Ushauri kwa waandaaji wa maandamano na waandamanaji tarehe 23/09/2024

Ushauri kwa waandaaji wa maandamano na waandamanaji tarehe 23/09/2024

1. What are the Motives for the demonstration?
2. What are the Goals that planned to be achieved at the end of the demonstration? What are the targets?

Inavyoonekana huko CHADEMA hakuna wataalamu au wanamikakati wazuri wa kuweza kupanga mambo Kama haya. Mambo mengi inavyoonekana huwa yanafanyika tu kiholela tena kwa kukurupuka bila ya kuwa na mpango dhabiti kwanza.
Mnapaswa kuwa wabunifu kwa kufanya kwanza utafiti wa kina, upembuzi yakinifu wa kina na Kisha mpange mipango na ajenda zenu vizuri zaidi ndipo mje kwa wananchi kuomba support yao ili waweze kuunga mkono mipango yenu na ajenda zenu. Mje kwa Wananchi mkiwa na Hoja zenye mashiko zinazogusa maslahi mapana zaidi ya umma, kwa kufanya hivyo, wananchi watajikuta wanalazimika kuwaunga mkono bila ya kulazimishwa. Hata kama Polisi watajaribu kuhujumu mipango yenu kwa Namba yoyote ile, automatically na wao watajikuta wanashindwa kuwahujumu kwa sababu kitendo cha kujaribu kuhujumu mipango yenu itakuwa ni kuwahujumu wananchi au kuanzisha vita dhidi ya wananchi.

Mimi binafsi nawashauri nyinyi Watu wa CHADEMA kwamba mjipange sawasawa kabla ya kuanzisha Jambo fulani, msiwenakurupuka.
Mwisho tambueni kwamba: Unapotaka kufanya Uamuzi wa Kudumu ni lazima uzingatie sababu za kudumu.
Na wewe ndiye wale wale tu.

Cdm waje na hoja gani kubwa kuliko hii ya kupinga mauaji na teka teka ya watu yanayofanywa na vyombo vya dola?

Ina maana wewe mpaka leo haujui logic ya kile Cdm wamekilenga pamoja na kauli mbiu yao?

Ni nani sasa awatetee raia wasio na mtetezi?

Kama raia hawataki kutetewa hawawezi kulazimishwa, isipokuwa Cdm itakuwa imetimiza wajibu na majukumu yake kwa raia.

Wanastahili kupewa shime na si kuvunjwa moyo.
 
Kutokana na vitisho vinavyotolewa na polisi dhidi ya haki za wananchi kutimiza haki zao kikatiba, ni wazi polisi wanaweza kuumiza watu hata kuua kwa kisingizio cha kuzuia maandamano.

Nashauri waandaaji wa maandamano kuandaa media coverage kubwa sana hasa kwa upande wa picha mnato na picha mwendo yaani video kwa kila tukio watakalolifanya polisi iwe hadharani au sirini.

Kamera za siri na vinasa sauti viwe vingi kukusanya ushahidi wa uhalifu unaotegemewa kitendwa na dola kama ule uliofanyika Mbeya. Waandamanaji wote nao simu zao kamera ziwe on kurekodi kila tukio la uvunjifu wa amani utakaofanywa na wenye mabavuna kisha kuliweka wazi ikitokea wahalifu wakaruka kimanga.

Kuandamana ni kutembea. Ninyi polisi shida iko wapi watu wakiachwa watembee huku wakiimba na kulia? Kunahitajika akili na busara badala ya mabavu.

Soma Pia: Freeman Mbowe: Tutaandamana kudai watu waliopotea
Naunga mkono na KUKAZIA.

Pia napendekeza, pamoja na ugumu wa kuwepo kwa utulivu wakati wa vitisho; ni muhimu waandamanaji waepuke kukimbia kimbia hovyo hovyo bila ya mpangilio. Katika hali ya vurugu ya namna hiyo ndipo mauaji hufanywa na wauaji wasijulikane.

Polisi anapo tishia, simama au kaa chini kwa utulivu. Shikamaneni kama kundi. Waache wao waonekane wakifanya uhalifu waziwazi.
 
Na wewe ndiye wale wale tu.

Cdm waje na hoja gani kubwa kuliko hii ya kupinga mauaji na teka teka ya watu yanayofanywa na vyombo vya dola?

Ina maana wewe mpaka leo haujuiclogic ya kile Cdm wamekilenga pamoja na kauli mbiu yao?

Ni nani sasa awatetee raia wasio na mtetezi?

Kama raia hawataki kutetewa hawawezi kulazimishwa, isipokuwa Cdm itakuwa imetimiza wajibu na majukumu yake kwa raia.

Wanastahili kupewa shime na si kuvunjwa moyo.
1. Kwa hiyo unataka kusema kwamba kufanya maandamano ndio guarantee ya kwamba vitendo vya utekaji havitaweza kufanyika tena hapa Tanzania??
2. Je, unajua Nini hasa kiini cha kujirudia rudia vitendo hivi vya utekaji hapa Tanzania?? Do you know the root cause of this tragedy of kidnapping or abduction?????
3. Je, umeshawahi kujiuliza ni kwa nini hao Watekaji hadi leo wako huru uraiani licha ya kwamba tayari wameshatekeleza matukio mengi Sana ya utekaji na mauaji hapa nchini?

Kwa taarifa yako: Hao Watekaji, Watesaji na Wauaji huwa wanapongezwa na kupandishwa vyeo mara tu baada ya kutekeleza vizuri hayo matukio ya utekaji ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na Watu wengi hapa nchini.

NOTE:
Ukitaka kuua mti Basi yakupasa lazima kuchimbua mizizi yote ya mti huo, Wala usikate matawi yake tu kwani ipo siku matawi hayo lazima yatachipua tena.

Aidha, muda wote unapotaka kufanya Uamuzi wa kudumu ni lazima uzingatie sababu za kudumu.
 
1. Kwa hiyo unataka kusema kwamba kufanya maandamano ndio guarantee ya kwamba vitendo vya utekaji havitaweza kufanyika tena hapa Tanzania??
2. Je, unajua Nini hasa kiini cha kujirudia rudia vitendo hivi vya utekaji hapa Tanzania?? Do you know the root cause of this tragedy of kidnapping or abduction?????
3. Je, umeshawahi kujiuliza ni kwa nini hao Watekaji hadi leo wako huru uraiani licha ya kwamba tayari wameshatekeleza matukio mengi Sana ya utekaji na mauaji hapa nchini?

Kwa taarifa yako: Hao Watekaji, Watesaji na Wauaji huwa wanapongezwa na kupandishwa vyeo mara tu baada ya kutekeleza vizuri hayo matukio ya utekaji ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na Watu wengi hapa nchini.

NOTE:
Ukitaka kuua mti Basi yakupasa lazima kuchimbua mizizi yote ya mti huo, Wala usikate matawi yake tu kwani ipo siku matawi hayo lazima yatachipua tena.
Inasikitisha kwamba unajiandikia lolote linalo kuijia kichwani bila ya kutafakari.

Wewe hapo ulipo unaona CHADEMA ni vichaa kupanga maandamano bila ya sababu na malengo maalum?

Wewe unafikiri kuitisha maandamano ni jambo rahisi tu; kama mchezo mchezo tu?
Hata kama hujawahi kusikia lolote wanalo lalamikia CHADEMA, kwa nini usichukue muda kidogo kudadisi sababu zinazo wafanya waitishe maandamano!

Hata hiyo "NOTE" yako pia inaonyesha usivyo juwa kitu. Hata sayansi ya mimea huna hata chembe yake!

Sasa wewe ni kitu gani hasa unacho uelewa nacho?
 
Kwa hivyo ndio unataka kusema mzizi ni naniliu?, hivyo Chadema wa deal na naniliu na sio hayo matawi?.
P
Tatizo liko kwenye jamii. 1. Kwa washika tonge kuahirisha kufikiri kizalendo a.k.a kujizima data. 2.Jamii hadi mafuvu yarudishiwe akili zitarudi baada ya kukumbana, (kukabiliana) na changamoto nyingi. Changamoto, (uncertainty), husababishwa na majanga asilia na binadamu, Nionavyo mimi changamoto nyingi tunazo kumbana nazo, husababishwa na binadamu, huwasababishia wengine changamoto kwa makusudi ama kwa kutokujua, pia kwake mwenyewe kwa uzembe, uvivu, ujinga na ushamba
 
Sidhani kama POLISI itafanya vitendo vya kikatili kwa watu wanao andamana kwa amani kudao madai ya kutafutwa watekeji, kwakuwa hata hao POLISI ni Raia wa nchi pia wao hawapendi watu watekwe na kuuwa kwani baadhi ni ndugu zao rafiki zao majirani zao
Mkuu Jafe, Japhet gombe , ni kweli, na hii imewahi kutokea huko nyuma, Jeshi la polisi likifanya vyema, lipongezwe, hongera FFU kusambaratisha maandamano bila virungu, mabomu ya machozi, risasi za moto, bila maafa! na niliwahi kuwasisitiza hawa polisi wetu Ombi Muhimu Kwa Jeshi Letu La Polisi."Nyinyi ni Wenzetu, September Mosi, Please Msigeuke Makaburu!" na kwenye kusambaratisha maandamano kwa vurungu, mabomu ya machozi, maji ya washawasha na risasi za moto, nilishauri Je, Polisi washitakiwe kusababisha vifo kizembe vya random shootout? RIP Aqulina Akwilini, Baftaha, She is an Angel!
P
 
Inasikitisha kwamba unajiandikia lolote linalo kuijia kichwani bila ya kutafakari.

Wewe hapo ulipo unaona CHADEMA ni vichaa kupanga maandamano bila ya sababu na malengo maalum?

Wewe unafikiri kuitisha maandamano ni jambo rahisi tu; kama mchezo mchezo tu?
Hata kama hujawahi kusikia lolote wanalo lalamikia CHADEMA, kwa nini usichukue muda kidogo kudadisi sababu zinazo wafanya waitishe maandamano!

Hata hiyo "NOTE" yako pia inaonyesha usivyo juwa kitu. Hata sayansi ya mimea huna hata chembe yake!

Sasa wewe ni kitu gani hasa unacho uelewa nacho?
Don't think that I'm among of the people with the short-sighted mind.

Kwa taarifa yako, CHADEMA wanaweza wakawa na nia njema kabisa ya kutaka kufika mahali fulani, isipokuwa tatizo ambalo walilonalo ni kwamba wamekuwa wanakosea kupita kwenye njia sahihi ya kuweza kuwafikisha huko wanakotaka kwenda, they lack the right strategies to reach at their intended destination. Maandamano yenye positive impacts kwa jamii ni yale tu ambayo yamepangwa vizuri na kuratibiwa vizuri.

Narudia tena kusisitiza kwamba, muda wote unapotaka kufanya uamuzi wa kudumu basi ni lazima uzingatie sababu za kudumu.
 
1. Kwa hiyo unataka kusema kwamba kufanya maandamano ndio guarantee ya kwamba vitendo vya utekaji havitaweza kufanyika tena hapa Tanzania??
2. Je, unajua Nini hasa kiini cha kujirudia rudia vitendo hivi vya utekaji hapa Tanzania?? Do you know the root cause of this tragedy of kidnapping or abduction?????
3. Je, umeshawahi kujiuliza ni kwa nini hao Watekaji hadi leo wako huru uraiani licha ya kwamba tayari wameshatekeleza matukio mengi Sana ya utekaji na mauaji hapa nchini?

Kwa taarifa yako: Hao Watekaji, Watesaji na Wauaji huwa wanapongezwa na kupandishwa vyeo mara tu baada ya kutekeleza vizuri hayo matukio ya utekaji ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na Watu wengi hapa nchini.

NOTE:
Ukitaka kuua mti Basi yakupasa lazima kuchimbua mizizi yote ya mti huo, Wala usikate matawi yake tu kwani ipo siku matawi hayo lazima yatachipua tena.

Aidha, muda wote unapotaka kufanya Uamuzi wa kudumu ni lazima uzingatie sababu za kudumu.
Una mawazo mazuri.

Naomba sasa muongozo wako katika mantiki ya hoja yako, nini kifanyike katika kuhakikisha Serikali inafuata katiba na sheria na si kuikojolea?

Cdm wanawakilisha mawazo ya raia waliochoshwa na vitendo hivyo viovu vinavyofanywa na Dola.
 
Una mawazo mazuri.

Naomba sasa muongozo wako katika mantiki ya hoja yako, nini kifanyike katika kuhakikisha Serikali inafuata katiba na sheria na si kuikojolea?

Cdm wanawakilisha mawazo ya raia waliochoshwa na vitendo hivyo viovu vinavyofanywa na Dola.
Je, ulisoma vizuri na kuelewa comments zangu hizi:-

COMMENT YA KWANZA:-

1. What are the Motives for the demonstration?
2. What are the Goals that planned to be achieved at the end of the demonstration? What are the targets?

Inavyoonekana huko CHADEMA hakuna wataalamu au wanamikakati wazuri wa kuweza kupanga mambo Kama haya. Mambo mengi inavyoonekana huwa yanafanyika tu kiholela tena kwa kukurupuka bila ya kuwa na mpango dhabiti kwanza.
Mnapaswa kuwa wabunifu kwa kufanya kwanza utafiti wa kina, upembuzi yakinifu wa kina na Kisha mpange mipango na ajenda zenu vizuri zaidi ndipo mje kwa wananchi kuomba support yao ili waweze kuunga mkono mipango yenu na ajenda zenu. Mje kwa Wananchi mkiwa na Hoja zenye mashiko zinazogusa maslahi mapana zaidi ya umma, kwa kufanya hivyo, wananchi watajikuta wanalazimika kuwaunga mkono bila ya kulazimishwa. Hata kama Polisi watajaribu kuhujumu mipango yenu kwa Namna yoyote ile, automatically na wao watajikuta wanashindwa kuwahujumu kwa sababu kitendo cha kujaribu kuhujumu mipango yenu itakuwa ni kuwahujumu wananchi au kuanzisha vita dhidi ya wananchi.

Mimi binafsi nawashauri nyinyi Watu wa CHADEMA kwamba mjipange sawasawa kabla ya kuanzisha Jambo fulani, msiwe mnakurupuka.
Mwisho tambueni kwamba: Unapotaka kufanya Uamuzi wa Kudumu ni lazima uzingatie sababu za kudumu.

COMMENT YA PILI:-

Kwa taarifa yako, CHADEMA wanaweza wakawa na nia njema kabisa ya kutaka kufika mahali fulani, isipokuwa tatizo ambalo walilonalo ni kwamba wamekuwa wanakosea kupita kwenye njia sahihi ya kuweza kuwafikisha huko wanakotaka kwenda, they lack the right strategies to reach at their intended destination. Maandamano yenye positive impacts kwa jamii ni yale tu ambayo yamepangwa vizuri na kuratibiwa vizuri.

Narudia tena kusisitiza kwamba, muda wote unapotaka kufanya uamuzi wa kudumu basi ni lazima uzingatie sababu za kudumu.
 
Back
Top Bottom