Ushauri kwa serikali wa namna ya kudhibiti ukwepaji kodi bila kutumia mabavu.

Ushauri kwa serikali wa namna ya kudhibiti ukwepaji kodi bila kutumia mabavu.

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Mheshimiwa rais, natumaini unaendelea vema na majukumu yako ya kuongoza serikali.

Niende moja kwa moja kwenye ushauri wangu.

Tengeneza sera ya kubadili mfumo wa manunuzi nchini kuondoka kutoka kwenye matumizi ya cash na kuwa wa kieletroniki.

Na jambo hili lisifanyike kwa kutunga sheria ya kulazimisha watu wahamie, bali ziwekwe matisha za kuwashawishi walaji / wanunuzi kutumia zaidi mifumo ya kielectroniki.

Mfano;
  • Futa tozo zote kwenye miamala ya simu na mobile banking.
  • Ongea na mitandao ya simu na mabenki ili huduma ya kufanya malipo kwa kutumia kadi ya benki na mobile money ziwe bure kabisa.
  • Weka tax refund (kwa mfano 2% ya total VAT) kwa mwaka kwa wateja wote waliofanya malipo kwa njia ya kieletronic.

Baada ya miaka miwili mitatu nakuhakikishia mambo ya cash yatakuwa ni historia.

Ni kweli serikali itapoteza mapato kidogo kwa miaka michache lakini faida yake ni kubwa zaidi.

Ni vigumu sana kukwepa kodi na kudanganya mahesabu pale miamala inapofanyika kwa njia za kielectroniki tofauti na cash.

Hakutakuwa na haja ya TRA kwenda na polisi kukagua kama mfanyabiashara anatoa risiti au la, as long as anatumia account ya benk au mobile money kupokea malipo kutoka kwa wateja basi anaweza kukaguliwa 'remotely' bila mabavu.

Sijui ni nani alikupa ushauri wa kuweka tozo kwenye miamala lakini kaa ujue kuwa uwezo wa mtu huyo wa kufikiri na kupanga mipango ya muda mrefu sio mzuri. Huyo mtu ni mzigo ambao unapaswa kuutua.

Ni hayo tu, cashless market = easy tax collection.
 
Tusilazimishane , hii ni nchi huru . Kwanza wananchi hatupendi kutumia benki wala kufanya miamala mara kwa mara . Benki zitakufa .
 
Tusilazimishane , hii ni nchi huru . Kwanza wananchi hatupendi kutumia benki au kufanya miamala mara kwa mara .
Kama nilivyosema wasilazimishe bali waweke motisha.

Kwasasa kwenye kila unachonunua (bidhaa au hudumu) kuna VAT ya 18%.

Serikali inaweza kuamua kukurudishia 2% mwisho wa mwaka kama umefanya manunuzi hayo kielectroniki ili kuwavutia watu wahamie huko kwa hiyari yao.

Watu wasilazimishwe bali wapewe motisha ya kuachana na cash.
 
Cashless huu mfumo bado sana Africa.
Ulaya ukitoa cash wanakushangaa wanajua ametoka Africa huyu
Ni kweli, kule kila kitu na card tena wengi wanaunganisha na simu zao (apple pay na google pay) unasogeza tu simu yako mchezo umeisha.

Sisi huku tunayo nafasi ya kuzigeuza M-Pesa, tigo pesa N.K kuwa 'apple pay' na 'google pay' zetu. Serikali ikiacha tamaa za muda mfupi hizi mobile money zinaweza kutuvusha kabisa.
 
Google Pay yenyewe haipatikani Bongo, Google Wallet ila kwa wenzetu kama China na India hata muuaza Madafu mtaani ana Electronic Payment method Una Scan QR unalipa
 
Back
Top Bottom