Ushauri kwa Adamu Mchomvu (Baba Jonii) na game ya mziki

Ushauri kwa Adamu Mchomvu (Baba Jonii) na game ya mziki

DOGofGOD

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2015
Posts
1,341
Reaction score
480
Jamaa anapenda sana mziki.Lakini inavyoonekana mziki haumpendi. Ameshajaribu kutoa ngoma kibao. Lakini hazifanyi vizuri kwenye game. Hebu tumshaurini huyu jamaa wapi anabugi na nini afanye ili aweze kutoka kimuziki. Kwa sababu anaonekana ana hamu sana ya kutoka lakini hajui apime njia gani.

Ushauri wenu ni muhimu sana kwake na kwa wengine wanaotamani kutoka kama yeye. Karibuni tufunguke wadau especially mnaojua ABC za game hili. Game ngumu mazee!
 

Attachments

  • adam3.jpg
    adam3.jpg
    20.3 KB · Views: 1,698
Kidogo kwenye wimbo wa kitaa wiise alioshirikishwa na KCK kafanya fresh!! Ila PAMOJA na uduwanzi wake A+ Yuko real SANA, sema tu mfumo
 
Mtangazaji Mwanamuziki
Mwanamuziki Mtangazaji
Hapo ndio kwenye mtego!
 
Siyo talent yake, akomae na fani yake lkn cyo mziki.
 
Akili.inataka mwili hautaki. Atafute kitu kingine cha kufanya. Yaani anachekesha tu kwenye game. Hata kwenye kutangaza nako ni shiida tupu. Hana.lolote!!
 
Kama anapenda kuimba/kuchana na mziki haumtaki bora awe promota,sijawahi kusikia nyimbo zake zikipigwa radio nyingine zaidi ya CLouds FM/TV tu.
 
Acha majungu na wivu..mie namuelewa sanaaa!!
 
Mwanangu Adam Soma hapa.

We una kipaji tatizo promo za nyimbo zako zipo sehemu moja tu ambapo ni ofisini kwenu pekee Clouds.. bado sijaskia ngoma zako zikipigwa kama radio free africa,east africa radio,EATV,e fm.. nafkiri hii yote ni kwa sababu wewe mtangazaji kwenye kituo ambacho kinachukiwa na baadhi ya kampuni nyingi za media kutokana na ushindani wenu so mtu aki play wimbo wako anaona kama anapigia promo clouds.Mawazo yangu ni haya we kaza tu but jitahidi kutengeneza ushirikiano mwema na other radio stations na tv stations usijenge beef na mtangazaji yeyote wa kituo shindani na nyie maana atakinukisha kwa Meneja.Kuhusu kuimba/kuchana kila mtu anaweza but aidea ndo mpango mpango vilivile miziki ya sasa hivi wala haiangalii sauti ya mtu ni mkito wa kibabe/Beat kali pamoja na simple lyrics.

Epuka kutaja au kusifia kampuni yenu kwenye nyimbo zako.

asante
 
Kua karibu na media sio sababu ya kukubalika kwa Chochote utakacho kifanya...,.

Adam, Anna yule wa eatv na baadhi ya watangazaji wengine Wanadhani kwakua wao ni watangazaji basi wataweza kutoka na kukubalika....... wajifunze kua wabunifu tu basi.
 
Hata Diva loveness sidhan kama nyimbo zake zinapigwa media nyngn
 
Tuna gawanaga tu viroba vya konyawisee fasi ya dwas mafekeche shigid shiida Jamaa anajuwise kinowisee sema ni majuwise ya wadawise ila n hataree kw froo namkubali knomaaa
 
Back
Top Bottom