Ushauri kwa wizara ya elimu ifute adhabu ya viboko kuwanusuru walimu na wanafunzi

Ushauri kwa wizara ya elimu ifute adhabu ya viboko kuwanusuru walimu na wanafunzi

Kazi ni nyingi shuleni unaweza kumpa adhabu ya kufanya usafi eneo fulani kwa siku ama zaidi ya siku moja kulingana na ukubwa wa kosa.

Kumwagilia maua maji na kutunza bustani ni miongoni mwa adhabu ambazo mwanafunzi ataona ni kubwa zaidi na atajiepusha na kutenda makosa akihofia kufanya kazi hizo.

Adhabu za viboko ni urithi wa kipumbavu tulioachiwa na wakoloni na sisi tukaendelea kufanyiana Waafrika wakati hao walioiasisi wala hawaitumii kwao.

Afrika ni laana wakati mwingine maana hatuna muda wa kujiuliza na kutafakari badala yake ni kuiga tu vitu tulivyokuta tunafanyiwa na wakoloni. Too pathetic.
Wewe ndo unasema ni mtetezi wa haki za binadamu na unapendekeza badala ya mwanafunzi kupewa "adhabu" apewe "kazi"?

Kwanza kabisa unatakiwa ujue kutofautisha "adhabu" na "kazi". Kumwagilia maua, kutunza bustani, kufanya usafi si adhabu bali ni shughuli ambazo inabidi watoto wafundishwe kuzipenda na kuzithamini

Kazi kama hizo zikigeuzwa kuwa adhabu maana yake ni kuwajenga kisaikolojia watoto waamini wanaofanya kazi hizo wanaadhibiwa kwa makosa fulani fulani. Ukiwa naakili timamu utanielewa nachokisema hapa

Adhabu kwa mujibu wa kamusi ya kiswahili ni "mateso anayopata mtu kwa lengo la kumrekebisha kutokana na makosa aliyofanya". Tuwazoeshe watoto kuwa kufanya usafi ni mateso? Kutunza bustani ni mateso?

Nabaki kuishauri serikali kupitia wizara ya elimu kufanya tathimini upya ya adhabu ya viboko itakayopelekea kufuta adhabu hiyo shuleni lakini pamoja na ushauri huo sioni kama kutunza bustani, kufanya usafi ni mbadala wake
 
Kuna muongozo wa adhabu mashuleni, mwalimu asipouzingatia unaweza muingiza hatiani.
Lakini pia na Walimu waangalie upande wa pili wa maisha yao, mtoto akikosea na akastahili adhabu,mwalimu aite mzazi wa mtoto aje amalizane na mtoto wake.
 
Mtumwa huyu hapa anayeamini fimbo ni suluhisho.

Fimbo haijawahi kuwa suluhisho la utukutu wa mtoto bali humfanya azidi kuwa mtukutu.

Wapo waliosoma shule ambazo hazitoi adhabu ya viboko wapo vizuri mno kimaadili hadi kimasomo.

Binafsi nimeitwa shuleni kwa kosa alilofanya mwanafunzi namna wanavyodili naye kumpa nasaha mbele ya mzazi unakuta mtoto anabadilika anakuwa mwema na hapo hajaguswa hata kiboko kimoja.

Ushoga ni tabia ya mtu haina uhusiano na mtoto kuchapwa ama lah.

Wewe unaonekana dhahiri ni mwalimu hivyo usipobadilika mwenyewe basi utabadilishwa na mkono wa sheria endapo mtoto ataumia hata kwa jeraha dogo tu tutakupeleka mahakamani kwa kosa la kujeruhi.

Natoa ushauri kwa walimu waachane na adhabu hizi za kikoloni maana mwisho wake ni mbaya jamii na serikali watakushambulia hadi unaingia jela.
Unakumbuka kuna mwaka dogo mmoja alihojiwa tu na walimu akaenda kujinyonga bado walimu wakaandamwa kwa hilo!!! Pendekezeni suruhu ya kudumu,
 
Unaonekana umelelewa na mama wa kambo umekulia bakora ndiyo maana umeathirika kisaikolojia.

Acha kuwadanganya walimu wenzako watajiingiza kwenye mtego wapoteze ajira na waishie gerezani kizembe sana.

Mimi ni mmoja wa wadau wa kutetea haki za binadamu nimekuwa nikizunguka maeneo tofauti tunapopata taarifa za mwalimu kumshambulia mtoto na kwakweli binafsi nimeshiriki kuhakikisha walimu kadhaa wamefungwa kwa kutofuata sheria na muongozo wa utoaji adhabu mashuleni.

Huwa najitolea bure kabisa ili mradi kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa kikamilifu.

Walimu wasipoacha kwa hiyari yao kuchapa watoto bila utaratibu basi their final destination ni jela.
Suruhu ni kuwa wafundishe tu mengine waachane nayo maana likitokea tatizo lolote mwl ni kutukanwa tu
 
Kifaa kinachotumika ni fimbo ambayo bila kutarajia inaweza kusababisha jeraha hasa ikipasuka na kipande cha fimbo kuchana sehemu ya mkono au bila kutarajia fimbo ikagusa sehemu ya kidole kikavimba hasa kwa wenye ngozi laini

Ikumbukwe kuwa, mtoto akishakuwa na jeraha au uvimbe ni vigumu jamii kuelewa kwasababu wao "focus" yao itakuwa kwenye jeraha au uvimbe hata kama alichapwa fimbo moja tu!

Kitu kingine kinachonishawishi kushauri tamko la kufuta hii adhabu ni pale linapotokea tatizo kwa mwanafunzi kuumizwa, hakuna anayekumbuka kuangalia dhamira ya Mwalimu iliyomsukuma kutoa adhabu aliyotoa

Kuna watu nimeona wameshauri kuwa adhabu mbadala kama kumwagilia maua, kufyeka, kulima, kufanya usafi, nk zitolewe kwa wanafunzi wanaofanya makosa. Hawa wamesahau kuwa hizi shughuli hazipaswi kupandikizwa vichwani kwa watoto kama adhabu badala yake wanatakiwa kujengewa mazingira ya kupenda shughuli za mikono kwani mbeleni zinaweza kuwa msaada kwao

Adhabu ni tendo analofanyiwa mtu kumuonywa kufanya jambo baya. Kwa maana nyingine tendo hilo lazima liwe la kuumiza au kumnyima mtu uhuru au haki fulani kwasababu amevunja sheria. Tukiwazoesha watoto kuwa kumwagilia maua ni kazi za wenye makosa tutakuwa tunatengeneza jamii ya aina gani?

Kuna shule moja mtoto alipoteza maisha kwa kuangukiwa na jiwe wakati wanachimba kifusi, wahusika wa shule ile waliyopitia wanayajua. Kuna shule watoto walikutwa wanazimbu chemba za choo zilizoziba (kwa matumizi yao mabaya), bado ilionekana walimu wamekosea

Mbaya zaidi anayependekeza watoto wapewe adhabu za kumwagilia maua au kufanya usafi anajiita "mtetezi wa haki za binadamu". Yaani kwake kufanya usafi anataka iwe adhabu isiwe kazi ya kawaida na ya kuwajenga watoto wapende kufanya usafi

Mimi nadhani adhabu ndogo ndogo zinawezakuwa kama kupigishwa magoti bila kujali kwa muda gani kulingana na kosa, kukalishwa chini, kunyimwa fursa zinazopatikana shuleni kama kufungiwa kushiriki michezo (kama ni mwanamichezo), kuzuiliwa kushiriki masomo kwa kipindi fulani (suspension), na wenye makosa makubwa kufukuzwa shule kama ilivyo kwa sasa

Nashauri adhabu ya fimbo ifutwe lakini mbadala wake haiwezi kuwa shughuli za mikono kwasababu "adhabu" ni tendo la kumuonya mtu hivyo tendo hilo lazima liwe lisilo la kawaida
Yaani umpe adhabu ya kulima mtt wa mkulima [emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Kifaa kinachotumika ni fimbo ambayo bila kutarajia inaweza kusababisha jeraha hasa ikipasuka na kipande cha fimbo kuchana sehemu ya mkono au bila kutarajia fimbo ikagusa sehemu ya kidole kikavimba hasa kwa wenye ngozi laini

Ikumbukwe kuwa, mtoto akishakuwa na jeraha au uvimbe ni vigumu jamii kuelewa kwasababu wao "focus" yao itakuwa kwenye jeraha au uvimbe hata kama alichapwa fimbo moja tu!

Kitu kingine kinachonishawishi kushauri tamko la kufuta hii adhabu ni pale linapotokea tatizo kwa mwanafunzi kuumizwa, hakuna anayekumbuka kuangalia dhamira ya Mwalimu iliyomsukuma kutoa adhabu aliyotoa

Kuna watu nimeona wameshauri kuwa adhabu mbadala kama kumwagilia maua, kufyeka, kulima, kufanya usafi, nk zitolewe kwa wanafunzi wanaofanya makosa. Hawa wamesahau kuwa hizi shughuli hazipaswi kupandikizwa vichwani kwa watoto kama adhabu badala yake wanatakiwa kujengewa mazingira ya kupenda shughuli za mikono kwani mbeleni zinaweza kuwa msaada kwao

Adhabu ni tendo analofanyiwa mtu kumuonywa kufanya jambo baya. Kwa maana nyingine tendo hilo lazima liwe la kuumiza au kumnyima mtu uhuru au haki fulani kwasababu amevunja sheria. Tukiwazoesha watoto kuwa kumwagilia maua ni kazi za wenye makosa tutakuwa tunatengeneza jamii ya aina gani?

Kuna shule moja mtoto alipoteza maisha kwa kuangukiwa na jiwe wakati wanachimba kifusi, wahusika wa shule ile waliyopitia wanayajua. Kuna shule watoto walikutwa wanazimbu chemba za choo zilizoziba (kwa matumizi yao mabaya), bado ilionekana walimu wamekosea

Mbaya zaidi anayependekeza watoto wapewe adhabu za kumwagilia maua au kufanya usafi anajiita "mtetezi wa haki za binadamu". Yaani kwake kufanya usafi anataka iwe adhabu isiwe kazi ya kawaida na ya kuwajenga watoto wapende kufanya usafi

Mimi nadhani adhabu ndogo ndogo zinawezakuwa kama kupigishwa magoti bila kujali kwa muda gani kulingana na kosa, kukalishwa chini, kunyimwa fursa zinazopatikana shuleni kama kufungiwa kushiriki michezo (kama ni mwanamichezo), kuzuiliwa kushiriki masomo kwa kipindi fulani (suspension), na wenye makosa makubwa kufukuzwa shule kama ilivyo kwa sasa

Nashauri adhabu ya fimbo ifutwe lakini mbadala wake haiwezi kuwa shughuli za mikono kwasababu "adhabu" ni tendo la kumuonya mtu hivyo tendo hilo lazima liwe lisilo la kawaida
Kama wale madogo walichomaga mabweni kipndi cha Magu wangepewa adhabu ya kumwagilia maua sio!??? [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Viboko visifutwe. Sisi wenyewe tulichapwa sana lakini still wengi wetu bado stupid. Watu weusi hawana akili, usipowachapa utotoni ndio watakuwa more stupid. Muhimu kuwe na idadi ya viboko
 
Si kweli kwamba walimu wanaotoa adhabu ya viboko ni "empty". Huo ni mtazamo wako na kukosa uzoefu wa kushughulika na tabia za watoto / vijana wanaokua. Kuna wazazi pia wanachapa watoto wao nyumbani nao ni "empty"! Serikali hadi leo imeshikwa na kigugumiza kufuta kabisa adhabu ya viboko shuleni nao tuseme wako "empty" lakini unataka wewe unayejiita "mtetezi wa haki za binadamu" ambao mnatetea hadi zile haki za "kishetani" ndo tuone mna akili. Hapo umepuyanga.

Itoshe kusema adhabu ya viboko inatakiwa kufanyiwa tathimini upya lakini si kweli kwamba wanaoitekeleza hawana akili.
Wewe utakuwa pia empty kichwani mwalimu. Mbona sisi wengine tumesoma shule ambazo mambo ya viboko hakuna na watu wanafaulu kwa ufaulu wa juu kabisa.

Narudia tena, ukiona mwalimu anapenda kutoa adhabu kwa watoto basi huyo ni empty kichwani hivyo anatumia ukali kama defense.

Usibishe mwalimu. Huu ni utafiti rasmi tumekuwa tukitembelea shule mbalimbali na kuongea na watu mbalimbali hivyo matokeo ya utafiti mdogo yanaonesha walimu wasiojihusisha na kutoa adhabu wanapendwa na wanafunzi na masomo wanayofundisha yanaeleweka sana.
 
Wewe ndo unasema ni mtetezi wa haki za binadamu na unapendekeza badala ya mwanafunzi kupewa "adhabu" apewe "kazi"?

Kwanza kabisa unatakiwa ujue kutofautisha "adhabu" na "kazi". Kumwagilia maua, kutunza bustani, kufanya usafi si adhabu bali ni shughuli ambazo inabidi watoto wafundishwe kuzipenda na kuzithamini

Kazi kama hizo zikigeuzwa kuwa adhabu maana yake ni kuwajenga kisaikolojia watoto waamini wanaofanya kazi hizo wanaadhibiwa kwa makosa fulani fulani. Ukiwa naakili timamu utanielewa nachokisema hapa

Adhabu kwa mujibu wa kamusi ya kiswahili ni "mateso anayopata mtu kwa lengo la kumrekebisha kutokana na makosa aliyofanya". Tuwazoeshe watoto kuwa kufanya usafi ni mateso? Kutunza bustani ni mateso?

Nabaki kuishauri serikali kupitia wizara ya elimu kufanya tathimini upya ya adhabu ya viboko itakayopelekea kufuta adhabu hiyo shuleni lakini pamoja na ushauri huo sioni kama kutunza bustani, kufanya usafi ni mbadala wake
Kumbe umeelewa ila unajifanya kichwa ngumu.

Kama lengo ni kuondoa adhabu basi kuwafundisha watoto kazi kama kumwagilia maua na usafi wa mazingira ya shule ni jambo jema kabisa.
 
Suruhu ni kuwa wafundishe tu mengine waachane nayo maana likitokea tatizo lolote mwl ni kutukanwa tu
Mwalimu anayejitambua hawezi kuhangaika na kutoa adhabu bali atajikita kwenye kufundisha tu hayo mengine atawaachia wazazi.

Maana ukijifanya una hasira za kuwaadhibu watoto mwisho wa siku jamii yote inakuandama pale ambapo mtoto atapatwa na jambo lolote baya litokanalo na adhabu ya mwalimu.

Kwani mwalimu akifundisha bila kutoa adhabu huwa wanakatwa mshahara?
 
Kama wale madogo walichomaga mabweni kipndi cha Magu wangepewa adhabu ya kumwagilia maua sio!??? [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Ndio adhabu inayopendekezwa na mtetezi wa haki za binadamu. Yeye anazunguka kujitolea walimu wafungwe kwa kutoa adhabu
 
Wewe utakuwa pia empty kichwani mwalimu. Mbona sisi wengine tumesoma shule ambazo mambo ya viboko hakuna na watu wanafaulu kwa ufaulu wa juu kabisa.

Narudia tena, ukiona mwalimu anapenda kutoa adhabu kwa watoto basi huyo ni empty kichwani hivyo anatumia ukali kama defense.

Usibishe mwalimu. Huu ni utafiti rasmi tumekuwa tukitembelea shule mbalimbali na kuongea na watu mbalimbali hivyo matokeo ya utafiti mdogo yanaonesha walimu wasiojihusisha na kutoa adhabu wanapendwa na wanafunzi na masomo wanayofundisha yanaeleweka sana.
Bahati mbaya uliyonayo ni kwamba hujui hata unachoandika. Hujui kwamba hata kwenye hizo shule unazosema wanafunzi wanachapwa sio wanafunzi wote wanachapwa bali wale wenye makosa ndio hupewa adhabu. Ndani ya shule hizo hizo ambazo bado zina utaratibu wa adhabu ya viboko kwasababu serikali haijatamka kufuta adhabu hiyo wapo wanafunzi wanaanza na kumaliza shule bila kupigwa fimbo hata moja. Tatizo umekuja kwenye hoja yangu kimuhemuko sana bila kuwa na hoja ndani yako.

Ni kama hapo ulipo unahasira ambazo ulikosa pa kuzipeleka sasa umeona uzilete hapa pasipo kuwa na hoja ndani yako

Serikali ipo na jamii ipo inaangalia na bahati nzuri siku hizi kuna hizi media za kidigitali zinafikisha habari kirahisi sana kwenye jamii. Usijifanye una akili sana kuliko hao wanaosita sita kufuta adhabu hii kabla hawajapata mbadala wake kwasababu wao ndio hufanya tafiti zinazohusiana na tabia za watoto hasa wanapokuwa shuleni. Wewe unahemuka tu lakini huna unachokifahamu

Akili zako (unazodai kwamba unazo) zinaamini kwamba kazi ya mwalimu ni kufundisha somo lake basi. Kwamba mwalimu hahusiki na malezi, kuhakikisha mtoto anakua katika maadili mema. Kwako wewe Mwalimu anatakiwa ashughulike na somo lake tu bila kujali watoto wanavuta bangi, "wanafanyana" shuleni, wanajihusisha na ukahaba, umalaya, wizi, uhuni, wanakuja muda na siku wanazotaka shuleni, wanavaa wanavyotaka wao, lugha za matusi zimewajaa mdomoni, na tabia nyingine chafu chafu sio kazi ya mwalimu kushughulika nazo. Mwalimu akiacha kushughulika na haya yote hiyo itakuwa shule? Taifa litakuwa na watu wa aina gani?

Hujui kuwa wapo watu wamejua kuvaa vizuri kwasababu ya shule? Hujui kuwa kuna watu shule zimewarekebisha kutoka kwenye hali ya uchokoraa na sasa ni watu wazuri na raia wema wa nchi hii? Hujui kwamba kuna watu wametoka familia za makahaba, wavuta bangi, na wenye kila aina ya tabia za "kiswazi" lakini kupitia shule hizi hizi sasa hivi ni watu wa maana katika jamii?

Kabla ya kusema mwalimu ashughulike na somo lake tu mengine amuachie mzazi inabidi ujiulize kama lengo la kuwa na walimu shuleni ni kufundisha masomo tu. Huo ni mtazamo wa mtu asiyejua chochote kuhusu elimu kwa mapana yake

Kwa akili zako serikali au shule binafsi imemuajiri mwalimu kufundisha masomo kama Physics, chemistry, Mathematics na kadhalika basi?

Kasome wajibu wa mwalimu kwanza halafu ndio utajua nani ni "empty mind" kama sio wewe
 
Viboko visifutwe. Sisi wenyewe tulichapwa sana lakini still wengi wetu bado stupid. Watu weusi hawana akili, usipowachapa utotoni ndio watakuwa more stupid. Muhimu kuwe na idadi ya viboko
Viboko vifutwe kwa kuwa vimeshapitwa na wakati, zama zinabadilika. Kuhusu mtu kutumia akili yake vizuri ni suala la mfumo wa elimu na bidii ya mtu kutafuta maarifa ila viboko haihisiani na kumpa mtu akili.
 
Bahati mbaya uliyonayo ni kwamba hujui hata unachoandika. Hujui kwamba hata kwenye hizo shule unazosema wanafunzi wanachapwa sio wanafunzi wote wanachapwa bali wale wenye makosa ndio hupewa adhabu. Ndani ya shule hizo hizo ambazo bado zina utaratibu wa adhabu ya viboko kwasababu serikali haijatamka kufuta adhabu hiyo wapo wanafunzi wanaanza na kumaliza shule bila kupigwa fimbo hata moja. Tatizo umekuja kwenye hoja yangu kimuhemuko sana bila kuwa na hoja ndani yako.

Ni kama hapo ulipo unahasira ambazo ulikosa pa kuzipeleka sasa umeona uzilete hapa pasipo kuwa na hoja ndani yako

Serikali ipo na jamii ipo inaangalia na bahati nzuri siku hizi kuna hizi media za kidigitali zinafikisha habari kirahisi sana kwenye jamii. Usijifanye una akili sana kuliko hao wanaosita sita kufuta adhabu hii kabla hawajapata mbadala wake kwasababu wao ndio hufanya tafiti zinazohusiana na tabia za watoto hasa wanapokuwa shuleni. Wewe unahemuka tu lakini huna unachokifahamu

Akili zako (unazodai kwamba unazo) zinaamini kwamba kazi ya mwalimu ni kufundisha somo lake basi. Kwamba mwalimu hahusiki na malezi, kuhakikisha mtoto anakua katika maadili mema. Kwako wewe Mwalimu anatakiwa ashughulike na somo lake tu bila kujali watoto wanavuta bangi, "wanafanyana" shuleni, wanajihusisha na ukahaba, umalaya, wizi, uhuni, wanakuja muda na siku wanazotaka shuleni, wanavaa wanavyotaka wao, lugha za matusi zimewajaa mdomoni, na tabia nyingine chafu chafu sio kazi ya mwalimu kushughulika nazo. Mwalimu akiacha kushughulika na haya yote hiyo itakuwa shule? Taifa litakuwa na watu wa aina gani?

Hujui kuwa wapo watu wamejua kuvaa vizuri kwasababu ya shule? Hujui kuwa kuna watu shule zimewarekebisha kutoka kwenye hali ya uchokoraa na sasa ni watu wazuri na raia wema wa nchi hii? Hujui kwamba kuna watu wametoka familia za makahaba, wavuta bangi, na wenye kila aina ya tabia za "kiswazi" lakini kupitia shule hizi hizi sasa hivi ni watu wa maana katika jamii?

Kabla ya kusema mwalimu ashughulike na somo lake tu mengine amuachie mzazi inabidi ujiulize kama lengo la kuwa na walimu shuleni ni kufundisha masomo tu. Huo ni mtazamo wa mtu asiyejua chochote kuhusu elimu kwa mapana yake

Kwa akili zako serikali au shule binafsi imemuajiri mwalimu kufundisha masomo kama Physics, chemistry, Mathematics na kadhalika basi?

Kasome wajibu wa mwalimu kwanza halafu ndio utajua nani ni "empty mind" kama sio wewe
Gazeti reeefu halafu mashudu matupu.

Nimekuuliza, mwalimu asipochapa mtoto mshahara unapungua?

Ni dhahiri walimu wanaoadhibu watoto mara nyingi wana stress za kimaisha hilo limethibitishwa hata na wao wenyewe kwasababu tunao marafiki huko.

Hayo malezi unayozungumzia ukatafsiri ni kuchapa watoto?

Ufinyu wako wa uelewa ndiyo maana ulienda kusomea ualimu baada ya alama zako kutokukuruhusu kusoma kozi zingine.

Walimu wachache wanaojitambua wameacha biashara ya kuchapa watoto wamejikita kufundisha maana wameshtukia mtego linapotokea jambo baya jamii, viongozi wa serikali na wanasiasa wote wanawashambulia mwisho wa siku unapoteza kibarua kizembe sana.

Kusikia kwa kenge hadi damu zimtoke masikioni. Endelea kuchapa watoto lipo linalokusubiri utakuja kujuta.
 
Viboko vifutwe kwa kuwa vimeshapitwa na wakati, zama zinabadilika. Kuhusu mtu kutumia akili yake vizuri ni suala la mfumo wa elimu na bidii ya mtu kutafuta maarifa ila viboko haihisiani na kumpa mtu akili.
Sahihi kabisa mkuu.

Yaani kuna vitu tunaiga tu kutoka kwa wakoloni ambao walitu treat kama mnyama pori kutandikwa bakora.

Malezi ya viboko hayajawahi kuwa suluhisho kwa binadamu yeyote sana sana utamjengea mtu usugu.

Ukiona mtu anaunga mkono adhabu za viboko ujue huyo ni muathirika wa malezi ya bakora kuanzia kwenye familia yake.

Binafsi sijui kumshikia mwanangu fimbo lakini kauli yoyote ninayoitoa mtoto anafanya jambo nililomwagiza fasta na wananiheshimu sana kwakuwa nimewafanya kuwa marafiki zangu wa karibu.
 
Sahihi kabisa mkuu.

Yaani kuna vitu tunaiga tu kutoka kwa wakoloni ambao walitu treat kama mnyama pori kutandikwa bakora.

Malezi ya viboko hayajawahi kuwa suluhisho kwa binadamu yeyote sana sana utamjengea mtu usugu.

Ukiona mtu anaunga mkono adhabu za viboko ujue huyo ni muathirika wa malezi ya bakora kuanzia kwenye familia yake.

Binafsi sijui kumshikia mwanangu fimbo lakini kauli yoyote ninayoitoa mtoto anafanya jambo nililomwagiza fasta na wananiheshimu sana kwakuwa nimewafanya kuwa marafiki zangu wa karibu.
Tatizo wazazi wengi wa Bongo wanashindwa kutofautisha pale ambapo mtoto anamheshimu au anamuogopa. Wazazi wengi wanaochapa watoto wanadhani watoto wao wanawaheshimu kumbe wanawaogopa matokeo yake mtoto akianza kujitegemea anafanya mambo ya hovyo.
 
Tatizo wazazi wengi wa Bongo wanashindwa kutofautisha pale ambapo mtoto anamheshimu au anamuogopa. Wazazi wengi wanaochapa watoto wanadhani watoto wao wanawaheshimu kumbe wanawaogopa matokeo yake mtoto akianza kujitegemea anafanya mambo ya hovyo.
Sahihi kabisa mkuu.

Mtoto anapaswa kumheshimu mzazi na sio kumuogopa.

Kuna raha mtoto na mzazi kuwa na urafiki hapo lazima familia itakuwa na utulivu na maelewano.
 
Gazeti reeefu halafu mashudu matupu.

Nimekuuliza, mwalimu asipochapa mtoto mshahara unapungua?

Ni dhahiri walimu wanaoadhibu watoto mara nyingi wana stress za kimaisha hilo limethibitishwa hata na wao wenyewe kwasababu tunao marafiki huko.

Hayo malezi unayozungumzia ukatafsiri ni kuchapa watoto?

Ufinyu wako wa uelewa ndiyo maana ulienda kusomea ualimu baada ya alama zako kutokukuruhusu kusoma kozi zingine.

Walimu wachache wanaojitambua wameacha biashara ya kuchapa watoto wamejikita kufundisha maana wameshtukia mtego linapotokea jambo baya jamii, viongozi wa serikali na wanasiasa wote wanawashambulia mwisho wa siku unapoteza kibarua kizembe sana.

Kusikia kwa kenge hadi damu zimtoke masikioni. Endelea kuchapa watoto lipo linalokusubiri utakuja kujuta.
Watu kama wewe ni hasara kwa familia. Kitu pekee nachoweza kukiona kwako yawezekana najibishana na mtu aliyejaa stress za maisha na pengine ni "under age" kwasababu unatabia zote zinazoashiria hivyo.

Hata hujishughulishi kujua mjadala huu nimeunzisha kwa lengo gani umekazana tu kuongea upuuzi na kufunua matope yaliyojaa kichwani mwako.

Hao walimu wamejiamulia tu kutoa adhabu hiyo ya viboko? Msingi wa hoja yangu ni kuishauri serikali kufuta kisheria adhabu ya viboko na kuweka utaratibu mwingine, badala ya kuja na hoja unageuka kushambulia walimu na taaluma ya ualimu kana kwamba wao ndio walitunga sheria hiyo kama sio utaahira ni nini.
 
Back
Top Bottom