Ushauri kwa Rais: Ili kukuza uchumi wa nchi na kupata fedha za ujenzi wa miundombinu, Mishahara ya watumishi wa umma na viongozi wa kisiasa ipunguzwe

Hongera "mzarendo ",mimi beberu 😂😂😂
 
Hahaha [emoji23]


Mitano tena.

Unawatakia nini waajiriwa.?
 
Mkuu kwa nini usipendekeze wafanya kazi wote wapewe allowance tu.
Allowance za kwenda kazini na kula mchana na usiku tu.
China wameweza sisi je?
Kwani watu wanahitaji mishahara?
 
Kichaaa cha uchumi wa kati 😂
 
Kweli umaskini mbaya sana,,mkuu Kwa hiyo umeona laki tisa ni hela nyingi sana umefika hatua unasema ikatwe,,,"umaskini wako/wetu unaanzia vichwani mwetu" sina imani kama utaelewa nachotaka kumaanisha kama laki 9 unaona ni hela nyingi,,tchao
 
Sawa, umesahau kuweka no za simu mkuu
 

Kabisa. Na Botswana ni mfano mzuri sana katika hilo ulilolisema.
Ukiondoa Katiba mbovu kabisa tuliyonayo, shida kubwa nyingine ni hilo la ufanisi duni katika kutumia maliasili na mapato yatokanayo na uchimbwaji wake. Mikataba mibovu, rushwa na matumizi mabaya ya pesa zipatikanazo uchangia sana.
 
Pale mbumbumbu anapokuwa mshauri wauchumi. Sijui Kama unaelewa impact ya hicho unachokisema. Unajua tu hataimpact ya kuhamishia fedha zoteza serikali BOT kutoka benki binafsi ilivyoleta shida kiuchumi. Japo impact yake huwa haelezwi
 
Wewe kamshauri raisi wako atengeneze mazingira ya uwekezaji Hili investors wawe wengi na taxbase iwe kubwa hatimae hata revenue itaongezeka, na hatapata shida ni wapi pakutoa hela ya kununulia mandege na mabehewa ya treni za mwaka 47.
 
We nawe tahira
Badala ungeshauri hata serikali iwekeze nguvu zaidi katika kilimo na uzalishaji mazao ya viwango tuwe tunauza nchi za nje na kupata faida kukuza uchumi

Usikute hapo ulipo hata ajira yenyewe huna unanunuliwa vocha na dadako mfyuu
 
Ulichokiandika ni kizuri Lakini haujatafiti kwa kina kujua kwa nini imakuwa hivyo. Hakuna mshahara mkubwa Tanzania.

Labda nikueleze tu wanaongoza kulipwa hizo hela ni wabobezi wa masuala mbalimbali ambao serikali ama imewatoa ng'ambo kwenye mamilioni ya dola na kuwaleta kwenye visenti. Kama akina Bilali makamu wa Rais mstaafu, Akina Shein, Prof Muongo na wengineo. Ukiona wanalipwa hela nyingi kaifanye wewe kazi ile wanayofanya au tafuta watu watakaoweza kuifanya kwa pesa kidogo.
 
Uko sahihi mkuu
 
Nakubaliana nawe serikali kupunguza mishahara ya viongozi (wote wakisiasa na wasio wakisiasa) na watumishi wengine wanaopata nyingi 'husasani kwenye mataasisi'

Pia serikali ipunguze viwango 'rate' za posho (marupurupu)
Uko sahihi mkuu
 
Hizo huwa ni Siasa tu kwamba mtu ametolewa ng'ambo kuja kusaidia nchi. Siwezi kuamini kuwa hatuna wataalamu humu ndani hayo Ni mambo ya kupeana ulaji tu. Unataka kuniambia hakukuwa na watu wanaoweza kufanya zaidi ya alichokifanya Pro Muhongo? Kwanza ameletwa kuliibia taifa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…