USHAURI: Kwako Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu

Umeeleza vema mkuu,lkn ujinga wangu uko wapi?
Kwenye hoja zako No. 1 & 2 ambazo unamshauri TL juu ya;

1. UTATUZI WA MATATIZO YA JAMII.
Watanzania wanapenda kutatuliwa matatizo katika jamii, hawataki kujua aliyeyaleta au kuwasababishia.


2. USITUMIE MUDA MWINGI KUMLAUMU MAGUFULI, HILI WATANZANIA WANALIJUA VIZURI KWA SASA.
tunaenda kuingia kwenye uchaguzi mkuu tukiwa na katiba hii tuliyonayo je asigombee mpaka ipatikane katiba mpya?
Tundu Lissu hapiganii katiba mpya kwa ajili ya tukio moja la uchaguzi wa 2024 na 2025 au ili apate uongozi tu i.e mbunge au Rais. Bali anaipenda Tanzania na Watanzania bila kujali yeye ni kiongozi wa nchi hii ama la.

Tundu Lissu ni mtu anayependa kuona haki inatamalaki ktk jamii ya Kitanzania. Na haki haiwezi kuja kama mifumo ya utoaji haki na utawala iko compromised..

Hapa ndipo unaposhindwa na pengine ulivyoshindwa kumwelewa Tundu Lissu mpaka sasa!!
na ili ashinde anahitaji kura,anahtaji ushawishi kwa jamii unafkri kila mmja anawaza kama unavowaza wewe?
Ni makosa kuishawishi jamii kilaghai ili ikuchague tu uwe kiongozi huku ukijua unayoahidi huwezi kuya - accomplish..

Hivi ndivyo CCM ilivyolaghai na kudanganya Watanzania kwa takribani miaka 60+ ikitoa ahadi kibao ambazo ilishashindwa kuzitekeleza tangu uhuru. Mwisho imeshakuwa mazoea na utamaduni tu kuishi ktk uongo na ulaghai wa ki - CCM..

Kwa Tundu Lissu haiko hivyo ndugu yangu Myfriend . Tundu Lissu agenda yake kuu ni kujenga mfumo mpya wa kisiasa na kiutawala Tanzania unaozingatia sheria na katiba kwa kuhakikisha nchi hii inapata katiba mpya na bora ya kutusimamia ktk shughuli zetu za kiasiasa, kiuchumi, kiutawala na kijamii...

Ni kweli kabisa kuwa, kama mwanasiasa kwenda kwenye "siasa za uchaguzi" na agenda hii pekee is too risky. Maana hutaeleweka kirahisi kwa watu waliozoeshwa kupewa vitu vidogodogo kama khanga, tisheti, sukari, pombe kama hongo ili wawachague viongozi wabovu, wajinga na wezi na wasio na nia njema na watu wa nchi hii..

Tundu Lissu si mwanasiasa laghai ambaye mission yake ni kupata uongozi tu kwa gharama yoyote ikiwemo kudanganya kwa nia ya kupata nafasi za kisiasa serikalini ili kupata fursa ya kuiba mali ya umma tu na kushibisha tumbo lake..

I therefore advice you to do your homework very properly about this guy.

Once you've finished, utagundua kuwa Tundu Lissu is a truthfully and honest politician for more than 95% ambaye nia yake ni kui -transform Tanzania kuwa nchi mpya na ya haki tofauti na wanasiasa walio wengi selfish wa Tanzania ambao wao huitumia siasa kutafuta kula tu..

Tundu Lissu huwaambiaga watu ukweli mtupu kuwa, kama nchi hii inataka kupiga hatua za haraka za maendeleo ya uchumi na kijamii, basi sharti ni lazima kujenga upya mfumo wa kisiasa, kiutawala na kisheria wa nchi hii uliokwisha kuharibiwa na CCM kwa miaka takribani 60+

Agenda ya namna hizi☝️☝️☝️ktk siasa za Tanzania ni ngumu sana ndugu yangu Myfriend. Hii zi agenda za uchaguzi tu. Hizi ni agenda za kisiasa zinazolenga kuleta mabadiliko (transformation) katika jamii na ni endelevu na ikishaeleweka, mlipuko wake hakuna wa kuuzuia...!
Anyways mm nltoa ushauri wangu lkn inawezekana angle yangu ya jicho la pili si sahihi sana
Nauheshimu ushauri wako. Na don't take me wrong dear Myfriend. My contra - opinions do not intend to offend you..

Na sio kwamba uko wrong 100%. Isipokuwa kuna maeneo kadhaa ya ushauri wako yana make sense. Lakini yaliyo mengi ni senseless na ni kwa sababu humwelewi au hujamfahamu vya kutosha TL...

Mathalani;

1. Ni makosa makubwa kumfananisha TL na Magufuli. Hawa wawili wako tafauti kama giza lilivyo tafauti na nuru..!!

2. Ni makosa makubwa kumshauri TL atumie njia za "ki - populist" kama za Magufuli zilizokuwa zimejaa hila na ulaghai ndani yake za eti kujifanya kutatua matatizo ya jamii temporarily huku akiacha njia sahihi na za kudumu za kutatua changamoto ktk jamii ya watu..

3. Ni makosa makubwa kufikiri kwamba unaweza kutatua tatizo fulani ktk jamii bila kwanza kutafuta chanzo (cause) ya tatizo hilo. Kama wewe ulifundishwa hivyo katika mapito yako ya kumtafuta elimu, basi bila shaka ulikuwa na walimu wa hovyo sana..!!

Mfano, hivi wewe kwa akili yako unadhani oppositions wataachaje kuwaambia watu jinsi ya kutatua matatizo yao ya kiuchumi na kijamii ktk nchi hii yaliyosababishwa na utawala mbovu wa CCM wa takribani miaka 60+ bila kuitaja CCM na viongozi wake kuanzia Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na sasa huyu mama Samia..?

Bila kufanya hivi, wewe utakuwa mwanasiasa mjinga na mpumbavu kabisa na utakuwa huielewi siasa na jinsi inavyochezwa..!!
kama wewe ni miongoni mwa washauri wake basi chukua option ya pili ya kuudharau na kuupuuza tu huu ushauri
Ya kudharauliwa na kupuuzwa yamedharauliwa na yameshapuuzwa wala huhitaji kusema lolote. Na yanayo make sense ktk ushauri wako bila shaka yako appreciated wala usiwe na wasiwasi...

Kwa hiyo usiwe na hofu kabisa kutoa maoni yako kwa mara nyingine. Na zaidi sana mimi si mshauri wa Tundu Lissu. Mimi ni kama wewe tu yaani mfuatiliaji wa siasa za Bongo na wanasiasa wake...

Kwa hili nadhani tunaweza kukubaliana katika jambo moja kuwa, Tundu Lissu is among the best politicians from the opposition parties...!!
 
Ery, uko sahihi, ila kwa sasa huyo mtu hayupo. Ukimtajataja marehemu, kwa ujinga na kwa mila zetu Waafrika, hawachelewi kukubambikizia. Kuwa wewe ndo ulihusika.
Una point ya msingi, ila, tumsaifie TL namna nzuri ya kufikisha ujumbe bila kumtaja mtu hasa kwa "JINA"
 

Kwamba?

1. Watanzania wanapenda kutatuliwa matatizo katika jamii, hawataki kujua aliyeyaleta au kuwasababishia. 🀣🀣

2. USITUMIE MUDA MWINGI KUMLAUMU MAGUFULI, HILI WATANZANIA WANALIJUA VIZURI KWA SASA. 🀣🀣

3. Watanzania wengi wanajua hukutendewa haki,ulionewa na halkuwa jambo jema kabisa kushambuliwa lakin kwa sasa wanawaza sana matatizo. 🀣🀣

Mkuu huu ungeita ushauri toka jamhuri ya chattle.

Pia ungeweza kufaa kwenye comedy!
 
Hongera. Thread ya aina hii nimeisubiri muda mrefu, imeibua hisia za wengi.
Nasema hivi, endapo CHADEMA watachukua ushauri huu, na kurekebisha mambo madogo madogo kama ya kina Mdee na wenzake, 2025 Rais ni ATL. Sina shaka na hilo.
Niongeze mawili:
1. Kikokotoo kipya cha mafao ya Watumishi. Hiki ni kichimba kaburi kwa wastaafu. Wastaafu wanakufa kwa kuacha laana kubwa kwa nchi hii. It is a big shame, mtu akufanyie kazi hadi miaka 60, leo anastaafu,unaanza kumpangia namna ya kutumia akiba yake. Kama kuna laana kubwa ambayo serikali itaipata ni kupitia hawa wazee wetu wastaafu. TL, jikite hapo pia. Ninajua ulipokuwa mbunge pamoja na wenzako hamkukubali hilo jambo. Anzieni hapo.
2. Hakikisha unakirudisha Chama kilipokuwa ukiwa Mbunge, muda huu kabla ya Uchaguzi. Hili la Dada zenu kina Mdee,liangalieni kwa jicho la kipekee. Wanaoshabikia wafukuzwe chamani hawana nia njema. Hata hivyo, mkirithia wafukuzwe, sawa, ila wakiomba kurudi, waonyeni muendelee. Muda ni mfupi sana uliobakia kwenza 2025 na kabla,huu wa 2024 wa S/ mitaa.
3. Simamia Chama piga marufuku wanaowashawishi kususia Uchaguzi wa aina yoyote na ngazi yoyote ya ushiriki wa vyama. Neno "KUSUSIA" liondoeni kwenye fikra zenu. Nikupe siri, Majimbo mengi ni kama hayana Wabunge, wananchi wanajua 2020 hawakuwachagua waliopo,sasa hofu ni ya nini?
 
Mtu anayetaka mapema hii Magufuli aache kusemwa haitakii mema nchi hii. Uharibifu uliofanywa nchi hii na Magufuli kwa kujipendekeza na kujifanya mtetezi wa wanyonge ni mkubwa sana kuliko chochote kizuri alichofanya. Baya kuliko yote ni kuvuruga mifumo yote ya nchi ya kusimamia siasa, uchumi, ustawi wa jamii na kutoa haki. Aligeuza mihimili ya bunge na mahakama kuwa idara za serikali zinazopkea maelekezo kutoka Ikulu. Aligeuza vyombo muhimu kama ofisi ya DPP na TAKUKURU kuwa silaha za kudhibiti washindani wa kisiasa. Pamoja na mambo mengine maendeleo endelevu ya nchi yanatokana na uongozi wenye maono makubwa wa kuweka sera nzuri na kutekeleza; ,uwezo wa uongozi kushawishi na kushirikisha, mifumo endelevu ya usimamizi na uwajibikaji pamoja na utawala bora. Kama alivyosema Hayati Kingunge Magufuli hakuwa kiongozi hivyo alikuwa mbumbumbu wa haya yote. Wenzake aliowarekodi wakimuita "mshamba" hawakukosea. Kwa hisani ya Kingunge alikuwa nyapara wa kusimamia vibarua. Kutokana na kutokuwa kiongozi alijitafutia umaarufu kwa kujifanya mungumtu, mjua kila kitu, kukaripia na kuwatendea watumishi wa umma kama wafanyakazi wa nyumbani kwake. Wapo wananchi wengi walivutiwa na hiyo tabia yake ya kibabe, lakini kwa uhakika siyo tabia ya kiongizi mzuri na kusema kweli ni tabia ya mtu ambaye hajaelimika wala kustaarabika.
 
Umemeliza kila kitu. Watu wenyewe wanaojaribu kujitengenezea personality cult ni weupe kabisa. Matokeo yake wamekabidhi wapambe kuendesha nchi na kuwapigia propaganda za kitoto na kijima!
 
Maandishi mengi yote tu kutaka kumsifia Magufuli!! Pumbavu. Nchi hii haina nafasi kwa mtu mwenye chembechembe za Ki Magufuli.

Hatutaki DIKTETA atakayetufanya tuishi kwa wasowasi na woga, hatutaki mti atayekuwa anaua wakosoaji au kunyang'qnya fedha za wafanyabiashara.
 
FAM ni Mchagga aliye na mungu wa dini (si Mungu aliye hail aiyeweza kumzuia kujiuza au kuuza utu wake. Ila ni money monger
 
Una matusi ya reja reja kwa Myfriend , sijui kama anaweza kukujibu tena. Umepiga penyewe
 
q


mleta mada ameongea ukweli .

Watanzania hatuwezi kumsahau Magufuli kwa mazuri aliyoyafanya na misimamo yake .
.Kumponda magufuli ni kujipunguzia kura.
.
Hivi nyie ni vipofu au mmelogwa msije mkaingia madarakani.?

Hivi hamuoni jinsi Makonda anavyopendwa watanzania kwa kujipambanua wazi kuwa ni mfuasi wa Magufuli.

Angalieni Mpina n.k. Hakuna kijana anayeweza kugombea Urais akashindana na Makonda. Kama wanaomuunga mkono ni wahinga basi hii nchi ni ya wajinga na wajanja wahame watafute nchi yao na Mungu aliamua kuwapa wajinga nchi hii . Haiwezekani watu mil. 63 zaidi ya 80% wanamkubali Makonda halafi eti hakuna cha kujifunza kwake. Ni kichaa na fisadi ndiye anayeweza kudharau nguvu aliyonayo Makonda kwa kumuenzi JPM.

Lisu alijipatia umaarufu kwa kuwataja mafisadi na kuwakemea Hadharani kule Mwembe Yanga na Bungeni.

Kwa mbinu za kutaka tu kuipinga CCM kwa kila kitu akaanza kupinga hatua za magufuli kuwataja mafisadi hadharani na na kuwatumbua . Akaitwa Dikteta. Lakini aliyeanza kutaja mafisadi adharani alikia ni Lisu na Slaa.
.Kwa hiyo Tundu Lisu asije akadhani kuwa atapata umaarufu kwa kuuwa mstarabu kwa wezi wa mali za umma . Anajipunguzia kura nyingi sana .

Mrema ,Mtikila ,Maalim Seif Dr.Slaa ,Magufuli, na sasa Makonda walijipatia umaarufu kwa kuwataja Mafisadi hadharani.
Hii nchi ni mali ya Watanganyika wote ndio maana wanataka kuona wezi wa mali za umma wakiwa wanatajwa na kushughulikiwa hadharani.

Lisu akipuuza Hisia za Watanzania basi 2025 atashangaa kuona kura nyingi zinarudi CCM endapo Majaliwa atachukua fomu .Vingunevyo tuombe Mungu CCM wakosee na kuzuia kundi la Wazalendo kuchukua fomu hapo Lisu akicheza vizuri atamwacha yule mwenyekiti wa CCM kwa mbali sana. Lakini pia ni Lazima Lisu ajiepushe na za kumponda JPM mana CCM wanajua kusoma hisia na kwenda nazo ili kujipatia kura. Wanachotaka CCM ni ushindi wakati wapinzani wanataka kukosoa tu manjukwaani
 
Umpumbavu mtupu na kukosa uwezo wa kuchambua mazuri na mabaya. Ni mazuri gani unataka kuniambia Magufuli na Makonda walifanya?

Hivi Watanzania akili zenu ziko wapi?
 
Wtz wajinga waelimishwe kuwa umasikini wao wa sasa ni mkakati mibovu na mipango ya Jana iliyofanywa na magufuli

Mwanasiasa makini na mahiri lazima aeleze jinsi magufuli alivyoua uchumi
Kuanzia juuu mpaka level ya chini ambayo matokeo yake ni yanaonekana sasa

Mfano ni magufuli huyu aliyeharibu biashara ya korosho mikoa ya kusini
Kisa nape na majaliwa wasineemeke
 
Namshauri asigombee urais, hatuwezi kuwa na Rais wa hivyo, mzani haujabalansi fizikali
 
Umpumbavu mtupu na kukosa uwezo wa kuchambua mazuri na mabaya. Ni mazuri gani unataka kuniambia Magufuli na Makonda walifanya?

Hivi Watanzania akili zenu ziko wapi?


Wewe unataka kumzungumzia Magufuli au Makonda kwa misingi ya kimagharibi wanaoruhusu ushoga na usagaji kama uhuru na haki za binadamu.

Kama huoni aliyoyafanya Magufuli na anayoyafanya Makonda kwenye jamii ya watu maskini basi sina la kukuchambulia mana utakua ni mtu wa hovyo hovyo na unapenda siasa za hovyo hovyo .

Magufuli nilitofautiana naye sehemu Mbili tu. Kuacha kulizungumzia kwa ukali suala la Lisu kupigwa risasi japo siku ya kwanza alilaani jambo lile na Kuvuruga Uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Hayo mambo mawili yalinikera sana mana Lisu ni kati ya watu Waadilifu sana na Mzalendo wa kweli .

Uchaguzi ulituletea wabunge wa hovyo na mawaziri wasiofaa na wenye kiburi tulionao leo.

Lakini Mengine yote aliyoyafanya magufuli tangu akiwa Waziri wa ujenzi ni mambo mazuri sana kwa taifa hili na vizazi vijavyo watamuenzi. Ameamsha Roho ya uzalendo kwa Taifa hili. Haikwepeki Makonda anafaa kukaa kwenye ofisi za umma popote. Wachache walioumizwa ni katika kukenga Taifa.

Vita ya uganda kuna maelfu ya wanajeshi walikufa kwa ajili ya kulipigania Taifa . Wengine waliuawa kama moja ya kanuni za kivita ili kujenga moyo wa ujasiri na wengine waliuawa katika majibizano ya risasi na Adui.

Vijana wa leo hamuyajui hayo.
R.I.P JPM.

Hata mimi nilikua nampinga wazi wazi alipokua analosea. Sikuwa chawa wa kusifia kila kitu.
Alilinda Taifa na rasilimali zake.
 
Nape nav Majaliwa wananeemekaje na wakulima kama sio kujitoa ufahamu.?

Leo Nape ananeemeka na Dubai au wakulima?πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Katiba tuliyonayo ni ya kijeshi .Mana Amiri jeshi mkuu amepewa mamlaka yote kama Rais wa mapinduzi. Rais asiyehojiwa ni rais wa mapinduzi ya kijeshi. CCM haikuitwa cha cha mapinduzi kwa bahati mbaya.

Ndio maana Leo tunaongzwa na watu wasiochaguliwa na wananchi na hataki kukosolewa . Mchana wanakuchekea usiku wanakuwinda kuliko simba.

Hakuna nchi Duniani iliyoendelea kirahisi . Wametuletea Demokrasia sio kwa nia nzuri bali kwa ajili ya kutuwekea wanasiasa watakaofuata masharti yao na kutunyonya.


Ukiisinamiabliraia Majajo watageuka kuwa wala rushwa wakubwa na watu waihujumu serikali kwa mbinu nyingi sana .
 
No doubt Magufuli ali-master sana the art of propaganda. Alizishika media zote, hadi za nje kuna wakati ikatangazwa kwamba hazipaswi kurusha maudhui ya ndani bila kibali.

Media zote nchi, binafsi na zile za serikali hadi zile ambazo ziko tu online ambazo hazina usajili wa serikali zilijaa woga kumtaja Magufuli katika namna ambayo isingempendeza. Media nchini ziliimba mapambio ya kumsifu na kumtukuza mawizo mpaka machweo.

Propaganda za Magufuli zinanikumbusha propaganda za Adolf Hilter, Joseph Stalin na Mao Ze Dong. Hawa watu walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuaminisha mambo ambayo hayapo, walikuwa na uwezo wa kupandikiza nadharia zao na imani zao juu ya kadamnasi na ikaamini vivyo, huku nyuma ya pazia wakiwa na mauzauza yao kibao.

Magufuli alitupiga wapi? Kwanza alijifanya Rais wa wanyonge, akijua kwamba watanzania wengi over 40% tuko chini ya mstari wa umasikini wa $1 kwa siku, masikini wengi tulimpenda sana tukidhani ni mwenzetu lakini katu, hakuwa mwenzetu, JPM alikuwa tajiri sana.

Magufuli alijua kwamba watanzania hatupendi mafisadi, wengi tunadhani umasikini wetu kuna watu wanatuibia serikalini. JPM akaona atangaze nao vita kali, tukamsahau yeye ambaye alijilimbikizia mali nyingi sana, huku tukijua kwamba anapambana na mafisadi kwa ajili yetu, kumbe ni kwa ajili yake kwani kila alipotaifisha mali zao, zikawa zake na jamaa zake.

JPM master the art of public manipulation. Kwenye ziara zake alisimama barabarani, alizungumza na watu, akatoa fedha hadharani kwa watu wa hali ya chini, alitembelea hospitali na kutoa misaada hadharani kwa watu waliokuwa na hali ngumu huku kila media ikimulika. Vitendo vile vimewalevya wengi kudhani kwamba JPM was saviour, tukasahau kabisa na yeye ni mwanadamu mwenye tamaa na uchu, aliweza kufanya chochote pasi nasi kujua kuwa mali zetu zinaibwa na kuwekezwa kwenye hotels zake, real estate, mashamba na kuficha fedha nje ya nchi. Mtoto wa dada yake, aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya fedha Dotto James alifanya kazi kubwa sana kusafirisha fedha za mjomba wake nje.

Nasikitika sana kuona wengi wakimkumbuka JPM pasi na wao kujua kwamba bado wamo kwenye dimbwi la mning'inio wa propaganda za JMP. Ila kama tungejua uozo na madudu aliyofanya nyuma ya pazi, pengine tungezinduka kutoka kwenye hangover hiyo.

Vile vile akalidhoofisha Bunge kwa kumgeuza Spika kuwa wakala wake. Sijawahi kuona Spika ambaye ni puppet wa Rais hata enzi za chama kimoja. Akaitishia Mahakama isifanye maamuzi kwa uhuru.

Alijuwa pia kuwa 80% ya Watanzania ni wajinga, yaani hawana uwezo wa kuchambua ukweli na uwongo, hivyo basi kila alichosema wakakiamini na wanakiamini hadi leo. Kuna wajinga wanaamini eti aliishinda COVID-19 wakati yeye mwenyewe na akina Kikazi wamekufa kwa COVID-19 kwa jinsi walivyoipuuza.

Magufuli amefanya UFISADI mkubwa sana na kikundi cha wateule wake wachache lakini bado Watanzania wanamuona ni "shujaa" licha ya CAG kuonyesha discrepancies kubwa kwenye Ripoti ya 2020/21.

Magufuli aliiba mpaka uchaguzi wa vitongoji wa 2019 na uchaguzi Mkuu wote still watu wamesahau wanasema eti alikuwa mzalendo.
 


Duuh ,watanzania sio wajinga kwa kiasi hiki .
Propaganda za mashoga zlimezidi.

Uchumi unaotawiwa kwa usanii unaonekana kwa vitu kupanda bei , miradi mikubwa kukwama, watumishi na wanajeshi kukosa mishahara , uchaguzi kushindwa kufanyika na mikopo ya masharti ya kishoga kuongezeka.


Nionyeshe mali za kufuru za Magufuli mana ameshafariki .
Fedha walitorosha na kusafisha hazina wakati alipokuwa mahututi karibu mwezi mzima.

Wahusika wanajua na wanajijua.
 
Lissu akishakunywa konyagi huwa hana break
L
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…