Ushauri: Nioe yupi Kati ya hawa wanawake wawili?

Ushauri: Nioe yupi Kati ya hawa wanawake wawili?

Mwisho wa siku...
1 atakupiga na kitu kizito kichwani.
2 atakupiga na kitu chenye ncha kali kichwani..

Jipe muda kuchunguza mmoja baada ya mwingine.



Utastaajabu wote hawakufai.
 
Mkuu,
Binti namba 1, umefahamiana naye kwa miezi 3
Binti namba 2, umefahamiana naye kwa wiki 1
Leo, upo mbele yetu ukiomba tukupe ushauri wa uoe yupi kati yao...

Ushauri:
Jenga mahusiano ya angalau mwaka (yaani si chini ya mwaka), ili uweze tambua tabia ya mwanamke, muda uliokaa nao ni mfupi mno kuweza kuamua yupi wa kuoa...

Unapotaka kuoa, hutizami tabia tu ya mwanamke, unadadisi kujua hadi familia wanazotokea hao unaowahitaji...

Kitu ninachoona kitakuponza, ni kulinganisha binti 1 na binti 2 badala ya kutazama ni vitu gani unavyohitaji mkeo mtarajiwa awe navyo...

Oa mtu unayemfahamu ndani na nje
Baada ya kuoa atakuja na thread ya msioe [emoji23]
 
wa miezi 3 hajakupa wa wiki amekupa.....si ndio??? au?
Huyu wa kwanza nilipomuuliza kama yupo tayari kuolewa na mimi aliniambia ameniamini nisijali kuhusu hilo muda ukifika nitamuoa.

Wa pili tumejuana muda mfupi ila kila napo muhitaji anakuja huyu yupo tayari kuolewa na mimi muda wowote pia kasema yupo tayari kuvumilia madhaifu yangu.
 
Una rangi gani mkuu mpaka imependwa hivyo? Hakuna kingine kakupendea huyo wa pili?

Una umri gani na unajishughulisha na nini?
Akikujibu nitag.maana wanawake wanapenda rangi walifia mv bukoba, wanawake tunajuana tabia zetu sio za kupenda rangi ya mwanaume
 
Wa 1 ni asilimia kubwa hakupendi na unavyozidi gharamia ndo kabisaaaaa unapoteza mvuto.KwanZa mwanamke akupende akuzungushe hivyo


Wa pili anaweza kuwa ana interest na wewe

Ila udhaifu wako wewe ni mzee wa kukurupuka Huna unalolijua kuhusu hao wanawake na mihemuko yako itaku cost sana,punguza wenge tulia relax kwanza na kwa mawenge yako hayo USioe yotote kati ya hao km huyajitimiza nae mwaka1
 
Huyu wa kwanza nilipomuuliza kama yupo tayari kuolewa na mimi aliniambia ameniamini nisijali kuhusu hilo muda ukifika nitamuoa.

Wa pili tumejuana muda mfupi ila kila napo muhitaji anakuja huyu yupo tayari kuolewa na mimi muda wowote pia kasema yupo tayari kuvumilia madhaifu yangu.
umewala?????
 
Habari za siku wadau

Kama kichwa cha habari kinavyosomeka hapo juu katika mapambano ya kutafuta mwenza wa maisha nimejikuta naangukia kwa wanawake wawili ambao wote naona ni bora wanavigezo vile nilivyokuwa nahitaji.

Mimi siku zote nimekuwa navutiwa zaidi na mwanamke ambaye hana tamaa ya vitu vikubwa hapo ndipo nilikuja kumpata binti mmoja hivi miaka 20 mpaka sasa tunamiezi mitatu ya uchumba nilimuhaidi mambo mengi sababu kweli na lengo kumuoa kabisa huyu mwanamke.

Huyu mwanamke hana tamaa halafu ni mzuri sema mazingira ya kwao ni magumu kwa kipato nilikuja kugundua ata chakula kwao hapati milo mitatu nikamuuliza kwanini alikuwa aniambii akasema yeye analizika tu na hali iliyopo mana ndio maisha aliyokulia.

Hivyo nilijitahidi kumpa mahitaji yake yote ambapo pale anaona anakwama ata pale alipoumwa mimi nilikuwa bega kwa bega na huyu mchumb wangu kuna siku alipata homa mama yake akaenda kumchukulia dawa bila vipimo hapo nilipogundua hawakuwa na hela kwenda hospital. Ikabidi mimi nitoe hela akaenda hospital.

Sasa kiufupi huyu binti yeye akiomba hela basi ni ya kusukia tu ama vocha ana aibu Sana ata nikimpigia tuongee huwa haoneshi ushirikiano kuna vitu vingi huwa nahitaji kuvijua lakini hanipi ushirikiano.

Na shida zaidi katika hii miezi mitatu kuja kwangu inakuwa changamoto kila tunavyohaidiana kukutana siku ya jumapili yani sababu lazima itokee mara sijaja sababu ya jambo fulani najaribu tukutane hata sehemu nyingine tofauti na kwangu, bado sababu zinajitokeza ikabidi nimuulize kwanini inakuwa hivi akaniambia mama anavoenda kutafuta anamuachia bibi hivyo anashindwa kutoka.

Sasa huu ni mwezi wa tatu nachojiuliza siku zote yeye yupo bize sitaki kukubaliana na hili mpaka sasa sioni dalili mimi pia nahitaji mahitaji yangu kama mwanaume nahitaji kupata kwa mwanamke naye mpenda.

Mpaka sasa nipo njiapanda sijui nimuache ama niendelee kumpa muda? Mana nimemuuliza kama yupo tayari kuishi na mimi kasema nisijali muda ukifika nitamuoa Imebidi nitafute mbadala ili niweze kupata mahitaji yangu.

Wiki hili nimejikuta nakutana na binti mwingine hapa mtaani ni binti wa huko geita huyu anamiaka 22 huyu naona yupo tofauti Sana na yule mchumba wangu katika hizi siku chache tulizokutana huyu binti amenielewa San.

kila Napo muhitaji anakuja atakama yupo bize na yupo tayari tuanze kuishi pamoja mana inaonekana kaipenda rangi yangu yupo tayari tuzae sasa jana amerudi kwao kusalimia ila nae tumepanga mengi
Pole Sana Kaka kwa mkanganyiko huo nataka nkusaidie kwamba mtu hapimwi kwakuja kwako marakwa Mara mke anapimwa kwa tabia nataka nkupe angalia faida na hasara za wote ndipo uchukue maamuzi yakuwa nae mmoja jiulize swli huyo anaekuja kwako Mara kwa Mara he akipata mchepuko mwingine hawezi kuwa mwepesi kwenda kwake Ivo basi Kuna watu wanaheshimu misimamo yao ili waweze kuwa mama Bora Asante
 
Yakupasa kuwa mvumilivu kijana maisha ya ndoa utayafuraia pindi tu mnapoingia kwenye ndoa lkn badae mambo uja kujitokeza yale makucha yaliyofichwa apo sasa ndio utaanza kujuta wakati ndio ushaingia ndoani kaa chunguza kwanza kabla ya kufanya maamuzi yoyote alafu utakuja kushukuru badae
 
Back
Top Bottom