Ushauri kwa mliopo JKT wa kujitolea (WAZALENDO)

Ushauri kwa mliopo JKT wa kujitolea (WAZALENDO)

Aaah sio kweli...hapa bongo usalama ndo wanaongoza kwa mshahara na malupulupu
usiishi kwa kukalili... Jeshi wapo juu...na wana favor nyingi kuliko wote...inawezekana unapima uwezo wa mtu kwakuwa ni kiongozi huko USALAMA...

anzia posho za askari wa chini PRIVATE...​
 
Hongera kwa bandiko lako,hili bandiko lilifaa miaka iliyopita,kwa sasa inaanza connection hayo mengine ni baada ya message kuisha.Yote kwa yote wayazingatia haya uliyowaambia.
Uzalendo ilikuwa miaka hiyo sasa hivi tunasaka ajira,mtu amemaliza chuo ajira hakuna option iliyobaki ni jeshi,wazalendo wachache sana.
walau umenielewa... asante kwa appreciate yako...! japo ulicho kiandika ndio uhalisia...!​
 
Jeshini tulifundishwa Somo la ujanja wa porini, umuone adui kabla hajakuona na hapo unaruhusiwa Ata kutoroka kwenye kazi ila hakikisha hawajakuona, Sasa Kila kitu wewe unakuwa kimbelembele utasota Sana, na utajila na kujivuna Hadi uchakae
 
Hapana hujichagulii bali elimu yako na kipaji chako ndio itaamuwa pa kukupeleka...japo kuna muda huwa kuna amri za Lazima ikitokea uhitaji wawatu wenye ujuzi fulani.

Hivyo kitatafutwa kikundi cha watu wenye sifa na wasio na sifa ili wafanikishe hiyo kazi...!​
Nilikuja kulujua hilo baadae sana, binafsi nilikuwa napenda sana u sniper, nilikua nasema lazima nikikua nitaenda kuwa sniper kumbe najidanganya
 
Jeshini tulifundishwa Somo la ujanja wa porini, umuone adui kabla hajakuona na hapo unaruhusiwa Ata kutoroka kwenye kazi ila hakikisha hawajakuona, Sasa Kila kitu wewe unakuwa kimbelembele utasota Sana, na utajila na kujivuna Hadi uchakae
MMU huwezi kuiapply kwenye maisha harisi ya kambini ama mafunzoni...utapotea na awato kwambia kuwa umepotea...!​
 
Ndugu zangu kwanza niwapongeze sana kwa moyo wenu wa pekee wa kutamani kwa dhati kabisa kuitumikia nchi yetu richa ya JESHI LA KUJENGA TAIFA kujidhatiti dhahiri kuwa awatoi Ajira😭😭😭

Kitendo cha JKT kutoa Rai kuwa awatoi Ajira huo ni kama mchujo wa kwanza tunaita🤣🤣🤣🤣 kwa ambae hatolizika maana yake hato jiunga, kwa MZALENDO wa dhati atapiga hatua mbele bila kujali kuwa hato pata Ajira.

Ili uweze kufanikiwa JKT kuna vitu vichache ambavyo ukivizingatia huwezi kurudi nyumbani bila ajira.

Ieleweke kuwa mchujo wawatu watakao sajiliwa kwenye ajira huanzia pale utakapo karibishwa ndani ya kambi ya JKT uliyo pangiwa. vitu vingi uzingatiwa

i. Kwenda na muda ulio pangwa kuwasili kambini ukichelewa itakula kwako bora uwahi.

ii. Kuwa na vifaa vinavyo endana sawa sawa na ulivyo agizwa ili kuruka kiunzi hiki ni bora ukabeba pesa na kwenda kununua vifaa huko huko kambini uliko pangiwa. maduka yaliyopo jirani na kambi huwa na vifaa vyote vinavyo hitajika.

iii. Kutokubeba vitu vya ziada ambavyo hujaagizwa.

Baada ya kupokelewa kwenye kambi za JKT kuna makatazo na sheria za JKT mtasomewa na kueleweshwa hizo ni za kuzizingatia sana kwani ndio zitakazo waongoza maisha yenu yote ndani ya kambi.

ukifanikiwa kuruka kiunzi cha hapo juu bado utatakiwa kuyaishi maisha vizuri ndani ya kambi kama ifuatavyo.

1. UTIIFU unapo pangiwa kazi fanya kama mtumwa maliza kazi ya watu mapema huku mwili wako ukiwa teyari kusubiri order nyingine. USIONYESHE umechoka though ni kweli kuwa wewe sio mashine ila jifunze kumtumikia kafiri upate mradi wako.

2. SUBIRA kuna muda ndani ya kambi inaweza kutolewa order na afande tumwite Coplo kuwa msiondoke hadi atakapo rudi kwa kihere here baada ya masaa mengi kupita mkidhani amewasahau mnaamu kutawanyika😭😭😭 mchujo unaanzia hapo

3. NIDHAMU uoga na nidhamu ni vitu viwili tofauti askari yeyote anafundishwa ujasiri sio uoga. kutokana na sababu mbali mbali kwenye kambi za JKT kumekuwa na madalaja yamewekwa kati ya viongozi wa kati ndani ya kambi na viongozi waandamizi. viongozi wa Kati ambao ndio wapo field muda wote na Kuruta huwa awapendi sana KURUTA wasogelee au kuzoea sehemu za viongozi WAANDAMIZI jambo hili huwafanya KURUTA kuwa na uoga pindi wakutanapo na viongozi WAANDAMIZI.

Kuruta atashindwa hata kujieleza pindi akutanapo na kiongozi MUANDAMIZI ndani ya kambi. mimi nikuondoe hofu ukipata nafasi ukakutana na kiongozi MUANDAMIZI kambini usiogope kuzungumza nae kwa NIDHAMU. anaweza akaja Afande akakupiga bila sababu ama akakupa adhabu matharani ya kupiga push_up au kuibeba dunia fanya hiyo adhabu uliyo pewa bila manung'uniko na usijenge chuki na mkufunzi yeyote kambini hata kama ana kuonyesha chuki ya Wazi kabisa.
Ndani ya kambi mpende sana yule Afande atakae jitolea kukuchukia kwa kukupa adhabu, kukutukana, kukukejeli ama kukusimanga. Afande huyu ndie mwenye funguo za AJIRA yako.

Ila muogope sana AFANDE ambae ukifanya kosa atakufundisha namna ya kuchomoka kwenye hilo kosa bila kukupa Adhabu,

Muogope afande ambae anaweza akakuona unapita kwenye njia zisizo Rasmi {UNAJONGOMEA} na aka kuacha kama ajakuona...😭😭😭 huyu atakumaliza chini kwa chini na huto fika popote.

Ikitokea umekamatwa pengine ukawekwa mahabusu au umekutwa na kosa lolote lile ambalo limepelekea upewe adhabu hakikisha unaifanya hiyo adhabu bila kuonyesha kuwa umeonewa na baada ya kuimaliza hiyo adhabu kaa mbali na jambo lililokufanya upewe adhabu kifupi badilika ili ata yule alie kupa adhabu aone kuwa adhabu yake imekubadili tabia na kuwa mtu bora zaidi. usipo badilika watakuacha na utajipotezea muda bure.

Jitahidi sana kwenye roll call za usiku, siku za sikukuu ama Ijumaa, Jumaamosi na Jumaapili usikosekane. ukitokea mmepewa kazi nzito siku hiyo kimbilia kufanya hiyo kazi ama chochote kitakacho fanywa siku hizo hakikisha unashiriki.

✓ Muda wa kupumzika mkiwa mmechoka kweli kweli ghafra wakiitwa watu 20 pangeni foleni. piga ua gara gara hakikisha kwenye hilo kundi uwepo.

✓ Mkiwa kwenye starehe zenu akaja Afande akaomba askari 30 waende kumsaidia kushusha magunia ya mahindi jitahidi uwe miongoni mwa hilo kundi.

Hivyo ndivyo watu hupoteaga na wasionekane siku unakuja kukutana nae yupo kwenye msafara wa viongozi unabaki mdomo wazi🤭🤭🤭🤭

N.B
kwenye haya maisha yetu kitu ukikipenda sana hukipati.

hivyo jitahidi ukilipenda sana jeshi wakufunzi wako wasijue kwani wakijua kuwa wewe ni mfia jeshi possibility za kukosa huwa ni kubwa.

lipende jeshi ndani ya moyo sio nje ya moyo... ukilipenda nje ya moyo kila mtu atajua na huo ndio mwanzo wa kulikosa.

inajulikana kuwa WANAJESHI WA KWELI, WANAO LIPENDA JESHI KWA DHATI KABISA WAPO MITAANI, awajawahi kusajiliwa😭😭😭😭
Hello brother, nimatumaini yangu uko salama
Naomba niulize kuhusu JWTZ

1. NI LAZIMA UPITE JKT KWENDA JWTZ?
2. NI LAZIMA UKAE JKT MIAKA 2 NDIO UWEZE KWENDA JWTZ?
3. KIPINDI CHA KOZI YA JKT UNAWEZA PATA FURSA YA KUINGIA JWTZ ?
JE MINIMUM NI BAADA YA MDA GANI IZO FURSA ZA JWTZ HUANZA KUJA KAMBINI?
4. UKIPATA FURSA YA KUJIUNGA JWTZ UNAENDA MAFUNZO KWA MDA KIAS GANI?
5.BAADA YA KUPATA MAFUNZO YA AWALI JWTZ KWA KAWAIDA UNAKUA KWENYE LEVEL IPI YA JESHI?
6. UKIWA JWTZ UNAWEZA KWENDA KUSOMA NDANI AU NJE YA TANZANIA?
7. IF YES NI BAADA YA MDA GANI WA KUWA JWTZ UTAWEZA KUENDELEA NA MASOMO?
8. JWTZ UKIWA MASOMO BADO UTAINGIZIWA SALARY YAKO YA KILA MWEZI?

NI HAYO TU BROTHER KWA LEO
THANKS YOU IN ADVANCE!
 
Hello brother, nimatumaini yangu uko salama
Naomba niulize kuhusu JWTZ

1. NI LAZIMA UPITE JKT KWENDA JWTZ?
2. NI LAZIMA UKAE JKT MIAKA 2 NDIO UWEZE KWENDA JWTZ?
3. KIPINDI CHA KOZI YA JKT UNAWEZA PATA FURSA YA KUINGIA JWTZ ?
JE MINIMUM NI BAADA YA MDA GANI IZO FURSA ZA JWTZ HUANZA KUJA KAMBINI?
4. UKIPATA FURSA YA KUJIUNGA JWTZ UNAENDA MAFUNZO KWA MDA KIAS GANI?
5.BAADA YA KUPATA MAFUNZO YA AWALI JWTZ KWA KAWAIDA UNAKUA KWENYE LEVEL IPI YA JESHI?
6. UKIWA JWTZ UNAWEZA KWENDA KUSOMA NDANI AU NJE YA TANZANIA?
7. IF YES NI BAADA YA MDA GANI WA KUWA JWTZ UTAWEZA KUENDELEA NA MASOMO?
8. JWTZ UKIWA MASOMO BADO UTAINGIZIWA SALARY YAKO YA KILA MWEZI?

NI HAYO TU BROTHER KWA LEO
THANKS YOU IN ADVANCE!
ndugu yangu usikilizi hata vyombo vya habari🤣🤣🤣

1. bunge la mwaka huu limeamua kuondoa kigezo cha JKT kwenye ajira za majeshi yote. hivyo kupata usajili ndani ya JWTZ hakutegemei uwe na JKT.

2.Hapana... kigezo hiki kimepitwa na wakati kimetenguliwa na bunge.

3. Ndio unaweza kukutana na fursa kama ukibahatika kuingia Jkt fursa ikakukuta huko huko...hazina muda maalum japo ni mpaka pale kuruta wa JKT watakapo fuzu na kuwa service man/girl... muda wowote nafasi zikitoka unafanya interview ukibahatika unasajiliwa jeshini..!

4. mafunzo ya JWTZ huwa ni miezi 3. level za juniors kuna level 1,2 na 3... kila level inapigwa kwa muda wake tofauti ila mafunzo ya awali ni miezi 3 tu...!

5. unatambulika kama junior au private...!

6. ukisha sajiliwa jeshini sahau kuhusu safari za nje ya nchi... japo unaweza kwenda kusoma popote ulimwenguni kama jeshi likikutuma...! elimu unazoweza kusoma nje ya nchi ni elimu maalum za Jeshi...!

7. kusoma unasoma muda wowote endapo utakuwa na nafasi hiyo... maana kuna vitengo vinabana jeshini unaweza kujikuta unapata muda wa kulala tu ukiamka kazini🤣🤣🤣 hivyo ukiweza kukimbizana na muda wa kijeshi unaruhusiwa kusoma elimu za hapa hapa nchini kwa elimu zetu hizi za kiraia sijui, certificate, diploma, degree au master's...! japo jeshini napo kuna elimu zao... maalum ambazo huwezi kuzisoma kama wewe sio mwanajeshi...! mfano kurusha ndege za kivita... sayansi za kivita, sayansi ya utengenezaji wa silaha... elimu za kijeshi pia zina certificate, diploma, degree, masters na kuendelea usimuone mtu kawa mkuu wa Majeshi ukamchukulia poa...!

8. sijalielewa... ila kwa kifupi ukishasajiliwa hapo hapo unaanza kupata posho... hadi pale utakapo hitimu...!
 
Pamoja na kutokupenda kazi inayohusu mafunzo ya jeshi pia huwa sipendi kazi ya kumlinda mwenzangu hata kidogo.

Yaani nisifikirie kuzungukwa na walinzi nianze kupitia usumbufu woote huo eti ili nikamlinde mwenzangu (kuwa kwenye msafara)?
 
Pamoja na kutokupenda kazi inayohusu mafunzo ya jeshi pia huwa sipendi kazi ya kumlinda mwenzangu hata kidogo.

Yaani nisifikirie kuzungukwa na walinzi nianze kupitia usumbufu woote huo eti ili nikamlinde mwenzangu (kuwa kwenye msafara)?
sio kila unacho tarajia unakipata... maisha ni kama tairi... ni rahisi kuwa chini au juu ina tegemea mzinguko,🤭🤭🤭​
 
Back
Top Bottom