Ushauri kwa wizara ya elimu ifute adhabu ya viboko kuwanusuru walimu na wanafunzi

Ushauri kwa wizara ya elimu ifute adhabu ya viboko kuwanusuru walimu na wanafunzi

Viboko visifutwe. Sisi wenyewe tulichapwa sana lakini still wengi wetu bado stupid. Watu weusi hawana akili, usipowachapa utotoni ndio watakuwa more stupid. Muhimu kuwe na idadi ya viboko
Umelifanyia taifa kipi? Uwa nashangaa kizazi chetu kujisifu tulichapwa sana halafu hamna impact yoyote kwenye jamii zaidi ya uchawa.

Kizazi cha kina Nyerere au Kambona ndio wahoji uhalali wa viboko sio wewe unaejisikia fahari kuwa mtumwa

Kizazi chenyewe hiki chenye magonjwa yasiyoyakuambukiza hata kwa watoto wenye u18, maticha mtaua wengi
 
Watu kama wewe ni hasara kwa familia. Kitu pekee nachoweza kukiona kwako yawezekana najibishana na mtu aliyejaa stress za maisha na pengine ni "under age" kwasababu unatabia zote zinazoashiria hivyo.

Hata hujishughulishi kujua mjadala huu nimeunzisha kwa lengo gani umekazana tu kuongea upuuzi na kufunua matope yaliyojaa kichwani mwako.

Hao walimu wamejiamulia tu kutoa adhabu hiyo ya viboko? Msingi wa hoja yangu ni kuishauri serikali kufuta kisheria adhabu ya viboko na kuweka utaratibu mwingine, badala ya kuja na hoja unageuka kushambulia walimu na taaluma ya ualimu kana kwamba wao ndio walitunga sheria hiyo kama sio utaahira ni nini.
Ndio umeongea nini sasa?😅
 
Kifaa kinachotumika ni fimbo ambayo bila kutarajia inaweza kusababisha jeraha hasa ikipasuka na kipande cha fimbo kuchana sehemu ya mkono au bila kutarajia fimbo ikagusa sehemu ya kidole kikavimba hasa kwa wenye ngozi laini

Ikumbukwe kuwa, mtoto akishakuwa na jeraha au uvimbe ni vigumu jamii kuelewa kwasababu wao "focus" yao itakuwa kwenye jeraha au uvimbe hata kama alichapwa fimbo moja tu!

Kitu kingine kinachonishawishi kushauri tamko la kufuta hii adhabu ni pale linapotokea tatizo kwa mwanafunzi kuumizwa, hakuna anayekumbuka kuangalia dhamira ya Mwalimu iliyomsukuma kutoa adhabu aliyotoa

Kuna watu nimeona wameshauri kuwa adhabu mbadala kama kumwagilia maua, kufyeka, kulima, kufanya usafi, nk zitolewe kwa wanafunzi wanaofanya makosa. Hawa wamesahau kuwa hizi shughuli hazipaswi kupandikizwa vichwani kwa watoto kama adhabu badala yake wanatakiwa kujengewa mazingira ya kupenda shughuli za mikono kwani mbeleni zinaweza kuwa msaada kwao

Adhabu ni tendo analofanyiwa mtu kumuonywa kufanya jambo baya. Kwa maana nyingine tendo hilo lazima liwe la kuumiza au kumnyima mtu uhuru au haki fulani kwasababu amevunja sheria. Tukiwazoesha watoto kuwa kumwagilia maua ni kazi za wenye makosa tutakuwa tunatengeneza jamii ya aina gani?

Kuna shule moja mtoto alipoteza maisha kwa kuangukiwa na jiwe wakati wanachimba kifusi, wahusika wa shule ile waliyopitia wanayajua. Kuna shule watoto walikutwa wanazimbu chemba za choo zilizoziba (kwa matumizi yao mabaya), bado ilionekana walimu wamekosea

Mbaya zaidi anayependekeza watoto wapewe adhabu za kumwagilia maua au kufanya usafi anajiita "mtetezi wa haki za binadamu". Yaani kwake kufanya usafi anataka iwe adhabu isiwe kazi ya kawaida na ya kuwajenga watoto wapende kufanya usafi

Mimi nadhani adhabu ndogo ndogo zinawezakuwa kama kupigishwa magoti bila kujali kwa muda gani kulingana na kosa, kukalishwa chini, kunyimwa fursa zinazopatikana shuleni kama kufungiwa kushiriki michezo (kama ni mwanamichezo), kuzuiliwa kushiriki masomo kwa kipindi fulani (suspension), na wenye makosa makubwa kufukuzwa shule kama ilivyo kwa sasa

Nashauri adhabu ya fimbo ifutwe lakini mbadala wake haiwezi kuwa shughuli za mikono kwasababu "adhabu" ni tendo la kumuonya mtu hivyo tendo hilo lazima liwe lisilo la kawaida
Nimekuelewa mkuu.

Uko sahihi.
 
Mbadala wa viboko ni kutoa coment sahihi kwenye cheti cha mwamafunzi juu ya tabia yake.
Kama amekuwa na tabia mbovu coments hizo zionekane hadharani
 
Kazi ni nyingi shuleni unaweza kumpa adhabu ya kufanya usafi eneo fulani kwa siku ama zaidi ya siku moja kulingana na ukubwa wa kosa.

Kumwagilia maua maji na kutunza bustani ni miongoni mwa adhabu ambazo mwanafunzi ataona ni kubwa zaidi na atajiepusha na kutenda makosa akihofia kufanya kazi hizo.

Adhabu za viboko ni urithi wa kipumbavu tulioachiwa na wakoloni na sisi tukaendelea kufanyiana Waafrika wakati hao walioiasisi wala hawaitumii kwao.

Afrika ni laana wakati mwingine maana hatuna muda wa kujiuliza na kutafakari badala yake ni kuiga tu vitu tulivyokuta tunafanyiwa na wakoloni. Too pathetic.
Hizo kazi za mbadala unaweza mpa na akazigomea na akupa na tusi la kutosha huku akimalizia na neno hutonifanya chochote
 
Hizo kazi za mbadala unaweza mpa na akazigomea na akupa na tusi la kutosha huku akimalizia na neno hutonifanya chochote
uko sahihi kabisa, kuna watu haya mambo hawayajui. Kuna kazi kubwa sana kulea vijana waliotoka katika malezi tofauti tofauti
 
Back
Top Bottom