Ushauri: Rais Mstaafu Kikwete, kwa hili la bandari unajiaibisha na kujivua nguo

Familia ya manyang`au habari ya MJINI kwao Ni KUJILIMBIKIZIA Mali za NCHI YETU.siku yaja watazitapika.
Kumbumbuka hawa wote ni familia moja
1.Mama Mbunge
2.Mtoto waziri
3.Jokate mkuu wa wilaya
4.Mwana FA naibu waziri
5..........
6...........
 
Kusema Kinana ni dalali wa DP ni kukosa ufahamu wa kinachoendelea. Waarabu wanamiliki migodi huko DRC na Rwanda, na huko yupo Kinana?.

Jitahidi uipate picha nzima ya uchumi wa dunia wa wakati huu itakusaidia kuondoka na hizi fikra nyingi hasi unazotembea nazo kichwani.
 
Umenena ukweli mtupu.

Yani huyu baba anangejua angeendelea kukaa kimya lakini sasa katuonyesha upande aliopo kitu ambacho si kizuri

Wananchi hatuutaki huu mkataba mbovu wa Bandari periodt.
 
Picha nzima ya uchumi wa dunia?
Africa Kuna utu?
Kuna mwenye kujenga uchumi wa Nchi yake?

Kinana na kikwete Ni maswahiba wanaoshirikiana katika kuzitafuna RASILIMALI za TAMGANYIKA YETU.

Mwenye tuhuma za kuua Elephant huko Tarangire wakati wa Kikwete ni RAIS Ni Nani,Si ni Kinana huyu huyu?

Bado mtu Kama Kikwete Ugonjwa huo huo au Maradhi Yale Yale ya kuiba RASILIMALI zetu amemrithisha Ridhiwani wake.
Lengo lao Ni wazidi kuwa na nguvu za kiuchumi vizazi na vizazi ili watu change walafi waendelee kutuamua Ni Nani atakuwa RAIS wa kila awamu zijazo.

FEDHA wanazozipata watazitumia kuwahonga Wananchi wasio na uelewa kwa :-
1).Kanga
2).Unga
3).chumvi
4). The. 5,000/=
Kujazwa kwenye Malory na kupewa CHAKULA ili wao wafanikiwe lengo lao.
 
Hoja kama hizi zinaishia humu humu JF haziendelezwi kwa vitendo ili ziweze kuleta tija ya maana. Kikwete na familia yake ni wanasiasa wanajishughulisha katika masuala yote ya kisiasa, wanachama wa CCM wenye kuzifanya kwa vitendo siasa za majukwaani na zile za ufuatiliaji.

Sisi wengine ni mpaka tutakapoacha kulialia na kulalamika na kunyoosheana vidole nadhani ndio tutaweza kuonyesha kuwa anachokifanya JK na familia yake sio suala la kistaarabu hata kidogo. Kwani wa kutakiwa kujua kuwa sio kiongozi mzuri ni hao hao wanaopewa kanga, unga na vitenge katika mikutano ya siasa baada ya kukaa juani kwa muda mrefu wakisikiliza hotuba.

Hao wanaopewa fulana ndio mtaji wa kutakiwa kukombolewa kiakili, lakini ni ukombozi wa kivitendo sio huu wa nadharia nyingi za JF.
 
Hotuba ile ya kikwete iliwalenga TEC kuwa wanatumia jukwaa la dini kuhubiri siasa,jee yeye pale kwenye jukwaa la Kanisa la Wasabato alikuwa anahubiri Injili? Mimi naona serikali baada ya kukosa majibu kwa hoja za wale wanaohoji vipengele visivyokuwa na maslahi kwa nchi kwenye mkataba wa DPW ndiyo walilielekeza sakata hili kwenye mkondo wa dini ili kupata uungwaji mkono toka kwa Waislam. TEC walitoa waraka wao majuzi tu lakini tangu muda wote kabla ya waraka wao mijadala kwenye mitandao ni kuwa mkataba huu unahojiwa kwa vile Rais ni Muislam na na wanaotaka kuwekeza pia ni Waislam na baadhi ya wanaharakati wa Kiislam walisimamia hoja hii mbona Kikwete hakusema kitu hadi ulipotoka waraka wa TEC? Kikwete amejidhalilisha sana kwa kuchukua upande katika sakata hili.
 
Yawezekana wewe Ni mmoja hao wanafaidika na UBOVU wa KATIBA ya 1977 tuliyonayo,huenda una cheo ama u mmoja wa watoto wa wakubwa.

Yamkini pia u mlamba miguu na wenye kufuata viatu vya Alina ridhiwani.
Katika mazingira hayo huwezi Ina ubaya wa Ufisadi mkubwa unaendelea NCHINI.

UKIFUMGUA KINYWA NA KILA CHAKULA
UMALIZI VILIVYOKO KWENYE SAHANI,VILIVYOBAKI MNAMWAGA KWA KIBURI BILA KUJALI HALI HALISI YA MAISHA MAGUMU WALIYONAYO.

Kama wewe Ni mwanamke mume wako akiwekwa ndani na kubanwa sehemu na Siri huenda ungeelewa Nchi hii Hali sio swari.

Iko siku MUNGU atawalipa mabaya na kufuru zenu Kama si hapa duniani,
Msiporidhika na mishahara yenu/ kipato chenu halali na mkajilimbikizia Mali kwa DHULUMA hata pasipo kuwa na hofu ya MUNGU na huruma kwa WANANCHI.
Mkawa na mioyo migumu isiyo na Toba,
Siku moja kfo chako kitafika na utaenda kutoa hesabu mbele ya MUNGU.

Huko HAKUNA logo logo na hutaweza kusema haya yanaishia JF.
 
Umeandika kwa hisia kali ungejua mimi ni sawa tu na yoyote yule. Hawa tunaowanyooshea vidole kwa sababu shida zetu ni nyingi na tunaziona kama vile hazimaliki, ni binadamu kama sisi na wanayo madhaifu kama yetu.

Cha muhimu ni kujitokeza kwa vitendo kupambania kile tunachokiamini kuliko kuishia kulalamikia na kulaani tu
 
Usimzuie kutoa maoni yake, ila ni ruksa kumkosoa kwa staha.
 
Hata kelele hizi zinasaidia Sana TU.
 
Nimesema Kinana ndio dalali/broker wa UAE hapa Tanzania!
Hao madalali wa DRC na Rwanda wa UAE utawatafuta wewe!🤣🤣
 
Nimesema Kinana ndio dalali/broker wa UAE hapa Tanzania!
Hao madalali wa DRC na Rwanda wa UAE utawatafuta wewe!🤣🤣
Kupakana matope ndio sifa ya mtanzania. Mwarabu anamiliki migodi huko Rwanda na DRC na kutumia bandari yetu ni masuala ya logistics sio masuala ya udalali wa Kinana, hizo ni conspiracy theories za kitanzania ni maneno ya udaku.

Mwarabu anafanya biashara ya uwekezaji wa kwenye sekta ya bandari duniani Investor Port.

Anakwenda kuishikilia shughuli nzima ya uletaji wa mizigo bandarini na upelekeaji wa makontena ya madini huko ughaibuni.
 

Kinana na udalali wake hapa Tanzania vinahusiana nini na waarabu kuchimba Madini DRC na Rwanda? Kama hujui udalali wa Kinana na hawa Masheikh wa Dubai kaa kimya!!
Acha ujinga wako huyo mwarabú anafanya biashara ya uwekezaji huko unakosema kote Duniani kwa contractual terms gani? Ni hizi hizi terms alizosaini Samia na hiyo Kampuni?
Kule ulaya unakosema anafanya kazi kwenye banadari umeona mikataba yao waliosaini hata ukawa unawakingia kifua? Acheni njaa zenu wakati mwingine ni bora kukaa kimya badala ya kuwa ili mradi na wewe uonekane umechangia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…