Pako VIZURI sana...Oooh, vizuri! Vp kuhusu Korea ya kusini
Hapana wadenish si wakatili... Mtu mpaka akualike ujue amekupenda.
Mkuu inategemea unataka kwenda inchi gani kujilipua...zipo inchi zipo ulaya lakini utatamani ubaki Africa..sasa wewe nidokeze unataka uende inchi gani?
mulemule kumbe afya ndio dili ee ngoja nami nitasogea huko mkuu tujumuike wote nisaidie tu barua ya mwaliko niwe kama mgeni wako nikija nakuachia fungu kidogo natafuta njia yangu nami yakutokea by the way nami ni health personal...tropical diseases....researcher...
Kweli mkuu..na hata hyo euro y.. INASHUKA thamani sababu ya inchi kama Greece.. Na zinginezo masikini....kwnza hawa watu wanapenda sana raha kuliko kazi...wewe umeona wapi ofisi zinafungwa SAA saba wafanyakazi wanakwenda KULALA MAJUMBANI mwao halafu wanarudi tena ofisini SAA Tisa..wanatoka SAA kumi na moja... Greece ndy utaratibu wao wa kufanya kazi... Ile INCHI....inawabebesha wenzie mzigo wa madeni.tuHalafu German ni super power Nchi za Umoja wa Ulaya. Yeye ndiye aliyebeba mzigo wote wa Euro Curency,
maana wakati hii Euro inaanza fedha yake ndiyo ilikuwa na thamani sana.
Mkuu wewe ushakaa ULAYA? nianzie hapo kwnza...halafu nikupe sifa za hao Nigerians na wakenya..huko majuu...Acha uvivu ndugu yangu, kuna wakenya na wanigeria wenzako wanakwambia wakitua tu nchi yoyote ya ulaya wamewin tayari!! Haya niambie ni nchi gani ulaya kati ya alizotaja Lusungo ni sawa na Africa?? Acha watu wakatafute maisha nchi yenyewe hii Ngosha kakaba mpaka penalty na huku akisema waloshikwa wafungwe au wanyongwe tu, sasa kupi bora??
Safi, hiki ndo tunachotaka....mulemule kumbe afya ndio dili ee ngoja nami nitasogea huko mkuu tujumuike wote nisaidie tu barua ya mwaliko niwe kama mgeni wako nikija nakuachia fungu kidogo natafuta njia yangu nami yakutokea by the way nami ni health personal.
Eti mkuu mtu unaweza kuwa considered kuwa ww ni expat wa madini kwakuwa a diploma holder from Tanzania kwenye nchi ulizozitaja hapo juu, au paka uwe na kiwango gani cha elimu ndo utakuwa considered kuwa expert???Lusungo, Ahsante kwa uzi huu na kwa uzalendo huu.
Kwa wale ambao wanauzoefu wa migodi ya Tanzania please msing'ang'anie humo Geita, Kahama, buly... tafuteni kutoka kwenda nje ya mipaka ya Tanzania kama expat tuiletee nchi fedha za kigeni. Watanzania wanaheshima kubwa Congo DR, Zambia, Senegal, Ivory Coast, Mali, Ghana, Ethiopia, .........
Nimezunguka migodi ya nchi hizi nyingi nimekutana na watanzania wengi na wanafanya kazi nzuri na wanalipwa vizuri kwa average ya USD7000 kwa mwezi ambayo ni sawa na 15M ya Tanzania.
Tukiwa na Watanzania 100 wanaliingizia pato Taifa ya USD700,000 kwa mwezi pesa za kigeni
Tukiwa na Watanania 1000 wataingiza USD 7,000,000.
Tukiwa na Watanzania 10,000 wataingiza USD 70M which is possible for now tuache woga
Kuna mtu nilimuita kuna nafasi ya kazi nilipokuwa mgodi mmoja wa Lumwana kule Zambia wakati ule yeye alikuwa anafanya kazi pale TBS akaniambia hawezi kuiacha familia wakati ule dili za mikutano zilikuwa ziko chart mala leo wako movenpick, kesho Kunduchi beach full usanii lakini nilimwambia usitumainie kazi za dili hakunisikia leo hii yuko chali.
Tulenge kufikisha maexpat 100,000 ambao wataletea Taifa fedha za kigeni 700M USD kwa mwezi ambayo ni sawa na 1.5Tillion Tanzanian shs. sidhani kama kuna zao lolote tunao export lenye kuleta hizi pesa kwa mwezi. If we have failed to export products let us export human skills/resources please. mpaka sasa nimeweza kuwaconnect watu 12 kufanya kazi hizi na wengine mpaka sasa wananizidi hata mshahara but I am proud of this, I want Tanzanian to flood Africa as expats in the mining industry, doctors, IT and accounting. Tusibaki kupigana vikumbo Vodacom, TIGO, Airtel, TRA, Bandarini, huko dili hakuna na zilikuwa siyo halali tutachukia watawala bure. Stand up and get out there.
Huku unafanya kazi week 6 site na week 2 uko home unaendeleza miradi yako na ukiwa site hutumii hata shilingi yako vitu vyote unakuwaprovided mshahara unaukuta nyumbani Tanzania kwenye A/C unakusubiri (very clean money, hakuna kutega dili).
Mimi nilipata kazi kwa ku-apply online application kwa mara ya kwanza AngloGold Ashanti na kutokana na uzoefu niliokuwa nimepata hapo TZ wakanikubali and now I am changing from one company to another, country to country within Africa, sitaki kwenda ulaya au America, huko nitakuwa mtumwa. I like my Africa.
Google makampuni then apply na usiamini au usisubiri kutafutiwa apply ukiamini utapata ila ikitokea amejitokeza mdau kukusaidia it is very fine.
Thanks.
Kuna wakuu Copenhagen na Tokyo 40 wanaweza kuja kusaidia hapa, kwa wale watakao kwenda Denmark na Japan kutafuta maisha.
Marekani na Uingereza kwa sasa ni vigumu mno labda kama wewe ni mtaalam yaani "expert".
Zipo nchi nyingine kama Australia na Canada ambako bado wanatafuta watu wenye utaalam khasa kwenye maeneo ya afya na teknolojia.
Ila tusidanganyane kuzamia Ulaya na kwenda kujilipua inategemea na nchi unayotokea, ukiwa mweusi tii wawezatumia Sudan kama "reference" lakini maji ya kunde basi ujue itakula kwako.
Nchi zingine kama Eritrea wao wana bahati kutokana na hitoria ya nchi yao kuwa na rekodi mbovu ya ukiukwaji wa haki za binadamu.
Ingia WORKAWAY.INFO uende ukajitoleeizzo. Mkuu hao wa kujitolea Malta wanapatikana kwa njia gani?
Kama kuna website tuwekee
Mkuu kama wakenya wanabebana leo sisi tuwe waroho wa ulaji?Safi, hiki ndo tunachotaka....
Mkuu mimi na wewe ni wamoja sote tunachukua maujanja hapa..Mkuu wapi nawwza kuishi nakupata kazi European country na Asian country na kuna urahisi wa kupata visa?
Ina maana blacks wanaweza aminika jeshini huko mbele mkuu? Mfano Norway wanaweza kukuchukua black?
Ujamaa ulituponza na ndio uliwapa fursa majirani kufanya hivyoWase***ng* sana wakenya yaani watuwahi mapema wakautangaza mlima wetu upo kwao dunia nzima ikawajua.
Duuh.... Kwa huu ushuuda basi ile sehemu hapafai kuishi hata kima.Yaa..pale ni viza free mkuu kwa tanzanian passport holder.. mkuu hapafai..pana njaa hatari...halafu cha ajabu ukifika wanakuita muafrica...wao wanajiona sio waafrica...nimekaa Antananarivo pale...kwnz hawajuwi English wanaongea kimashangaa...au French kwa mbali... Ukifika pale ndy utajuwa Tanzania tumepiga hatua kiasi gani ktk Africa yetu hii...kuanzia chakula chao KIBOVU...hata CHUMVI hawaweki kwny CHAKULA
...hata UGALI hawaujuwi.. Wao ni wali tu..kuna siku tulihangaika kusaka UNGA WA MAHINDI shoprite zote hawajuwi...ila PAPUCHI INJE INJE MKUU..kule ukiwa disco...ukiona mwanamke kavaa viatu virefu means anauza..wewe uliza BEI tu...ndy style yao..kile kisiwa wafaransa kibao wanakuja kula raha tu na kuondoka..tena UFARANSA wanaingia ENTRY TU....ila cha kushangaza MKUU pale MTU akifa...anawekwa KWENYE shelfu ndani ya nyumba ila inajengwa makaburini....kule MTU akizikwa na city ndy anazikwa ardhini..au anaonekana ni MTU LOFA SANA..hana uwezo wa kujenga BANDA LA KUHIFADHI JAMAA ZAKE..kwa hyo wakimuweka maiti kwenye shelfu....then baada ya mwaka wanakuja kufunguwa ile nyumba wanachukuwa maiti wanacheza nayo mziki..tena mziki mkubwa unafunguliwa makaburini.watu wanajaa kushuhudia maiti wanavyocheza nayo mziki.na ndugu wanakuwa na bajeti hiyo ya sherehe hiyo.kila ikifika mwaka.maiti itatolewa wanacheza nayo ngoma na kuibadilisha nguo.HALAFU WANAIRUDISHA TENA KWENYE SHELFU ...wanafunga HOUSE wanaondoka....na wanaamini wasipofanya hivyo maiti itawaletea mikosi....mkuu niliogopa sana siku za mwanzo..pia pale rais wao Fulani alifukuzwa na mawe kqmq mwizi.. na wanainchi...akakimbilia mafichoni south...rais alikuwa na uwanja wake wa ndege mwenyewe na pesa inaingia mfukoni kwake..mkuu hapafai pale...Tanzania yetu ni marekani...nyumba ZAO zipo milimani na mabondeni tu...
Mkuu nimeshuhudia mwenyewe au itafute Madagascar na utamaduni wao ktk Google uta niamini mkuu...Mara ya mwisho kufika pale ni 2014...na ajabu ingine ukitoka airport unalipa airport fee kama dola 30 hivi...labda waitoe juzi...ww umeona wapi mambo hayo..kulipa pesa ya gharama za airport...Duuh.... Kwa huu ushuuda basi ile sehemu hapafai kuishi hata kima.
Ndugu wana JF
Kwa muda mrefu kumekuwa na masuala mbalimbali yahusuyo kujilipua (kwenda nje ya nchi) ambayo watu wanauliza mmoja mmoja kwa lemgo la kutaka msaada na ushauri namna ya kufika na jinsi ya kuanza maisha huko nje.
Kutokana na kutoa msaada kwa wengi (binafsi) kwa kutumia njia binafsi nimeona nifungue uzi huu ili kuweka mambo yote wazi kwa kadiri itakavyowezekana na kualika wengine pia waweze kutoka maoni yao.
Ndugu zangu nchi yetu ya Tanzania ki uwezo bado ni changa, fursa za kutoka ni chache na hata changamoto ni nyingi. Huko kwa wenzetu fursa ni nyingi ndio maana imekuwa chanzo cha kuvuta wahamiaji wengi sana toka mataifa masikini.
Nchi masikini wenzetu huko mbele raia wao wamejaa haswa kutokana na moyo wa kusaidiana na kuvutana.
Nimeamua nilete hoja hii kama ambavyo wenzetu hufanya huko Nairaland ya Nigeria ili kila mtu mwenye ujuzi au ufahamu juu ya namna ya kutoka (kujilipua) atoe msaada kwa wengine kwenda huko... si lazima wewe binafsi usaidie mtu binafsi NO, hata mbinu tu za jinsi ya kufika huko.
Kabla sijaingia kwenye kiini cha mada naomba nitoe faida na changamoto za kujilipua.
FAIDA
1. Fursa nzuri za kiuchumi na kujiinua hasa ukiwa na malengo.. Wakuu binafsi nimeishi Marekani kwa miaka nane. moja ya faida nilizopata huko ni kujiinua kiuchumi.... binafsi wakati naenda kusoma huko nilijiwekea malengo ya kujenga ghorofa nyumbani, kufungua mashine za kusaga na kukoboa nafaka pamoja na kumiliki fuso za mizigo...
kipato cha mfanyakazi wa kule ni kikubwa mno kushinda hata cha baadhi ya maboss wetu hapa... hivyo nilijitahidi nilipokuwa kule malengo yangu yaimie... ni kweli baada ya muda huo nilifanikiwa kutimiza yote.
2. Huduma nzuri za afya, Elimu, Sheria, miundombinu.
CHANGAMOTO
1. changamoto kubwa kwa kuwa kule ni upweke (ku feel home mara kwa mara japo wakati mwingine ukizoea hutoweka)
2. Xenophobia hii ni kwa baadhi ya nchi tu sio zote.
USHAURI WA WAPI UENDE NA NAMNA GANI UENDE
Kwa wale wahitaji wa masuala ya maisha kujijenga na kuchuma nashauri nchi hizi, USA, UK, NORDIC COUNTRIES, NA WESTERN EUROPE COUNTRIES. kwa Afrika nashauri SA.
Jinsi gani utaenda namna ni nyingi.... naorodhesha baadhi hapo chini...
1. kwenda kimasomo ambapo unaweza tafuta sponsors then ukapata scolarship itayokuwezesha kupata visa na kujilipua huko baada ya masomo...
2. Kutafuta mwenzi wa nje ambaye atakualika huko kisha mtaoana na kukuwezesha kupata resident permit na baadae uraia.
3. Kuhamisha mataji na biashara njia hii unakubaliwa popote alimradi uwe na biashara halali,
4. kwenda kwa shughuli za utamaduni
Wenzetu wakenya na wanigeria wameunda mfumo wa kualikana wao kwa wao, kwamba mtu anakutumia barua ya mwaliko, then unakwenda ukifika huko anakutafutia mtu mnaoana kisheria tu ili upate karatasi kisha kila mtu anasika hamsini zake....
Wapendwa mambo ni mengi siwezi andika yote ndio maana nimeanziasha uzi huu tutaendelea kujuzana kwa kairi michango ya watu itakavyokuwa na maswali yatayojitokeza.
Nawakaribisha wafuatao: BAK kui Isanga family Sky Eclat
Matola MziziMkavu Copenhagen DN Ng'wamapalala Pascal Mayalla Nyani Ngabu rev kishoka Bavaria FaizaFoxy farkhina MfalmewaKiha mwandende Slim5
Na wote wenye maujuazi au mauzoefu ya huko mbele... karibuni tusaidiane tujenge taifa letu... Tuwasaidie vijana wakasake fursa.
Mkuu ukaona upataje hapa gheto kabisa nlipolala(tandika) heheMkuu mbona hujaitumia mali hiyo.... Maana ukiwa na passport South Africa unakwenda kama tandika tuuu... Ni nauli yako
Huko unakokwenda pia kuna matumizi, tena kama ni hizi kazi za unskilled labour utajikuta wewe ni mtu wa hand to mouth. Kinachoumiza sana ni kodi ya nyumba, watu wengi inabidi wafanye kazi mbili ili kupata pesa ya ziada.
Sana hata Denmark ndo ilivyo.... Ukifika mlangoni unakuta list ya majina na button so wewe ni kubonyeza tu jina unalotaka kengele italia kwa mhusika then utaongea nae ukiwa nje basi akikubali uingie ye atabonyeza tu huko huko juu aliko mlango utafunguka...
Wenzetu wako mbali sana jamani.