Red Giant;Wandugu age tuliyopo sasa inaitwa information age.
Bila kujisomea hii age itatusumbua sana.
Ilikushindana nayo lazima tuwe watu wa kujisomea na tabia ya kuujisomea huanzia nyumbani.
Mimi ni msomaji sana wa vitabu na credit zote nampa mama yangu. Maza ni la saba na anakazi ya kima cha chini lakini ni mtu anapenda sana kujisomea.
Nyumbani kulikuwa na vitabu kama mwanamalundi, kikosi cha kisasi, tutarudi na roho zetu, dunia uwanja wa fujo, abunuasi, adili na nduguze na vingine vingi na magazeti mengi tu.
Kwa hiyo kitu cha kwanza hakikisha vitabu vipo nyumbani. Watoto ni wadadisi watasoma tu, sasa wewe umejaza bongo movie na series za kikorea halafu unaona ufahari, kabati zima na hamna hata kitabu kimoja.
Dingi hujawahi hata kurudi na gazeti we unarudi na merlin, legend of the seeker na mambo kama hayo unafikiri watoto watapenda kujisomea?
Kama wewe uko hivi nakushauri uchonge shelf la vitabu na uanze kununua vitabu, mbona bei ni sawa na series za jaki bawa.
Jambo la pili ni wewe pia kuweka mfano kwa kujisomea, hata kama haupendi just do it for the sake of your children. Usitegemee wanaokupenda kujisomea wakati wewe mwenyewe ni mtu wa Isidingo na la Mujer.
kaka point taken ila kumbuka kwa nchi kama yetu ambao tabaka kubwa ni maskini na hawajasoma ni ngumu kuelewa hali halisi ya jinsi mambo yanavyoenda,na hata kama watajua basi hawatatilia uzito mkubwa saaana...ndiyo maana tunasema taaluma ya mtoto it is a dual process,both state and individuals are concerned to make it foster...na kaka kumbuka nyakati ambazo umesoma wewe na sisi watoto wa kata are quite different,...kipindi hicho mtoto alikuwa akifeli mara nyingi ilikuwa ni yeye mwenyewe aidha(utukutu uliokithtiri),au(hali ngumu ya maisha nyumbani) au(serikali iwe imeshindwa kumuendeleza).Ila yote kwa yote ujumbe wako ni mzuri lakini mpaka sasa umetufikia sisi watanzania watanzania wachache saaana almost 15 percent wenye umeme na pia 0.000002 wenye access na internet,mathalani siyo watanzania wote tuko jamiiforums...na hata kama tupo basi tumejikita TROLLING kwenye JUKWAA LA SIASA na MAPENZI...IN OTHER WAYS I CAN SAY THIS IS A PARADOX,YOU HAVE ADDRESSED A RIGHT ADVICE TO A WRONG PERSON,..thou some of us have taken it because it does matter.,..
Sasa mkuu RED GIANT illiteracy is a global catastrophy,wewe labda ungetoa ushauri jinsi gani tutawafikia wale wazazi ambao wana watoto but ukali wa maisha umewafanya washindwe kufanya kama mama yetu alivyokujengea mazingira wewe mazuri.
😛eace: :tea:
😛eace:😛eace:
NI KUJUMU LETU SOOOOOOTE.
cheers