Ushauri: Niende Serikalini au nibaki private sector

Ushauri: Niende Serikalini au nibaki private sector

Ni kweli mimi baada ya kumaliza chuo niliwahi kufanya kazi halmashauri kama internship japo ni miaka mingi.
Nikayasoma mazingira nilichogundua ni kweli kuna watu wananufaika kwenye miradi ila si wote ni Mkurugenzi na Chief Engineer watu wa chini hawashirikishwi labda utaambulia hela ndogondogo za nauli ukitumwa ukabebe materials,so baada ya kuona hali hiyo nikaachana napo nikaendelea na mambo yangu mengine.
Swadakta. Ukiwa halmashauri usipojiongeza utadumazwa na mazingira ya kazi i.e. hutaweza kupata ujasiri wa kufukuzia Fursa nyingi kama wakubwa. Ila ukishagundua game limekaaje; utapapenda kwani ni almost nobody is behind tailing you kama inavyokuwa huko private.
 
Acha kukariri sio sehemu zote kuna maeneo anayeanza anaanza na 3M
Ni kweli ziko baadhi ya taasisi/mamlaka wanapokea hii mishahara ila kupata hadi uingie hapi huo mtanange wake sio wa kitoto hapo utakuwa unapambana na watoto wa vigogo ukipenya ujue mizimu ya kwenu imekusimamia kwelikweli
 
Mdogo wangu nikwambie ukweli tu.
Kama hiyo kazi ya serikali ingekuwa ni kwenye taasisi kama EWURA,TANAPA,BOT,TPDC ,TAZAMA hapo sawa ningekushauri uende serikalini lakini kwa hiyo kazi ya halmashauri ni kwenda kujitia umaskini tu na kibaya zaidi kwa hiyo fani yako hautajifunza chochote cha maana zaidi ya kuwa na maneno mengi kama dalali.
Kwa hiyo fani yako ukienda halmashauri utaenda kuwa fundi magari kwenye gereji yao ambayo huwa haipo active kivile maana gari zao zingine huwa wanazipeleka Temesa kwa ajili ya matengenezo.
Mwisho wa siku ndoto yako itakuwa tu uwe Supervisor wa gereji uanze kugombania cheo na wazee wakupige kipapai achana napo huko hakufai kabisa endelea kufanya private ili uwe smart kwenye kazi zako
Dah sio poa, haiwezekani kuhama taasisi?
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
Unataka uende serikalini kufanyaje? Unafata nini kipya?
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
....Wanaofanukiwa serikalini ni MACHAWA tu.....kama hauna element za uchawa nakushauri baki Private.....utanikumbuka
 
E government ndio nn kiongozi
Wakati unasubiri majibu hebu nichangie kidogo hapa: Kama unakumbuka miaka iliyopita sio zamani sana, uendeshaji wa Serikali ulikuwa ni ule wa Kianalogia. Siku hizi Utendaji wa Mamlaka za Serikali huenda Kidigitali (Egoverment). e.g. Unanunua na kulipia huduma za Serikali popote ulipo na wakati wowote kwa kutumia Mtandao wa Serikali bila kwenda dirishani au Ofisini ili ukalipe.
Hakuna tena "cha juu" labda kwa nadra sana. Hakuna usiri mkubwa kwenye utendaji wa Serikali e.g. Waziri wa Maji anaweza (akitaka) kujua kinachoendelea huko DAWASA leo bila hata kumwita mkurugenzi. kwa kutumia mtandao Website yao. Jambo hili limeziba mianya mingi sana ya Upigaji Serikalini e.g. watoza ushuru ni lazima watumie mashine za EFD n.k.
 
Kama siyo competent wahi serekalini kule hata uwe mbabaishaji unaenda kazini hufanyi kazi unazurura tu kutoka ofisi hii kwenda ofisi ile hadi jua linazama mshahara utapata wakikuchoka na ubabaishaji wako wanakuhamisha tu
Ila huo ujanja ujanja usiujaribu private sector wanakutumbua kabla hujavuta pumzi ya pili
Kwa hiyo mtu huoni hata aibu kupokea mshahara wakt unajua kabisa hakuna cha maana ulichofanya?
Ni taasisi gani hiyo ya umma mnaishi maisha hayo ya kuzurura kutoka office hii kwenda office hii?
 
Serikalini ni Job security tu,hasara yake ni kuwa unabweteka kuona kuwa bado una muda mrefu kazini,pili kuna mambo ya transfer za mara kwa mara,hapo Private ukikomaa kwakuwa pia mindset yako inasema "chochote kinaweza tokea at anytime" unaweza kukuta ndani ya muda mfupi umefanya mambo ya kutisha...
:AYOOO:
 
Kwa hiyo mtu huoni hata aibu kupokea mshahara wakt unajua kabisa hakuna cha maana ukichofanya?
Ni taasisi gani hiyo ya umma mnaishi maisha hayo ya kuzurura kutoka office hii kwenda office hii?
Nakazia hoja. Umemwambia ukweli. Ni jambo la kushangaza sana eti mTz tena msomi anamawazo hayo.
 
Umenena sawasawa. Umesema: "...private ni kwa ajili ya watu smart na competitive ambao wanajiupdate kila wakati ili kutengeneza impressive CV kuwavutia waajili wapya watakaokuchukua kwa dau refu zaidi."
1. Unadhani wasomi walioko kitaa sio smart na competitive halafu hawana CV zinazovutia? Kumbuka mshahara Private mara nyingi huwa ni negotiable.
2. Private Sector wanao mtandao wa mawasiliano baina yao. Ukiomba kazi huwa wanakufanyia usaili na kama huna "connection au mtu wa kukupigia debe" wanalo swali lao lile Ni kwa nini uliacha kazi huko na unataka kuja huku? Na je huku nako si utaacha kazi kama ulivyoacho kule? Badadaye hufuatilia utendaji wako na tabia yako huko ulikoacha kazi. Wakigundua madhaifu yako e.g. ww hapo udhaifu wako ni kutokutulia kazini i.e. ww ni mwindaji mashuhuri wa big salaries (Salary monger). Wanaweza wasikuchukue au wakaweka dau la chini ili ukatae kazi mwenyewe.
3. Sijakuelewa unaposema Kuji-update unamaanisha nini. Kusoma au Kupata mshahara mpya wa juu zaidi? Kama ni kusoma mbona hata hata ukiwa Halmashauri hukatazwi kujiupdate? Lakini uwe na sponsers vinginevyo unaishia Urusi frontline vs Ukraine.
Nitakujibu maswali yako kama ifuatavyo.
1.Impressive CV huwa inaandaliwa kwa miaka mingi mkuu kwenye uzoefu wa kazi sasa kama umekaa tu kitaa CV yako itapanda vipi ili iwe impressive.
Tunapoongelea CV hatumaanishi kumiliki mavyeti makubwa ya darasani la hasha bali CV inahusisha zaidi uzoefu ulioupata kazini baada ya kusomea fani yako.
2.Private sector huwa hawana mtandao rasmi unaowaunganisha kampuni zote na kampuni za private huwa zina ushindani/uhasimu baina yao kama ilivyo simba na yanga(mchezaji mzuri wa yanga simba wanamnunua),mfanyakazi hodari wa Cocacola Pepsi wanamnunua,mfanyakazi mahiri wa Tigo Vodacom wanamchukua iko hivyo yaani sasa wakishaikubali kazi yako hawawezi kukuacha eti kwa vile uliacha kazi kampuni yako ya zamani,hiyo ni propaganda tu.
3.Kujiupdate namaanisha ni kuangalia je ni kipengele gani cha kazi yako kipo hot cake sokoni kwa sasa kisha unajifunza kwa vitendo kisha unakiongeza hicho kipengele kwenye CV yako na siku ukiitwa interview ukaulizwa maswali kuhusu hicho kipengele utaprove kwamba unajua kisha ukisgaipata hiyo kazi unakifanyia mazoezi zaidi ili kuwa mbobezi.
Sasa hapo utaangalia wewe ni wapi utaenda kujifunza kwa vitendo either kazini au kwenye professional courses training centres ambao wako practical oriented.
Ukifanya hivi utajikuta kila mwaka CV yako inapanda na mshahara nao utakuwa unapanda kwa spidi unayoitaka wewe.
 
Nitakujibu maswali yako kama ifuatavyo.
1.Impressive CV huwa inaandaliwa kwa miaka mingi mkuu kwenye uzoefu wa kazi sasa kama umekaa tu kitaa CV yako itapanda vipi ili iwe impressive.
Tunapoongelea CV hatumaanishi kumiliki mavyeti makubwa ya darasani la hasha bali CV inahusisha zaidi uzoefu ulioupata kazini baada ya kusomea fani yako.
2.Private sector huwa hawana mtandao rasmi unaowaunganisha kampuni zote na kampuni za private huwa zina ushindani/uhasimu baina yao kama ilivyo simba na yanga(mchezaji mzuri wa yanga simba wanamnunua),mfanyakazi hodari wa Cocacola Pepsi wanamnunua,mfanyakazi mahiri wa Tigo Vodacom wanamchukua iko hivyo yaani sasa wakishaikubali kazi yako hawawezi kukuacha eti kwa vile uliacha kazi kampuni yako ya zamani,hiyo ni propaganda tu.
3.Kujiupdate namaanisha ni kuangalia je ni kipengele gani cha kazi yako kipo hot cake sokoni kwa sasa kisha unajifunza kwa vitendo kisha unakiongeza hicho kipengele kwenye CV yako na siku ukiitwa interview ukaulizwa maswali kuhusu hicho kipengele utaprove kwamba unajua kisha ukisgaipata hiyo kazi unakifanyia mazoezi zaidi ili kuwa mbobezi.
Sasa hapo utaangalia wewe ni wapi utaenda kujifunza kwa vitendo either kazini au kwenye professional courses training centres ambao wako practical oriented.
Ukifanya hivi utajikuta kila mwaka CV yako inapanda na mshahara nao utakuwa unapanda kwa spidi unayoitaka wewe.
Nimekupata mkuu.
 
Wakati unasubiri majibu hebu nichangie kidogo hapa: Kama unakumbuka miaka iliyopita sio zamani sana, uendeshaji wa Serikali ulikuwa ni ule wa Kianalogia. Siku hizi Utendaji wa Mamlaka za Serikali huenda Kidigitali (Egoverment). e.g. Unanunua na kulipia huduma za Serikali popote ulipo na wakati wowote kwa kutumia Mtandao wa Serikali bila kwenda dirishani au Ofisini ili ukalipe.
Hakuna tena "cha juu" labda kwa nadra sana. Hakuna usiri mkubwa kwenye utendaji wa Serikali e.g. Waziri wa Maji anaweza (akitaka) kujua kinachoendelea huko DAWASA leo bila hata kumwita mkurugenzi. kwa kutumia mtandao Website yao. Jambo hili limeziba mianya mingi sana ya Upigaji Serikalini e.g. watoza ushuru ni lazima watumie mashine za EFD n.k.
Shukran kiongozi
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.
Una umri gani? Upo fani gani? Malengo yako ni yapi?
 
Baki ulipo !! Labda ukishapata CHQ No. ukae huku ukiangalia namna ya kutoka hapo (kama unauwezo wa kufanya hivyo) kwenda kunakoeleweka kulingana na taaluma yako !! Otherwise baki ulipo !!
 
Nimekupata mkuu.
Ndio hvyo mkuu private ni kuwa na confidence inasaidia sana usiwe na wasiwasi kwamba mwakani mkataba ukiisha sijui itakuwaje sijui nitaishi vipi usiwe na haya mawazo.
Yaani mimi enzi zangu ni kijana mdogo bado niko wa moto nimetoka chuo nina kauzoefu kama cha miaka miwili hivi ukiniita interview najikoki kuna maswali ukiingia kwenye mfumo wangu kama wewe ndio HR lazima unichukue kwa mikwara na mbwembwe nilizokuwa nazo unaniuliza swali moja nakupa majibu matatu.
Ikafikia hatua nikawa malaya wa kazi na kila mwezi nahudhuria interview angalau moja.
Na ilikuwa kila mwezi nahudhuria interview moja kwa ajili ya mazoezi
 
Wakuu habari, niliomba kazi taasisi flani ya umma (utumishi) sikupata nafasi jina langu likahifadhiwa kwenye database juzi kati kuna mkeka wa kuitwa kazini umetoka na jina langu likiwemo kwenye kazi za halmashauri. Ila kwa sasa kuna taasisi binafsi nafanya kazi ambayo nalipwa vizuri sana nimefuatilia mshahara wa hapa ni zaidi ya mara mbili ya mshahara huo wa serikalini na haki nyengine zote za mwajiriwa napata kama bima n.k ila changamoto ya hapa private mkataba wao ni wa miaka 3 ila unarenew kila mkataba unapoisha hawana shida.

Serikalini nimepangiwa Tabora na mimi makazi yangu miaka yote ni Dar sasa nikienda huko naenda kuanza moja.

Nilifikiria kutoenda huko ila kuna mtu kaniambia nisipoenda utumishi jina langu litakuwa blacklisted na sitopata tena nafasi nyengine ya kuingia serikalini maisha yangu yote.

Kuna ukweli wowote juu ya hili au nifanye nini wakuu I'm so confused nakosa usingizi kabisa.

Jibu haya maswali:

1. Shirika limeanza lini?
2. Mapato ya Shirika ya natoka wapi?
3. Una nafasi gani kwenye shirika?

Ajira haipimwi kwa mshahara peke yake, kuna factors nyingi sana!

Amua mwenyewe!
 
Back
Top Bottom