiyo benki.?
Kama ni Visa au Mastercard utatumia nchi yoyote kwenye ATM zenye mfumo huo
 
Mkuu unisamehe lakini sijajua hasa unacholalamika wewe ni nini?

Let's say mwanzo ulitumia bodaboda kuitafuta hiyo ATM yao ilipo ukaipata but unfortunately mpango wako ukakwama,ukaingia ndani wakakusikiliza vizuri kwamba hiyo pesa itarudi kwenye acc yako ndani ya muda fulani sasa utatumia tena gharama gani kuifata ilhali ikisharudi kwenye acc yako utakuwa na uhuru wa wakuitoa popote karibu na wewe?

Kuna mambo wakati mwengine unaachana nayo tu.
Jamaa atakua anawaza nauli aliyosafiria kutoka kijijini
 
Back
Top Bottom