Ushauri: Nimeokota wallet yenye Tsh. 50,000 pamoja na risiti za miamala ya pesa nyingi nahofia kurudisha nahisi naweza bambikiwa kesi

Natamani kupata namba Yako nikupe Walau vocha kwa ushauri mzuri tatizo hela imeshaishaπŸ˜‚
 
Ukishaamua kurudisha basi kubali kua unafanya wema. Jamaa angemwambia tu kua nakuletea simu yako ila andaa kichache sasa hajaongea analalamika nini tena.
 
Ukishaamua kurudisha basi kubali kua unafanya wema. Jamaa angemwambia tu kua nakuletea simu yako ila andaa kichache sasa hajaongea analalamika nini tena.
Kimazoea ili siku ingine awe na moyo mengine yanaua uaminifu
 
Kimazoea ili siku ingine awe na moyo mengine yanaua uaminifu
Hamna hiyo kitu mzee, kama yeye karudisha kwa wema na uaminifu malipo ya nini?? Mwema ni mwema tu kama ni muumini basi hapo hamna baraka aliyopata maana karudisha kwa kinyongo.
 
Wallet inakuwaje na mil 10?umeiokotea wapi ,katika mazingira gani?ni wewe tu umeiona?kama kweli msamalia mwema peleka polisi
Hajasema wallet ina milion 10 """ amesema wallet ina risiti za miamala ya 10 m na 40m
 
Nini maana ya kuokota! Kuokota ni kujimilikisha kitu ambacho sio chako eti kwasababu umekikuta katika mazingira yanayoonyesha hakina mwenyewe! Lakini ukikuta kitu kina viambatanishi vinavyoonyesha jina, anuani, namba ya simu basi hapo sio kuokota ni wizi. Una njia mbili: moja ni kupita tu na kukiacha kitu hicho (hii ndo njia salama kabisa), njia ya pili ni kukipeleka polisi na kutolea maelezo (hii njia sio salama) sababu hujui mazingira yaliyonyuma ya kukutwa kwa kitu hicho hapo. Kama ulikuwa na njaa ya pesa basi dokoa kiasi sepa!
 
Una nyota nzuri mkuu.🀣🀣
 
Kuna uhusiano mkubwa wa kuwepo roho nyuma ya kuokota hela! Kuna kipindi nimepigika choka mbaya nilikuwa naokota mara, 10k, 5k, 2k, 1k na jeto, 200, 100, hadi 50. Sasa baada ya kujipata, sijawahi kuokota hata mia mbovu. Hapo ndo nikajua kupigika kwangu kulikuwa na mashetani yamekaa katika mlango wa kuzuia kipato. Yakiona vipi yananiachia hivyo vijisenti! Sasa mbona baada ya kujipata siokoti? Hata hivyo sitaki kuokota! Nataja za jasho langu
 
Mimi nikiona coins huwa siokoti πŸ˜€
 
Kwani unataka kurusha wapi?
 
Nenda polisi Mkuu waambie wampigie simu muhusika aje kuchukua vitu vyake achukulie hapo polisi. Ila polisi usiwaachie wenyewe hiyo wallet na wao ni binadamu kama kweli una nia ya kumrudishia basi wampe muhusika ukiwepo
Kama aliuawa kwa ujambazi then vitu vimetupwa makusudi ili wasihisiwe kwenye tukio, unaujua msemo wa 'anayekutwa na ngozi........ .
 
Hahahahaha,🀣🀣🀣
Nimecheka sana aiseee,
 
Hatokuja bahatika Tena,katu
Yaani elfu 50 ni kubahatika!!!!! Watu mna roho ngumu. Ingekuwa hata hela unayoweza kununua jumba sawa. Hiyo ukipanda daladala masaa mawili imeisha!!!



Siku za nyuma mtu alikosea akatuma laki moja kwenye namba yangu. Nikiangalia,namba ni ngeni. Nikajiuliza nani huyu ananipa hela ya siku kuu, na nilivyopinda hivi. Sikuitoa. Baada ya kama nusu saa, akapiga mdada, anaomba samahani, na kwamba alikuwa anamtumia mama yake mzazi hela ya siku kuu. Akaomba nikate 20k basi nimrudishie 80k. Nikafanya hivo. Badae roho ikakataa. Hii pesa si harari yangu, hujui kaipatapataje, na yenyewe nikamtumia. Hakuamini. Hatufahamiani, ila sometimes salamu salamu.

Kuna vitu vingine ni vidogo siyo vya kukushushia hadhi, na wakati mwingine unaweza kukuta kitu kidogo kama hicho kimekufungulia mlango.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…