Ushauri: Ndugu wameharibu ndoa ya dada yangu

Ushauri: Ndugu wameharibu ndoa ya dada yangu

Akiuawawa je na vipigo?

Anko wangu siku aligombana na mkewe na ulikuwa usiku wa saa sita wanapokaa ni karibu na wazazi wote wa mke na mume.

Walivyogombana mwanamke usiku usiku akaenda kwao akawakuta wazazi wake wamelala akawagongea kuulizwa haya vipi saizi akasema mmewe kampiga kwaiyo kaona bora akimbie asije akafa

Mama mtu akataka kumkaribisha ndani ila mzee akagoma akasema hizo taarifa ni za upande mmoja kwaiyo hawezi kumpokea kwani yeye ni mke wa mtu hata kama ni mwanae, mzee akamtimua japo ni usiku sana.

Anko alivoona mke kaondoka na hajui alipokwenda alienda kutoa taarifa kwa kwa wakwe kwamba mkewe kakimbia hajui alipokwenda na usiku ule basi mzee akamwambia alifika muda huu tukamrudisha huko basi alienda home ila hakumkukuta akaingia ndani akambonji hata dk kadhaa hazikukata anasikia mtu anagonga kufungua ni mkewe mahojiano yakaanza ila baadae walielewana na maisha yakaendelea hadi leo wapo pamoja.

Funzo: hapo hukutakiwa kumpokea kabisa hata kwa sekunde ila ungemwambia aje na mwenzie wajieleze wote ungenusuru ndoa ya dada ako.
 
Ndoa ni ya watu wawili ukiweka mtu wa tatu lazima ivunjike...

Mwambie dada yako Aache utoto...
Aache na tayari ameshayakanyaga. Hapo ndio basi tena. Yaani ukae mbali na mwanaume miezi 11 utegemee aendelee kuamini wewe ni muaminifu kwake?
 
Katika watu wenye viherehere kwenye mahusiano mapya ni ndugu wa kike wa mwanamke especially Mabinamu,dada na wadogo za mke,mama,mama wadogo na mashangazi plus marafiki zake mke.

Hawa watu huwa wanajipa custody ya kuendesha affairs za uhusiano wa mtu utadhani ndoa inawahusu na wao ndani.

Wanawake miaka yote huwa wanahadharishwa kuwa makini na hawa viumbe na kuzingatia swala la faragha ya ndoa. Lakini kutwa kucha wao ni kukazana kuwapa hawa watu siri za faragha za ndoa matokeo yake hawa watu wanageuza maswala ya kwenye faragha ya ndoa yake kuwa public topics na kuharibu ustawi wa hiyo ndoa.

Kosa ambalo utafanya kama mwana ndoa ni kuendekeza kuongea mambo ambayo yanazungumzika ndani ya ndoa kuyapeleka nje ya ndoa. Hili jambo halijakaa sawa kabisa. Kama mwenzako anakubali kukaa chini na wewe kuongea maswala yenu then acha kutoa mambo nje ili upate attention ya kijinga kwa watu ambao hawatakupa msaada wowote ndoa yako itakapovunjika.
 
Back
Top Bottom