USHAURI: Nahisi nimerogwa

Embu sahizi sikiliza RADIO Upendo upate maombi 107:7
 
khaaa🤣🤣🤣🤭🤭🤭

hebu kalale au kalalwe mkuu
 
Kwanza wewe ni mtu wa aina gani???

Pengine namna ulivyojiweka nirahisi kuhusishwa na matukio ya ajabu na Watu wakaamini.

Kabla hujatafuta mchawi anza nawewe mwenyewe jitathmini matendo na mienendo yako inashabihiana na matukio unayosingiziwa????

Kuna wakati matendo yako ndio mchawi wako.
 
aisee, israeli yupo mwaisela....kaa kitaalamu...wanajuaje jina lako kamili mkuu ?
 
Kiujumla tukuo la Kwanza alie nitaja namfahamu, lapili niliitwa tu na walimu.. Lkn hili la tatu nimestaajabu sana mtuhumumiwa ananitaja tena mbele yangu anakiri waz ku husika na Tukio na mm eti ndio mshirika wake.. Sura yake ni mara ya kwanza naiona
Niliwai kuwa katika viatu vyako mara 1.
Jamaa simjui, ndiyo mara ya kwanza ninakutanishwa nae mbele ya umati mkuu wa watu Alichokuwa akikisema jamaa ni the same na kesi yako.
Suluba zote, kipigo chote jibu langu ni SIJUI CHOCHOTE wakati huo nina miaka 17 tu na homu hawajui niko wapi.
Jamaa aliyeniingiza katika msala alikuwa ananizidi umri lakini alikuwa analia kama mtoto.
Niliteseka siku hiyo!! ni moja ya siku zangu mbaya, mauti niliyaona, walipiga wakachoka na jibu langu ni lile lile!!! baada ya wiki 1 hivi Bro mmoja simjui pia nikabumiana nae tu mtaani, akanivuta pembeni akaniambia:, BWANA MDOGO SIKU ILE NILIKUKUBALI , WEWE NI MTU SAHIHI WA KUFANYA NAE KAZI , MAADAM BADO UKO HAPA HAPA NITAKUTAFUTA BAADA YA SIKU MBILI. Ananiambia hivyo mimi nina tiket tayari ya kurudi skonga.
 
Mkuu hichi ndo kilichokua akilini mwangu nakiwaza baada ya kuusoma huu uzi. Jamaa wa RFA alikua anakiita kivuli. Kilikua kinamuharibia kila aendapo.

Mleta uzi bila shaka nawe una kivuli chako ambacho ndo kinatenda hayo yote.

Ushauri: Tafuta mtu wa dini haswa akuombee. Ikishindikana tafuta mganga haswa akufanyie tiba.
 
Acha kuvuta bangi na huo usela mavi, mtu unajiita chimbo boy maana yake nini?

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
Sivuti bangi.. Jina chimbo boy, kipind nasoma Nlikua na utaratibu wa kujichimbia kusoma peke yangu(bila discussions na wenzangu) ndio mwanzo wa Hilo jina chimbo boy
 
Nenda Kwa mganga isije ikawa una copy yako inafanya kazi, au huwa unatoka nje ya mwili bila kujijua
Kwa mganga Tena? Shetani kwa shetani wanashtakiana? Nakushauri uokoke then roho mtakatifu atakusaidia kushinda yote hayo in Jesus Christ name!
 
Achana na marafiki wahuni, Vibaka wanajuaje official names zako? Chimbo siyo kuzuri!
 
Nenfa kanisani onana na mchungaji mwelezee hiyo shida inakuandama na pia funga na kusali kwa MOYO WAKO WOTE Mungu atakuweka huru
 
Sivuti bangi.. Jina chimbo boy, kipind nasoma Nlikua na utaratibu wa kujichimbia kusoma peke yangu(bila discussions na wenzangu) ndio mwanzo wa Hilo jina chimbo boy
wengine achana nao usiwajibu watakusumbua kichwa, anza kuzingatia ushauri wa kidini ulioshauriwa na watu ktk comments...
Ila kamwe usijichanganye ukaenda kwa mganga, ni sawa na mbuzi kufia kwa muuza supu...
 
Kama kwenye ukoo wenu kuna asili ya mizimu ongea na wazazi wako mkafanye jambo,mi mwenyewe nimekumbana nayo sana
 
Kama kwenye ukoo wenu kuna asili ya mizimu ongea na wazazi wako mkafanye jambo,mi mwenyewe nimekumbana nayo sana
 
Unaroho ya kukataliwa...

Maombi ndio njia pekee...

YESU KRISTO ndio njia, anajua mwisho wetu kabla ya mwanzo.
 
Ogea chumvi ya mawe kwa siku mara mbili ndani ya siku saba....itakusaidia kuondoa kimavimavi au mikosi na nuksi zilizojaa divi la mkazuzu au divi la mkamwamba usiposhtuka mapema jamii itakuja kukuona ni kinyago cha mpapule
 
Kuwa makini sana, unapoelekea atafanya kosa mwingine hapa JF kisha wewe utapigwa ban.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…