Ushauri: Nataka nikope 10millions niache kazi serikalini, ili nijiajiri

Ushauri: Nataka nikope 10millions niache kazi serikalini, ili nijiajiri

Kwa wazo ulilonalo tu Naomba nikuite "Mdogo wangu"
Mdogo wangu, please USIACHE KAZI...

baki na Kazi yako na omba huo mkopo ufanye biashara, tena omba Mikopo kama hiyo Zaidi ya mmoja Baada ya kuona maendeleo ya kile utakachoanzisha
Tafuta watu 10 walioacha kazi.... Nakwambia waliofanikiwa hawazidi 3.
Usiache kazi tafadhalini, Mimi nimeajiriwa kampuni Binafsi na bado Nina biashara zangu na nimeajiri watu.
Kwenye biashara kuna changamoto nyingi Sana, unaanguka na kusimama, unaanguka, unajikwaa unasimama, wengine wanaanguka jumla...
Baki na Kazi yako na anzisha biashara
HAPA KIYOSAKI HANA NAFASI
 
Coment za watu waoga. Kusoma ndo nini kuenda Masters ili iweje? ndo apate pesa nyingi? awe huru? ndo mnavyo jidanganya kwamba ukiwa na Masters basi maisha kwako ni Bora na utakuwa na pesa?

Kwani akiwa kijana hawez acha kazi? wanao paswa kuacha kazi ni wazee?

Sent using Jamii Forums mobile app
umejibu vizuri sana japo hujui kwa undani umuhimu wa shule na umri wake. mimi hiyo master sina na sitegemei kwenda kwa sasa lakini naiona changamoto yake huko mbele umuhimu wa shule katika shughuli za kujitegemea. hivyo kwa umri wake anahitaji kufanya hivyo.
msimdanganye mwenzenu millioni kumi sio pesa nyingi katika biashara kuanza nazo anaweza kuanguka vibaya fikiria hana network kubwa na huenda wazo la biashara atafanya nini bado hana uhakika.
kwenda shule ni kupunguza risk na kuongeza mtandao zaidi.
ninaye mshauri naimani ana umri wa kati 24-32 yeye ananielewa msimdanganye kama ninyi mlifanikiwa kiurahisi ni bahati yenu lakini kwa huyu bado anachangamoto nyingi kwanza ndo kwanza kaanza maisha ukilinganisha na kazi aliyonayo.
 
Kwa wazo ulilonalo tu Naomba nikuite "Mdogo wangu"
Mdogo wangu, please USIACHE KAZI...

baki na Kazi yako na omba huo mkopo ufanye biashara, tena omba Mikopo kama hiyo Zaidi ya mmoja Baada ya kuona maendeleo ya kile utakachoanzisha
Tafuta watu 10 walioacha kazi.... Nakwambia waliofanikiwa hawazidi 3.
Usiache kazi tafadhalini, Mimi nimeajiriwa kampuni Binafsi na bado Nina biashara zangu na nimeajiri watu.
Kwenye biashara kuna changamoto nyingi Sana, unaanguka na kusimama, unaanguka, unajikwaa unasimama, wengine wanaanguka jumla...
Baki na Kazi yako na anzisha biashara
HAPA KIYOSAKI HANA NAFASI
kama nikubebe vile!
ili nichukua zaidi ya miaka mitatu kupata biashara siku niliyoipata nilimpata mteja mmoja mabaye mpaka leo namuhudumia kwa adabu.
 
Watu wengi mmetoa ushauri mzuri sana, naomba niwakumbushe kwamba aliyeleta hii post anaona akiendelea kubaki kwenye ajira, hawezi kuwa hata na huo mtaji mdogo wa kuanzisha biashara ili aone kama itafanikiwa.

Pili, akipata mkopo akaendelea kufanya kazi na biashara wakati huohuo, hataweza kusimamia vizuri biashara yake na matokeo yake hataweza kupata mafanikio kwa usimamizi mbovu. Kwa ufupi ajira yake ndio itakua hiyo biashara kufa na kupona.

Cha msingi ni umakini na utulivu wa kupata wazo na biashara sahihi. Vilevile kama hauna uzoefu wowote wa biashara, kuanza kwa 10M inaweza kuwa changamoto, ungeanza na 3 au 5 M kuona upepo unaendaje.
 
Kwanza consider mambo matatu
1. Unataka kufanya biashara gani
2. Mkopo utaanza kulipa baada ya muda gani
3. Jee una wanaokutegemea na wamekubaliana na uamuzi wako.

Haya mambo matatu ni muhimu sana. Nilipo acha kazi yangu sikujua haya mambo matatu yana umuhimu kiasi gani.

Kujua biashara utakayo fanya nje ndani ni muhimu sana, sababu hutopeteza muda mwingi kujifunza na hutokuwa kwenye risk ya kupoteza sehemu kubwa ya Mtaji.

Lini unaanza kulipa mkopo is very important, sababu kama unaanza kulipa ndani ya week chache basi ujue kabisa inabidi uwekeze kwenye cash cow business.

Familia lazima wasupport to some extent. kama umeowa na mke kila siku atakuwa anasema nilikwambia usiache kazi nilikwambia this and that basi ujue upo kikaaangoni kaka.
 
nakushauri omba ruhusa uende shule tena ukiwa unajiandaa kuanza biashara ili uweze kujua nje ya kazi kuna nini hii itakusaidia kuwa na muda wa kutengeneza network lakini ukiwa bado kazini na pia shule.
kama una shahada ya kwanza nenda master au post, miaka mitatu ni michache sana kuacha kazi ya serikali kumbuka kwamba hakuna fao la kujitoa.
hivyo tumia fursa hiyo kujipanga.
pia ni vizuri ukaweka wazi ni biashara gani unategemea kufanya ili tukushauri kwa ukaribu zaidi chagua hata tatu.
binafsi nafanya biashara ya ushauri lakini kuna kipindi wakati naanza ilipita miaka kama mitatu napata vijikazi vidogo sana kiasi vilikuwa haviwezi kulipa gharama za ofisi. ikawa nafika wakati naomba poo kwa kutafuta kazi.hivyo jipange taratibu kabla ya kujilipua
Hakuna fao la kujitoa??? LAPF wana hilo fao mbona
 
Miaka mitatu kazini midogo mkuu! Ungesubiria angalau kumi,then chukua huo uamuzi.
 
NAONA UNATAKA KUISOMA NAMBA KWA KUJITAKIA.KILA LA HERI MKUU
Watu kama wewe bila kuajiriwa hakuna maisha,kwa hiyo usimkatishe mwenzio tamaa,mwenzio kasoma alama za nyakat na anataman kuwa zaid ya alipo,hakuna ubishi kuajiriwa ni kuminywa akili yako ili ubaki ukimtegemea na kumnyenyekea aliyekuajir siku zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukikopa dhamana yako ni nini,serikalini ukikopa ujue mshahara ni wao,wewe ukisepa unakuja kujikuta wanaidaka pesion yako ila with miaka miiiingi interest kubwa. Biashara ni ngumu mno la msingi omba kazi sekta binafsi ya ofsi unayotaka kufanya.Mfn ukifanya kazi benki unaweza kufungua sacos.Biashara nyiiingi sasa ni kama zimeingiliwa na kilamtu,nothing new...kama ni msomi unajua kwanza inatakiwa ufanye reseach ya biashara hiyo na kuplan mapato na faida. Au shirikiana na vijana waliopo tayari uwe na hisa.
 
Wakuu habari za majukumu.

Natambua JamiiForums ni kijiwe cha wasomi na mchanganyiko wa watu wenye busara zao.

Najitokeza mbele yenu mnipe ushauri kidogo, kwa ufupi mimi ni muajiriwa katika serikali yetu hapa Tanzania, kutokana na changamoto za kazi na hali halisi ya maisha nina plan kukopa fedha kiasi cha 10m kisha nianzishe miradi yangu binafsi ili nijiajiri niachane na kuajiriwa maana naona napelekeshwa ilihali maslahi ni duni sana.

Kazi ni nyingi mno na maslahi ni kiduchu sana, nilitamani kuanzisha miradi nikiwa katika ajira lakini muda ninaoingia na kutoka kazini ni wastani wa masaa 11 mpaka 12 kwa siku, hali hii inanichosha sana kiasi kwamba hata nikifika home akili inakua imechoka sana naishia kulala tu.

Kwa mantiki hiyo naona umaskini wangu unaweza kua wa kudumu maana hata nikiwatazama walionitangulia naona hawana kitu kikubwa sana walichofanya maishani.

Nina dreams nyingi na kubwa, napenda kua mtu huru na mwenye mafanikio makubwa kupitia biashara na kilimo, naiona ajira kama kifungo cha kunifanya niwe maskini. Sasa kwakua nimekaa kwenye system kwa takribani miaka mitatu naona ni vema nijilipue nikafanye yangu.

Naomba ushauri na mapendekezo yenu, watu hatulingani akili endapo unaona niko wrong basi naomba unishauri namna ya kuboresha hili wazo.

Kejeli na matusi sio mahala pake hapa, mimi ni kijana kama ulivyo kijana pengine nikawa sawa na mwanao ni vema unishauri kwa kujua unamshauri ndugu yako na mwana JF mwenzako.

Natanguliza shukrani.

Ushauri wangu: Usithubutu kuchukua mkopo kufanya biashara wakati umeacha kazi! Hata kama unafanya kawi masaa mengi chukua mkopo anza biashara unayoitaka polepole, lala hata masaa matano tu kwa siku ikibidi (katika kipindi hicho cha mpto), uache kazi pale tu unapoona biashara inaanza kutoa mwanga. Usiache kazi kijana!
 
Ni wazo zuri kama pesa ungekuwa umesave mwenyewe lakini ya kukopa ndugu yangu kwenda kuanzisha biashara mpya, bila kujua changamoto zake sikushauri uache kazi, badala yake, tafuta kimtaji chako kidogo jaribu kufanya hiyo biashara ambayo unataka kufanya jaribu hata kwa mwaka hivi utakuwa umejifunza, hapo unaweza kukopa kuongezea kwenye biashara na kuacha kazi.

Mimi nilifikia hatua ya kuacha kazi baada ya miaka 6 kazini, sikuona mabadiliko yoyote kwenye maisha yangu, mwisho niliamua kuacha kazi, wakati nimeacha nilikuwa nimesave kama milion 3 zangu peke yangu, nikauza mpaka vitu vya ndani kuongezea mtaji, nilijitesa ndani ya miezi 6 mambo yakaanza kunyooka. Toka nimeacha kazi nina miaka 2 niliacha sina hata kiwanja, lakini sasa ni nyumba 1 na viwanja 3, watoto wanakula, shule wanakwenda, biashara imesimama, account inasoma, Natembelea miguu minne, nina muda wa kutosha kufanya mambo yangu, nimetengeneza ajira zaidi ya watu 15. Ninatoa amri mimi wala hakuna wa kunipangia. Maisha ya kitumwa nilishatoka. Karibu sana ndugu yangu

Sent using Jamii Forums mobile app

Flowery story with no specifics. Kama ushuhuda wa kanisani kabla ya kumpa mchungaji sadaka.
 
Anzisha kwanza biashara ikikolea ndio uzembee kazini usiache kazi kabla hujapata kazi. Mimi nakaribia kuacha baada ya kumaliza haka ka Master kangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Yani unaacha kazi sababubumepata mastaz au sababu unaenda kufanya biashara zako....ni vip masterz yako inahusiana na biashara unayotaka kufanya na inakupa assuarance ipi ya kufanikiwa katika mambo yako.
take from me .... hizi elimu za shule au vyuo huwa hazina tija katika mapambanobya mtaani...ndio maana mabilionea karibu wote duniani hakuna hata mmoja prof seuse doctor.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
....Amekuambia kazini daily anatumia 11- 12 hrs, na pia akirudi hoi bin taabani, vp tena ataweza kusimamia biashara?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawajua wanamshauri kwa nidham ya uoga...hakuana uoga kama umeajiriwa na unafanya biashara zako...zitaendelea kuwa za kawaida tuu na hazitokuwa mpaka siku utakayoacha kazi na kusimamia biashara zako mwenyewe.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
Kaka Nina mengi ya kukushauri lkn sina mda wa kutosha kuandika hapa pia nina uvivu sana wa kutype. Labda nikukumbushe jambo, kaka ni ngumu kuacha kazi ili ukatafute kazi, tafuta kazi ndiyo uache kazi. Anza shughuli ndogo ndogo kwanza za kiabiashara ndiyo ujue nini ufanye

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kumtia woga...from zero to hero. Haitaji kutafutavkazi wala ajira...anahitaji kufanya biashara zake....zimtoe utumwani mwa ajira isiyolipa wala kumuhakikishia mwisho mzuri wa maisha yake

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
Pole sana kwa changamoto unazopitia lakini ongera kwa kutafuta freedom. Wengi wa watu waliokushauri wanakwambia mtaji huo ni bora unge make mwenyewe alafu ukanzia biashara then badaye ndo uchukuwe mkopo ili kudevelop business ni lakini option mbili ni muhimu hasa ikijuwa unachotaka kufanya.Ngoja nikupe story yangu labda uka learn kitu.
Mimi nilianza kazi mwaka 2014 mkoani mtwara,katika maisha yangu ya kazi sikuwa kufurahia kazi yangu hata siku moja nilikuwa na ndoto in my life so nikaona nikitegemea kazi siwezi kufikia ndoto zangu.Nikaamuwa kuchukuwa loan 2015 nikanunuwa shamba la mikorosho ile kufika 2016 soko la korosho likacheuwa nikapiga pesa nzuri tu naweza sema nilichanga karata zangu vzr.Nilikamata 10mil kupitia shamba zile pesa nikafunguwa beiber shop.Thanks God mambo yanaenda powa nimewekeza sehemu nyingine ya kuuza juice ya miwa na matunda mengine.Pia this year nalimia shamba langu la korosho kama kawaida.Sijawahi juta since nimechukuwa loan. Nimeweza kujenga nyumba within 3yrs nina usafiri(ndinga) +viwanja 3.Mshahara wangu nautumia kwa kusaidia ndugu zangu na matumizi madogo tu.
Mytake .Use you're salary kama mtaji wa kuanzia biashara lakini nakuomba usiache kazi kwa haraka hadi uweze kusimama vzr.Mimi sijaacha kazi ila sitafikisha ten yrs kazini.Anza sasa usisubiri kesho

great thinker
Acha kumtia uoga na story yako...wewe unatumia masaa 11 kazini bado usafiri na uchovu huo muda hana wa kufanya kazi huku kajiajiri...mzigo mzito mpe mnyamwezi...wewe mzigo wako mwepesi beba mwenyewe ....yeye mnyamwezi atabeba mzigo wake mzito.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
Back
Top Bottom