Ushauri: Kumpa hela mama mkwe wako wa zamani ni sawa au niache kabisa kujipendekeza?

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Wakuu nilikuwa na msichana fulani niliyeishi naye miaka takribani mitatu ila bahati mbaya hatukupata baraka za kuwa na watoto na kibaya zaidi tukaja kuachana kwa mambo fulani fulani ambayo sioni haja ya kuanza kuwachosha kuyaelezea.

Ila sasa mama yake alikuwa ni mtu mwema kwangu kiasi kwamba nikawa namsaidia pesa ndogo ndogo kwa kuwa hali yake sio nzuri sana ya kiuchumi, kama ni ugomvi tunao mimi na mwanaye tu na toka niachane na mtoto wake sijawahi kuongea naye tena na ni takriban miezi sita sasa imepita na nimepata mchumba fulani ambaye bado tunapangana pangana.

Sasa nimeotea hela kwenye mitikasi yangu ninawiwa kumtumia pesa mama mkwe ila naona kama inaweza ukawa mwanzo wa kuanza kurudisha rudisha mahusiano tena mambo yakawa mengi tena maana wananijua in and out.

Mimi nina tabia ya upole na huruma natamani tu nimsadie ila nataka isiwe sababu kwamba bado nawawaza waza isitoshe ni watu fulani wa mambo za Kiswahili swahili nadhani mshaelewa yaani, mambo ya kiwitch witch wanaziamini.

Mnasemaje nimsalimie na ku boost kidogo ka 30000 au nile buyu tu.
 


John hivi kweli 30k ni jambo la kuandika huku? Kweli? Haya majina ya John kuna tatizo la asili
 
Utakufa maskini kwa kujihurumisha kutatua shida za kila mtu. Hizo elfu 30 ekeza au msaidie mamako mzazi. Having girlfriend wako atalichukuliaje swale hili?
 
Wewe huna hata kabiashara kanachohitaji boost ya mtaji? Hiyo 30k kama una duka la nguo ni Tshirts 3 kali ambazo utauza 15k au 20k na kupata faida ya 15k au 30k kabla ya matumizi. Kama ni mkulima unaweza hata kulipa vibarua wawili au watatu kwa siku.

Acha upumbavu wa kujifanya mkristo kuliko hata Yesu mwenyewe. Hizo hela zako fanyia mambo yako mengine ya maendeleo au mtumie mama yako mzazi. UMENIKERA SANA
 

Kukiwa na muitqji na una uwezo saidia
 
toa ndugu toa ndugu.....
maana Mungu anakuona
Ila kipanga samahani nikulize kitu sawa mimi sio babako , mamako wala bibiako ila humu jamii forums unatengeneza sh. Ngapi na mimi nipate ndugu yako mana kutwa kucha kila mada itakayowekwa humuu jamii forums kipanga haikupiti?
 
Daah mi sijui nikujibuje ila kiufupi mimi nina ex wangu tangu tuachane ni miaka mi 7 sasa japo bado ajafuta tatoo yangu na kashaolewa lakini yeye hachoki kumletea zawadi mama yangu kila atakapo pata nafasi pia hata mimi nikipataga shida yeyote huwa hachoki kinisaidia na kunishauri huwa analivaa jambo langu kama lake ni maisha tu haya sijui nitakuwa nimekujibu au lah!
 
We muhuni Nini?
30,000 unaileta kwenye group discussion?
 
Msaidie tu ,

Kama hapo tu mumeachana kwa muda unajifikiria kukatisha msaada, kama je huyo mwanamke angefariki kabisa ingekuaje?

Ushemeji na Ukwe huwa haufai hata nyinyi wapenzi mkitengana au mmoja wenu akifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…