Ushauri: Niende Serikalini au nibaki private sector

Ushauri: Niende Serikalini au nibaki private sector

Kwa hiyo mtu huoni hata aibu kupokea mshahara wakt unajua kabisa hakuna cha maana ulichofanya?
Ni taasisi gani hiyo ya umma mnaishi maisha hayo ya kuzurura kutoka office hii kwenda office hii?
Ndiyo hatuoni aibu njoo wewe unaeona aibu upige kazi kwa niaba yetu
 
Ndio hvyo mkuu private ni kuwa na confidence inasaidia sana usiwe na wasiwasi kwamba mwakani mkataba ukiisha sijui itakuwaje sijui nitaishi vipi usiwe na haya mawazo.
Yaani mimi enzi zangu ni kijana mdogo bado niko wa moto nimetoka chuo nina kauzoefu kama cha miaka miwili hivi ukiniita interview najikoki kuna maswali ukiingia kwenye mfumo wangu kama wewe ndio HR lazima unichukue kwa mikwara na mbwembwe nilizokuwa nazo unaniuliza swali moja nakupa majibu matatu.
Ikafikia hatua nikawa malaya wa kazi na kila mwezi nahudhuria interview angalau moja.
Na ilikuwa kila mwezi nahudhuria interview moja kwa ajili ya mazoezi
Umetisha sana. Kongole mkuu.
 
Acha kukariri sio sehemu zote kuna maeneo anayeanza anaanza na 3M
Watu wengi wanajua serikalini watu wanategemea mishahara hawajui kama kuna per diem kuna dereva mmoja wa RUWASA na bonde anapotea mwezi site huko akirudi karatasi za madokezo kama karatasi za mtihani wa mathematics ila mishahara yao midogo ila wanapiga pesa za site sio mchezo.
 
Aisee! Kumbe ww pia unao uzoefu na hao watu. Kwa bahati mbaya au tuseme kwa kutokujua, vijana wengi baadhi yao wanaangalia hapa karibu na kiasi cha hela atakachopata ndani ya muda mfupi na kusahau kwamba siku zinakimbia mno na mabadiliko ni mengi. Hao watu hawaangalii makunyanzi. Private Sector siku za mwanzoni utaona kama umefanikisha lakini baadaye wanakubadilikia.
Asante kwa kushare uzoefu wako. Huyo bwana 2in1 kama atatulia na kuzisoma comment kwa umakini atakuwa amejifunza kitu hapo.
Kweli mkuu sisi tunatoa experience kutokana na tuliyo yashuhudia sio lazima afuate ushauri wetu ila afanye kwa akili yake ili baadae asimlaumu mtu kama amelazimishwa akili za kuambiwa changanya na zako.
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
Nenda serikalini utakuja nikumbuka!
 
Jibu haya maswali:

1. Shirika limeanza lini?
2. Mapato ya Shirika ya natoka wapi?
3. Una nafasi gani kwenye shirika?

Ajira haipimwi kwa mshahara peke yake, kuna factors nyingi sana!

Amua mwenyewe!
Ningekujibu mkuu ila wenzangu wanapita sana humu nikikujibu hayo wazee wa kuunganisha dots watanijua na mm sitaki mtu anifahamu hasa wa kazini mana mpka sasa hamna anayejua kama nimepata kazi nyengine. Ukiangalia hata post yangu kuna vitu vingi sijavisema kwa maksudi kabisa kuna watu wana akili sana humu Jf
 
Ningekujibu mkuu ila wenzangu wanapita sana humu nikikujibu hayo wazee wa kuunganisha dots watanijua na mm sitaki mtu anifahamu hasa wa kazini mana mpka sasa hamna anayejua kama nimepata kazi nyengine. Ukiangalia hata post yangu kuna vitu vingi sijavisema kwa maksudi kabisa kuna watu wana akili sana humu Jf

Huna haja ya kujibu; hayo majibu yatakupa mwangaza, angalia;

1. Goin concern ya unapofanya kazi.
2. Ukuaji wako katika ajira.
3. Mahusiano yako kazini!

Serikalini kuna security tu na ufukuzwaji sio rahisi, ila kwa kweli nitoke Dar na connection zake niamie Tabora? Hapana aisee!
 
Serikalini Kuna uwezekano wa kupata muda wa kufanya mambo Yako binafsi tofauti na private wanabana mpaka penalty kutegemeana na nafasi uliyonayo.

Ni ngumu sana kutoboa Kwa mshahara pekee. We jiulize tu tangu umeanza kazi hapo private sector umesave kiasi Gani? Au chukua Pato lako Kwa mwaka na angalia vitu ulivyofanya uone kama vinaendana na kipato chako.

Mwisho. Nenda serikalini kama sehemu ya kujishika ili uweze kufanya mambo Yako binafsi coz utakuwa na access ya mkopo kama mtaji ni tatizo kwako.

Maamuzi ni Yako ww ndo unajua undani wa hizo kazi.
 
Serikalini Kuna uwezekano wa kupata muda wa kufanya mambo Yako binafsi tofauti na private wanabana mpaka penalty kutegemeana na nafasi uliyonayo.

Ni ngumu sana kutoboa Kwa mshahara pekee. We jiulize tu tangu umeanza kazi hapo private sector umesave kiasi Gani? Au chukua Pato lako Kwa mwaka na angalia vitu ulivyofanya uone kama vinaendana na kipato chako.

Mwisho. Nenda serikalini kama sehemu ya kujishika ili uweze kufanya mambo Yako binafsi coz utakuwa na access ya mkopo kama mtaji ni tatizo kwako.

Maamuzi ni Yako ww ndo unajua undani wa hizo kazi.
Asante kiongozi, ni kweli private mshahara mkubwa lakini sina muda wa kufanya jambo lolote la ziada nimebanwa sana ila pia sijapata uhakika kama na huko serikalini napo hakubani kama huku
 
Asante kiongozi, ni kweli private mshahara mkubwa lakini sina muda wa kufanya jambo lolote la ziada nimebanwa sana ila pia sijapata uhakika kama na huko serikalini napo hakubani kama huku
Serikalini haubanwi kivile; ndo mana jamaa hapo juu Lucha post # 75 amediriki hata kutumia neno kuzurura akimaanisha utakuwa na muda wako mwingi wa ziada uhamue utafanya nini au utautumiaje na bado mshahara utalipwa kama kawaida na hata Ndechumia post #132 amekazia hiyo hoja ya kufanya serikalini vs Private.
 
Back
Top Bottom