Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ndugu wana JF
Kwa muda mrefu kumekuwa na masuala mbalimbali yahusuyo kujilipua (kwenda nje ya nchi) ambayo watu wanauliza mmoja mmoja kwa lemgo la kutaka msaada na ushauri namna ya kufika na jinsi ya kuanza maisha huko nje.

Kutokana na kutoa msaada kwa wengi (binafsi) kwa kutumia njia binafsi nimeona nifungue uzi huu ili kuweka mambo yote wazi kwa kadiri itakavyowezekana na kualika wengine pia waweze kutoka maoni yao.

Ndugu zangu nchi yetu ya Tanzania ki uwezo bado ni changa, fursa za kutoka ni chache na hata changamoto ni nyingi. Huko kwa wenzetu fursa ni nyingi ndio maana imekuwa chanzo cha kuvuta wahamiaji wengi sana toka mataifa masikini.

Nchi masikini wenzetu huko mbele raia wao wamejaa haswa kutokana na moyo wa kusaidiana na kuvutana.

Nimeamua nilete hoja hii kama ambavyo wenzetu hufanya huko Nairaland ya Nigeria ili kila mtu mwenye ujuzi au ufahamu juu ya namna ya kutoka (kujilipua) atoe msaada kwa wengine kwenda huko... si lazima wewe binafsi usaidie mtu binafsi NO, hata mbinu tu za jinsi ya kufika huko.

Kabla sijaingia kwenye kiini cha mada naomba nitoe faida na changamoto za kujilipua.

FAIDA
1. Fursa nzuri za kiuchumi na kujiinua hasa ukiwa na malengo.. Wakuu binafsi nimeishi Marekani kwa miaka nane. moja ya faida nilizopata huko ni kujiinua kiuchumi.... binafsi wakati naenda kusoma huko nilijiwekea malengo ya kujenga ghorofa nyumbani, kufungua mashine za kusaga na kukoboa nafaka pamoja na kumiliki fuso za mizigo...

kipato cha mfanyakazi wa kule ni kikubwa mno kushinda hata cha baadhi ya maboss wetu hapa... hivyo nilijitahidi nilipokuwa kule malengo yangu yaimie... ni kweli baada ya muda huo nilifanikiwa kutimiza yote.

2. Huduma nzuri za afya, Elimu, Sheria, miundombinu.

CHANGAMOTO
1. changamoto kubwa kwa kuwa kule ni upweke (ku feel home mara kwa mara japo wakati mwingine ukizoea hutoweka)

2. Xenophobia hii ni kwa baadhi ya nchi tu sio zote.

USHAURI WA WAPI UENDE NA NAMNA GANI UENDE
Kwa wale wahitaji wa masuala ya maisha kujijenga na kuchuma nashauri nchi hizi, USA, UK, NORDIC COUNTRIES, NA WESTERN EUROPE COUNTRIES. kwa Afrika nashauri SA.

Jinsi gani utaenda namna ni nyingi.... naorodhesha baadhi hapo chini...
1. kwenda kimasomo ambapo unaweza tafuta sponsors then ukapata scolarship itayokuwezesha kupata visa na kujilipua huko baada ya masomo...

2. Kutafuta mwenzi wa nje ambaye atakualika huko kisha mtaoana na kukuwezesha kupata resident permit na baadae uraia.

3. Kuhamisha mataji na biashara njia hii unakubaliwa popote alimradi uwe na biashara halali,

4. kwenda kwa shughuli za utamaduni

Wenzetu wakenya na wanigeria wameunda mfumo wa kualikana wao kwa wao, kwamba mtu anakutumia barua ya mwaliko, then unakwenda ukifika huko anakutafutia mtu mnaoana kisheria tu ili upate karatasi kisha kila mtu anasika hamsini zake....

Wapendwa mambo ni mengi siwezi andika yote ndio maana nimeanziasha uzi huu tutaendelea kujuzana kwa kairi michango ya watu itakavyokuwa na maswali yatayojitokeza.

Nawakaribisha wafuatao: BAK kui Isanga family Sky Eclat


Matola MziziMkavu Copenhagen DN Ng'wamapalala Pascal Mayalla Nyani Ngabu rev kishoka Bavaria FaizaFoxy farkhina MfalmewaKiha mwandende Slim5

Na wote wenye maujuazi au mauzoefu ya huko mbele... karibuni tusaidiane tujenge taifa letu... Tuwasaidie vijana wakasake fursa.
Nimefight Sana kuingia uk, usa tangu 2009 nimefail, nimejaribu njia zote mpaka 2012 nikaenda burundi kujaribu kuondokea kule kama mrundi niingie belgium then nizame uk but nkafail...mwaka jana nimerusha kete yangu usa niingie kwa program ya mast nipate j1 visa nimetoswa nayo nshajikatia tamaa but uzi huu unataka niamsha tena nianze michakato..kuna mtanzania flan alijifanya kunisaidia niingie kwa bibi ye yupo coventry uk akaniliza pound 1300... wabongo wengine njaa kali majuu
 
Ok Mkuu
Ila sijaamini bado kuwa Italy fursa kuu ni ngada

Ni ngada kaka,wabongo wote % kubwa waliko italy ni ganda tu,ila kama uko smart kuna biashara za nguo viatu labda hizo uchukue huko ukauze bongo lkn ajira brother watu wanakimbia huko kila siku hakuna ajiri na mtu ni citizen kabisa lkn no job uchumi umeyumba sana Italy kama grace tu
 

Lithuania inapakana na Poland na poland inapakana na Ujerumani,Isitoshe Poland ipo Muungano wa Ulaya.
Toka hapo mbele kwambele .

Au pale Estonia anachukua ferry Tallin to Helsinki , ni kama dar to zenj.
 
Ni ngada kaka,wabongo wote % kubwa waliko italy ni ganda tu,ila kama uko smart kuna biashara za nguo viatu labda hizo uchukue huko ukauze bongo lkn ajira brother watu wanakimbia huko kila siku hakuna ajiri na mtu ni citizen kabisa lkn no job uchumi umeyumba sana Italy kama grace tu

Nimeshtuka sana!
Kuna ndugu zangu kule wamekaa zaidi ya 20 years nahofia wasijeishia jela kwa mtaji huo
 
Ok maisha ya hapa ulaya yaani siri kubwa saana wengi hawasemi ukweli,na kupata karatasi sio Kwamba ndio ticket ya kwenda Europe union countries na kufanya kazi kuna kitu inaitwa personal number kila nchi ina yake,pia watu kibao wa karatasi za Italy lkn hawapewi kazi Scandinavia,mpk uwe na contract ya kazi,nani sasa anakupa hiyo contract ya kazi?kuna kampuni moja tu inatoa contact nayo ni kusambaza mataganzo hapa wanaita REKLAM.hiyo kazi hailipi hata kidogo ni bora ubaki bongo uuze nyanya.

Acha kukatisha tamaa watu aisee,ukiwa na uraia wa nchi moja ya Ulaya,unaweza fanya kazi nchi yoyote ya ulaya,me na mwanangu Ana uraia wa kireno na kWa sasa anapiga kazi france bila tatizo lolote,tena anatumia uraia wake wa ureno
 
Nimefight Sana kuingia uk, usa tangu 2009 nimefail, nimejaribu njia zote mpaka 2012 nikaenda burundi kujaribu kuondokea kule kama mrundi niingie belgium then nizame uk but nkafail...mwaka jana nimerusha kete yangu usa niingie kwa program ya mast nipate j1 visa nimetoswa nayo nshajikatia tamaa but uzi huu unataka niamsha tena nianze michakato..kuna mtanzania flan alijifanya kunisaidia niingie kwa bibi ye yupo coventry uk akaniliza pound 1300... wabongo wengine njaa kali majuu
mkuu tumia njia ya kujitolea,pitia workaway.info...hii njia ni guarantee maana humpi mtu pesa mkononi..
 
Nataka kweda south Afrika kusoma Radiography kwa alie South afrika anipm au mnisaidie jamani sina mwanga kabisaaa
 
Acha kukatisha tamaa watu aisee,ukiwa na uraia wa nchi moja ya Ulaya,unaweza fanya kazi nchi yoyote ya ulaya,me na mwanangu Ana uraia wa kireno na kWa sasa anapiga kazi france bila tatizo lolote,tena anatumia uraia wake wa ureno

Sawa ila mimi naongea kitu ambacho nakijua hata mimi ni raia wa sweden lkn nafanya kazi Norway,Je unajua ni proces zipi unafuata ili upate number ya kulipia TAX? Mie siongei mambo ya vijiweni wala sina haja ya kumtisha mtu yoyote, kwa taarifa yako Europe kila nchi ina sheria zake na hata nchi kama sweden japo iko kwenye European union lakin hata hiyo euro haitumiki hapa.watu wengi wakiwa ulaya tatizo hawasemi ukweli ili watu wajue mzee
 
Ila Madagascar ni mchanganyiko wa WAHINDI... Wachina..yaani hata wao hawajuwi asili yao..maana watu weusi ni wachache sana...wengi wahindi...kama China China..kuna siku niliwauliza asili yao...wanasema ni wale wafanya biashara wa mwanzo wahindi na wachina walikuwa wakipita kuja east Africa waliviona visiwa wakawa wanapumzika...mwishowe wakaanzisha maisha...hawa jamaa na seashells wanafanana...hawa jamaa wanatabia zote za KIHINDI... UCHAFU na hata maumbo yao...kula pariki..kutema mate hovyo...nikaamini kweli unaweza ikawa story ya kweli...

Pale ni mchanganyiko wa Asia kaka,kuna wa Pakistan pale,kuna wa Afghanistan,wa hindi,wa China,etc na kuna weusi wengi tu ambao walienda kupigana vita kipindi kile cha ukoloni na france ambao inasemekana asili yao ni Senegal,sema asilimia kubwa wanawake wao ni wazuri sanaa na bei nafuu sana kuwapata,kWa mfano unaweza ukapata mwanamke mzuri kWa buku 10 ya kibongo,buku ni nyingi sana pale,walimu tu wanalipwa elfu 25 kWa mwez ambayo ni sawa na euro 10,kile kisiwa maskini sana lakin inaweza ikawa njia pia ya kuingia reunions na kuanzia maisha hapo,ukipata permit ya reunions unaingia france bila visa,nauli yako tu
 
Najua kuna wabongo wanasoma south afrikaaa nisaidieni jamanii nijapange kivipi kipesaaaa applications na mambo mengine ya msingi japo kiufupiiii utanipaaa mwangaaaaaa msaaada tafadhariii mwakani mwezi wa kwanza mungu akijalia niwe hukoo
 
ha
Ahsante mkuu kwa kuni tag. Ebu nipe uzoefu kuhusu jamaica yaweza kuwa rahsi pia. Kama unauzoefu. Kuna dada wa kijamaica kaniganda kama kupe na anakomaa niende huko
UK utalala kwenye nje kwenye mabox wewe kule maisha magumu sana pesa hakuna,vibarua hakuna kazi za box mpaka upitie kwa dalali hata kama unaenda kusoma inabidi uwe upo fresh sana kwenye swala la pesa.
Vinginevyo nenda Australia kule hata kupata PR nirahisi compare na UK ukimaliza masomo wanakuswaga unarudi tena mavumbini {tz}.
hahaha, mavumbini 😀😀😀😀
 
Najua kuna wabongo wanasoma south afrikaaa nisaidieni jamanii nijapange kivipi kipesaaaa applications na mambo mengine ya msingi japo kiufupiiii utanipaaa mwangaaaaaa msaaada tafadhariii mwakani mwezi wa kwanza mungu akijalia niwe hukoo

Falcon Mombasa
 
Lithuania inapakana na Poland na poland inapakana na Ujerumani,Isitoshe Poland ipo Muungano wa Ulaya.
Toka hapo mbele kwambele .

Au pale Estonia anachukua ferry Tallin to Helsinki , ni kama dar to zenj.

Sawa unachukua crusing ship boat za kula raha huko ndani ni jehanamu lkn sasa kutoka humo ukanyange ardhi ya helsink mzee mbinde wala sio tallin tallink na kuna vikingline pia security ni kubwa kutokana na issue za ugaidi jamaa wako makini.ni bora utafute tourist visa kwa nchi amabayo unataka kwenda ukifika huko ndio unazama mazima sasa mpk kieleweke lkn border to border utahagaika saana
 
Sawa ila mimi naongea kitu ambacho nakijua hata mimi ni raia wa sweden lkn nafanya kazi Norway,Je unajua ni proces zipi unafuata ili upate number ya kulipia TAX? Mie siongei mambo ya vijiweni wala sina haja ya kumtisha mtu yoyote, kwa taarifa yako Europe kila nchi ina sheria zake na hata nchi kama sweden japo iko kwenye European union lakin hata hiyo euro haitumiki hapa.watu wengi wakiwa ulaya tatizo hawasemi ukweli ili watu wajue mzee

Me siongei mambo ya kijiweni ndugu yangu,Scandinavian kidogo kuna sheria haziingiliani na Europe angalau pia wapo umoja wa ulaya na ndo mana hawatumii euro kama nchi zingine,wao Kama wamejitenga,lakin ukiwa na uraia wa ulaya wa nchi zinazotumia euro unaweza ingia nchi yeyote ya ulaya inayotumia euro na ukafanya kazi bila masharti yoyote yale,kWa mfano ukiwa una uraia wa ureno,Italy,hispania,ufaransa,ujeruman,belgium,uholanzi etc,hawa wanafanya kazi pamoja(umoja wa ulaya).
 
Kuhusu kuingia Jeshi lazima uwe na permit hata ya mda mfupi(mwaka 1)Kama hauna hauwezi ingia ndugu zangu,na hauingii jeshi kabisa,hapana unaingia jeshi la wageni ambao mnakuwa wengi sana na wengine kutoka nchi mbali mbali ikiwemo Africa,Asia pia na Europe wanakuwaga wachache,lakini pia ni kweli unakuwa na mkataba wa miaka 5 baada ya hapo unaomba uraia wanakupa bila tatizo lolote na kazi unakuwa hauangaiki,unapata kiraisi sana maana wanakuwa wanakuamini na unakuwa na vyeti ambavyo umesomea ulivyokuwa katika Hilo jeshi la wageni,kumbukeni hili jeshi pia ndo wale migambo wanaotangulizwa mbele wakati wa vita na wanapelekwa kwenye nchi zenye vita Kama Iraq,Syria,Libya, n.k,so usipokufa katika huo mkataba wako wa miaka 5 ndo umeyatoa maisha sema wengi wanakufaga,wengi wakimaliza hiyo miaka 5 wanakuwa vilema na madhara mengi sana,lakin maisha pia ni Risk,ukiamua umeamua Lakin hauwezi ingia katika Hilo jeshi Kama hauna Permit hata ya mda mfupi(mwaka 1).
 
Me siongei mambo ya kijiweni ndugu yangu,Scandinavian kidogo kuna sheria haziingiliani na Europe angalau pia wapo umoja wa ulaya na ndo mana hawatumii euro kama nchi zingine,wao Kama wamejitenga,lakin ukiwa na uraia wa ulaya wa nchi zinazotumia euro unaweza ingia nchi yeyote ya ulaya inayotumia euro na ukafanya kazi bila masharti yoyote yale,kWa mfano ukiwa una uraia wa ureno,Italy,hispania,ufaransa,ujeruman,belgium,uholanzi etc,hawa wanafanya kazi pamoja(umoja wa ulaya).

Kaka hujui unachokisema mie Nina mshikaji wangu ana uraia wa italy lkn kazi imeshidikana sweden,pia upatikanaji wa kazi hapa ulaya sio kama bongo ujue kwanza hiyo kuna agency ya serikali kila nchi amabyao inashughulika na kukutafutia kazi wewe mkazi wako radhi wakulipe hela hata kama huna kazi wkt wanakutafutia kazi na hata wanaweza kumwambia mwajirj akupe kazi akulipe 20%tu ya mshahara na 80% wanakulipa wao.sasa,kuhusu kutumia euro hiyo sio hoja italy wanatumia euro je mtu amaweza kutoka italy akafanya German?je unajua kila nchi hapa ulaya wana lugha yao?mzee mie niko ulaya huu mwaka 24 kabla ya hapa nimekaa saana German,Italy,Finland na huko kote nilikua natafuta maisha najua sheria za hawa jamaa sikia tu story za vijiwen siku ukifika ndio utajua
 
Back
Top Bottom