Ushauri: Kwa Utawala huu je ni biashara gani inafaa na inalipa japo kidogo

Sigara Kali

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2017
Posts
3,623
Reaction score
8,442
Salaam wana jukwaa

Naomba mnijuze/kushauri je kwa utawala huu wa Magufuli ni biashara gani ukiifanya inaweza kukulipa hata kama sio kwa faida kubwa lakini mzunguko wa bidhaa unakua nzuri

Hasa maeneo ya Mwanza ni biashara ipi?

Mtaji kuanzia Laki 5.
 
Hamna biashara ya kuku shauri mkuu. Hao wanao kushauri uingie kwenye chakula kwa mtaji wa laki 5, ni fine mbili au tatu tu za USAFI WA JIJI/CHAKULA (Jamaa Wa Afya) inakula kwako. Wanazunguka hao kukagua VIBANDA UMIZA (Mama Ntilie) vya misosi, we sikia tu.[emoji18]
 
Kopesha laki laki watumishi wa umma wakulipe hata laki na 50 wanashida sana
 
Habari mkuu.

Pole na majukumu yako ya kila siku.

Kwanzasiafiki kama Magufuli ndiye sababu ya ugumu wa maisha, sababu ni sisi wenyewe kutokuwa tayari kuendana na mabadiliko.

Nikija katika point, biashara ya kuifanya ili upate faida.

Anza na biashara ambayo ni lazima upate wateja, namaanisha nini? Angalia hapa chini.
  • Chakula
  • Urembo
  • Madawa
Hizo ni baadhi ya niche ambazo haziwezi kukosa wateja piga uwa galagaza.

Sasa unaweza ukaamua kuanzisha mgawa, au ukawa unasafirisha nafaka kutoka maeneo ya kijijini na kuziuza kwa faida maeneo ya hapo mjini.

Usisahau kujifunza jinsi ya kuuza.

Maulid njema.
 
Kuhusu urembo watu wanakopa sanaaa alafu kulipa n kwa mafungu usiangalia mtaji unakata.
 
Biashara inayolipa sana kwa utawala huu ni kuwa dalali wa kununua wabunge na madiwani wa upinzani mkuu!
 
Kwa mtaji wako anzisha Biashara ya mihogo ya kukaanga, tena biashara yako uiegeshe karibu na shule hizi za kata.
 
Salaam wana jukwaa

Naomba mnijuze/kushauri je kwa utawala huu wa Magufuli ni biashara gani ukiifanya inaweza kukulipa hata kama sio kwa faida kubwa lakini mzunguko wa bidhaa unakua nzuri

Hasa maeneo ya Mwanza ni biashara ipi?

Mtaji kuanzia Laki 5.

kuna sehemu nchii zina itaji huduma za vitu vingi.sema watu tumekalili waitaji wa huduma wapo mijini tu
 
Salaam wana jukwaa

Naomba mnijuze/kushauri je kwa utawala huu wa Magufuli ni biashara gani ukiifanya inaweza kukulipa hata kama sio kwa faida kubwa lakini mzunguko wa bidhaa unakua nzuri

Hasa maeneo ya Mwanza ni biashara ipi?

Mtaji kuanzia Laki 5.
Kwani ulikuwa unawaza kufanya biashara gani mpiga dili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…