Ushauri kwa chama cha ACT- Wazalendo na Maalim Seif Shariff Hamad

Ushauri kwa chama cha ACT- Wazalendo na Maalim Seif Shariff Hamad

Relief Mirzska

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2017
Posts
13,992
Reaction score
22,396
Salaam kwenu wakuu,

Mimi sijihusishi na siasa za Tanzania kidhati ya moyo, nimekuwa ni mfuatiliaji tu wa namna mambo yanavyokwenda/yanavyoendeshwa ndani ya nchi yetu. Niliwahi kuwa mwanachama wa CUF Habari mwanzoni mwa miaka ya 2010 na kadi yangu nilipewa na Julius Mtatiro, hata hivyo nilihamia CCM imara muda mfupi baadae baada ya kugundua hakukuwa na upinzani Imara nchini kwetu. Maamuzi hayo yalichagizwa na ule msemo wa "if you can't beat them, join them". Fikra kuu ni ile fikra ya aliemtoa gerezani ndugu Nelson Mandela, President FW De Klerk na namna alivyofika kuwa pale.

Ila rasmi baada ya kesi maarufuu visiwani Zanzibar ya mwaka 2013 kuanza niliamua rasmi kuachana na mambo ya siasa na kujikita kwenye kushughulikia mambo yangu na familia yangu huku nikiamini ni mimi, na ni mimi tu ambae ningeweza kuikomboa familia yangu nyonge kutoka kwenye umaskini na wala sio wana-siasa.

Yakawa yaliyokuwa na uchaguzi wa mwaka 2015 ukafika, kwa vile wengine tulikuwa kiakili kabla ya ki-umri tukakaa pembeni na kuangalia mambo yatakavyokuwa. Muda wa kwenda kwenye mikutano ya kampeni tukatumia kuzalisha mali huku fikra zetu pevu zikituambia hata kama CUF watashinda uchaguzi basi hawatopewa nchi kuiongoza (na hivyo ndivyo ilivyokuwa).

Uchaguzi ukafanyika, Jecha akaufuta, Maalim akahangaika mpaka kwa wadhamini wa demokrasia (Ulaya na Marekani) lakini hakuna lililokuwa. Kijambo kilikuwa kipo, mpaka leo tumefikia tunaingia tena kwenye uchaguzi na "kijambo kimeyayuka". Hii kamwe haimaanishi kukejeli harakati za Maalim katika kupigania demokrasia Zanzibar au kupigania haki ya Wazanzibar la hasha! Napenda kutambua mchango mkubwa wa Mh. Maalim Seif Shariff Hamad katika harakati za demokrasia nchini Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Mafanikio yake ni makubwa mno na hata kama atafariki leo basi Maalim ataiaga dunia hii akiwa mshindi. Kuipata SUK Zanzibar si mafanikio ya kubeza hata kidogo.

Kwa jitihada tu za Maalim na timu yake, leo hii hata wanaoitwa "wapinzani" watakuwemo kwenye baraza la mawaziri la Serikali ya Zanzibar kuanzia November mwaka huu In Shaa Allah. Haya ni mafanikio makubwa sana ambao wanasiasa wa Tanganyika na sehemu nyengine nyingi za Afrika hawajaweza kuyafikia bila umwagaji damu.

Mbali ya mafanikio haya, yapo makosa makubwa sana ya ki-msingi ambayo Maalim pengine na chama waliyafanya ambayo yanagharimu harakati hizi za kiukombozi wa demokrasia Zanzibar na Tanzania kwa ujumla mpaka leo hii. Na hili ndilo lililonisukuma kuandika makala hii ili iwe funzo kwa Maalim na chama cha ACT Wazalendo katika uchaguzi huu ujao. Labda tu kwa uchache niainishe ninayoyaona makosa makuu aliyoyafanya maalim hapo mwaka 2015 au kabla ambayo sasa yanagharimu harakati za ukombozi wa kidemokrasia kama ifuatavyo

1) Kukataa kurudia uchaguzi wa Mwezi Machi 2016- Hili lilipelekea Baraza la wawakilishi kuwa na wawakilishi kutoka chama kimoja tu, na tumshukuru Mungu kwamba walibaki kuwa wazalendo kwa Zanzibar yao maana kwa hali ile wangeweza kupitisha sheria kandamizi dhidi ya vyama vya upinzani na Wazanibar kwa ujumla na kwenda kinyume na yote yale ambayo CUF kipindi hicho walijinasibu kuyapigania.

2) Kutoandaa na/au kumtambulisha mtu ambae angekuwa/atakuwa mrithi wake baada ya yeye kuondoka kwenye siasa kwa namna yoyote ile i.e kifo, afya, umri n.k

NOTE: Kwa wanaojua habari za siasa hususan za Zanzibar, wanaelewa kwamba hayo hapo juu ni makosa ambayo yanagharimu harakati za kidemokrasia Zanzibar mpaka leo.

USHAURI:

1) Uchaguzi una kushinda na kushindwa, halafu hapa Tanzania kuna kupewa na kutopewa. Imani ya wengi ni kwamba Maalim amekuwa akishinda kila chaguzi lakini hapewi na hakuna chochote kiwacho, hivyo sitakosea kusema anaweza akashinda mwaka huu na pia asipewe vile vile, ushauri wangu ni kwamba hata asipopewa basi akubali kushindwa huko na atengeneze SUK pamoja na CCM kama ilivyokuwa mwaka 2010. Hii itasaidia kufanya upinzani ushiriki katika kuwatumikia wananchi katika level nyengine kabisa na pia itatoa nafasi ya wapinzania ndani ya Zanzibar kuwa na nafasi nzuri ya kuwashawishi viongozi wengine watakaotoka CCM masuala yahusuyo Zanzibar kila itokeapo (naamini nimeeleweka).

Lazima safari hii wapinzania wakubali kushiriki kutengeneza serikali maana heri nusu shari kuliko shari kamili.

2) IKitokea upinzania umeshindwa au umeshinda halafu hawakupewa basi Maalim Seif Shariff Hamad na chama chake cha ACT Wazalendo wamteue mtu mwengine mbali na Maalim kuwa Makamu wa kwanza wa Rais. Hili nadhani katiba ya Zanzibar inaliruhusu. Hii itatoa nafasi kwa huyo mteuliwa Mfano Nassor Mazrui au rafik yangu Mh. Mansoor Himid kuandaliwa kwa kipindi cha miaka 5 ijayo ili aweze kuwa mgombea tofauti (na Maalim) kwa mara ya kwanza tangu siasa za vyama vinig zilipoanzishwa nchini (maana Maalim amekuwa mgombea wa upinzani tangu 1995 na ni hakika hatoweza kusimama tena majukwaani ifikapo 2025).

Maalim asikubali kujiaminisha kwamba ni yeye tu ndie ataweza kuwa Rais Zanzibar kutokea upinzani maana hilo litakuwa ni kosa kubwa na itaendelea kuwa dosari kama ilivyo dosari sasa hivi katika harakati hizi za ukombozi wa kidemokrasia.

Naamini Zitto kama kiongozi mkuu wa chama mtaufikiria ushauri huu na kuufanyia kazi.

NB: Kwa wale wana-CCM mnaofuata tu mkumbo, sisi wengine ni wanachama halali wa CCM na tuna kadi za chama kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Tumeamua tu kutumia akili zetu kufikiria.
 
Mleta uzi umeongea mengi ya msingi ila wanasiasa wengi wa Tanzania ,mitizamo yao ina utata na ukakasi mkubwa. Wana msemo wao kuwa "siasa ni mchezo mchafu". Hali hiyo hupelekea siasa kuwa shaghalabaghala na ushauri wa msingi kupuuzwa na kubaki ushabiki na kuvishana vilemba vya ukoka.
 
Karibu kwa fikra mkuu!

Najaribu ku-play part yangu japo kwa kushauri tu
Kwanza nikupongeze kwa kutangaza maslahi yako mapema kwamba ulitoka upinzani ili kujinufaisha wewe na familia.

Pili umejitahidi kutoa mawazo yako ni vizuri.

Hoja ya Maalim na ACT kutosusia uchaguzi hio iko wazi na nadhani walishatangaza mapema. kuelekea 2020 Oktoba.
hapa Maalim ni jabari la kisiasa kweli. huyu mzee hajaacha kitu kwenye siasa za vyama vingi na somo tosha kwa afrika hii.
Unajuwa amewafundisha hadi wazungu? na alitaka kuwapeleka hadi mwisho wa njia kwenye dhana ya demokrasia.

kususia uchaguzi wa Machi, 2016 kwanza ilikuwa ni ujumbe kwa wale waliojifanya wao bi BABA la demokrasia Duniani, Maalim na wenzake walitaka kusaza hata hakiba na walitaka kujiridhisha Dunia itafanya nini hata baada ya Maridhiano na uwepo wa GNU. Kwamba inafika mahala CCM inavuruga hata maridhiano ya kikatiba na wanaachwa wafanye watakavyo.

Nadhani kwenye nukta hio Maalim na ACT wana majibu tayari.

Kuhusu hoja ya Kutayarishwa mtu mwengine ni muhimu lakini kila chama kina utaratibu wake. jiulize kwa nini maalim mara zote anagombea kwa nini ? umepata kuwadadisi wenzake na umepata majibu gani? sidhani kama hawajajiandaa. Timing labda ndio tatizo

Siasa ni sayansi na sanaa.

Hilo la mchango wa Maalim Seif kwa Zanzibar ni kweli historia imeshaandikwa. Uchaguzi huu wa 2020 utaonesha njia wapi Zanzibar inataka kwenda. Sidhani kama Maalim seif na wazalendo wengine watatoa fursa ya kumalizwa Zanzibar.

wakati hauko vizuri, viashiria si vyema. Acha Maalim na Wenzakle kupitia ACT KAMA HAOTOFUTWA waingie kwenye Serikali kwa maslahi ya Zanzibar. ( shika hayo maneno).

Wengine tuendelee kufaidisha familia zetu ndani ya CCM.
 
SUK ni makubaliano yamo ndani ya Katiba,
Ungeli kuwa ni CCM mzuri kama ungeliwashauri CCM wenzako kufuata katiba na kuach kuvunja sheria kwani kufanya hivyo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Washauri CCM wenzako waache kuendeleza ubabe na wizi wa kura, waliache taifa lisonge mbele.

Ushauri wako ulioutowa wa kushiriki SUK hata kam tumeshinda lakini tukadhulumiwa tukubali tuu, huko ni kutufannya sisi mapimbi.

Kwani CCM kule kutawala peke yao baada ya kuvunja katiba na sheria na sisi kususu kumepuguaza nini kwa upinzania?

Bali CCM wamejiona kuwa kweli ni wahalifu kwa aibu wakamfukuza mwenzao mwakilishi wa Jangombe alipofunguka na kuusema ukweli uliomo nafsini mwake.

Huyo Dr. Shein munamsifu nyinyi tuu ccm wenzake, lakini Duniani ni rubish tuu kwa kutokuwa Muadilifu kwenye Uchaguzi. Amejishushia 'profile' yeye na chama chake. Hiyo si fedheha ndogo.
Tungelikubali kushiriki uchaguzi wa marejeo ni sawa na mwana mume kukubali kukatwa Dhakar na kishwa kugeuzwa kinyume cha maumbile na kupigwa nao.

Siasa si kushiriki tuu wakati mwingine kugoma nayo pia ni siasa.

Pole ,Ushauri wako Hauna maana yeyote, pampja na nia yako nzuri,

Endelea kuhama hama ikiwa unaona CCM haikuridhishi.

Jaribu chama cha Wganga wa jadi maana siasa huiwezi kweli.

Wewe unadhani Kuleta ukombozi ni kazi ya kufumba na kufumbua?
Laaa, bali ni mihanga na Muda mwingi kupotea, na hata maisha na uchumi kuharibiwa mpaka lengo lifikiwe.
Watazame Wapalestina zaidi ya Miaka 50 wanapambana na hawajakata tamaa., wewe miaka mitano tuu kushaungana na Madhalim!
Pole Sana.
 
Mleta uzi umeongea mengi ya msingi ila wanasiasa wengi wa Tanzania ,mitizamo yao ina utata na ukakasi mkubwa. Wana msemo wao kuwa "siasa ni mchezo mchafu". Hali hiyo hupelekea siasa kuwa shaghalabaghala na ushauri wa msingi kupuuzwa na kubaki ushabiki na kuvishana vilemba vya ukoka.
Ni kweli usemalo mkuu.

Na hiloni miongoni mwa yaliyonifanya nikaamua kuachana na habari hizi na nikaangalia yahusuyo family yangu zaidi.

Watu ni lazima wajue kuwa unapokuwa mwanasiasa na ukafikia level za juu, basi mahusiano yako na family ni rahisi kuingia matatani.
 
Kwanza nikupongeze kwa kutangaza maslahi yako mapema kwamba ulitoka upinzani ili kujinufaisha wewe na familia.

Pili umejitahidi kutoa mawazo yako ni vizuri.

Hoja ya Maalim na ACT kutosusia uchaguzi hio iko wazi na nadhani walishatangaza mapema. kuelekea 2020 Oktoba.
hapa Maalim ni jabari la kisiasa kweli. huyu mzee hajaacha kitu kwenye siasa za vyama vingi na somo tosha kwa afrika hii.
Unajuwa amewafundisha hadi wazungu? na alitaka kuwapeleka hadi mwisho wa njia kwenye dhana ya demokrasia.

kususia uchaguzi wa Machi, 2016 kwanza ilikuwa ni ujumbe kwa wale waliojifanya wao bi BABA la demokrasia Duniani, Maalim na wenzake walitaka kusaza hata hakiba na walitaka kujiridhisha Dunia itafanya nini hata baada ya Maridhiano na uwepo wa GNU. Kwamba inafika mahala CCM inavuruga hata maridhiano ya kikatiba na wanaachwa wafanye watakavyo.

Nadhani kwenye nukta hio Maalim na ACT wana majibu tayari.

Kuhusu hoja ya Kutayarishwa mtu mwengine ni muhimu lakini kila chama kina utaratibu wake. jiulize kwa nini maalim mara zote anagombea kwa nini ? umepata kuwadadisi wenzake na umepata majibu gani? sidhani kama hawajajiandaa. Timing labda ndio tatizo

Siasa ni sayansi na sanaa.

Hilo la mchango wa Maalim Seif kwa Zanzibar ni kweli historia imeshaandikwa. Uchaguzi huu wa 2020 utaonesha njia wapi Zanzibar inataka kwenda. Sidhani kama Maalim seif na wazalendo wengine watatoa fursa ya kumalizwa Zanzibar.

wakati hauko vizuri, viashiria si vyema. Acha Maalim na Wenzakle kupitia ACT KAMA HAOTOFUTWA waingie kwenye Serikali kwa maslahi ya Zanzibar. ( shika hayo maneno).

Wengine tuendelee kufaidisha familia zetu ndani ya CCM.
Duh! saamahani sana mkuu usiniwekee maneno kwenye kinywa changu. Tena samahani na ukiona inafaa unitake radhi, hakuna niliposema nimetoka upinzani ili nijinufaishe mimi na family yangu. asilan abadan!!!!!

Halafu siongelei hoja ya Maalim na ACT kutosusia uchaguzi, soma uelewe ndugu. Nimeongelea suala la kukubali kushindwa ikitokea "watangazaji wa matokeo" wamesema kashindwa. Inaonekana mkuu hujasoma vizuri mada.

"kususia uchaguzi wa Machi 2016 kwanza ilikuwa ni ujumbe kwa wale wanaojifanya wao ni baba la demokrasia duniani" hayo ni maandishi yako. Swali langu, ujumbe huo umesaidia nini??? Kwani wewe ulikuwa hujui the so-called baba la demokrasia duniani ni wanafiki tu?? Huoni kwamba hatua ile ya kususia uchaguzi umerudisha nyuma harakati za ukombozi wa kidemokrasia na sasa baada ya miaka mitano inabidi tuanze pale tulipoishia September 2015??

Sitaki kuamini eti maalim na wenzake walitaka kujiridhisha jumuiya ya kimataifa itafanya nini juu ya lile la Jecha, na kama ndivyo basi walipiga hesabu mbovu sana maana jumuiya ya kimataifa cha kwanza wanachoangalia ni maslahi yao tu. Maslahi yao yakiwepo they don't care who runs "The shithole" countries. As long as CCM assured them their interest to be met jumuiya ya kimataifa haitoingilia chochote popote pale and of all the people Maalim alitakiwa alijue hili.

Kuhusu Maalim kuandaa na kumtambulisha mtu, hii ni mada on its own, and again Maalim should learn from history. Unajua tatizo la ushia na usunni duniani?? Sisemi kwamba Mtumw Muhammad alikosea kutomuandaa na kumtambulisha mtangulizi wake laaa, ila viongozi wa sasa ambao sio mitume wanatakiwa wajifunze kitu hapa.
 
SUK ni makubaliano yamo ndani ya atiba,
Ungeli kuwa ni CCM mzuri kama ungeliwashauri CCM wenzako kufuata katiba na kuach kuvunja sheria kwani kufanya hivyo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Washauri CCM wenzako waache kuendeleza ubabe na wizi wa kura, waliache taifa lisonge mbele.

Ushauri wako ulioutowa wa kushiriki SUK hata kakam tumeshinda lakini tukadhulumiwa, huko ni kutufannya sisi mapimbi.

Kwani CCM kule kutawala peke yao baada ya kuvunja katiba na sheria na sisi kususu kumepuguaza nini kwa upinzania?

Bali CCM wamejiona kuwa kweli ni wahalifu kwa aibu wakamfukuza mwenzao mwakilishi wa Jangombe alipofunguka na kuusema ukweli uliomo nafsini mwake.

Huyo Dr. Shein munamsifu nyinyi tuu ccm wenzake, lakini Duniani ni rubish tuukwa kutokuwa Muadilifu kwenye Uchaguzi. Amejishusha iprofile yeye na chama chake. Hiyo si fedhejha ndogo.
Tungelikubali kushiriki uchaguzi wa marejeo ni sawa na mwana mume kukubali kukatwa Dhakar na kishwa kugeuzwa kinyume cha maumbile na kupigwa nao.

Siasa si kushiriki tuu wakati mwingine kugoma nayo pia ni siasa.

Pole ,Ushauri wako Hauna maana yeyote, pampja na nia yako nzuri,

Endelea kuhama hama ikiwa unaona CCM haikuridhishi.

Jaribu chama cha Wganga wa jadi maana siasa huiwezi kweli.

Wewe unadhani Kuleta ukombozi ni kazi ya kufumba na kufumbua?
Laaa, bali ni mihanga na Muda mwingi kupotea, na hata maisha na uchumi kuharibiwa mpaka lengo lifikiwe.
Watazame Wapalestina zaidi ya Miaka 50 wanapambana na hawajakata tamaa., wewe miaka mitano tuu kushaungana na Madhalim!
Pole Sana.
Mkuu samahani, hebu tulia usome tena mada yangu.

Kwani unadhani sijui kwamba SUK ni makubaliano yamo ndani ya katiba???? Kwani sijaliongelea hili???

Unajuaje siwashauri CCM Wenzangu kufuata katiba na kkuacha kuvunja sheria??

Kutokushiriki katika SUK mwaka 2016 kuliwafanya msiwe mapimbi?? ni faida gani imepatikana sasa kwa kutokushiriki kule?? Unajua hasara zilizopatikana?? au nikutajie?? Hujui nini kimepunguwa kwa kuwaacha CCM kutawala peke yao since March 2016??

"Bali CCM wamejiona kuwa kweli ni wahalifu kwa aibu wakamfukuza mwenzao mwakilishi wa Jangombe alipofunguka na kuusema ukweli uliomo nafsini mwake." Hii ni kauli yako mkuu, na unadhani CCM wanajali kuhusu hili?? eti wamejiona hahahahhahahhah.

Sikatai kwamba inabidi kuna nyakati kwenye siasa uweke migomo lakini unatakiwa upige hesabu zako vizuri ndugu yangu. Sasa hebu niambie kule kugoma kumesaidia nini leo???? Hakuna takwa hata moja la Maalim na CUF ya muda ule lililofanyiwa kazi mpaka sasa na mbona wanashiriki uchaguzi?? Mkuu inawezekana huwezi kupangua hoja zangu nisijichoshe bure.

Inavyoonekana mimi ninajua zaidi kwamba kuleta ukombozi sio kazi ya kufumba na kufumbua zaidi yako, ndio maana namlaumu Maalim kwa kupoteza 5 precious years nje ya system ambayo ingemsaidia kuleta huo ukombozi. Ingekuwa rahisi zaidi kwake kuendelea kupigania maslahi ya Zanzibar akiwa kama makamo wa kwanza wa rais kuliko ilivyokuwa. Yaani kwa kifupi harakati zilibidi zisimame kwa miaka 5 ya thamani ya hali ya juu, na ndio maana namshauri this time asije akakubali kupoteza tena muda huo. Na pia Maalim ajue kwamba sio lazima yeye ahitimishe harakati hizi, inawezekana zikaja kuhitimishwa na mtu mwengine kabisa japo yeye ndio atakuwa ameweka misingi hiyo.
 
Duh! saamahani sana mkuu usiniwekee maneno kwenye kinywa changu. Tena samahani na ukiona inafaa unitake radhi, hakuna niliposema nimetoka upinzani ili nijinufaishe mimi na family yangu. asilan abadan!!!!!

Halafu siongelei hoja ya Maalim na ACT kutosusia uchaguzi, soma uelewe ndugu. Nimeongelea suala la kukubali kushindwa ikitokea "watangazaji wa matokeo" wamesema kashindwa. Inaonekana mkuu hujasoma vizuri mada.

"kususia uchaguzi wa Machi 2016 kwanza ilikuwa ni ujumbe kwa wale wanaojifanya wao ni baba la demokrasia duniani" hayo ni maandishi yako. Swali langu, ujumbe huo umesaidia nini??? Kwani wewe ulikuwa hujui the so-called baba la demokrasia duniani ni wanafiki tu?? Huoni kwamba hatua ile ya kususia uchaguzi umerudisha nyuma harakati za ukombozi wa kidemokrasia na sasa baada ya miaka mitano inabidi tuanze pale tulipoishia September 2015??

Sitaki kuamini eti maalim na wenzake walitaka kujiridhisha jumuiya ya kimataifa itafanya nini juu ya lile la Jecha, na kama ndivyo basi walipiga hesabu mbovu sana maana jumuiya ya kimataifa cha kwanza wanachoangalia ni maslahi yao tu. Maslahi yao yakiwepo they don't care who runs "The shithole" countries. As long as CCM assured them their interest to be met jumuiya ya kimataifa haitoingilia chochote popote pale and of all the people Maalim alitakiwa alijue hili.

Kuhusu Maalim kuandaa na kumtambulisha mtu, hii ni mada on its own, and again Maalim should learn from history. Unajua tatizo la ushia na usunni duniani?? Sisemi kwamba Mtumw Muhammad alikosea kutomuandaa na kumtambulisha mtangulizi wake laaa, ila viongozi wa sasa ambao sio mitume wanatakiwa wajifunze kitu hapa.
Mkuu kwanza samahani kama nimekukwaza.

Lakini nimefahamu mantiki ya kujiunga ccm imara, na mantiki ya wajibu wa kushughulikia zaidi familia kama kitu kimoja kwa muktadha wa stori. Sorry.

Hoja ya pili natofautiana kidogo. Unaposema Maalim Seif akubali kushindwa kwa lugha nyengine akubali kudhulumiwa na asisuse au kususia. Bado hoja ni ile ile.

Zanzibar inahitaji utashi kutoka pande zote. Maalim na wenzake wameonesha uthubutu muda wote na ndio ikapatikana miafaka zaidi ya 3.

Niliposema kususia kwa maalim na wenzake mwaka uchaguzi was marudio ilikuwa in kujenga new era ya kutaka kujiridhisha na kujenga credit ya kisiasa.

Ona Ccm walivyojichora hadi sasa na tazama siasa za Zanzibar zilivyogubikwa na kivuli cha uchaguzi wa marudio wa 2016.

Hio ni sayansi ya siasa. Unavuna nusu, unajenga imani, unavuta hisia za wadau na kummaliza mpinzani wako.

Maalim kawayumbisha ccm na dola kiasi cha kumfanyia figisu na mgogoro mkubwa Kyle CUF.

Bado tumpe nafasi na kumuamini.
 
Sisemi kwamba Mtumw Muhammad alikosea kutomuandaa na kumtambulisha mtangulizi wake laaa, ila viongozi wa sasa ambao sio mitume wanatakiwa wajifunze kitu hapa.
Sema astaghafiru Llah kwanza
Mtume huwa hafanyi mambo kwa utashi wake.
Maalimu si Mtume, yaweza kuwa hoja ya kumuanda mrithi wake ukawa sawa lakini si mtume.
 
Bado naamini kususia Kule( tuite kukubali kushindwa ) kulikuwa na mshauriano ya kimkakati ndani na nje ya nchi.

Katika hali ile ya kupatikana SUK mpya ndani ya miaka 5 ikavurugwa, suala la kugomea na kutokubali matokeo ni njia za kidemokrasia na kidiplomasia za kudai hatua nyengine. lazima kulikuwa na mashauriano Fulani.

Sidhani kama wamepoteza yote. Inawezekana kuna faida ambazo Mimi na wewe hatuzioni.
Muda ni shuhuda.
 
Sema astaghafiru Llah kwanza
Mtume huwa hafanyi mambo kwa utashi wake.
Maalimu si Mtume, yaweza kuwa hoja ya kumuanda mrithi wake ukawa sawa lakini si mtume.
Astaghfirullah llahu al adhwim, alladhi laa ilaha illa Llah, al hayyu al qayyum.

Nafurahi kukubaliana nami kwamba Maalim hajamuandaa na kumtambulisha mrithi wake na time is not on his side.
 
Mkuu kwanza samahani kama nimekukwaza.

Lakini nimefahamu mantiki ya kujiunga ccm imara, na mantiki ya wajibu wa kushughulikia zaidi familia kama kitu kimoja kwa muktadha wa stori. Sorry.

Hoja ya pili natofautiana kidogo. Unaposema Maalim Seif akubali kushindwa kwa lugha nyengine akubali kudhulumiwa na asisuse au kususia. Bado hoja ni ile ile.

Zanzibar inahitaji utashi kutoka pande zote. Maalim na wenzake wameonesha uthubutu muda wote na ndio ikapatikana miafaka zaidi ya 3.

Niliposema kususia kwa maalim na wenzake mwaka uchaguzi was marudio ilikuwa in kujenga new era ya kutaka kujiridhisha na kujenga credit ya kisiasa.

Ona Ccm walivyojichora hadi sasa na tazama siasa za Zanzibar zilivyogubikwa na kivuli cha uchaguzi wa marudio wa 2016.

Hio ni sayansi ya siasa. Unavuna nusu, unajenga imani, unavuta hisia za wadau na kummaliza mpinzani wako.

Maalim kawayumbisha ccm na dola kiasi cha kumfanyia figisu na mgogoro mkubwa Kyle CUF.

Bado tumpe nafasi na kumuamini.
Tuko pamoja mkuu.

Nakubaliana nawe mkuu kwamba Maalim ameifanyia Zanzibar ya kutosha, hata ukombozi wa kidemokrasia ukija ukipatikana basi histora haitomsahau Maalim kamwe, bila ya yeye kama yeye haya yasingewezekana. Kuwa na SUK ingekuwa ni ndoto tu ila leo tunayo na tunamshkuru kwa hilo.

Acha nikukubalie kwamba inawezekana Maalim na wenzake kususia uchaguzi wa Machi 2016 ilikuwa ni kwa ajili ya kujenga new era na kutaka kujiridhisha juu ya role ambayo "international community" ina play na sasa may be he knows better. May be pia ndio maana akatangaza mwaka huu akiibiwa hatowazuia vijana kudai haki yao. Nakubali usemayo maana sikufikiria hilo.

Mimi bado nampa nafasi, na ndio maana sijahauri amuachie mwengine agombee uchaguzi huu, ni kwa sababu naamini there is a better chance with him contesting than otherwise. Nimeshauri amuachie mwengine awe first vice president kama atashindwa/hatotangazwa ili kumtambulisha na kumuandaa vyema huyo atakaemuachia kwa uchaguzi wa 2025.

Nadhani unaelewa kwamba mimi na wewe sote tunajenga nyumba moja, hakuna haja ya kugombea fito. hahaha
 
Bado naamini kususia Kule( tuite kukubali kushindwa ) kulikuwa na mshauriano ya kimkakati ndani na nje ya nchi.

Katika hali ile ya kupatikana SUK mpya ndani ya miaka 5 ikavurugwa, suala la kugomea na kutokubali matokeo ni njia za kidemokrasia na kidiplomasia za kudai hatua nyengine. lazima kulikuwa na mashauriano Fulani.

Sidhani kama wamepoteza yote. Inawezekana kuna faida ambazo Mimi na wewe hatuzioni.
Muda ni shuhuda.
Acha tuamini hivyo, lakini tukubaliane kwamba mashauriano hayo yakimkakati hayakupigiwa hesabu vizuri.

Kama usemavyo ndugu, inawezekana kuna faida ambazo mimi na wewe hatuzioni.
 
Salaam kwenu wakuu,

Mimi sijihusishi na siasa za Tanzania kidhati ya moyo, nimekuwa ni mfuatiliaji tu wa namna mambo yanavyokwenda/yanavyoendeshwa ndani ya nchi yetu. Niliwahi kuwa mwanachama wa CUF Habari mwanzoni mwa miaka ya 2010 na kadi yangu nilipewa na Julius Mtatiro, hata hivyo nilihamia CCM imara muda mfupi baadae baada ya kugundua hakukuwa na upinzani Imara nchini kwetu. Maamuzi hayo yalichagizwa na ule msemo wa "if you can't beat them, join them". Fikra kuu ni ile fikra ya aliemtoa gerezani ndugu Nelson Mandela, President FW De Klerk na namna alivyofika kuwa pale.

Ila rasmi baada ya kesi maarufuu visiwani Zanzibar ya mwaka 2013 kuanza niliamua rasmi kuachana na mambo ya siasa na kujikita kwenye kushughulikia mambo yangu na familia yangu huku nikiamini ni mimi, na ni mimi tu ambae ningeweza kuikomboa familia yangu nyonge kutoka kwenye umaskini na wala sio wana-siasa.

Yakawa yaliyokuwa na uchaguzi wa mwaka 2015 ukafika, kwa vile wengine tulikuwa kiakili kabla ya ki-umri tukakaa pembeni na kuangalia mambo yatakavyokuwa. Muda wa kwenda kwenye mikutano ya kampeni tukatumia kuzalisha mali huku fikra zetu pevu zikituambia hata kama CUF watashinda uchaguzi basi hawatopewa nchi kuiongoza (na hivyo ndivyo ilivyokuwa).

Uchaguzi ukafanyika, Jecha akaufuta, Maalim akahangaika mpaka kwa wadhamini wa demokrasia (Ulaya na Marekani) lakini hakuna lililokuwa. Kijambo kilikuwa kipo, mpaka leo tumefikia tunaingia tena kwenye uchaguzi na "kijambo kimeyayuka". Hii kamwe haimaanishi kukejeli harakati za Maalim katika kupigania demokrasia Zanzibar au kupigania haki ya Wazanzibar la hasha! Napenda kutambua mchango mkubwa wa Mh. Maalim Seif Shariff Hamad katika harakati za demokrasia nchini Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Mafanikio yake ni makubwa mno na hata kama atafariki leo basi Maalim ataiaga dunia hii akiwa mshindi. Kuipata SUK Zanzibar si mafanikio ya kubeza hata kidogo.

Kwa jitihada tu za Maalim na timu yake, leo hii hata wanaoitwa "wapinzani" watakuwemo kwenye baraza la mawaziri la Serikali ya Zanzibar kuanzia November mwaka huu In Shaa Allah. Haya ni mafanikio makubwa sana ambao wanasiasa wa Tanganyika na sehemu nyengine nyingi za Afrika hawajaweza kuyafikia bila umwagaji damu.

Mbali ya mafanikio haya, yapo makosa makubwa sana ya ki-msingi ambayo Maalim pengine na chama waliyafanya ambayo yanagharimu harakati hizi za kiukombozi wa demokrasia Zanzibar na Tanzania kwa ujumla mpaka leo hii. Na hili ndilo lililonisukuma kuandika makala hii ili iwe funzo kwa Maalim na chama cha ACT Wazalendo katika uchaguzi huu ujao. Labda tu kwa uchache niainishe ninayoyaona makosa makuu aliyoyafanya maalim hapo mwaka 2015 au kabla ambayo sasa yanagharimu harakati za ukombozi wa kidemokrasia kama ifuatavyo

1) Kukataa kurudia uchaguzi wa Mwezi Machi 2016- Hili lilipelekea Baraza la wawakilishi kuwa na wawakilishi kutoka chama kimoja tu, na tumshukuru Mungu kwamba walibaki kuwa wazalendo kwa Zanzibar yao maana kwa hali ile wangeweza kupitisha sheria kandamizi dhidi ya vyama vya upinzani na Wazanibar kwa ujumla na kwenda kinyume na yote yale ambayo CUF kipindi hicho walijinasibu kuyapigania.

2) Kutoandaa na/au kumtambulisha mtu ambae angekuwa/atakuwa mrithi wake baada ya yeye kuondoka kwenye siasa kwa namna yoyote ile i.e kifo, afya, umri n.k

NOTE: Kwa wanaojua habari za siasa hususan za Zanzibar, wanaelewa kwamba hayo hapo juu ni makosa ambayo yanagharimu harakati za kidemokrasia Zanzibar mpaka leo.

USHAURI:

1) Uchaguzi una kushinda na kushindwa, halafu hapa Tanzania kuna kupewa na kutopewa. Imani ya wengi ni kwamba Maalim amekuwa akishinda kila chaguzi lakini hapewi na hakuna chochote kiwacho, hivyo sitakosea kusema anaweza akashinda mwaka huu na pia asipewe vile vile, ushauri wangu ni kwamba hata asipopewa basi akubali kushindwa huko na atengeneze SUK pamoja na CCM kama ilivyokuwa mwaka 2010. Hii itasaidia kufanya upinzani ushiriki katika kuwatumikia wananchi katika level nyengine kabisa na pia itatoa nafasi ya wapinzania ndani ya Zanzibar kuwa na nafasi nzuri ya kuwashawishi viongozi wengine watakaotoka CCM masuala yahusuyo Zanzibar kila itokeapo (naamini nimeeleweka).

Lazima safari hii wapinzania wakubali kushiriki kutengeneza serikali maana heri nusu shari kuliko shari kamili.

2) IKitokea upinzania umeshindwa au umeshinda halafu hawakupewa basi Maalim Seif Shariff Hamad na chama chake cha ACT Wazalendo wamteue mtu mwengine mbali na Maalim kuwa Makamu wa kwanza wa Rais. Hili nadhani katiba ya Zanzibar inaliruhusu. Hii itatoa nafasi kwa huyo mteuliwa Mfano Nassor Mazrui au rafik yangu Mh. Mansoor Himid kuandaliwa kwa kipindi cha miaka 5 ijayo ili aweze kuwa mgombea tofauti (na Maalim) kwa mara ya kwanza tangu siasa za vyama vinig zilipoanzishwa nchini (maana Maalim amekuwa mgombea wa upinzani tangu 1995 na ni hakika hatoweza kusimama tena majukwaani ifikapo 2025).

Maalim asikubali kujiaminisha kwamba ni yeye tu ndie ataweza kuwa Rais Zanzibar kutokea upinzani maana hilo litakuwa ni kosa kubwa na itaendelea kuwa dosari kama ilivyo dosari sasa hivi katika harakati hizi za ukombozi wa kidemokrasia.

Naamini Zitto kama kiongozi mkuu wa chama mtaufikiria ushauri huu na kuufanyia kazi.

NB: Kwa wale wana-CCM mnaofuata tu mkumbo, sisi wengine ni wanachama halali wa CCM na tuna kadi za chama kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Tumeamua tu kutumia akili zetu kufikiria.
mawazo yako sio mbaya lakini vipi yeye maalim ndie atuandaliye mtu wakushika nafasi yake huo ni umbumbu kwani kwani watu hawawezi kuchaguwa mtu anayeweza kuwaongoza lazima waandaliwe kwani yeye huyo maalim aliandaliwa na nani.
pili sahau kama mara hii watu watakubali upuuzi wa ccm wakufanya mapinduzi
 
Hivi ingekuwaje kama Maalim angekuwa kwenye SUK, halafu yakatokea haya ya kufukuzwa/kujitoa CUF na kuhamia ACT?
 
mawazo yako sio mbaya lakini vipi yeye maalim ndie atuandaliye mtu wakushika nafasi yake huo ni umbumbu kwani kwani watu hawawezi kuchaguwa mtu anayeweza kuwaongoza lazima waandaliwe kwani yeye huyo maalim aliandaliwa na nani.
pili sahau kama mara hii watu watakubali upuuzi wa ccm wakufanya mapinduzi
Hii nayo ni hoja mkuu.

Tena ni hoja fikirishi haswa, nimefaidika. Na huu ndio umuhimu wa mijadala.

Shukran sana mkuu
 
Back
Top Bottom