Ushauri: Nimebeba ujauzito wakati mshono wa mimba ya kwanza haujapona vizuri

Dunia

Member
Joined
Nov 8, 2014
Posts
96
Reaction score
19
Wakubwa shikamooni, wadogo habari zenu!

Mimi ni binti wa miaka 24, nilijifungua kwa operation mwaka jana mwezi wa pili tarehe 12.

Kwakuwa ngozi yangu laini na mshono unanisumbua, dokta alinishauri nisibebe ujauzito hadi miaka mitatu ipite, kwa bahati mbaya nimejikuta nina mimba ya wiki tatu.

Sasa sijui nifanyeje!, naogopa kwenda kwa daktari maana atanitukana, nikiwambia wazazi ndio kabisa hawatanielewa, nikisema niendelee na ujauzito mshono utafumuka na nitapoteza uhai.

Ushauri wenu jamani, asanteni.
 
Jibu liko wazi kuwa kama hutaki kufa maana Yake toa mimba,kama unataka kufa iache.
Hayo mengine ya kuogopa wazazi au Dokta hayana maana kwasababu hawataweza zuia kifo chako kama kweli suala ni kifo.
 
Ngozi laini muache kujichubua madhara yake ndio hayo!! Muombe sana Mungu maana kwake yote yawezekana, usitoe mimba.
 
Jibu liko wazi kuwa kama hutaki kufa maana Yake toa mimba,kama unataka kufa iache.
Hayo mengine ya kuogopa wazazi au Dokta hayana maana kwasababu hawataweza zuia kifo chako kama kweli suala ni kifo.
asante ndugu kwa ushauri, uwenda ukawa unajua vidonge vya kumeza au chochote kuhusu kutoa na maelezo yake uniinibox rafiki yangu
 
asante ndugu kwa ushauri, uwenda ukawa unajua vidonge vya kumeza au chochote kuhusu kutoa na maelezo yake uniinibox rafiki yangu
Huu sasa ufala

We chukua kisu jikate hapo tumboni kwa chini alafu toa mtoto alafu chukua Uzi wa viatu na sindano ya kushonea magunia ya viazi shona taratibu kuepuka maumivu makali,ukimaliza kausha na pasi ila angalia usigusishe kwenye kidonda.
Ukimaliza leta mrejesho.
 
Usitoe fanya sana ibada, mrudie Mola wako ili ikitokea umeondoka unauhakika wa pepo. Lakini kutoa unavunja amri ya USIUE.
 
wakubwa shikamooni, wadogo habari zenu! mimi ni binti wa miaka 24, nilijifungua kwa operation mwaka jana mwezi wa pili tarehe 12. kwakuwa ngozi yangu laini na mshono unanisumbua, dokta alinishauri nisibebe ujauzito hadi miaka mitatu ipite, kwabahati mbaya nimejikuta na mimba ya wiki tatu. sasa sijui nifanyeje!, naogopa kwenda kwa daktari maana atanitukana, nikiwambia wazazi ndio kabisa hawatanielewa, nikisema niendelee na ujauzito mshono utafumuka na nitapoteza uhai. ushauri wenu jamani, asanteni
 
Kamuone daktari. Hata kama akikutukana, mwisho wa siku atakutathmini kitaalamu na kukushauri kutokana na afya yako itakavyokuwa.
 
Pole sana. kamuone daktari. Kamuone daktari haraka iwezekanavyo. Ila usijaribu kutoa maana ni laana na ni mauaji kwa mtoto asiye na hatia. Daktari anaweza kukushauri kupata muda wa kutosha kupumzika na kukufanyia upasuaji mtoto akishakomaa tumboni. Ila baada ya hapo ongeza uangalifu lisijirudie tena. Pole na Hongera sana.
 
Kamuone daktari. Sidhani kama kuna daktari ambaye anaweza kumkemea mgonjwa. Umeolewa? Kama umeolewe nenda na mumeo kwa daktari ili pia apate ushauri wa namna gani ya kwenda mbele
 
Hapo kamwone daktari hata kama ni kukutukana maana hata usipoenda saiv in near future lazima uende. Usisubiri mpaka hali iwe mbaya ndio uende unaweza ukapoteza maisha. The sooner the better
 
Nikiwa form three nilisoma kuwa moja ya aina ya abortion ni ile inayoruhusiwa na madakitari ili kunusuru afya ya mama. Kwa usalama wako kamuone Dr.
 
Ngozi yako laini kivipi?hiyo sio kawaida utakua umejichubua sana,kuna mawili kama mnene sana mshono huwa unafumuka na kama umejichubua,binti kuchanwa tumbo utoe mtoto haihusishi ngozi ya juu pekee,
 
Pole, kamuone dokta.

Natumaini utajifungua salama.
 
Ngozi yako laini kivipi?hiyo sio kawaida utakua umejichubua sana,kuna mawili kama mnene sana mshono huwa unafumuka na kama umejichubua,binti kuchanwa tumbo utoe mtoto haihusishi ngozi ya juu pekee,
asante kwa ushauri, sijawai kujichubua, sema mimi ni mnene
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…